Zitto awataja mafisadi wa mabilioni ya Uswisi!

Zitto awataja mafisadi wa mabilioni ya Uswisi!

Badili kichwa cha habari kiwe Zito atoa fununu ya majina ya vigogo walioficha pesa nje ya nchi
 
mmh,nimeshaichoka hii muvi,yeye mwenyewe asafishe tuhuma za kuweka mamilioni ya ccm kwa kimada wake wa ujerumani..
 
Huu uandishi wa kibavicha yani kichwa cha habari na yaliyo ndani tofauti kweli bavicha ni janga sugu la wazawa.
 
nimekimbia haraka haraka kumbe bado ni fununu GLOBAL PUBLISHER AT WORKS.
 
Mbowe hayumo?
Maana nae nasikia ana majumba dubai na akaunti ya mabilioni.
Na kuna wakati tulisikia ametuhumiwa kukwepa kodi kwa baadhi ya miradi yake.
 
Ukweli ni kwamba Zitto amewataja mafisadi wa mabilioni ya Uswiss, kwa kutumia busara yeye kama mbunge. Upande wa jeshi, fedha kwenye account za nje za viongozi hutolewa wakati wa manunuzi ya silaha na vifaa vya jeshi. Upande wa mafuta, makampuni ya mafuta hutozwa kiwango kidogo kulipia serikalini "exploration blocks" wanazopewa, kwa masharti kwamba waweke fedha kwenye account za nje za viongozi wa serikali ambao majina yao kampuni hizo hupewa.

Kwa kifupi basi, hizi hela zimeibiwa toka serikalini.Tusimlaumu Zitto kwa kutotaja majina, na sie tumsaidie kumalizia, kwani ameshatutafunia kila kitu. Hebu malizia, mie naanza; (List itakuwa updated kadiri wana JF wanavyotoa majina ya nani alikuwa kwenye nafasi zilizoorodheshwa katika kipindi kilichotajwa na Zitto)

Watu waliokuwa kwenye hizi nafasi kipindi kilichotajwa wamesemwa kuwa na fedha katika akaunti za Uswisi

1. Mawaziri Wakuu, 2003-2010; Sumaye, Lowasa
2. Mawaziri wa Nishati na Madini - 2003-2010; Ngeleja, Karamagi, Msabaha
3. Mawaziri Wizara wa Ulinzi 2003-2010; Kapuya,
4. Mkurugenzi Mkuu wa TPDC 2003-2010; Yona Killagane
5. Wenyeviti wa Bodi ya TPDC - 2003 - 2010; Robert Mboma
6. Makatibu Mkuu wa Wizara ya Nishati 2003-2010; Patrick Rutabanzibwa, Arthur Mwakapugi
7. Makatibu Mkuu Wizara ya Ulinzi 2003-2010;
8. Wakuu wa Majeshi, 2003-2010; Robert Mboma,
9. Makamishna wa Nishati 2003-2010; Prosper Victus, Mrindoko
10. Wanasheria wa serikali, 2003-2010; Chenge,
11. Wajumbe wa Board ya TPDC, 2003-2010; Faida Bakari, Gosbert Blandes, Mudhihir Mudhihir, Emmanuel Ole Naiko, William Haji, Maduka Kessy, Prosper Victus, Mwalim A Mwalim, Ngosha Magonya

Source: Gazeti la Mwananchi, 9/11/2012: Kichwa cha habari; HOJA YA ZITTO YAIBUA MAJADALA MKALI,WABUNGE CCM WAIUNGA MKONO
Wameficha kiasi gani?ebu fafanua kiasi cha kila mmoja
 
Hv kuna haja gani ya kuficha Pesa zote hizo kisha siku Ukifa wengine wanazichezea tu ! Kwani wafichaji pesa wote hawana Ndugu wenye njaa?kwani vijijini kwao wananchi hawana shida ?kwa nini hawasaidii jamii?hizo pesa wanazoficha kuna uwezekano wa kuzirejesha Tz au Zito anajishaua tu ?
 
