Zitto aongea na Power Breakfast ya Clouds FM

Zitto aongea na Power Breakfast ya Clouds FM

Siasa mchezo mchafu sana. Acha kutuzuga dogo. Au umeshajua kuwa hati hati ya kupata kura 2010 ni ndogo ndiyo maana unajihami kuwa ulisema utakuwa Mbunge kwa term moja tu?? Pole kijana.

Kwa ufupi Chadema wameshakuchoka. Wanakutafutia tu tundu bovu la kuondokea!!! Kwa heshima wanasubiri umalize Ubunge tu. Zitto, wewe ni ndumi la kuwili. Your credibility has gone down to negative!!!

safi kabisa kuandika unachopenda kiwe. tusubiri tumwone 2010 huko mwandiga. duh, inaonesha ukimwona jamaa unaweza mmwagia tindikali maana machuk kibao
 
Mie nampa big up sana Zitto, huyu jamaa ana vision ya kipekee na laiti opposition leaders wengine wangefata model yake then tungekuwa mbali kama taifa..

Sishangai zitto kumpigia kifua Kafulila:
Eti b'se ni chama kinginine jamani plz eleweni kwamba he's doing that for the benefit of opposition side, rather than that, tukubali kuwa CCM itachukua tena hilo jimbo na ikumbukwe kuwa lilikosekana kizembe tuu (kutokuwa na umoja ndani ya upinzani) ni kwanini tusiachiane majimbo, kwanini tusipeane support na kwanini tusiwe na sauti moja?..

BIG UP "Zitto"!!
Kwa sababu maana halisi ya upinzani Tanzania ni ubinafsi na tamaa ya madaraka/kuhodhi mamlaka bila kujali maslahi ya taifa na wananchi wake! The most likely way to squeeze mafisa CCM out of the power is by opposition joining forces for the sake of national interests, but it's very unlikely that that would happen in today Tanzanian politics! I can't really see us doing a "Kenya" to treat that proven lethal CCM GLIOMA.
 
Kwa sababu maana halisi ya upinzani Tanzania ni ubinafsi na tamaa ya madaraka/kuhodhi mamlaka bila kujali maslahi ya taifa na wananchi wake! The most likely way to squeeze mafisa CCM out of the power is by opposition joining forces for the sake of national interests, but it's very unlikely that that would happen in today Tanzanian politics! I can't really see us doing a "Kenya" to treat that proven lethal CCM GLIOMA.

Kuiondoa CCM madarakani ndilo la msingi tu? Halafu baada ya hapo iweje?

Je, huu ndio utaratibu wa kuwaondoa ccm madarakani? Yaani tugawanyike kwanza ndipo tukusanye nguvu zetu pamoja; kweli hatutakuwa vichaa?

Hebu tusaidie, huu ushirikiano unakuwepo vipi bila kuwa na mkataba wa ushirikiano? Je, ni ushirikiano unapata nguvu zaidi pale unapovunja misingi iliyokuwa tayari imejengwa?

Tuanze tu ushirikiano kwa sababu kafulila kaenda nccr, ila kabla ya hapo sababu ya ushirkiano haikuwepo, kweli hatutakuwa vichaa?
 
Tuanze tu ushirikiano kwa sababu kafulila kaenda nccr, ila kabla ya hapo sababu ya ushirkiano haikuwepo, kweli hatutakuwa vichaa?

Acheni kudanganya umma. Zitto siku zote amekuwa akiamini katika ushirikiano wa wapinzani. Hata kabla ya uchaguzi wa 2005 yeye alikuwa mstari wa mbele kutika mikakati ya ushirikiano ambayo kama si umimi wa baadhi ya watu basi CUF, NCCR na CHADEMA wangeliweza kushirikiana na kusimamisha mgombea mmoja katika urais na kuachiana majimbo mengi tu.

Pia Zitto wakati wote amekuwa karibu na wanasiasa wengine hata wale wa CCM ambao hata kama alikuwa hakubaliani nao lakini pia haamini katika siasa za uadui. Waulize viongozi wa vyama vingine vya upinzani ni nani wanamuona muumini wa dhati wa ushirikiano ndani ya CHADEMA na watakutajia Zitto.

Hata wakati bado hajajitoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA moja ya ajenda yake kubwa aliyokuwa akitaja hata katika vyombo vya habari ni kujenga mazingira mazuri ya ushirikiano wa dhati wa vyama vya upinzani kuelekea uchaguzi ujao.

