Zitto Kabwe mwenyekiti mpya kamati ya PAC

Zitto Kabwe mwenyekiti mpya kamati ya PAC

Hongera Zitto ila binafsi naamini mpinzani wa kweli hawezi kupigiwa kura na CCM.
Lakini mwenyekiti wa kamati ni lazima atoke chama pinzani au unataka kusemaje?
 
Kila lililo la heri, na mungu akulinde wewe pamoja na chama chenu, maana kwa sasa mna wakati mgumu, mungu awaepushe na hujuma za maccm!
 
PAC itapitia hesabu za mashirika ya umma na za serikali kuu idawa. Ningekuwa Spika ningeunganisha Serikali za Mitaa na Serikali kuu maana kuna mwingiliano zaidi kuliko mashirika ya umma na serikali kuu
Shukrani mkuu Ndachuwa; nini kimepungua kutoka POAC hadi PAC...maana niliwasikia Chadema kwenye mkutano wao pale Temeke wakilalamika hili swala, bila shaka na wadau wengi walilipigia kelele...Leo Nashangaa wadau wanaunga mkono bila kuainisha mapungufu walio yapigia kelele mwezi uliopita tu...nimependa mkuu ulivyowasilisha maoni yako maana kwenye serikali za mitaa ndio kwenye uozo.!!
 
Last edited by a moderator:
Hongera Zitto. Hii inatokana na utekelezaji wako mzuri wa majukumu yako ya kila siku.

Keep it up!

Wenye kuweka reservation kwenye pongezi zao ni wapinga maendeleo na wabinafsi.
 
i was wrong nilidhani zitto wangemmwaga!!cheyo ovyo tu alikuwa anaifichia serikali maovu mengi kwenye ile kamati,kwa hiyo zitto hatii tena mkono kwenye mashirika kama tanesco na pspf?nielewesheni hapa
 
Hongera kamanda zitto. Mungu akutangulie mbele ya safari yako kuelekea 2015.
 
Another side of the SSM!!!! Mhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh!!!!
 
Hongera Zitto ila binafsi naamini mpinzani wa kweli hawezi kupigiwa kura na CCM.

Mkuu hapa unanichanganya... nijuavyo mimi hii kamati ni "oversight committee" na hivyo ni lazima iongozwe na upinzani, wakati composition kubwa ni wabunge (ambao ni wapiga kura) ni CCM, na nimeona safari hii wabunge wa chadema kwenye kamati hii ni 3 tu, sasa tulitarajia nani wampigie kura mwenyekiti wa kamati hii kama si hao CCM?
Kama una kumbukumbu nzuri utajiuliza wakati Dr. Slaa akiiongoza kamati ya LAAC ni nani walimpigia kura? je wale walikuwa ni Chadema?
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Zitto anafanya kazi nzuri... badala ya kumkatisha tamaa ni vyema tukampa moyo
 
Hongera Zitto ila binafsi naamini mpinzani wa kweli hawezi kupigiwa kura na CCM.
CCM wanajitambua hawana unazi wa vyama,sio kama Chadema walionyesha udhaifu,uchoyo,roho mbaya na ubinafsi katika kuchagua mawaziri vivuli wa kambi ya upinzani.

 
Hongera Zitto umma wa watanzania una imani na utendaji wako.
 
Pamoja na mapungufu aliyo nayo ZZK kama binadamu wengine tulivyo, ial kazi yake kwenye hizi kamati naikubali sana. Naamini Mkullo hatapenda kusikia hizi habari maana ZZK alipiga kazi mpaka jamaa akaonekana kilaza.
Hongera Mh. Zitto
 
  • Thanks
Reactions: SMU
CCM wanajitambua hawana unazi wa vyama,sio kama Chadema walionyesha udhaifu,uchoyo,roho mbaya na ubinafsi katika kuchagua mawaziri vivuli wa kambi ya upinzani.


Mkuu japo hii sio sehemu ya mada ya uzi huu ial unaweza kutafakari japo kwa miguu kama ubongo wako uko likizo, uendeshaji wa CCM na familia ya JK?
 
