Zitto chupuchupu kutimuliwa CHADEMA!

Zitto chupuchupu kutimuliwa CHADEMA!

CHONDE CHONDE!!!!!! HALA HALA CHDM!!!!!!!!!!! ZZK ni nguzo ya chadema. asiguswe!
 
Kwa nini MBOWE hakutoa fursa kwa ZITTO kujitetea kuhusu kashfa hizo???? alikuwa anamlinda ZITTO au Chama?
wengemtimua tu. kwani akina machange, juliana shonza, mwampamba na wengineo walipewa nafasi kujitetea? kwanini chadema inakuwa bias hivi kwa wanachama wa chama hichohicho? kama ni kiongozi bwana hata shonza alikuwa kiongozi na hakupewa nafasi ya kujitetea?
 
Zitto mwenyewe alipotafutwa kuzungumzia suala hilo alijibu kwa kifupi, “I have no comment” akimaanisha kwamba hakuwa na cha kusema kabla ya kukata simu.

Kauli kama hii inakuza mjadala., haipo kibusara sana..

John Mnyika ambaye hata baada ya kupigiwa simu kwa zaidi ya mara moja, hakuwa tayari kueleza lolote.

“Pengine katika hayo uliyouliza, miye binafsi sina majibu nashauri ungewasiliana na huyo aliyekupatia taarifa hizo kwa ajili ya kukupa maelezo sahihi,” alieleza Mnyika.

Kauli hii inaonyesha kukomaa kisiasa na hekima
 
ikifika december bado Zitto Kabwe hajafukuzwa ndani ya CHADEMA ntarudisha kadi yangu kwa hiari...nikiwa kama mwanachama wa kawaida sana, nasikitiswa sana na jinsi kijana huyu anavyohujumu mipango na mikakati ya chama, zito ni mbinafsi, msiri, mchochezi, mpika majungu na M-CCM pia...anamatukio ya ajabu ajabu sana..SHAME ON ZITTO ZUBERI KABWE.
December mbali rudisha leo! kwani! una mchango gani ndani ya chama? chama hakiwezi kukurupuka kumfukuza Zitto au mwingine yoyote kabla ya taratibu kufuatwa kwa mujibu wa katiba! rudisha kadi hata leo!
 
ikifika december bado Zitto Kabwe hajafukuzwa ndani ya CHADEMA ntarudisha kadi yangu kwa hiari...nikiwa kama mwanachama wa kawaida sana, nasikitiswa sana na jinsi kijana huyu anavyohujumu mipango na mikakati ya chama, zito ni mbinafsi, msiri, mchochezi, mpika majungu na M-CCM pia...anamatukio ya ajabu ajabu sana..SHAME ON ZITTO ZUBERI KABWE.

Ninakushauri usisubiri december ondoka sasa kama kweli wewe ni mwanachama.
Cdm siyo cuf mlioisambaratsha kwa mbinu zenu za zilipendwa.
Tunaenda kuchukua dola ktk uchaguzi ujao na watu kama wewe hamna nafasi kwenye Taifa letu. Shame to you ' kibaraka'
 
.....Duniani kuna watu wasiojitambua ...... wako ambao wanajua lakini hawajui kwamba wanajua...... na wako ambao hawajui lakini wanajiona wanajua.. na wapo ambao hawajui na hawajui kwamba hawajui.. take care... unapojiona wewe ni super bila nidhamu ujue ni bure...Hata Messi pamoja na u - star wake lakini kwake nidhamu ni kitu kikubwa na muhimu sana
 
Haya mambo ya kufukuzana uanachama tafadhari waachieni magamba na ndio mwanzo wa kujenga matabaka,mwanachama anaondoka mwenyewe kwa kushindwa kulipa ada,lakini hizi hoja za usaliti ni upuuzi mtupu,hoja zote zinajadiliwa na kupigiwa kura sasa usaliti umetoka wapi?
 
Kikao kilikwisha salama na tukiwa wamoja. Hata siye ambao hatukuwepo tumepata amani na imani kubwa na chama chetu
 
Hizi hoja za zito kutaka kutimuliwa zinatokea kwenye vyanzo ambavyo vina upande!!!!!!!!!!! ndio wale wale wanaotaka kuchonganisha watu ndani ya CDM ili chama Kianguke. hamtaweza
 
chamsingi mie ninacho ona zitto kabwe kuandamwa kwake kuna sababu maalum nyuma ya pazia hii kitu sio bure kutajua kuna watu either ndani au nje ya chma wanao dhamini mpambano na zitto anaonekana kua mwiba sababu ni mtu asie pelekwapelekwa tuu na kiongozi au chama chochote na hii ndio inamfanya aonekane kama kutofautiana kimtizamo na wengine BIG UP ZITTO KEEP GOING......
 
