Zitto - Kamati ya madini - CHADEMA

Kuntakinte

JF-Expert Member
May 26, 2007
701
31
:: CHADEMA sasa waanza kumchimba
:: Chacha amshauri ajiuzulu, yeye agoma
:: Asema hajausaliti upinzani, hatishiki
:: Leo anamaliza adhabu ya kufukuzwa


na godfrey dilunga

HATUA ya Rais Jakaya Kikwete kumteua Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Kabwe Zitto, kuingia katika Kamati ya Kuchunguza Mikataba ya Madini inaelekea imezusha mgogoro wa ndani katika Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Hatua hiyo imetokana na Mbunge wa Tarime (CHADEMA), Chacha Wangwe, kutamka hadharani kuwa Zitto anapaswa kujiuzulu kutoka kwenye Kamati hiyo iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete, hali inayopingana na fikra za Zitto.

“Zitto anapaswa kujiuzulu si zaidi ya saa 24 kuanzia leo. Kukubali uteuzi ni sawa na kuusaliti upinzani nchini,” Chacha alikaririwa akimwambia mmoja wa wabunge mjini Dodoma jana.

Mbali na kauli hiyo, gazeti moja la kila siku jana lilimkariri Wangwe, hivi: “Alisema anapinga suala hilo kwa madai kwamba, kuundwa kwa kamati hiyo kumelenga kudhoofisha hoja ya msingi ya wapinzani ya kutaka sheria ya madini ifutwe kabla ya kwenda katika hatua ya pili ya kujadili mikataba. ‘Kizingiti kikubwa ni sheria, ndiyo haijakaa vizuri. Hivyo kilichotakiwa ni sheria kufutwa kwanza halafu ndiyo tuzungumze mikataba mipya’.”

Mwandishi Wetu alipowasiliana naye mjini Dodoma jana, Wangwe alisema amsubiri kidogo amalize kikao cha Kamati na hadi tunakwenda mitamboni ilikuwa hajapatikana na simu yake ya mkononi muda wote ilikuwa imezimwa.

Kwa upande wake Zitto, aliliambia Mtanzania kuwa hajausaliti upinzani na wala kuteuliwa kwake katika kamati hii hakupingani na dhana yoyote kwani imebeba malengo yanayowiana na dhamira ya kambi ya upinzani na kwamba hatajiengua kutoka katika kamati hiyo.

Kauli hiyo ya Zitto inapingana na ile iliyotolewa na Wangwe. Wangwe na Zitto wote ni wabunge kutoka CHADEMA na Zitto ni bosi wake Wangwe kwani ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho. Hata hivyo, Wangwe ni mmoja kati ya viongozi wenye nguvu kubwa ya ushawishi ndani ya CHADEMA.

Zitto alisema si busara kwake kujiondoa katika kamati hiyo kwa kuwa malengo yake yanarandana na ya kambi ya upinzani.

Akifafanua Zitto alisema baadhi ya hadidu za rejea za Kamati ya Madini iliyoundwa na Rais Kikwete, zinarandana na baadhi ya vipengele vya Azimio la Songea, ambalo lilitangazwa na upinzani mjini Songea, Septemba 10, mwaka huu.

Alisema azimio hilo linahimiza kuundwa kwa kamati ya madini pamoja na kufanyika kwa marekebisho ya sheria za; madini, kodi ya mapato ya mwaka 2004 na sheria ya uwekezaji.

“Si kweli kwamba kambi ya upinzani ilitaka kufutwa kwa sheria ya madini, matakwa yake ni kufanyiwa marekebisho ya sheria hiyo pamoja na sheria nyingine,” alisema Zitto.

Alisema vipengele hivyo ni sehemu ya hadidu za rejea za kamati ya madini iliyoundwa na Rais Kikwete.

Rais Kikwete alitangaza dhamira ya kuunda Kamati ya Madini wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Nane wa Chama Cha Mapinduzi mjini Dodoma, hivi karibuni.

Alitimiza dhamira yake hiyo juzi kwa kuwateua Mwenyekiti wa Kamati, Jaji Mark Bomani, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige na Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe.