Ule msemo wa kumpiga chura teke ni sawa na kumwongezea kasi ya safari umetimia kwa Zitto Z. Kabwe huko Bungeni ndani ya Kamati za Bunge.

Alipigwaje teke?

Ikumbukwe kuwa hivi karibuni Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) iliyokuwa ikiongozwa na Zitto Kabwe ilivunjiliwa mbali na kuhamishia majukumu yake kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) ambayo kwa muda mrefu ilikuwa chini ya Mhe. John Momose Cheyo.

Kwa mantiki ya kuvunja POAC na kupeleka majukumu yake kwa PAC, ilitegemewa kuwa Zitto Kabwe sasa hatakuwa na kimbilio la kuwa mwenyekiti wa kamati kwani umaarufu wake ulikuwa katika POAC lakini kwa upande mwingine ilitegemewa kuwa nguvu ya Cheyo itaongezeka zaidi kwani ni yeye atakaye deal na hesabu za Wizara na Mashirika ya umma.

Kilichojitokeza huyu Dogo Zitto "katoroka kambini" JKT, kaingia kwenye Kamati aliyopangiwa kwa mbinu za ki-JKT, kapanga mashambulizi balaa yaliyopelekea kumng'oa Mhe. John Momose Cheyo.

Mwendo wake umeongezekaje?


Sasa Hesabu za Mashirika ya umma zitahojiwa na Kamati yake
Hesabu za Wakala wa Serikali zitahojiwa na Kamati yake
Hesabu za Wizara zote nchini zitahojiwa na Kamati yake

Dogo ana mikakati mizito kama jina lake
 
Shukrani mkuu Ndachuwa; nini kimepungua kutoka POAC hadi PAC...maana niliwasikia Chadema kwenye mkutano wao pale Temeke wakilalamika hili swala, bila shaka na wadau wengi walilipigia kelele...Leo Nashangaa wadau wanaunga mkono bila kuainisha mapungufu walio yapigia kelele mwezi uliopita tu...nimependa mkuu ulivyowasilisha maoni yako maana kwenye serikali za mitaa ndio kwenye uozo.!!

Mapungufu idawa ni kwamba kamati itakuwa inashughulikia mambo yasiyoingiliana kabisa mfano leo wanahesabu za UDSM kesho labda hesabu za Wizara ya Elimu siku ingine hesabu za bandari inayofuata labda wizara ya Afya. Mashirika ya umma kila moja lina sheria yake wakati Wizara ziko kwa mujibu wa Raisi aliye madarakani alivyopenda ziwe
 
Last edited by a moderator:
Mkuu japo hii sio sehemu ya mada ya uzi huu ial unaweza kutafakari japo kwa miguu kama ubongo wako uko likizo, uendeshaji wa CCM na familia ya JK?

Kwa hiyo kwa makusudi umeamua kujitoa fahamu na kuandika utumbo.
 
Mhe Zitto Kabwe ameibuka kidedea kwenye uchaguzi wa kumtafuta mwenyekiti wa kamati ya hesabu za Serikali (PAC) baada ya kumbwaga Mhe. Cheyo kwa kupata kura 13 kati ya 17.

Zitto awali alikuwa ni mwenyekiti wa POAC, kamati iliyovunjwa siku chache zilizopita na kuunganishwa na kamati ya PAC.

Binafsi nampongeza Zitto na kumtakia utendaji mzuri kwenye majukumu yake hayo mapya. Taifa linamtegemea.

awajibike.
 
i was wrong nilidhani zitto wangemmwaga!!cheyo ovyo tu alikuwa anaifichia serikali maovu mengi kwenye ile kamati,kwa hiyo zitto hatii tena mkono kwenye mashirika kama tanesco na pspf?nielewesheni hapa
nyabhingi kama una maelekezo ya POAC ambayo wewe na bodi ya shirika lako hamjafanyia kazi bora ukaanze utekelezaji maana kamati ya PAC sasa inashighulika na hesabu za mashirika ya umma (PSPF/TANESCO yako) na Serikali kuu (Hesabu za Wizara).

Kazi itakuwa rahisi wizara ikisema imepeleka pesa xxxxx tanesco wao wataangalia tu hesabu za Tanesco kama hizo pesa XXXXX zimefika
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom