Zitto Kabwe: Kama ningepata mamlaka ningefanya tofauti

Zitto Kabwe: Kama ningepata mamlaka ningefanya tofauti

Imekaa vizuri sana hiyo,Tanzania tumejaliwa natural resources za kutosha,inashangaza kwanini tunaendelea kuwa ombaomba.
 
Nilikuelewa sana na ndiyo maana nakuambia kumlinganisha mbunge mtu mmoja tu asiye na dola wala vyanzo vya mapato hata kupanga bajeti ya jimbo lake na serikali dudu kubwa ni kutojitendea haki mwenyewe!!

Well. Hoja yako kutokuwa na taarifa na afanyayo ktk jimbo lake haina maana kwa sababu zifuatazo:

1. Elewa kazi na majukumu ya mbunge. Kubwa kabisa ni kuwa sauti ya kuwasemea wananchi wa jimbo lake (kuwakilisha). Kwa lugha rahisi kabisa mbunge huwa ni "link" kati ya wananchi na serikali


2. Zitto Kabwe mbunge wa Kigoma Mjini ni miongoni mwa wabunge walioifanya kazi hii (ya ku - link wananchi na serikali) kwa umaridadi usio mithirika. Sina hakika kama hili hulioni ama hujawahi kuliona. Na sina hakika wataka uone nini zaidi ya hili!!

3. Amefanya nini jimboni kwake? Hili ni swali awezaye kujiuliza mtu asiye na ufahamu wa kutosha tu dhidi ya kazi na majukumu ya mbunge. Nakushauri, iulize serikali imefanya ni jimboni kwa Zitto Kabwe na Tanzania kwa ujumla...

Ndiyo. Serikali ndiyo yenye dola, inakusanya kodi na kupanga matumizi yake. Kazi ya mbunge ktk hili ni kuomba na kushauri tu na hili wabunge wanafanya sana. Kama huoni, basi hili ni tatizo lako ndugu yangu Kalamu1....

4. Sina hakika kama ni kazi ya mbunge kujenga shule, vituo vya polisi, kuajiri walimu, kujenga barabara, reli, madaraja, kununua madawa na kupeleka mahospitalini nk....

Kama nilivyokuambia hapo awali mbunge anachoweza kufanya ni kuhamasisha wananchi kushiriki ktk shughuli za maendeleo zilizo ndani ya uwezo wao mf. Kilimo ili wapate chakula, kuibua miradi ya maendeleo ambayo mwisho wa siku ni lazima tu wapate support ya serikali ktk kuikamilisha kupitia mfumo wa kibajeti....

Sasa unadhani Zitto Kabwe kama mbunge kama mbunge ktk jimbo lake hafanyi hili kwa kushirikiana madiwani wa eneo lake?

Kukusaidia tu ni kuwa, you don't need any evidence ktk hili.

Ushahidi nambari one ambao ni sharti ukuijie kichwani mara moja kabla ya ku - argue ni huu: YEYE NI MBUNGE na ni mwakilishi wa watu na hata sasa yuko jimboni kwake baada ya kikao kirefu cha bunge la bajeti ya 2018/2019!!

Umeng'ang'ania 'kazi za mbunge-----" na hapo hapo unaeleza 'umenielewa' nilichoeleza! Siwezi kubishana kihivyo.
 
bahati mbaya hauwezi kuwa kiongozi kwa hiyo zitabaki ndoto za mchana ulipokuwa waziri wa fedha kivuli ulishindwa kuandaa bajeti mbadala, ulipokuwa mjumbe wa tume ya madini ulinyamazishwa kwa rushwa na hata madudu yaliyompa umaarufu rais magufulu yalikuwa yanatokea kipindi cha nyuma wakati wewe ukiwa mwenyekiti wa PAC sidhani kama utafanya chochote ikiwa hata demokrasia kwenye chama chako umeiminya na wewe kuwa kiongozi mkuu
 
Mda aliotumia kuandaa hili kwanini asitumie kuandaa desa ni jinsi gani kama mbunge atawasaidie ili wanufaike na zao la chikichi?
Kwa hiyo ndiyo ule uamuzi kuwa mwanasiasa afanye siasa ktk jimbo lake tu unautaka utumike hata kwenye fikra?

Vv
 
Umeng'ang'ania 'kazi za mbunge-----" na hapo hapo unaeleza 'umenielewa' nilichoeleza! Siwezi kubishana kihivyo.

