Zitto chupuchupu kutimuliwa CHADEMA!

Zitto chupuchupu kutimuliwa CHADEMA!

Wajumbe wa kikao cha Baraza Kuu waliokuwepo juzi Jumatatu Diamond Jubilee, wakisoma hii habari watashangaa sana na kuhoji umakini wetu wanahabari...

hivi kweli Mbowe kakosa ujasiri wa kuruhusu Zitto ajibu tuhuma zake? Inaonekana Zitto angepewa Fursa kuna watu wangebaki Mbupu nnje!
 
Wajumbe wa kikao cha Baraza Kuu waliokuwepo juzi Jumatatu Diamond Jubilee, wakisoma hii habari watashangaa sana na kuhoji umakini wetu wanahabari...
Ni makosa kuwazuia wanahabari wasiwepo ndio maana wanaweza kuandika namna hii. Hakukuwa na sababu ya msingi ya kuzuia waandishi wa habari kushuhudia ufanyaji kazi wa demokrasia...
 
Ndo maamuz magumu mlokuwa mnasema chadema wanayafanya,je hamjastuka sasa hamna demokrasia na kwamba mliwaonea kina shonza? Halafu msije mkalalamika mkinyimwa habari na taasis za umma mana meelewa kuna tarifa nyeti hazitolewi nje so msiwe mnachonga mkiambiwa no comment na maafisa habari wa serikali japo wanatumia kodi za umma kama walivyo chadema.
 
Wajumbe wa kikao cha Baraza Kuu waliokuwepo juzi Jumatatu Diamond Jubilee, wakisoma hii habari watashangaa sana na kuhoji umakini wetu wanahabari...

ZITTO na MNYIKA walipoulizwa hawakukanusha au kukubali huoni kwamba habari ya Mtanzania inapata nguvu
 
Mere spin , ona anasema walichangia wajumbe tisa, 3 wakasema Zitto na Shibuda washughulikiwe, 2 wakasema hapana, hapo jumla ni 5 hao wanne walisema nini?

Ni ujinga kuendelea kuamini stori zuilizoandikwa na Charles Mulinda .........mkakati huu ni wa kijinga sana ......
 
Wewe rudisha kadi tu kwani Zitto ndo alikuleta chadema.Gamba wewe.
chama makini ni kile kinachowachukulia watu hatua bila kujali wadhifa,rangi au tabaka, na chadema imekua makini katika kutekeleza hayo ispokua tu inapofika kwa Zito. Je ni kweli kuwa hufahamu ni jinsi gani zito amekua akifanya mambo yake kinyume kabisa na misingi ya chama. Sasa kama chama kikianza kuwa na matabaka hasa katika kuchukua maamuzi hatutakua tofauti na CCM waliowafunga kima falijala hussein na kuwaacha kagoda, au wanaposhinwa kuwashughulikia magamba aka mapacha watatu. Huoni kuwa misingi ya chama hapo itaanza kuwa ya kiupendeleo? hasa pale viongozi wa chini wanapowajibiswa kwa adhabu kali kali ikiwemo kufukuzwa uana chama, lakini huyu bwana haguswi? yeye ni nani?

kwa misingi hii ntarudisha kadi
 
Muda wa kumsakama ZZK umekwisha, sasa ni muda wa kila mwanaChadema kufanya kazi kwa nguvu akili na umahiri mkubwa. Kila mmoja atapimwa kwa uwajibikaji sio majungu.

Wanachadema waacheni Magamba wanapenda sana kushabikia fujo mitaa ya wenzao wakufukuzwa wameshafukuzwa kitabu kimefungwa mchaka mchaka mpaka ikulu.
 