Ukoo wa hao wenye kuficha pesa Uolozeshwe vizuri Waangaliwe wale Wote wenye Dhiki kubwa wakusanywe pamoja Zichukuliwe hizo pesa Wapewe au waundiwe miladi na kujengewa Nyumba nzuri na wao wanufaike na Ufisadi wa Ndugu zao badala ya kufaidi peke yoa na Nyumba ndogo zao na kuzidisha Foleni jijini .
 
hakun akipya hapa.ujinga mtupu....Yaani sijui hata Zitto ulienda kufanya nini huko Uswiswi..
 
hakun akipya hapa.ujinga mtupu....Yaani sijui hata Zitto ulienda kufanya nini huko Uswiswi..

Anatikisa kiberiti ili kujijengea mazingira ya Rushwa kwani waficha Pesa wataweza kumpoza ili akae Kiimya
 
Vuta picha Chadema ingekuwa imeshika dola wao walio ndani ya makabrasha ya Zitto n wengineo walio na ma_swizz accounts ingekuwaje?? Bado nina imani na Chadema kuwa ndo suluhu ya nchi yetu kupiga hatua ktk nyanja zote.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Tahadhari: ni muhimu tusije tukamkabidhi fisi bucha, ikiwa ufisadi umeanza ndani ya chama tukipewa serikali itakuwaje? Tuanze kujisafisha ili turudishe imani kwa wanachama.
 
Hv kuna haja gani ya kuficha Pesa zote hizo kisha siku Ukifa wengine wanazichezea tu ! Kwani wafichaji pesa wote hawana Ndugu wenye njaa?kwani vijijini kwao wananchi hawana shida ?kwa nini hawasaidii jamii?hizo pesa wanazoficha kuna uwezekano wa kuzirejesha Tz au Zito anajishaua tu ?

Hizo fedha huko nje zinakaa tu, na kwa vile zinahusiana na madhambi basi ni maandalizi ya kukimbilia nje. (si ajabu zitakuja kutumika kununulia silaha kama ilivyo Kongo-Mungu aepushe) Na hao ndio wanaopigia debe uraia wa nchi mbili ili wakikimbia wasiweze kurudishwa na kushtakiwa.
Hata hivyo wangekuwa wazalendo hasa wangetumia hizo fedha kuanzisha miradi hapa hapa nchini hivyo kuongeza ajira na kuendeleza nchi kiuchumi.
 
mimi nina vijisenti katika benki moja iliyopo katika kisiwa cha Jersey.
 
Ni kweli mkuu lakini nijuavyo mimi Mh.Zitto pia alihakikishiwa usalama wake kwa kuwa zile info hazijatoka mbali sana na kwa wanaCCM so he will be safe!

Na mie nafikiri hii hoja si ya Zitto bali ni ya CCM na inatokana na mtifuano wao kuelekea 2015, hivyo Zitto keshahakikishiwa full usalama 24 hrs
 
2003~2010 Mkapa akifuatiwa na JK hawawezi kukwepa. Maana walikuwa ndiyo mabosi wa juu kabisa serikalini. Mawaziri wa fedha wa vipindi hivyo ambao ni pamoja na Meghji, Pesambili hawawezi kubebwa hapo. Wasajili wa Hazina wa vipindi hivyo wanajua kila kitu. Mabosile wa BOT, TAKUKURU, na CAG wamo pia. Kifupi Zitto siyo mkweli anatumiwa kuwapiga vita baadhi tu ya wagombea URAISI ndani ya CCM. Mbona Zitto halipui ufisadi mkubwa ulioshamiri ndani ya CDM?
 
Mikupe ya nchi hii, imetunyonyaaaaa, haya tukamueni kabisa mtuanike! Kuna watu wanatia hasira!
 
Back
Top Bottom