Hatubishani. Ukinitazama mimi na wengine ktk mtazamo huo wa kudhani tunabishana, hutapata mawazo mbadala, hutajifunza kwa wengine.....

Tuvumiliane tu mkubwa. Najua mimi na wewe tuliokwenda shule, tulifundishwa msemo huu..

"........kujua ni kutojua na kutojua ni kujua......"

Tafsiri yake ni kuwa, hakuna ajuaye yote na wala hakuna asiyejua chochote kabisa hata kama hakuona mlango wa darasa la chekechea!!

Nakutakia kila la kheri
 
Ni rahisi sana kusema lakini sio kutenda.

Turudishe mpira kwako Mbunge wa Kigoma mjini: Huko kwako umefanyaje nje ya sera ya serikali kuu?
umenifanya nikumbuke jamaa yangu aliyekuwa anakosoa walioko uwanjani wakisakata kabumbu, alipewa nafasi baadaye ili akarekebishe makosa ila alichofanya alienda kuboronga kuliko aliyetolewa.
 
Nimepitia baadhi ya hoja za wachangiaji na kubaki mdomo wazi.
Kuna tatizo kubwa la uelewa kwa sisi wananchi na pengine wasomi wa kizazi hiki

Kuhusu Zitto amefanya nini jimboni kwake. Tunashindwa kuelewa Mbunge akiwa Dodoma si wa jimbo bali mwakilishi wa wananchi popote walipo.
Ndio msingi wa Bunge kupewa nguvu za kutunga sheria hata kama hazigusi eneo jingine

Mswada wa korosho haumhusu Zitto, lakini kama mbunge wa JMT anawajibika kuona korosho inayotoka Kusini inaleta mchango kwa taifa na unafuu kwa kila mmoja

Hoja za Zitto . Nilitegemea wachangiaji wabomoe hoja kama alivyozileta kwa mantiki. Kinyume chake wana attack personality yake na nafasi ya ubunge.

Alichosema Zitto ,badala ya kutegemea kodi kutekeleza miradi, tunaweza kutumia rasilimali zetu tukijipunguzia mizigo ya kodi na kutengeneza uchumi imara kwa sekta zote

Mfano, Chuma ya Liganga na Ludewa, tunaitumiaje kuendeleza miundo mbinu kama reli? Ujenzi wa reli utafungua milango ya ''industrialization'' na services katika maeneo mengine

Hoja ya Zitto ni kuwa tutumie rasilimali kujiendeleza na kibiashara.
Tukiwa wazalishaji wa chuma, nchi za Afrika mashariki na kati zingekuwa wateja

Tulipojenga kiwanda cha Sarauji Tanga, kiwanda hicho kilitoa saruji ya ndani na tuliweza kuuza Afrika kusini wakati wa kombe la dunia. Tunaweza kufanya mengi tukiwa na mipango

Hatuwezi kufanikiwa bila dira ya taifa. Mipango ya kitaifa ibaki kuwa ya Taifa na sera za vyama zieleze namna ya kufikia matarajio ya mipango ya Kitaifa 'vision'

Kwavile hatuna dira ya Taifa, hatuna sera za mambo kama nishati.
Leo tunaongelea gesi Mtwara, kesho Stigler gorge,siku nyingine makaa ya mawe na kuni

Tujadili hoja za Zitto kwa mantiki, tuzibomoe kwa hoja au tuziunge mkono kwa reasoning

Tusimwangalie Zitto kama mtu bali Raia na Mbunge.

Utamaduni wa kufikiri kazi ya mbunge ni jimboni kwake wakati anakupangia mshahara, anatunga sheria zinazokuathiri nje ya eneo lake ni ubutu mkubwa wa kufikiri

Hivi unawawezaje kufikiri kazi ya Mbunge ni jimboni kwake wakati akiwa Dodoma anakupangia kodi, mshahara na sheria zinazokuathiri nje ya jimbo lake!