Wengine ni Peter Machunde kutoka Soko la Hisa Dar es Salaam (DSE), David Tarimo kutoka Kampuni ya Uhakiki wa Hesabu ya PriceWaterCoopers, Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa katika Wizara ya Nishati na Madini, Maria Kejo na Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange.

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Kamishna wa Sera katika Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha na Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Makazi katika Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Edward Kihundwa.

Kamati hiyo bado haijaanza kazi ingawa imepewa kipindi cha miezi mitatu kukamilisha kazi na kukabidhi ripoti kwa Rais Kikwete.

Ina maana wananchi ni wa CCM au wa CHADEMA? Mhe. Chacha bado sijamuelewa maana kuteuliwa na Rais lazima kuna sababu za msingi au umeonekana ufanisi na upeo wa mtu as Individual kwenye kupanga na Kujenga Hoja sasa iweje waseme amewasaliti? Au alitaka awe yeye kwenye Kamati. Kwani katiba ya CHADEMA inasemaje kuhusu wajumbe hawatakiwi kushiriki kwenye mambo ya Kujenga nchi?
 
it is very possible kuwa huyo Wangwe mwenyewe ndio anatumika, i personally do not see why Zitto should not be a member. Angeitwa msaliti kama angejua maovu na akayakalia kimya. Itakuwa ni utoto kusema hii yetu ile yao, issue ya madini in my opinion ni ya tanzania wote, wapinzani na wana CCM, na wengine wote. Yeye Wangwe hapa ndiyo tatizo, hii kauli angeitunza hadi baada ya wiki nne kazi ya hiyo kamati itakapoisha.
 
Hakuna hatia yeyote, hayo ni mawazo yake Chacha kama ambavyo wananchi wengine wametoa, na tunaheshimu mawazo yake; Pamoja na kwamba yeye ni kiongozi wa CHADEMA, mawazo yake hayawezi kuwa msimamo wa CHADEMA. I am sure Zitto alifanya consultation ya kutosha na viongozi wenzake kabla ya kukubali uteuzi. Uteuzi wake kimsingi upo ndani ya basic principles za CHADEMA moja ikiwa ni kutumia uwezo wa kila mwanachama kwa ajili ya maendeleo ya nchi. There is no conflict of interest whatsover. Chacha anahitaji kuelimishwa pamoja na mambo mengine, kuwa katika ulimwengu wa leo jazba haina nafasi. Kinachotakiwa sasa ni umahiri wa kujenga hoja based on scientific evidence. Kilichofanyika hapa ni kwamba Mhe Zitto Zuberi Kabwe amepata fursa na forum ya kujenga hoja zake vizuri kuhusu madini yetu na kama hoja zake zitapata nafasi akishirikiana na wanakamati wenzake, maana yake ni kwamba Taifa letu litapona. Sasa Taifa letu likipona na likaanza kufaidika na madini, CHADEMA kama chama inaathirika vipi?
 
Kitila,

Nakubaliana na wewe juu ya hili na sio wakati wote ni wa kupinga kila kitu, inabidi chama cha upinzani wakati mwingine kiwe tayari kushirikiana na serikali kwa faida ya nchi.

Kwenye hili la kamati ni afadhali kuwa ndani na ku influence maamuzi ya kamati na hivyo sheria ya madini kwa faida ya nchi kuliko kuwa nje.

Pamoja na kusema hayo, Wangwe naye ana right ya kupinga na hata siku moja kupinga kwake kusichukuliwe kama amechukia kwasababu hayumo kwenye kamati.

Siasa ni ngumu sana na wakati mwingine inabidi kuachana na misimamo mikali na kuchukua msimamo wa kati ili kupata ufumbuzi wa tatizo.
 
kwa kuwa Wangwe hajatoa maelezo hayo hadharani, zaidi ya kumsimulia mtu ambaye Identity haijawekwa wazi;
Napenda kutoamini kuwa yaliyosemwa ni kweli.
 
