Zitto - Kamati ya madini - CHADEMA

Kwa hiyo umeamua kuuchuna kabisa kuhusu vyombo vya habari binafsi wakati wa Nyerere...?
 
Huyu Chacha Wangwe inavyoonekana si Mpinzani wala haipendi Tanzania.Kikwete katumia akili sana kumteua mtu aliyeibua hiyo hoja bungeni ili akaishauri kamati vizuri kwenye suala hilo,kwa sababu ni dhahiri kwamba anaonekana kuwa na uelewa wa mambo hayo,walau kisiasa.Huyu Wangwe sasa alikuwa anataka mbunge mpinzani yupi ateuliwe?yeye?Hebu wamwache Zitto bwana,huenda akawa mkombozi wa nchi hapo baadaye.

Mungu Ibariki Tanzania.
 
Jamani wandugu acheni kutumia vibaya elimu kiasi hicho...Mnaposema Zitto hana elimu ya madini mna maana gani hapa?..
Hivi nyie nyote mloona kasoro ktk mikataba hii mmesomea madini? ama nyote ni wanasheria?.
Duh! mimi naona karibu hata bunge letu litahitaji watu wenye shahada ya sheria ili kutunga sheria nikifuata mtazamo wenu kwani yaonyesha wazi mnaamini kuwa huwezi kufahamu uzito na athari ya kitu bila kuwa na elimu yake. Yaani hata njaa inahitaji elimu ya upishi wa chakula uweze ku solve tatizo la njaa bila kujua kwamba njaa kinachotakiwa ni mahesabu ya kiwango cha shibe sio degree ya upishi.
Jamani haya si ndio maswala tunayosema huhitaji kuwa mwana sayansi! - ama.
Damn!
 
Jamani wandugu acheni kutumia vibaya elimu kiasi hicho...Mnaposema Zitto hana elimu ya madini mna maana gani hapa?..
Hivi nyie nyote mloona kasoro ktk mikataba hii mmesomea madini? ama nyote ni wanasheria?.
Duh! mimi naona karibu hata bunge letu litahitaji watu wenye shahada ya sheria ili kutunga sheria nikifuata mtazamo wenu kwani yaonyesha wazi mnaamini kuwa huwezi kufahamu uzito na athari ya kitu bila kuwa na elimu yake. Yaani hata njaa inahitaji elimu ya upishi wa chakula uweze ku solve tatizo la njaa bila kujua kwamba njaa kinachotakiwa ni mahesabu ya kiwango cha shibe sio degree ya upishi.
Jamani haya si ndio maswala tunayosema huhitaji kuwa mwana sayansi! - ama.
Damn!

Mkandara,

Hilo ndio tatizo la sisi Waafrika, tunathamini mno certificates badala ya kuthamini elimu.

Watu wanaona ili uwe na elimu lazima uwe na Ph.D kwenye jambo husika, that is nosense.

Kuna mwalimu mmoja alikuwa anatufundisha kazini, akasema wanapotuma mtu Afrika, wanambandika cheo cha Dr. hata kama ana degree moja, maana waafrika hawawezi kuamini kama jamaa anajua anachokifundisha kama sio Dr.

Ndio maana hata bungeni kila mtu anakimbilia kujiita Dr au prof. wakati kazi wanazofanya bungeni haziendani na hizo Ph.D.

Mara ngapi umesikia huku nje wanaita Dr. Condorize au Dr. Brown kwa UK? Hawa wote wana Ph.D lakini unaweza kukaa miaka kumi usisikie hata mtu anaongelea hizo Ph.D

Wangelikuwa wanafundisha au kwenye research basi hizo Ph.D zao zingetajwa lakini wanapofanya kazi tofauti, hizo Ph.D zao zinakuwa na faida ndogo sana.

Nina MD wangu, imenichukua miaka miwli kuja kujua ni Dr. Hata hiyo nilijua through ku serach kwenye internet na wala sio kupitia kazini. Lakini ingelikuwa Tanzania, hata kusahau kumwita Dr. ingelikuwa nongwa na balaa kubwa.

Zitto kwa kufuatilia madini, tayari ana elimu kubwa ya madini labda hata kuliko hao waliosomea madini miaka 20 iliyopita na sasa ni wanasiasa. Elimu ya madarasa sawa inasaidia lakini elimu bora zaidi ni ile unayojifunza kila siku na ile unayotumia kutatua matatizo yanayokuzunguka. Elimu ya kutundika ukutani ni upuzi mtupu wa kutudanganya na kututambia watanzania, wakati madini yanaibiwa wanashindwa hata kutetea.
 
Mtanzania,

Nashukuru kuwa umenielewa hapo nilipozungumzia swala hili maanake navyofahamu mimi Zitto hapa ni mshauri ktk upimaji wa kiasi gani cha chakula tunahitaji na sidhani kama shibe inahitaji elimu ya mapishi. Tunapenda sana kuchanganya vitu hivi kiasi kwamba tunadhani mtu yeyote asiyekuwa na elimu ya mapishi hawezi kufahamu ni kiasi gani cha chakula anahitaji ili apate kuridhika na shibe...
Jamani hii elimu imekuwa hata kuagiza chakula mgahawani!...maanake navyofahamu wapishi ndio hao kina Barricks, Zitto hataingia jikoni kufunga mkataba nao.
 
Mheshimiwa Spika, utata huu ambao umegubika sekta hii ya madini unaweza kufafanuliwa na Bunge lako Tukufu kupitia Kamati Teule. Kamati Teule ya Bunge ichunguze upitiaji wa mikataba hii na kuona kama kuna vitendo vyovyote vya uvunjaji wa sheria za nchi na kupotea kwa mapato ya Serikali na ufisadi.
Mheshimiwa Spika, suala hili ni suala la kitaifa. Halina hata chembe ya itikadi za kivyama. Naamini Wabunge wataamua kwa maslahi ya Taifa letu. Uundwaji wa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza mapitio ya mikataba ya madini na mazingira ya kusainiwa kwa mkataba mpya wa Buzwagi utatoa msaada mkubwa kwa azma ya Rais wetu, Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete ya kuona rasilimali za madini zinafaidisha nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja.
Mhe. Zitto akizungumza Bungeni kutoa hoja ya kuundwa kamati teule ya Bunge


SWALI: Je, Kamati ya Rais iliyoundwa ndiyo kile ambacho Zitto alitaka kifanyike; na je yeye mwenyewe kuwemo imemridhisha?
 
Kitila,

Nakubaliana na wewe juu ya hili na sio wakati wote ni wa kupinga kila kitu, inabidi chama cha upinzani wakati mwingine kiwe tayari kushirikiana na serikali kwa faida ya nchi.

Kwenye hili la kamati ni afadhali kuwa ndani na ku influence maamuzi ya kamati na hivyo sheria ya madini kwa faida ya nchi kuliko kuwa nje.

Pamoja na kusema hayo, Wangwe naye ana right ya kupinga na hata siku moja kupinga kwake kusichukuliwe kama amechukia kwasababu hayumo kwenye kamati.

Siasa ni ngumu sana na wakati mwingine inabidi kuachana na misimamo mikali na kuchukua msimamo wa kati ili kupata ufumbuzi wa tatizo.
Magreat Wa wakati huo..HIV wapo?
 
Back
Top Bottom