Gesi ya Mtwara ina tija Kigoma, Chuma ya Liganga ina tija Kagera, Pamba ya Mwanza inatija Ruvuma. Tusifungie akili zetu katika vibuyu vya upotevu wa fikra

Wale wanaosema ni rahisi kusema kuliko kutenda wana upeo mdogo. Asian Tiger tuliokuwa nao kundi moja wametuacha kwasababu ya uthubutu na vision

Kama Zitto kasema kiurahisi, wanaombeza watuonyeshe ugumu kwa kubomoa hoja zake
 
Mwami Zitto,naubaliana na wewe ila pia naungana na mkuu Nguruvi3 kuwa hapo uliposema "ningekuwa" ndipo panapo liharibu Taifa hili.
Naamini tatizo la msingi sana ni kuwa kiongozi mkuu wa TZ anakuwa amepewa majukumu mazito,makubwa na mengi zaidi ya kibinadamu. Yaani yeye ndiye anayetegemewa na kila Mtanzania na kila linalomtokea Mtanzania.
Dhana hii ndiyo inayopelekea muuza "mteke" wa pale soko la Mwandiga akihojiwa na mwandishi wa habari kuhusiana na ushuru wa soko kupanda,aombe mh. rais aliangalie suala hilo.
Hii pia ni sawa na mwanafunzi wa mwaka wa pili wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kumlalamikia rais kuwa mabafu ya mabweni ya wanafunzi hayana milango hivyo anamuomba mh. rais awasaidie kwani hapo bwenini kuna mchanganyiko wa rika mbali mbali.
Ili kufanikiwa kama taifa,hii dhana inabidi tuhakikishe inafutika vichwani mwetu. Naweza sema kwetu inawea ikawa ngumu kuifuta,lakini jambo la msingi zaidi ni kuhakikisha vizazi vyetu vinaweza kufikiri njia za kutatua tatizo na si kufikiri kitatizo tatizo kuhusu tatizo.
Msingi mkubwa ni elimu iliyo bora inayomfunza mwanafunzi kujiamini na kuwa anaweza kukabiliana na changamoto yoyote ile,na kwamba UMOJA ni NGUVU.
Kumalizia,napenda kama kungekuwa na mijadala mipana ya kitaifa kuhusu changamoto mbalimbali za taifa letu,kama huu uliouanzisha,naamini mijadala hii ingeibua suluhisho bora za changamoto nyingi inazolikabili taifa na zingeweza kutatuliwa vyema.
 
Wewe ulikuwa CCM na ulihama na baba yako Lowassa tuambie ulipokuwa CCM ulifanya cha maana kipi na sasa uliko umefanya kitu gani cha kukumbukwa? Au kwa kuwa umebanwa kwenye ufisadi wako ndiyo maana una bwabwaja tu!! Mtapata taabu sana awamu hii...!!
Wewe ni mzushi na muongo mkubwa.Lini nimewahi kuwa shabiki wa CCM? Tangu nimepata akili na kuanza kufuatilia siasa za nchi hii huwa nashangaa sana kuona mtu anajitambulisha kuwa ni mfuasi wa CCM chama ambacho viongozi wake wengi kwa miaka mingi wanatuhumiwa kwa kashifa karibu kila siku alafu leo eti leo mimi niwe mpenzi wa CCM.

CCM ndio imetufikisha hapa tulipo leo hii alafu eti niiunge mkono CCM kisa kuna mtu anunua ndege na kujenga fly over!! Never ever!
.
Leo hii badala ya kutumia hizi fedha kufufua ATCL, fedha hizo zilistahili kufanya shughuli nyingine na kibaya walioua shirika hatuoni wakichukuliwa hatua yoyote zaidi ya kila siku kuona wapinzani ndio wanandamwa na kesi za ajabu ajabu.

Kwa hayo na mengine mengi ya siku za nyuma, kamwe sijawahi na wala sitawahi kuwa mshabiki wa CCM.
 
Zitto vipi zile "terrible teens" ulizozivalia njuga?
No! Mjadala wa terrible teens ni tofauti na huu. Please tungefarijika kama ungemjibu hoja zinazohusiana na alichosema

Zitto anasema tujijengee uwezo wa matumizi ya rasilimali kama Chuma ili kupata uwezo wa kutekeleza miradi mingine ya miundo mbinu.
Hili litatusaidia kukwepa mikopo, kuwekeza pesa nchini na kujitanua kibiashara.

Hoja zako ni zipi kuhusu hayo?
 
Zitto my brodah!!!

Haya unayoyasema ni mambo mazuri sana ambayo yanaonyesha kuwa umefanya tafiti ya kina kwa kiwango chako.
Nije kwenye hoja ya msingi, hivi je kimewh kuwa na national priority kwenye serikal hii ya CCM zaid ya wakati ule wa uongozi wa mwalim?