Mimi sishangai sana, Wangwe akili zake huwa siyo nzuri licha ya kuwa na ushawishi hususan katika jimbo lake. Na mimi naamini ushawishi wake si kwa CHADEMA kwa ujumla, bali zaidi ni kwenye jimbo lake. Kwanza Wangwe is too mechanical. Pili, Wangwe huwa ana utamaduni wa kupinga karibu kila kitu. Haelewi maana ya upinzani.

Hata wakati vyama vya upinzani vilipoanza kuendesha mazungumzo ya kutaka kuungana, Wangwe alikuwa ni miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kuponda muungano huo. Nilisoma makala yake Tanzania daima ambayo ilikuwa na maneno makali mno na ya kuvunja moyo.

Hata yanayotokea Tarime tusiyapuuze sana, inawezekana yanachangiwa na hekima ndogo ya Wangwe. Vilevile, Bungeni kauli zake mara nyingi zimekuwa za jazba badala ya kutawaliwa na hoja.

Nikirejea hili la Zitto, kitendo cha Wangwe kupinga uteuzi wa Zitto kwanza ni utoto na kukosa hekima na uelewa wa maana ya siasa na lengo la upinzani. Vyama vya upinzani havipo kwa ajili ya kupinga kila kit bali kwa ajili ya kukosoa na kurekebisha penye dosari kwa nia ya kujenga na kuboresha maendeleo ya nchi.

Sasa Zitto alikuwa ameongea masuala mengi ya msingi kuhusu mikataba ya madini na mambo mengine kuhusiana na rasilimali za nchi. Bila shaka aliyoyatamka Bungeni na kwenye majukwaa ya siasa ni sehemu ndogo tu ya yale aliyokuwa nayo au anayoyafikiria. Sasa akiwa kwenye kamati hiyo, atasaidia sana kutoa mawazo yenye kujenga na kusaidia katika kuboresha mikataba ya madini kwa manufaa ya wananchi. Lakini, kwa ujinga wa Wangwe anataka avuruge tena.

Mimi naomba tumpuuze Wangwe.
 
Kitila,


Pamoja na kusema hayo, Wangwe naye ana right ya kupinga na hata siku moja kupinga kwake kusichukuliwe kama amechukia kwasababu hayumo kwenye kamati.

Ooh, yes, sana tu. Ana haki sana tu tena na wajibu pia. In fact, Wangwe ana haki ya kuwa na wasiwasi kwa sababu historia yetu inaonyesha kuwa serikali inatabia ya kuwa-coopt watu wote ambao huwa radical na huo ndio unakuwaga mwisho wao. So, wasiwasi wa Wangwe mimi binafsi naulewa sana. Sema tu kwa mazingira ya sasa ya siasa zetu, kukataa kwa Zitto kuingia kwenye kamati kungekuwa counter productive to him and to our party as well!
 
Hodo! hodi! hapa, wana-forum wenzangu habari za siku kidogo?

Nami pia naunga mkono uteuzi wa mheshimiwa Zitto Kabwe.

Uamuzi wa mheshimiwa Kabwe kukubali uteuzi wa raisi ni sahihi kabisa kama una baraka zote za wanachama waandamizi wa Chadema.

Katika jamii yoyote ile ilioendelea kunapokuja suala la maslahi ya Taifa basi wananchi wote kwa mujibu wa katiba wana wajibu wa kushiriki na hapa wanawakilishwa na watu wa aina ya mheshimiwa Zitto Kabwe.

Mheshimiwa Zitto Kabwe alijenga hoja nzito kuhusu madini moja ya rasilimali zetu za taifa na kimeeleweka kwamba kuna haja ya kufanya uchunguzi wa kina kwa kupitia hizo sheria za madini na jinsi mikataba ilivotungwa huko kusikojulikana.

Katika siasa ambazo bado hazieleweki kama za nchi yetu watu wa aina ya Chacha na Wangwe wanatakiwa waaangaliwe kwa makini, kwani kwa kauli mchanganyiko wanazozitoa wanaonekana ni walewale wasindikizaji upinzani na watu wa aina hii ni hatari sana.
 
