Ukweli ni kwamba Zitto amewataja mafisadi wa mabilioni ya Uswiss, kwa kutumia busara yeye kama mbunge. Upande wa jeshi, fedha kwenye account za nje za viongozi hutolewa wakati wa manunuzi ya silaha na vifaa vya jeshi. Upande wa mafuta, makampuni ya mafuta hutozwa kiwango kidogo kulipia serikalini "exploration blocks" wanazopewa, kwa masharti kwamba waweke fedha kwenye account za nje za viongozi wa serikali ambao majina yao kampuni hizo hupewa.
Kwa kifupi basi, hizi hela zimeibiwa toka serikalini.Tusimlaumu Zitto kwa kutotaja majina, na sie tumsaidie kumalizia, kwani ameshatutafunia kila kitu. Hebu malizia, mie naanza; (List itakuwa updated kadiri wana JF wanavyotoa majina ya nani alikuwa kwenye nafasi zilizoorodheshwa katika kipindi kilichotajwa na Zitto)
Watu waliokuwa kwenye hizi nafasi kipindi kilichotajwa wamesemwa kuwa na fedha katika akaunti za Uswisi
1. Mawaziri Wakuu, 2003-2010; Sumaye, Lowasa
2. Mawaziri wa Nishati na Madini - 2003-2010; Ngeleja, Karamagi, Msabaha
3. Mawaziri Wizara wa Ulinzi 2003-2010; Kapuya,
4. Mkurugenzi Mkuu wa TPDC 2003-2010; Yona Killagane
5. Wenyeviti wa Bodi ya TPDC - 2003 - 2010; Robert Mboma
6. Makatibu Mkuu wa Wizara ya Nishati 2003-2010; Patrick Rutabanzibwa, Arthur Mwakapugi
7. Makatibu Mkuu Wizara ya Ulinzi 2003-2010;
8. Wakuu wa Majeshi, 2003-2010; Robert Mboma,
9. Makamishna wa Nishati 2003-2010; Prosper Victus, Mrindoko
10. Wanasheria wa serikali, 2003-2010; Chenge,
11. Wajumbe wa Board ya TPDC, 2003-2010; Faida Bakari, Gosbert Blandes, Mudhihir Mudhihir, Emmanuel Ole Naiko, William Haji, Maduka Kessy, Prosper Victus, Mwalim A Mwalim, Ngosha Magonya
Source: Gazeti la Mwananchi, 9/11/2012: Kichwa cha habari; HOJA YA ZITTO YAIBUA MAJADALA MKALI,WABUNGE CCM WAIUNGA MKONO