Kipindi nakua nilikuwa najua vipaumbele vya taifa ilikuwa ni kuondoa ujinga umaskin na maradhi. Kila mtu alibeba vipaumbele hivi na kuvivaa shingoni. Bibi afya alikuwa anapata majumban kukagua usafi hadi wa nyumban na chooni, bwana shamba alikuwa anashinda shambani kutuelekeeza hata jinsi ya kuchuma kahawa. Madarasa ya elimu ya watu wazima tuliyashuhudia vipindi vya region kuelimisha umma kuhusu vipaumbele hivi vilikuwa vingi na vya Kila wiki.

Baada ya mwl haya yalidumu kwa muda mfupi tuu yakatoweka.

Kwasasa nimekuwa nikishuhudia aina ya viongozi ambao wanakuja na ndoto zao wanamaliza muda wao ndoto hazijatimia.

Kasheshe ni kwa serikal hii ya awamu ya tano, yaan imebidi overspend kwa k7fanya investment kwenye more of luxurious goods kuliko kwenye production. Viwanda vinavyopigiwa kelele ni vya cherehani na ususi wa nywele vikienda mbali sana ni vya maji. Ndio ww unakuja kuongelea swala la makaa ya mawe na chuma???

Kwa kipaumbele gani tulicho nacho?

Ni uzalishaji, ukuzaji mtaji wa kitaifa, elimu, afya ama ni ubabe??
Zitto huwa nakubaliana nae sana lakini kwahili hapana tunahitaji reli kwa haraka yeye anasema tuanze na kujenga viwanda vyachuma nisawa na umefikiwa na magonjwa ya kipindupindu alafu dawa ipo kwa jirani unasema mgonjwa asipewe mpaka nitengeneze dawa yakwangu Leo tunanunua chuma kesho tutatengeneza chakwetu tutauzia wengine ndio biashara nakumbuka mzee mwinyi aliwahi kusema biashara nikununuliana nakuuziana uchumi haujengwi kwa wivu naninunue kwake tunahitaji reli haraka tuondoe mizunguko
 
Zitto huwa nakubaliana nae sana lakini kwahili hapana tunahitaji reli kwa haraka yeye anasema tuanze na kujenga viwanda vyachuma nisawa na umefikiwa na magonjwa ya kipindupindu alafu dawa ipo kwa jirani unasema mgonjwa asipewe mpaka nitengeneze dawa yakwangu Leo tunanunua chuma kesho tutatengeneza chakwetu tutauzia wengine ndio biashara nakumbuka mzee mwinyi aliwahi kusema biashara nikununuliana nakuuziana uchumi haujengwi kwa wivu naninunue kwake tunahitaji reli haraka tuondoe mizunguko
Hapana, Zitto anahoja tatizo hujamsoma vizuri

1. Hatuhitaji reli haraka. Nasema hivi kwasababu iliyokuwepo imeota majani. Tumeng'oa mataruma, hatuna injini na tuliuza kwa Wahindi. Leo tunahitaji uharaka upi?

2. Zitto anasema miaka 2 ilikuwa ya kujenga uwezo wa kujenga reli kwa rasilimali zetu
Hapa ana maana tatu. (1) Chuma ya liganga ingekuwa uwekezaji katika ajira na biashara
2) Katika miaka 2 tungejenga reli kwa uwezo tu, si kukopa na kulipa riba miaka 10
3) Chuma-Liganga na Ludewa ingetumika kibiashara kutujengea uwezo wa mambo mengine

3. Uchumi unajengwa kwa wivu. Asian tiger walikuwa na wivu wa kuwa katika dunia ya kwanza. Wivu umewafikisha walipotaka.

4. Biashara ni kununuliana na si kununua. Sisi tunanunua chuma, tulipaswa kuuza chuma ili tununue injini za treni.
 
Swali langu kwako ni moja tu,wawekezaji wengi,huagiza bidhaa nyingi kutoka kwao hata zile zinazopatikana hapa nyumbani,
Je nini itatuhakikishia kwamba tukizalisha hicho chuma,watakinunua na kukitumia,Vila kuwepo story za maembe yenu sio bora,tutachukua southafrica
 
["1000 digits, post: 27676781, member:Kumbuka kuwa Kwa wenzetu walioendelea kuna Sera ya Taifa ambayo inajengwa na wataalam.Kwetu Sera inatengenezwa na wanasiasa wa chama kimoja.
Hapa kuna tatizo kweli kwa wananchi wetu na nina shaka Wabunge wetu kama wanaelewa tofauti ya Dira au Sera za Kitaifa na Sera za vyama

Hili si jambo geni , huko nyuma wakati wa chama kimoja lilifanyika.
Kulikuwa na sera ya 'kilimo' ikieleza ndio uti wa mgongo wa taifa.

