logician mkuu
JF-Expert Member
- Jun 2, 2014
- 792
- 221
Kwanza si kweli kuwa nguvu ya Zitto ndio iliyojenga chama. Si kweli hata kidogo. Zitto amejengwa na chama na kufanywa maarufu na chama, kisha kiburi cha sifa kimemwingia.
Pili, inadhihirisha dhana ya usaliti. Zitto akiwa ndani ya CHADEMA, alipaswa kuainisha changamoto za chama na kujaribu kuzitatua katika timu iliyopo, na si kudhani kuwa AKILI YAKE ndio itajenga chama. Hii imedhihirika sasa. Baada ya yeye na vibaraka wenzake kama Juliana Shonza kuondoka CHADEMA, chama kimekuwa imara zaidi. Chama kimekuwa hakina migogoro kabisa. Chama kimejengeka zaidi na watu wana imani zaidi na chama.
Tatu, kama kweli uongozi wa Zitto ndicho kilichokuwa kinahitajika kukuza chama, Zitto ana nafasi katika chama chake kipya cha ACT-Tanzania. Zitto atoke CHADEMA, tuone kama ACT-Tanzania itakua kama anavyoota.
Nne, wewe kama mwana CCM ambaye una hakika kuwa Zitto ni hazina, kwa nini haushauri viongozi wa chama chako wamchukue Zitto na kumfanya kiongozi ndani ya CCM ili mumkomboe Mtanzania kwa kubadili fikra za kifisadi na za ulevi wa madaraka zilizo CCM na zenye madhara makubwa kwetu sisi kwa kuwa ndio wanaogawa rasilimali za Taifa?
Tano, unathibitisha kuwa kazi ya Zitto ndani ya CHADEMA ilikuwa kutengeneza makundi ya kumjenga yeye mwenyewe. "I have a fear of being ruled by a lesser" hii ni kauli isiyokilenga chama, ni ya kibinafsi. Ni mtu anayetafuta yeye madaraka, tena asiye na subira. Bora chama kivurugike kwa sababu ni yeye tu anayedhani anaweza. Kauli hii inadhihirisha kuwa mtu huyu anajitafuta mwenyewe.
Sita, kama ulidhani umeandika uzi huu kumjenga Zitto, hakika unazidi kumchafua.
Mwisho, jifunze kiingereza. I didn't find him, he finds me hii inadhihirisha kuwa bado unahitaji kujifunza si kiingereza tu, na mengine mengi...
Pili, inadhihirisha dhana ya usaliti. Zitto akiwa ndani ya CHADEMA, alipaswa kuainisha changamoto za chama na kujaribu kuzitatua katika timu iliyopo, na si kudhani kuwa AKILI YAKE ndio itajenga chama. Hii imedhihirika sasa. Baada ya yeye na vibaraka wenzake kama Juliana Shonza kuondoka CHADEMA, chama kimekuwa imara zaidi. Chama kimekuwa hakina migogoro kabisa. Chama kimejengeka zaidi na watu wana imani zaidi na chama.
Tatu, kama kweli uongozi wa Zitto ndicho kilichokuwa kinahitajika kukuza chama, Zitto ana nafasi katika chama chake kipya cha ACT-Tanzania. Zitto atoke CHADEMA, tuone kama ACT-Tanzania itakua kama anavyoota.
Nne, wewe kama mwana CCM ambaye una hakika kuwa Zitto ni hazina, kwa nini haushauri viongozi wa chama chako wamchukue Zitto na kumfanya kiongozi ndani ya CCM ili mumkomboe Mtanzania kwa kubadili fikra za kifisadi na za ulevi wa madaraka zilizo CCM na zenye madhara makubwa kwetu sisi kwa kuwa ndio wanaogawa rasilimali za Taifa?
Tano, unathibitisha kuwa kazi ya Zitto ndani ya CHADEMA ilikuwa kutengeneza makundi ya kumjenga yeye mwenyewe. "I have a fear of being ruled by a lesser" hii ni kauli isiyokilenga chama, ni ya kibinafsi. Ni mtu anayetafuta yeye madaraka, tena asiye na subira. Bora chama kivurugike kwa sababu ni yeye tu anayedhani anaweza. Kauli hii inadhihirisha kuwa mtu huyu anajitafuta mwenyewe.
Sita, kama ulidhani umeandika uzi huu kumjenga Zitto, hakika unazidi kumchafua.
Mwisho, jifunze kiingereza. I didn't find him, he finds me hii inadhihirisha kuwa bado unahitaji kujifunza si kiingereza tu, na mengine mengi...