Kwa mtazamo wangu Zitto hatakiwa kujitoa kwenye kamati. kumbuka suala la madini ni la kitaifa si la Chadema. Zitto akijitoa atakuwa amewasaliti watanzania na huo ndiyo unaweza kuwa mwisho wake kisiasa.

Wangwe analiangalia suala la madini Kichadema na si kitaifa. nadhani Rais ameliona suala la madini kama la kitaifa na si CCM, vivyo hivyo Chadema walione kwa mtazamo huo.
 
Engineer Mohammed, usisubiri kuchambuliwa au mawazo yako kujengwa na mtu fulani. does it mean that unaamini kila wanalolisema hao waheshimiwa ulowataja. Unapsema Giza totoro means, Hujaelewa kitu, no hio haiipi sifa yako ya Engineer. Najua ww si kati wale walojipa majina waso na Hadhi nayo, ww Enginee ni sehem ya maisha yako...Kuwa HURU kutoa fikra zako.
Mie Naamini Zitto ni Kijana wa JK since UDSM. so sishangai akipewa post yoyote na hata huo ubunge, naturally, Jamaa hukaa kuamua kiti gani wampe nani...
Nikiungana na wengine...tuone kamati baadi ya kukaa na kufanya uchambuzi wao watatoka na nini. Ila Swali kwa JF wenzangu JK alikuwa anasema kuwa tatizo lipo kwa wataalam wetu. Sijui ktk Hio Kamati kuna watu wanaujuzi wa Kitaalam au La na Utaalam wake ni relevant na MADINI. Nijuavyo Tanzania wataalam as engineers wapo wachache sana ktk MADINI. Kozi ya Madini pale UDSM ilianzishwa rasm 2001/2002. Kabla ya hapo tulikuwa tukifanya exchange program na wazambia. Watanzania wanakwenda Zambia kusoma Madini na Wazambia wanakuja TZ kusoma GEOLOGY. sina statistics, ndo maana nikasema wachache. So kimsingi kama kamati ina wataalam wenye kutoshelezana, basi wafanye kazi ya maana.
 
Turudi nyuma kidogo...

Gazeti lililoandika habari hiyo ni MTANZANIA.

Je, linamilikiwa na nani?
 
zitto naye njaa tu,Mie nilishajua Mpinzani wa kweli ni nani mpaka sasa!,si mtikila ambaye alitumiwa na kina Jk kumuungamiza Sumaye..
wapinzani wa kweli ni watannzia
 
Nimeandika leo kwenye Tanzania Daima kwanini binafsi naamini Zitto hastahili kuwemo kwenye Kamati hiyo ingawa kwa sababu tofauti na hizo za Wangwe. Ni makala ndefu kidogo na nimeonesha kuwa Watanzania wawe na matumaini zaidi na Kamati Teule ya Bunge kuliko hiyo ya Rais!!!
 
huyu Wangwe naye hebu akae kimya yeye analeta siasa kwenye maslahi yetu hapa naona,kabwe ingia hapo ufanye kinachotakiwa labda yakitokea matatizo na unachotetea na kamati haiwezi kukubaliana na wewe na hutaona kama inaweza kubadilisha kitu ndio ujitoe lakini sasa take that opportunity kuweka mabo sawa tusiendelee kuibiwa na wewe Wangwe inabidi utumie akili sio jazba tuu
 
Engineer Mohammed, usisubiri kuchambuliwa au mawazo yako kujengwa na mtu fulani. does it mean that unaamini kila wanalolisema hao waheshimiwa ulowataja. Unapsema Giza totoro means, Hujaelewa kitu, no hio haiipi sifa yako ya Engineer. Najua ww si kati wale walojipa majina waso na Hadhi nayo, ww Enginee ni sehem ya maisha yako...Kuwa HURU kutoa fikra zako.

Natumai Engineer amepata ujumbe
 
Sitaki kuamini sana kama kweli chacha ameongea maneno haya. Kwa maoni yangu hii ni njia ya kutaka kubomoa umaarufu aliokwisha upata mchapa kazi zito, ingawa naamini hawatafanikiwa. Nina imani na uwakilishi wa zito kwenye kamati.
 