Ni makosa kuwazuia wanahabari wasiwepo ndio maana wanaweza kuandika namna hii. Hakukuwa na sababu ya msingi ya kuzuia waandishi wa habari kushuhudia ufanyaji kazi wa demokrasia...

MM

Kikao cha juzi cha Baraza Kuu kilikuwa ni kikao cha ndani. Waliruhusiwa kuwepo wakati wa uzinduzi. Kuruhusu wanahabri kuendelea kuwepo wakati kikao cha ndani kinaendelea ni sawa na kuanika mikakati yote ya CHADEMA.

CHADEMA huwa kina kawaida ya kuwaalika waandishi wa habari kushuhudia proceedings zote za mkutano mkuu wa chama, mwanzo hadi mwisho.
 
December mbali rudisha leo! kwani! una mchango gani ndani ya chama? chama hakiwezi kukurupuka kumfukuza Zitto au mwingine yoyote kabla ya taratibu kufuatwa kwa mujibu wa katiba! rudisha kadi hata leo!

ACHA UVIVU WA KUFIKIRI MKUU OSOKONI..we unajua zito kaanza chokochoko lini??? au umejiunga chadema jana?? ulikuepo wakati ule zito na kafulila walipokua wanaleta mipasuo chadema?? wakati wa zito na chacha wangwe??wakati zito anabaki ndani ya bunge wakati chama kiliamua wabunge wote wa chadema watoke??wakati tunampigia kampeni nasari, yeye zito anatoa waraka kua atagombea uraisi tena akiwa kigoma na kuanzisha mijadala mingine??wakati zito akifanya vikao vya siri na mkuu wa usalama wa taifa?? few to mention..Ulikuepo wewe?? wakati zito akimtumia kikwete sms ya kinafiki?? Usipende ushabiki mkuu toa hoja kwa nini unamtetea zito...KIMSINGI WANACHAMA WENGI HATUMUAMINI TENA, ukibisha mpitisheni basi agombee uraisi kama atapata ata 10% ya kura.....
 
chamsingi mie ninacho ona zitto kabwe kuandamwa kwake kuna sababu maalum nyuma ya pazia hii kitu sio bure kutajua kuna watu either ndani au nje ya chma wanao dhamini mpambano na zitto anaonekana kua mwiba sababu ni mtu asie pelekwapelekwa tuu na kiongozi au chama chochote na hii ndio inamfanya aonekane kama kutofautiana kimtizamo na wengine BIG UP ZITTO KEEP GOING......
Zitto ni Mwiba hongera zake basi lakini kuna majina kibao ndani ya chadema kwa sasa mpaka mawazo analiza watu
 
Nilimpenda na bado nampenda saaaaana ZITO ZUBERI KABWE! tatizo ni kwamba nashindwa kuelewa haya mambo ya kuvuruga chadema ni kweli ZITO anashiriki au anasingiziwa??? Maana ZITO ni mmoja Wa wanasiasa walioitoa mbali chadema!sasa anawezaje kuvuruga juhudi alizozianzisha? Anyway probably it's true labda kwakua anaona hajapewa nafasi kubwa ndani ya chadema!! Au labda anaona nafasi aliyonayo haimtoshi au pengine amesharubuniwa na ccm maana hakuna lisilowezekana chini ya jua! Binafsi naona ZITO angekuwa na umaarufu mkubwa zaidi Kama asingekua na haya makashafa yanayotia aibu ya kuvuruga Chama!
 
CDM inatakiwa ilichukue suala la mh ZZK kwa busara na tahadhari kubwa.......inawezekana kweli anatumiwa na wapinzani wa CDM katika kukidhoofisha chama.....inawezekana kweli hii inatokana na majungu majungu na fitna za wapinzani wake ndani ya CDM.......inawezekana pia ni njama za wapinzani wa CDM inawatumia baadhi ya wanachama (sio mh ZZK) katika kutaka kuleta mtafaruku/udhoofu ndani ya chama.Yote yanawezekana. Lakini CDM kama chama (Viongozi wake) nao wanatakiwa walinde uhai wa chama. Kwa chama kama CDM kinachotajwa kukithiri kwa ubaguzi wa kidini na kikabila hasa katika ngazi za kitaifa mh ZZK amekuwa ndiyo nguzo kubwa ya kukikinga chama dhidi ya kutajwa huko (kwa mtizamo wangu). Vijana wengi ukiondoa kutoka kaskazini wamekuwa wakimuangalia Mh ZZK kama mfano wa kujipigia wao. Sasa kwa hayo machache kama huyu Mh atafukuzwa chamani ni dhahir kuwa CDM itapata vidonda vikubwa sana na si ajabu ikajishushia muonekano wake kwa wananchi hasa wapiga kura kwani yale ambayo chama kinatuhumiwa yatajidhihirisha wazi.......mfano rahisi ni CUF jinsi ilivyopotea kwenye ramani ya kisiasa.....ni mawazo yangu tu jamani
 
Back
Top Bottom