Tatizo katika upinzani bado wengi wao wamegubikwa na umimi, usisi, falsafa pinga na kujidanganya kuwa wanaweza pekee yao wakati realities says otherwise.

Wapo hata wanaofikia kudefine muingiliano wa Zitto na wanasiasa wa vyama vingine kuwa ni usaliti na sio mkakati chanya.

Tafuteni majungu mengine lakini katika hili Zitto ameonyesha muono mpana wa suala zima la maendeleo ya demokrasia nchini mwenu katika mtazamo wa mbali kuliko wanasiasa wengine.



omarilyas
 
Mag3 na Asha

Asanteni sana. Kubonyeza hakufai bila kuandika. Najua tunasafari ndefu but will get there.
 
Hivi jamani kauli ya Zitto kuhusu Kafulila inatufundisha nini?
 
Ukiwa na akili za kawaida utaelewa kwamba zitto yuko mbali kabisa na uongozi mzima wa chadema.maamuzi yote yatakayofanywa kinyume na mtazamo wake atawapinga wenzake kwenye vyombo vya habari ,sasa tusubiri muda siyo mrefu tutamjua zitto kwa rangi zake kamili.
 
Ndugu yangu Omar

Acheni kudanganya umma. Zitto siku zote amekuwa akiamini katika ushirikiano wa wapinzani. Hata kabla ya uchaguzi wa 2005 yeye alikuwa mstari wa mbele kutika mikakati ya ushirikiano ambayo kama si umimi wa baadhi ya watu basi CUF, NCCR na CHADEMA wangeliweza kushirikiana na kusimamisha mgombea mmoja katika urais na kuachiana majimbo mengi tu.

Huu ni ubinafsi wa Zitto na wale wanaomtetea, kwa Kwao (Kwake) likifanyika Jambo jema ni Zitto, likifanyika baya ni CHADEMA, ni udhaifu wa Zitto

Pia Zitto wakati wote amekuwa karibu na wanasiasa wengine hata wale wa CCM ambao hata kama alikuwa hakubaliani nao lakini pia haamini katika siasa za uadui. Waulize viongozi wa vyama vingine vya upinzani ni nani wanamuona muumini wa dhati wa ushirikiano ndani ya CHADEMA na watakutajia Zitto.

Unazidi kuthibitisha kauli yangu ya hapo Juu


Hata wakati bado hajajitoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA moja ya ajenda yake kubwa aliyokuwa akitaja hata katika vyombo vya habari ni kujenga mazingira mazuri ya ushirikiano wa dhati wa vyama vya upinzani kuelekea uchaguzi ujao.

Tatizo katika upinzani bado wengi wao wamegubikwa na umimi, usisi, falsafa pinga na kujidanganya kuwa wanaweza pekee yao wakati realities says otherwise.

Wapo hata wanaofikia kudefine muingiliano wa Zitto na wanasiasa wa vyama vingine kuwa ni usaliti na sio mkakati chanya.

Mh Yale yale

Tafuteni majungu mengine lakini katika hili Zitto ameonyesha muono mpana wa suala zima la maendeleo ya demokrasia nchini mwenu katika mtazamo wa mbali kuliko wanasiasa wengine.

Katika Hili Zitto ameonesha bado anahitaji kukuwa ili watu waweze kumbebesha mzigo wa matumaini, Ni Kiongozi Mzuri ila akiondoa Ubinafsi anaweza kuwa kiongozi bora zaid


omarilyas
 
Hivi jamani kauli ya Zitto kuhusu Kafulila inatufundisha nini?

Hivi Kabla ya Kafulila Kuondoka CHADEMA, hivi CHADEMA walikuwa na mpango gani kuhusu Kigioma Kusini? Je walikuwa na Mpango wa kuwaachia NCCR jimbo?
 
Zitto siku hizi ananishangaza sana. Anawezaje kutangaza kuwa NCCR ina nguvu kuliko CHADEMA Kigoma Kusini wakati ambapo Uchaguzi wa mitaa 2009 CHADEMA ilipata viti vingi kuliko NCCR? Halafu anaji-contradict, kama kweli NCCR ina nguvu kama alivyosema, na kwamba anataka CHADEMA iachie NCCR ili NCCR ishinde; vipi siku zote amekuwa akisema hapa kwamba anataka Kafulila ashinde jimbo hilo kupitia CHADEMA? Sasa kwa kuwa tu Kafulila kahamia NCCR basi ndio amebadili msimamo sasa anataka NCCR ishinde?