Magazeti ya mkoloni na mwizi Rostam Aziz utayaweza kwa propaganda zao? Rostam yuko kwenye mission ya kumuharibu zitto na attack dogs wake wa habari corporation wanajua hilo.

Hata kama Chacha ameyasema hayo, kwani hiyo ni sababu ya kusema kuwa kuna mvutano CHADEMA? Watu kibao tu ndani ya CHADEMA na nje wameunga mkono zitto kuwa ndani ya kamati kama vile ambavyo wengi tu wamepinga.

Chacha ana kila right ya kusema alichosema maana yeye ni mbunge wa Tarime ambako kuna migodi mikubwa kabisa ya dhahabu karibu mitatu! Na sio kwamba Chacha alitaka kuwa kwenye kamati hiyo ambayo so far inaonyesha kuwa hakuna chochote itakachofanya zaidi ya kuja na stori ndefu zilizopita.

Huyu Rostam siku yake inakuja tu! very soon!
 
Hivi kwani Chacha si katoa mawazo yake kama mwanachama mwingine yeyote? Hata kama chacha kasema,kasema hivyo kwa sababau ndani ya Chadema kuna Demokrasia zaidi to the extent mwanachama au kiongozi yeyote ndani ya chama hicho anaweza kutoa mawazo yake bila kutishiwa na mtu yeyote.

CHADEMA ni chama makini sana kinachompa kila mtu uhuru wa kutoa mawazo,naamini ingekua ni ndani ya CCM mbunge katofautiana na wakuu wake basi ingekua balaa kwa mhusika.

So haya magazeti yasituletee spinning zisizo na mantiki,Ingekua ni Chadema wameshika dola kama CCm nadhani huko bungeni wabunge wasingeamuliwa la kuzungumza kama wanavyofanya CCM leo hii.La Richmond lingekua limeshajadiliwa,Rada,IPTL etc.
 
16/11/2007


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Profesa Baregu na Dr Slaa kuongoza mjadala wa wasomi
kuhusu
Ufisadi na Hatma ya Rasilimali za Tanzania

• Wabunge Zitto Kabwe, Chacha Wangwe na Suzan Lyimo nao kushiriki
• Hakuna kuchimbana CHADEMA; tunaheshimu uhuru wa mawazo
• Maoni ya kongamano kupelekwa kwenye Kamati

Kesho 17 Novemba, 2007 ni siku ya Wanafunzi Duniani. Kurugenzi ya Vijana wa CHADEMA imeandaa Kongamano la Vijana Wasomi wa Vyuo Vikuu katika siku ya wanafunzi duniani. Kongamano hilo litafanyika katika Ukumbi wa DDC Mlimani uliopo barabara ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuanzia saa 2 asubuhi mpaka saa 8 mchana ambapo wanavyuo, wanafunzi wa sekondari na vijana wafanyakazi nao wanaalikwa kushiriki. Watoa mada katika kongamano hilo ni Dr Wilbroad Slaa(Mb), Zitto Kabwe(Mb) na mwanasheria Tundu Lissu. Wajadilifu(discussants) katika kongamano hilo ni Dr Azaveli Lwaitama, Makwaia wa Kuhenga, Chacha Wangwe(Mb) na Suzan Lyimo(Mb). Mada zitakazojadiliwa ni pamoja na: Katiba, Sheria, Mikataba na mustakabali wa madini yetu; Vuguvugu la Demokrasia na Maendeleo; na Ufisadi na hatma ya Tanzania.

“Maadhimisho ya siku hii na kongamano hili ni shughuli ambayo ilishapangwa siku nyingi kwamba ingefanyika katika tarehe hii kutokana na mpango wa mwaka wa vijana wa CHADEMA. Hata hivyo tunategemea watoa mada na wajadilifu watazingatia pia matukio ya kisiasa yaliyotokea hapa nchini hivi karibuni”.

“Kongamano hili limekuja wakati mwafaka ambapo Rais Kikwete amepanua wigo wa Kamati ya kupitia sheria na mikataba ya madini na wakati huo huo Bunge limeunda Kamati Teule ya kuchunguza mkataba tata wa Kampuni ya Richmond. Hivyo tutawasilisha hoja na maoni mbalimbali yatakayotolewa kwenye kongamano hilo kwa kamati hizi mbili pamoja na wadau wengine”.

Kurugenzi ya Vijana wa CHADEMA inaamini kuwa kuundwa kwa kamati hizi mbili hakupaswi kusitisha mjadala wa umma unaoendelea hivi sasa kuhusu ufisadi na rasilimali za Taifa. Kuundwa kwa kamati hizi ni sababu ya ziada ya mjadala wa umma kuhusu masuala haya kuwa mkubwa zaidi ili kamati zipate mawazo ya kina ya umma kwa ajili ya kuyazingatia; na mjadala huu hauwezi kukoma mpaka matakwa ya umma yatakapotekelezwa na kuleta mabadiliko katika maisha ya watanzania. Kadhalika ikumbukwe kwamba kamati hizi mbili zinashughulikia sehemu ndogo sana ya tuhuma zilizopo kwenye orodha ya mafisadi(list of shame), hivyo tunarejea rai ya viongozi wakuu wa vyama vya upinzani ya kuundwa tume huru ya kuchunguza tuhuma za ufisadi zilizotolewa.

Wakati huo huo, Kurugenzi ya Vijana ya CHADEMA inakanusha habari iliyoandikwa na gazeti la Mtanzania(16/11/2007) kwamba “Zitto yuko matatani kutokana na CHADEMA kumchimba”; hivyo ifahamike rasmi kwa umma kwamba “CHADEMA haimchimbi Zitto Kabwe”. CHADEMA ni chama chenye umoja na ushirikiano baina ya viongozi wetu. Kwa mujibu wa katiba yetu, CHADEMA ni chama kinachoamini katika uhuru wa fikra ikiwemo katika kuheshimu uhuru wa kutofautiana kimawazo. Hivyo, Chacha Wangwe ama kiongozi mwingine yoyote wa chama ana uhuru wa kutoa maoni yake kuhusu uteuzi wa Zitto Kabwe kwenye Kamati aliyoitangaza Rais ya kupitia mikataba ya Madini. Wakati wanachama mbalimbali wa CHADEMA na watanzania kwa ujumla wanaendelea kutoa maoni kuhusu uteuzi huo, izingatiwe kuwa suala hili litatolewa msimamo rasmi na wasemaji wakuu wa chama kwa mujibu wa katiba na itifaki ya chama chetu. Izingatiwe pia kuwa CHADEMA ni chama kinachoongozwa kwa falsafa ya “nguvu ya umma” na itikadi ya “mrengo wa kati”; hivyo tunaamini katika siasa zilizo juu ya vyama zinazosimamia zaidi maslahi ya taifa.

“ Nimezungumza na Zitto akiwa Kigoma, na nimezungumza na Chacha akiwa Dodoma; wote watakuja Dar es salaam kwa ajili ya kuwepo kwenye kongamano, na watazungumzia suala la vuguvugu la demokrasia ya rasilimali na kutoa fikra mbadala ikiwemo kuhusu masuala ya madini”

Katika kuadhimisha siku ya wanafunzi duniani ya mwaka huu tunatarajia vijana wasomi watapata wasaa wa kuutafakari wosia ufuatao uliowahi kutolewa na Hayati Mwalimu Nyerere kwao “Msomi ni sawa na mtu aliyepewa chakula katika kijiji chenye njaa ili apate nguvu akatafute chakula kwenye nchi ya mbali kisha awaletee wananchi wa kijiji chake. Kadhalika msomi yoyote aliyepewa elimu kwa kodi ya wananchi akishindwa kuleta maendeleo yeye ni msaliti kwa watanzania”

Imetolewa na:


John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa
mnyika@yahoo.com
0754694553
 
Back
Top Bottom