Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Mimi ni mmoja wa watu tunaoamini katika uwezo wa zitto kabwe kisiasa, lakini napata shida sana na upepo wa mwenendo wake tangu kuuibuka kwa richmond. ana uwezo wa kujenga hoja makini, lakini tangu kashfa hiyo kauli zake zimekuwa tata. CHADEMA imetuambia watanzania kuwa JK ameingia madarakani kwa kuchakachua kura. Kitendo cha mgawanyiko kwa minajili ya mitazamo na kuiita hiyo ni demokrasia ni kuwachanganya watanzania. TUNATOA WITO KWA DK SLAA NA CHADEMA kudhihirishia umma wa watanzania UCHAKACHUAJI wa CCM kwenye kura za URAIS vinginevyo Madai yenu yatapoteza haki ya kuaminiwa. THE RIGHT MAN ALWAYS STANDS ALONE.
 
Mimi nimefarijika na habari hii, kwa sababu mbunge wangu ninayemkubali sana Halima Mdee nae hakuwepo kabisa siku ile, na pamoja na Zitto, Mzee Ndesamburo, Shibuda, John Mnyika, na Lucy Owenya pia hawakuwepo bungeni siku ile. Hawa ndio wabunge wa Chadema ambao hawakukubaliana na Chairman Freeman na mwenziwe Slaa kuhusu kuwalk out.

Kuna redemption in a way, because I had high hopes for Halima Mdee--and we can give her benefit of doubt kwamba she had to go with the decision of the party.
 
Off Nipashe Jumapili

21st November 10

Chadema watupiana lawama

Mwandishi Wetu

Siku chache baada ya Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kususia hotuba ya ufunguzi wa Bunge iliyotolewa na Rais, Jakaya Kikwete, baadhi ya wabunge wapya wa chama hicho walioshiriki kitendo hicho, wameibuka na kusema hatua ile haikuwa utashi wao, bali kwa shinikizo la baadhi ya viongozi wa juu wa chama hicho.

Wabunge hao, wamesema iliwabidi kushiriki uamuzi ule kwa shingo upande, kwa kuhofia kuwa wasingeeleweka kwa viongozi wao na kuonekana wasaliti, lakini mioyoni mwao hawakuona mantiki yoyote ya kususia hotuba ya Rais ya ufunguzi wa Bunge, ikizingatiwa kuwa walikuwa mahali hapo kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi waliowachagua.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti kwa masharti ya kutoandikwa majina yao gazetini kwa sababu zinazoeleweka, wabunge hao ambao hii ni mara ya kwanza kuingia bungeni baada ya kushinda wakati wa uchaguzi mkuu uliopita, walisema kitendo hicho ambacho kimepokewa kwa hisia tofauti na watu wengi, kimekidhalilisha chama chao badala ya kukisaidia.
Mmoja wa wabunge hao, alisema hapingani na chama chake kulalamikia matokeo yaliyompa ushindi Rais Kikwete, bali hakufurahishwa na uamuzi wa kuonyesha hisia hizo kwa kususia kikao muhimu cha ufunguzi wa bunge wakati Rais akihutubia.
Alisema kitendo hicho kimewachukiza wananchi wengi na kimejenga picha mbaya kwa wananchi kuwa chama hicho ni cha watu wenye visasi, wasio wavumilivu wa kisiasa na wanaopenda kutumia njia za mitafaruku kutatua matatizo badala ya njia za kidiplomasia.
Mbunge mwingine kijana wa chama hicho, alisema alitamani asishiriki kitendo cha kususia hutuba ya rais, lakini alishindwa kufanya hivyo, kwa kuwa baadhi ya viongozi wa juu walikuwa na msimamo mkali kuhusiana na suala hilo, hivyo asingeshiriki angejiweka katika mazingira magumu ndani ya chama.
"Unajua sisi bado ni wageni ndani ya chama na hili ndiyo bunge letu la kwanza, tusingeweza kwenda kinyume na matakwa ya viongozi wetu, japokuwa sisi wenyewe hatukufurahia jambo lile", alisema mbunge huyo.
Mbunge mwingine mpya wa Chadema, ambaye hakutaka kuandikwa jina lake kwa kile alichosema kuepuka msuguano na viongozi wake, alisema kuwa kitendo hicho kimewafanya wabunge wa Chadema kueleweka vibaya kwa wapiga kura wao waliowatuma kwenda bungeni kuwawakilisha.
"Lazima tukubaliane na ukweli kuwa baadhi ya wananchi waliotuchagua kwenye nafasi ya ubunge kwenye urais waliamua kumpa kura Kikwete, sasa tunapomsusia tunakuwa hatueleweki tunaonekana kama tumewasaliti wananchi".
"Hata ukiangalia wanaotuunga mkono kwenye jambo hili ni walewale walioonyesha kutuunga mkono tangu wakati wa kampeni, lakini kiukweli wananchi wengi hawajafurahia na hili si jambo jema. Lakini nadhani viongozi wetu watakuwa wamejifunza kitu, kwani binadamu tunajifunza kutokana na makosa", aliongeza kusema mbunge huyo.
Aliongeza kusema kuwa, kitendo hicho kinaweza kuwapa wasiwasi wananchi kuwa wabunge wa chama hicho watatumia muda mwingi kuvutana na serikali badala ya kushughulikia matatizo yao na kutekeleza ahadi walizoahidi wakati wa kampeni.
Hata hivyo, baadhi ya viongozi waandamizi na wabunge maarufu wa Chadema ambao inaelezwa hawakuunga mkono msimamo wa wenzao kususia hotuba ya Rais Kikwete hawakushiriki katika kitendo hicho.
Inaelezwa kuwa wakati wa kikao cha kujadili kama ipo haja ya wabunge wa chama hicho kususia hotuba ya rais au la kulitokea mvutano mkali, baadhi wakipinga na wengine wakiunga mkono msimamo huo.
Baadhi ya wabunge ambao hawakuingia kabisa bungeni siku lilipotokea tukio hilo kwa sababu ambazo hazijajulikana na hivyo kutoshiriki katika kitendo hicho cha kutoka nje ya ukumbi wa bunge ni, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo, Mbunge wa Mpanda Said Arfi, Mbunge wa Viti Maalum Lucy Owenya.
Wabunge wa Chadema walisusa na kutoka bungeni wakati Rais Jakaya Kikwete anaanza kulihutubia Bunge kulifungua rasmi Alhamisi iliyopita.
Hali hiyo isiyo ya kawaida ilisababisha kelele bungeni zikiwemo za wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwazomea wenzao waliosusa.
Mara baada ya wabunge wa Chadema kutoka ukumbini, wabunge wa Chama Cha Wananchi (CUF) walikwenda kukaa kwenye viti vya waliosusa, Rais Kikwete akaendelea kuhutubia.
Katika hotuba yake, Rais Kikwete amesema, waliofanya hivyo wanapaswa kutambua kuwa hawana Rais, yeye ndiye Rais wao na kwamba hawana sehemu nyingine ya kupeleka mahitaji yao hivyo watakwenda, watarudi.
"Hata wale ambao hawakuichagua CCM bado hawana Rais, Serikali yao ni hii hii", amesema Kikwete kabla ya kumaliza kulihutubia Bunge mjini Dodoma wiki hii.
Mara baada ya Rais kumaliza kulihutubia Bunge, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda aliwaeleza wabunge kuwa, baadhi ya vyama vimeanza kuonyesha mwelekeo usio sahihi.
Waziri Mkuu ametoa rai kwa Watanzania wasiruhusu mtu yeyote kuwagawa hivyo waseme hapana.
Kwa mujibu wa Chadema, wakati wa uchaguzi mkuu mwaka huu, kura za mgombea wao, Dk. Willbrod Slaa ziliibwa ili kumpa ushindi Kikwete.
Chama hicho kimesema, licha ya kutomtambua Kikwete, wabunge na madiwani wake wataendelea na kazi kama kawaida katika vyombo hivyo vya uwakilishi.
Wabunge wa Chadema pia wamekataa uteuzi alioufanya Kikwete kumteua Pinda kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania.
Kitendo hicho cha Chadema kimepokelewa kwa hisia mbalimbali na wananchi huku wengine wakisema kimetekeleza haki yao ya kidemokrasia, wengine wakilaani na kukieleza kuwa ni utovu wa nidhamu, kukosa busara na kutokamaa kidemokrasia.
NIPASHE JUMAPILI
 