Halafu si Zitto huyo huyo aliandika hapa JF kuwa NCCR imefadhaliwa mwaka 2005 na bado inaendelea kufadhiliwa kwa fedha za EPA? Sasa leo Zitto anatangaza kuunga mkono chama ambacho amekitangaza kuwa kinaendeshwa na fedha za ufisadi na wagombea wake wanafadhiliwa na mafisadi?

Zitto huyu huyu alimnadi Muslim Hassanal kupitia CHADEMA mwaka 2005, Muslim ambaye ni mjumbe wa baraza la wadhamini mpaka sasa kupitia CHADEMA? Je, Zitto anamaanisha kuwa kiongozi wake huyu wa CHADEMA hafai anayefaa ni Kafulila wa NCCR? Labda Zitto atueleze bayana mapungufu ya Muslim na CHADEMA mpaka atangaze live kumuunga mkono Kafulila na NCCR.

Asha

This is FUndamental Hoja, je Kabla ya Kafulila kwenda NCCR-Mageuzi Chadema walikuwa na Mpango gani na Kigoma Kusini?
 
Acheni kudanganya umma. Zitto siku zote amekuwa akiamini katika ushirikiano wa wapinzani. Hata kabla ya uchaguzi wa 2005 yeye alikuwa mstari wa mbele kutika mikakati ya ushirikiano ambayo kama si umimi wa baadhi ya watu basi CUF, NCCR na CHADEMA wangeliweza kushirikiana na kusimamisha mgombea mmoja katika urais na kuachiana majimbo mengi tu.

Omar,

Watu gani hao? Na ubinafsi upi huo? Mimi ninachokumbuka ni maandishi ya Zitto mwenyewe humu JF kuwa NCCR ni chama kilichokufa na kwamba chama hicho mwaka 2005 kilifadhiliwa na mafisadi kwa fedha za EPA. Kwa hiyo hadithi ya kuwa Zitto alitaka ushirikiano na NCCR ndio naisikia kwako.


Pia Zitto wakati wote amekuwa karibu na wanasiasa wengine hata wale wa CCM ambao hata kama alikuwa hakubaliani nao lakini pia haamini katika siasa za uadui. Waulize viongozi wa vyama vingine vya upinzani ni nani wanamuona muumini wa dhati wa ushirikiano ndani ya CHADEMA na watakutajia Zitto.

Omar, Zitto kuwa karibu na Mrema na Mbatia akashindwa kuwa karibu na Mbowe sio sifa wala sio ishara ya kutanguliza utaifa. Ndio maana watu wanashangaa kwamba baada ya matukio ya Tarime yaliyofanywa na Mrema na Mbatia, na matukio ya Mrema dhidi ya Mutungirehi Zitto akawa mwanasiasa pekee wa CHADEMA aliyekwenda Mkutano Mkuu wa TLP na kuchangia dola mia. Siku ambayo kulikuwa na mkutano wa CHADEMA hakuuchangia wala kuhudhuria pamoja na kuombwa. Maneno kama haya yanapotolewa na wewe ambaye umetajwa humu na Zitto mwenyewe kuwa ni msaidizi wa Salim na umetajwa kuwa ni msaidizi wa Zitto ni vyema ukatueleza zaidi

Ndio maana sishangai unavyosifia Zitto kuingiliana na wanasiasa wa vyama vingine ikiwemo CCM. Kama msaidizi wake ni msaidizi pia wa Dr Salim wa CCM si jambo la ajabu. Lakini wapo wanajiuliza pia mbona kila Zitto anapoulizwa role models wake hutaja orodha ndefu ya wazee wa CCM? Hivi wazee kama Mtei, Makani nk wa CHADEMA hawaoni kuwa na maana yoyote?


Hata wakati bado hajajitoa katika kugombea nafasi ya Uenyekiti wa CHADEMA moja ya ajenda yake kubwa aliyokuwa akitaja hata katika vyombo vya habari ni kujenga mazingira mazuri ya ushirikiano wa dhati wa vyama vya upinzani kuelekea uchaguzi ujao.

Kwa hiyo kwake mazingira ni CHADEMA kushirikiana na NCCR na TLP? Hebu tueleze vizuri faida ya huo mkakati, na kwanini mkakati huo haukuanzia Tarime, Busanda na Biharamulo? Vyama hivyo vimejiandaaje kwenda 2010 ili iwe sababu ya CHADEMA kuviachia majimbo kama ambavyo huo mkakati ulioita wa Zitto na ajenda uliyoitaja inavyosema?