Ahahahahah..jamaa wameogopa panya wao watakufa.Siku nyengine mkiwa na migogoro yenu imalizeni huko huko kwenye vikao vyenu sio mje mitandaoni pye pye nyingi baadaye mambo yanawashinda mnaanza kulia magamba yalitaka kutuchonganisha.Pambaf
 
Wewe rudisha kadi tu kwani Zitto ndo alikuleta chadema.Gamba wewe.

wewe ni wale tunao waita MASHABIKI WA CHAMA..kama unaupenda uhai wa chama ungukua unafahamu uhai wa chama unbaimarishwa nanini??
 
chadema hawana uwezo wa kumuondosha Zitto, Zitto ndiye pekee aliyeipaisha chadema, nani alikuwa anaijuwa chadema kabla ya Zitto? labda kwa kina Mbowe na wakweze tu.
 
chadema hawana uwezo wa kumuondosha Zitto, Zitto ndiye pekee aliyeipaisha chadema, nani alikuwa anaijuwa chadema kabla ya Zitto? labda kwa kina Mbowe na wakweze tu.

Na wewe ni ule mtambo anaolalamikia Kinana kuwa ...Makada wengi ni mitambo ya kupika majungu?........
 
Mwandishi huyu kajanjaau. Hebu soma hiki kipande hapa
'Wapasha habari wetu walieleza kuwa hatua ya Mbowe kuruhusu hoja hiyo kuibuka ilisababisha Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe aliyekuwa akiongoza kikao hicho alazimike kuzima kuendelea kwake baada ya mkutano kukumbwa na tafrani.'
sasa aliruhusu au alizima hiyo hoja
 
ikifika december bado Zitto Kabwe hajafukuzwa ndani ya CHADEMA ntarudisha kadi yangu kwa hiari...nikiwa kama mwanachama wa kawaida sana, nasikitiswa sana na jinsi kijana huyu anavyohujumu mipango na mikakati ya chama, zito ni mbinafsi, msiri, mchochezi, mpika majungu na M-CCM pia...anamatukio ya ajabu ajabu sana..SHAME ON ZITTO ZUBERI KABWE.

rikodi ya zitto na heshima yake iko juu sana
 
THERE WERE NO SIGNS OF YOUR ALLEGATIONS...I WAS THERE MR INFORMER!

What are you doing, Putting the blame of the news on me? Mara zimekuwa allegations zangu? Usisome heading tu mkuu soma habari yote hadi sosi. Mjumbe hauwawi!
 
Ni makosa kuwazuia wanahabari wasiwepo ndio maana wanaweza kuandika namna hii. Hakukuwa na sababu ya msingi ya kuzuia waandishi wa habari kushuhudia ufanyaji kazi wa demokrasia...

Kama gazeti liliandika Uongo, Chadema wanasemaje kuhusu chupuchupu hiyo?
 
chadema hawana uwezo wa kumuondosha Zitto, Zitto ndiye pekee aliyeipaisha chadema, nani alikuwa anaijuwa chadema kabla ya Zitto? labda kwa kina Mbowe na wakweze tu.

MFANO WA MAGUGU NA NGANO (Mathayo 13: 29)
29Lakini akasema, "Hapana, msiyang'oe, kwa maana wakati mking’oa magugu mnaweza mkang'oa na ngano pamoja nayo. 30Acheni ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia wavunaji, wayakusanye magugu kwanza, wayafunge matita matita ili yachomwe moto, kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani mwangu."
 
Kwa wanaotaka ZZK aadhibiwe watachoka kusubiri.

Kwanza adhabu ya kumpuuzia mtu katika jamii yoyote, chamani au katika familia ni tosha kabisa. kwa sababu mhusika anabaki akijiuliza maswali na kujijibu mwenyewe. Watanitoa? Kimya, watanishitaki kimya, watagombana na mimi kimya.

Mahali ambapo hakuna anayekuuliza kuhusu jambo au tabia tofauti unayoionyesha, unateseka sana, unatamani hata wagombane tu nawewe ujue moja.

Wakisema tu wareact ni bingo kwa ZZK, kwa sababu hiyo reaction ndio mlo unaosubiriwa kwa hamu na wale wanaomtuma pamoja na yeye mwenyewe, kumpaisha na kuporomosha CHADEMA.
 
Chadema hawana uwezi wa kumtimua Zitto ilo wanalijua wajaribu waone.
 
Back
Top Bottom