Katika ku define sera hiyo, kulianzishwa viwanda vya mbolea, zana za kilimo , kusisitiza kilimo cha kisasa, viwanda vya kubangua, kuchambua na kusindika mazao n.k.

Katika zama za vyama vingi sera za taifa ni dira ya kutueleza sisi kama taifa tunakwenda wapi
Kwa mfano, sera ya nishati inatakiwa itueleze katika muda gani tutaweza kujitosheleza na kutumia nishati hiyo katika kupanua maendeleo ya taifa

Sera za vyama zinatakiwa zi-define njia za kufikia lengo hilo.
Zitto anasema ACT wangetumia makaa ya mawe kuzalisha nishati ya umeme inayohitajika kuyeyeusha chuma itakayotuwezesha kujenga reli katika kuimarisha miundo mbinu na kujenga wigo wa biashara ya chuma, makaa, na madini yanayotokana nayo.
ni sera ya ACT iki define dira ya taifa

CCM wanasema, tuanze na gesi ya Mtwara kwanza ili kutosheleza matumizi ya ndani na kupata nishati ya umeme ya uhakika. Katika hali inayotatanisha, sera hiyo ya CCM imetoweka ghafla na sasa kuna sera ya stigler gorge

Vivyohivyo kwa Chadema na CUF wanaweza kuwa na sera zao za nishati,lengo likiwa kufikia dira ya taifa ya kuwa na nishati ya kutosha

Ikifika hapo ndipo vyama vinapita kuuza sera zao kwa wananchi.

Kwa vile hatuna dira ya kitaifa, kinachoonekana ni dira ya CCM kuwa ya kitaifa

Dira ya CCM vyovyote iwavyo ni lazima ieleze dira ya Taifa. Swali, lini tumekaa tukaweka dira ya taifa ya nishati? Kwavile hatuna dira ya taifa kilichopo tunadhani ni dira ya Taifa, si kweli!

Kwavile hatuna dira ya Kitaifa, kila anayeingia anakuja na sera yake au ya chama chake
Elimu kwanza , kilimo kwanza, viwanda kwanza n.k.

Kwa sehemu fulani sera hizo za CCM zina uhalali. Utahoji vipi ikiwa hujui unakwenda wapi?

Mfano, kama tungekuwa na sera ya kitaifa ya 'agricultural revolution' ingekuwa rahisi kuhoji, jamani hii ya elimu kwanza na kilimo kwanza inatoka wapi? Hatuna, lazima tukubaliane na kilichopo
 
Hili suala la Dira ya taifa ninalirudia kwa umuhimu wake hapa jamvini unajionyesha wazi.

Wachangiaji baadhi wanasema Zitto anasema kwasababu ni rahisi kusema kuliko kutenda. Wanasema hivyo kwasababu hawana majibu ya alichosema.

Hawajui sera ya taifa ya nishati na matumizi ya rasilimali zetu, wanadhani sera za CCM ndiyo dira ya taifa

Wengine wanasema Zitto amefanya nini jimboni kwake. Well, tuseme hajafanya lolote kwasababu uwezo wa kutenda hana.

Katika makala yake ameongelea kodi na kama tunavyojua hata zile za serikali za mitaa sasa zimehamishwa. Je, tutegemee miujiza gani kwake?

Kwa kutambua hilo anashauri njia za kupata mapato si jimboni kwake bali kama nchi ili tutende makubwa zaidi. Hilo ni jambo kubwa kuliko mnalotaka afanye jimboni

Je, mjadala wa Chuma na makaa ya mawe si jambo lenye afya?

Nikikubaliana au kutokubaliana na hoja za Zitto nitashambulia hoja na si yeye

Kwa makala yake naona imesimama wima! haina majibu mbadala jamvini

Zitto endelea kuamsha mijadala kama hii, unasaidia taifa hata wanaokubeza wanajua hilo
 
Ungefanyaje mkuu,maana PAC siku hizi haisikiki kabisa kama kipindi alichokuwepo Zitto mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
Kutwa alikuwa akiuza sura vyombo vya habari wenzie ripoti wakitoa wanaipeleka bungeni ambako ndiko unatakiwa kupelekwa sio media kama zitto alivyokuwa akifanya
 
Back
Top Bottom