Tatizo katika upinzani bado wengi wao wamegubikwa na umimi, usisi, falsafa pinga na kujidanganya kuwa wanaweza pekee yao wakati realities says otherwise.

Wapo hata wanaofikia kudefine muingiliano wa Zitto na wanasiasa wa vyama vingine kuwa ni usaliti na sio mkakati chanya.

Tafuteni majungu mengine lakini katika hili Zitto ameonyesha muono mpana wa suala zima la maendeleo ya demokrasia nchini mwenu katika mtazamo wa mbali kuliko wanasiasa wengine.

Wapinzani gani hao wamegubikwa na umimi? wataje kwa majina na umimi wao ili tuujadili. Lakini usiandike hoja za kuchokoza zenye kumuingiza Zitto kwenye malumbano humu


omarilyas

Serayamajimbo
 
This is FUndamental Hoja, je Kabla ya Kafulila kwenda NCCR-Mageuzi Chadema walikuwa na Mpango gani na Kigoma Kusini?

kwa kuwa NCCR walipinga CHADEMA na CHADEMA ipinge NCCR? Visasi visasi visasi. Wapinzania walipoteza majimbo mangapi mwaka 2005 kwa kugawana kura?
Watanzania wanachosha kabisa
 
Zitto siku hizi ananishangaza sana. Anawezaje kutangaza kuwa NCCR ina nguvu kuliko CHADEMA Kigoma Kusini wakati ambapo Uchaguzi wa mitaa 2009 CHADEMA ilipata viti vingi kuliko NCCR? Halafu anaji-contradict, kama kweli NCCR ina nguvu kama alivyosema, na kwamba anataka CHADEMA iachie NCCR ili NCCR ishinde; vipi siku zote amekuwa akisema hapa kwamba anataka Kafulila ashinde jimbo hilo kupitia CHADEMA? Sasa kwa kuwa tu Kafulila kahamia NCCR basi ndio amebadili msimamo sasa anataka NCCR ishinde?

Halafu si Zitto huyo huyo aliandika hapa JF kuwa NCCR imefadhaliwa mwaka 2005 na bado inaendelea kufadhiliwa kwa fedha za EPA? Sasa leo Zitto anatangaza kuunga mkono chama ambacho amekitangaza kuwa kinaendeshwa na fedha za ufisadi na wagombea wake wanafadhiliwa na mafisadi?

Zitto huyu huyu alimnadi Muslim Hassanal kupitia CHADEMA mwaka 2005, Muslim ambaye ni mjumbe wa baraza la wadhamini mpaka sasa kupitia CHADEMA? Je, Zitto anamaanisha kuwa kiongozi wake huyu wa CHADEMA hafai anayefaa ni Kafulila wa NCCR? Labda Zitto atueleze bayana mapungufu ya Muslim na CHADEMA mpaka atangaze live kumuunga mkono Kafulila na NCCR.

Asha

Hai CCM wamepa 92% ya vijiji, unasema CHADEMA waiachie CCM?

Huyo Zito alitoa ushahidi wa NCCR kufadhiliwa na pesa za kagoda? Maana nasikia CHADEMA nao walipata mgawo huo kupitia kwa mwenyekiti wao ambaye alikuwa mgombea Urais. Zito mwanasiasa tu kama wengine leo tukimuuliza ushahidi hana na hapa hamkumuuliza ushahidi.

Kwani huyo Muslim alipata kura ngapi huko Kigoma Kusini?
 
Katika kipindi cha power breakfast Zitto alonga live nakusema hato ondoka chadema wala atarajii kuondoka Chadema.

Kwani kusema ndio kutenda?nakumbuka hata kina Tambwe Hizza walisema hivyo hivyo tena Tambwe alisema kama akienda CCM labda akamfufue mama yake na kulala naye but yuko CCM sasa bila aibu. Wengi huwa wanasema lakini mambo yanapowawia magumu hufanya tofauti na maneno yao.chama cha siasa sio baba wala mama mzazi kusema kwamba lazima ufe nacho.
 
Katika kipindi cha power breakfast Zitto alonga live nakusema hato ondoka chadema wala atarajii kuondoka Chadema.

According to Wagagagigikoko News Network, the damage has already been done and Chadema will NEVER be the same again!!!!
Let's hope for the best for Chadema for the 2010 elections!
 
