Mkuu Mungi,hivi kiongozi ni mwenye kundi Chadema ni Zitto peke yake?
chama makini ni kile kinachowachukulia watu hatua bila kujali wadhifa, rangi au tabaka, na CHADEMA imekua makini katika kutekeleza hayo ispokua tu inapofika kwa Zitto. Je ni kweli kuwa hufahamu ni jinsi gani Zitto amekua akifanya mambo yake kinyume kabisa na misingi ya chama. Sasa kama chama kikianza kuwa na matabaka hasa katika kuchukua maamuzi hatutakua tofauti na CCM waliowafunga kima Farijala Hussein na kuwaacha KAGODA, au wanaposhinwa kuwashughulikia magamba aka mapacha watatu. Huoni kuwa misingi ya chama hapo itaanza kuwa ya kiupendeleo? hasa pale viongozi wa chini wanapowajibiswa kwa adhabu kali kali ikiwemo kufukuzwa uanachama, lakini huyu bwana haguswi? yeye ni nani?
kwa misingi hii ntarudisha kadi
chadema hawana uwezo wa kumuondosha Zitto, Zitto ndiye pekee aliyeipaisha chadema, nani alikuwa anaijuwa chadema kabla ya Zitto? labda kwa kina Mbowe na wakweze tu.
Ni makosa kuwazuia wanahabari wasiwepo ndio maana wanaweza kuandika namna hii. Hakukuwa na sababu ya msingi ya kuzuia waandishi wa habari kushuhudia ufanyaji kazi wa demokrasia...
Ni haki yako kurudisha kadi kama kusudio lako ni kupata raha na amani katika moyo wako. Hivi unadhani kipi chenye thamani ndani ya CDM kati ya kadi yako na ZZK??ikifika december bado Zitto Kabwe hajafukuzwa ndani ya CHADEMA ntarudisha kadi yangu kwa hiari...nikiwa kama mwanachama wa kawaida sana, nasikitiswa sana na jinsi kijana huyu anavyohujumu mipango na mikakati ya chama, zito ni mbinafsi, msiri, mchochezi, mpika majungu na M-CCM pia...anamatukio ya ajabu ajabu sana..SHAME ON ZITTO ZUBERI KABWE.
Chadema hawana uwezi wa kumtimua Zitto ilo wanalijua wajaribu waone.
Hapo kwenye red nimecheka mpaka basiWewe mwanakijiji na wewe umezidi kujifanya mjuaji DEMOKRASIA pia ina mipaka yake yani watu wanapanga mipango yao na mikakati lazima waandishi wawepo kwani si watapewa taarifa na mikutano ya hadhara si ipo sikuungi mkono ata kidogo tatizo unaishi kwa kanuni za darasani sana.
Huu ni ukweli ambao unawauma Chadema, madai yanaletwa kila kukicha juu ya usaliti wa Zitto, hapa wapo kumtetea Mbowe hii habari siyo ya kweli na ni mtu wa kutochukua maamuzi ya pupa. Wamesahau wiki chache zilizo pita walidai kuwa Zitto ni msaliti na atavuliwa uongozi sababu ni msaliti. Inakuwa kama vile hawajitambui katika hoja zao linapokuja suala la Zitto. Mie nina hamu afukuzwe nione nguvu ya Chadema katika maamuzi iko kiwango kipi. Na asipofukuzwa ina maana hata habari na ushahidi ulioletwa na Ben Saanane wote ni magumashi siyo kweli na kuwa alikuwa anatafuta cheap popularity!
Ni haki yako kurudisha kadi kama kusudio lako ni kupata raha na amani katika moyo wako. Hivi unadhani kipi chenye thamani ndani ya CDM kati ya kadi yako na ZZK??
Mzee Mwanakijiji kama una mji wako najua huwa unawakaribisha wageni sebuleni, sidhani kama huwa unawakaribisha kwenye Bedroom yako! Vikao vya ndani ya chama si kwa ajili ya kila mtu! Ndo maana vyama vina watu wanaohusika na uhabarishaji wa shughuli za vikao vya ndani, chadema yuko John Mnyika na CCM yupo Nape Nnauye. Huu utaratibu uko dunia nzima kwenye taasisi kubwa!Wewe mwanakijiji na wewe umezidi kujifanya mjuaji DEMOKRASIA pia ina mipaka yake yani watu wanapanga mipango yao na mikakati lazima waandishi wawepo kwani si watapewa taarifa na mikutano ya hadhara si ipo sikuungi mkono ata kidogo tatizo unaishi kwa kanuni za darasani sana.
Zitto ni zaidi ya superstar cdm,hakuna anayemuweza kwa kujenga na kusimamia hoja
Songoka jipime kwanza wewe na Zitto umuhimu wenu ndani ya Chadema.