Elvis Legacy
JF-Expert Member
- Aug 10, 2017
- 4,629
- 7,166
Nimesoma kwa makini tafakari ya Zitto Kabwe (Mb), Nilichogundua ni kwamba vipaumbele vya namna ya kufikisha Taifa la Tanzania kwenye uchumi wa FOUR ASIA TIGERS (Hong Kong, Singapore, Taiwan na South Korea) ita-wezekana tu pale tutakapo kuwa na sera ya nchi na si sera ya CCM, sera ya CHADEMA & CUF. Au mbaya zaidi utashi wa mtu mmoja ambaye maamuzi yake tu ndio yatakuwa mwongozo wa Taifa. Mfano miradi yote mikubwa anayoifanya Raisi ina tija kwa Taifa, ipo miradi ambayo tija itaonekana baadaye sana lakini itaiacha nchi kwenye hali mbaya ya uchumi kwa sasa sababu inatekelezwa kwa kasi kubwa tofauti na ukuaji wa uchumi wa nchi yetu. Lakini kama miradi hiyo ingewekwa kwenye sera ya nchi haikuwa na lazima kuisha ndani ya miaka mitano au kumi. Hivyo kila kiongozi anayeingia madarakani angekuwa na wajibu wa kuendeleza sera za nchi kama nchi kwa kutumia mikakati yake. Hivyo Zito Kabwe(Mb) una mikakati mizuri nadhani ungeishauri serikali ukiwa bungeni. Pia mbunge wa eneo hilo ana deni kwa watanzania maana amekalia mali ghafi ambazo zinaweza kuliokoa taifa, aishauri serikali