1. Alithubutu kugombea uenyekiti chadema
2. alikuwa kwenye kamati ya JK ya kuangalia madini (sijui ilikuwa ni yangapi hii na sijui ripoti zake huwa ziko wapi)
3. Anamsapoti kafulila Kugombea ubunge Kigoma kusini kwa tiketi ya NCCR Mageuzi (Zitto ni CHADEMA)
4. Aliwahi kuwa kiongozi DARUSO
5. Ni mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya mahesabu ya mashirika ya umma (aliwahi kupendekeza kuwa tununue mitambo ya Dowans ili kusiwe na mgawo. Ugumu wa mioyo yetu tu hatimaye mgawo kweli ukawepo)

Mpwa huna macho tu ukaona? Mengine wataendelea....

1. Akaogopa wazee akajitoa!
2. Wangapi wamekua wenyeviti wa kamati? Nothing special here!
3. Hapo ndi anaonyesha udhaifu haswaaaa, hajui definition ya political party?
4. Tena PM, aliyoyafanya tuliokua nae naomba tu tunyamaze...aibu...na watanzania wangeua wala wasingemwamini hivyo!
5. Hapo ndipo nilipodhibitisha everyone has a price...uliona wapi umegombana na mtu afu unamshauri mwanao akaoe palepale? kesi badi iko mahakamani akataka tununue mitambo yao...
 
Hivi Kabla ya Kafulila Kuondoka CHADEMA, hivi CHADEMA walikuwa na mpango gani kuhusu Kigioma Kusini? Je walikuwa na Mpango wa kuwaachia NCCR jimbo?

Swali zuri...naomba wanamsapoti Zitto wasilikimbie walijibu tu vizuriiii.

Na ndio hicho nnachosema mimi, kumsapoti mtu wa chama kingine sio vibaya, ila Zitto anamsapoti Kafulila coz ni mfuasi wake au kwa ajili ya kuimarisha upinzani?

Utamsapoti vipi mtu wa chama kingine wakati hujui chama chako kitamsimamisha nani katika jimbo hilo?

Nyerere alimsapoti yule wa upinzani baada ya kuona wa CCM hafai, sasa Zitto anamsapoti kafulila bila kujua chama chake kinamsimamisha nani, does that make sense?

UBINAFSI tu ndio umemjaa kijana huyu, na kujiona yeye yuko juu ya chama!
 
1. Akaogopa wazee akajitoa!
2. Wangapi wamekua wenyeviti wa kamati? Nothing special here!
3. Hapo ndi anaonyesha udhaifu haswaaaa, hajui definition ya political party?
4. Tena PM, aliyoyafanya tuliokua nae naomba tu tunyamaze...aibu...na watanzania wangeua wala wasingemwamini hivyo!
5. Hapo ndipo nilipodhibitisha everyone has a price...uliona wapi umegombana na mtu afu unamshauri mwanao akaoe palepale? kesi badi iko mahakamani akataka tununue mitambo yao...

Hakuwa PM alikuwa Katibu Mkuu. Serikali aliyoongoza DARUSO pamoja na Waziri wao wa fedha Makundi ndio serikali ya kwanza kuita wakaguzi kukagua hesabu za DARUSO. Nilikuwa chuo miaka yake na kijana huyu alikuwa imara na hakuwa na mchezo na haki za wanafunzi. Kama huna CHUKI, basi wewe ni mwongo tu. Sifagilii siasa zake, lakini kwenye uadilifu huyu kijana rekodi yake ni safi sana.
 
Swali zuri...naomba wanamsapoti Zitto wasilikimbie walijibu tu vizuriiii.

Na ndio hicho nnachosema mimi, kumsapoti mtu wa chama kingine sio vibaya, ila Zitto anamsapoti Kafulila coz ni mfuasi wake au kwa ajili ya kuimarisha upinzani?

Utamsapoti vipi mtu wa chama kingine wakati hujui chama chako kitamsimamisha nani katika jimbo hilo?

Nyerere alimsapoti yule wa upinzani baada ya kuona wa CCM hafai, sasa Zitto anamsapoti kafulila bila kujua chama chake kinamsimamisha nani, does that make sense?

UBINAFSI tu ndio umemjaa kijana huyu, na kujiona yeye yuko juu ya chama!

CHUKI tu zimekujaa. Hebu eleza huo ubinafsi wake kwa mifano maana inawezekena tujadili hewa. bamiza mtu kwa facts sio hisia zinazotokana na inferiority complex
 
Back
Top Bottom