valuvalu wa kweli
New Member
- Feb 22, 2013
- 4
- 0
Hongera ZZK.Kaza buti shughuli bado pevu
Ndiyo maana nikasema, CCM imeamua kufanya hivyo ili kuonyesha kile ambacho kilipelekea mpaka maandamo kwa baadhi ya wanaCHADEMA zilikuwa ni kelele ambazo hazina mashiko.Ng'wamapalala unataka kutuambia kwamba huna taarifa kuwa party caucus ya ccm ndo iliamua kumpa uenyekiti wa PAC kamanda Zitto?? usitake kuhadaa watu hapa na ngonjera zako, na tunajua ni kwanini ccm wameamua kumchagua zitto na kumtupa kapuni mwanachama wao wa mlango wa uani mzee cheyo.
Hongera Zitto we ni jembe mzee wa Bariadi anatakiwa kupumzishwa 2015
Mhe Zitto Kabwe ameibuka kidedea kwenye uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa kamati ya hesabu za Serikali (PAC) baada ya kumbwaga Mhe. Cheyo kwa kupata kura 13 kati ya 17.
Zitto awali alikuwa ni mwenyekiti wa POAC, kamati iliyovunjwa siku chache zilizopita na kuunganishwa na kamati ya PAC.
Binafsi nampongeza Zitto na kumtakia utendaji mzuri kwenye majukumu yake hayo mapya. Taifa linamtegemea.
Ndiyo maana nikasema, CCM imeamua kufanya hivyo ili kuonyesha kile ambacho kilipelekea mpaka maandamo kwa baadhi ya wanaCHADEMA zilikuwa ni kelele ambazo hazina mashiko.
Kama CCM ingetaka kumtupa kwenye kapu Mh. Zitto, ingefanya hivyo bila hata kufumba mboni zake. Spika alikuwa ana uwezo wa kumpeleka Mh. Zitto hata kwenye kamati ya bunge ya UKIMWI bila hata ya kutaka kushindanisha kwenye kura na kuweka watu inaotaka PAC.
Mhe Zitto Kabwe ameibuka kidedea kwenye uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa kamati ya hesabu za Serikali (PAC) baada ya kumbwaga Mhe. Cheyo kwa kupata kura 13 kati ya 17.
Zitto awali alikuwa ni mwenyekiti wa POAC, kamati iliyovunjwa siku chache zilizopita na kuunganishwa na kamati ya PAC.
Binafsi nampongeza Zitto na kumtakia utendaji mzuri kwenye majukumu yake hayo mapya. Taifa linamtegemea.
Huwezi kumsikia akilalamika tena na kusema majukumu ya PAC ni mengi kama alivyosikika baada ya kuvunjwa kwa POAC.
Huwezi kumsikia tena akisema hizi ni njama za serikali kudhoofisha upinzani kuimulika serikali.
Huwezi kumsikia tena akisema Spika anafanya kazi kwa maagizo ya CCM.
Huwezi kumsikia tena akisema wajumbe wa kamati ya PAC wanaendekeza uchama badala ya utaifa.
Hawa ndiyo wanaSiasa wetu na yule ndiyo spika wa bunge.
Mkuu Mwita Maranya wewe kweli ni nguli wa siasa za Tanzania, halafu kwa jinsi Mkurya alivyobarikiwa ubishi, The package is complete. Hukosi hata kidogo pa kutokea.Spika makinda amefanya mgawanyo wa wabunge katika kamati mbalimbali kwa maelekezo ya chama chake. Na chama chake ndicho kimeamua kumpa uenyekiti wa PAC zitto kwahiyo hoja ya msigi inabaki pale pale kama nilivyokueleza hapo awali.
Wamefanya hivyo kwa nia moja tu ambayo iko wazi siku zote, wanajaribu kumtumia kufanikisha mipango yao ya siri ambayo sasahivi si siri tena.
Maelekezo toka CCM partycocus! Mana wangemwaga jamaa wananchi tungeichukia zaidi CCM coz tungeamini CHADEMA kaonewa! HONGERA Z. Z. Kabwe.
Spika makinda amefanya mgawanyo wa wabunge katika kamati mbalimbali kwa maelekezo ya chama chake. Na chama chake ndicho kimeamua kumpa uenyekiti wa PAC zitto kwahiyo hoja ya msigi inabaki pale pale kama nilivyokueleza hapo awali.
Wamefanya hivyo kwa nia moja tu ambayo iko wazi siku zote, wanajaribu kumtumia kufanikisha mipango yao ya siri ambayo sasahivi si siri tena.
Mkuu jifunze kuheshimu maoni ya watu nawe kutoa yako unavyoona inafaaHuwa sitaki kabisa kuweka mategemeo ya Taifa kwa mtu mmoja. Tumpe Hongera lakini pia akumbushwe kwamba u-kigeugeu kama aliojaribu kuonyesha pale Tanesco, Nooooo!
Hizi kamati pia nina mashaka nazo sana! Yabidi warudishe mtindo wa kuingiza wataalamu toka nje ya Bunge maana naona kama Bunge linajaribu kuwa na utaalamu wa kila kitu wakati tuonavyo, hali yao kichwani wengi ni mbaya na hawako tayari kuazima washauri.