Usomi na exposure yake vingemwelekeza kuwa baada ya kura ya ndani (demokrasia) uamuzi ulifanywa na yeye ilikuwa ikimbidi afuate uamuzi huo. Kama msomi alifahamu pia tuna sheria ya kiajabu inayoruhusu kupinga matokeo kura za ubunge lakini inazuia kupinga matokeo ya kura za uraisi. Hivyo basi busara ya chama ilikuwa ni kuchukua njia ambayo haivunji sheria bali inalionyesha taifa na marafiki wa taifa kutoridhika kwa Chadema na matokeo ya kura za uraisi. Kutoshiriki kwa mhe. Zitto katika kitendo kilichokubaliwa kidemokrasia ni sawa na kusema - "mimi sikumpigia mbunge yeyote kwa hiyo bunge likipitisha kodi ya mwaka huu mimi nitakataa kulipa kodi hiyo". Kama hiyo ndiyo exposure ya kisiasa ya mhe. Zitto - ni dhahili kuwa bado anahitaji exposure zaidi.
 
I saw it coming......! Ogopa sana mtu ambaye yuko tayari kutumia mbinu yoyote aendelee kuwa popular, Zitto fits this descreption, like a hand and glove. Fuatilia mambo yake utaona anachojaribu kukifanya, CDM wamemlea and now he thinks, he's indispensable.
 

Sasa kama walipiga kura, maanayake zitto pamoja na wenzake walikuwatari kukubaliana na maamuzi au uamuzi ambao ungepatikana baada ya kupiga kura na huo ndio ungekuwa uamuzi wa mwisho na msimamo wa chama,sasa kama alikubali kupiga kura maanayake nikwamba alikuwa tayarikupokea matokeo na kufuata msimamo wa chama,sasa kama alijua yeye anamsimamo wake kwanini alishiriki kupiga kura? siangekaanje na hata kura asishiriki kupiga.
 
Amri jesh mkuu ambae alishinda kwa wizi wa kura. Zitto, hoja ya kitoto. Sema nyingine.

Pia alito sababu nyingine kuwa eti wapigakura wake wanampa shinikizo kuwa JK ni rais ambaye ameleta maendeleo kigoma sasa yeye anampiganga je? Sijui umakini wa huyu bwana uko wapi? kuiba kura hakuhalalishwi na kuiletea maendeleo kigoma. Uwizi ni uwizi tu hakuna haja ya kuuonea haya hata kidogo.

Lakini hapa niwape angalizo Chadema, wanatakiwa wachukue tahadhari sana na watu watakaotumiwa au kupenyezwa na system kuwa vuruga na hatimaye kuwasambaratisha kama ilivyo kuwa kwa NCCR. Na haya ndio matumizi mabaya ya vyombo vya usalama vya nchi hii ambayo yatatakiwa kupatiwa ufumbuzi na katiba mpya. Nitashangaa wavurugaji wa chadema kama kati yao hawatakuwapo Zitto na Shibuda natusuiri muda utatufubulia kitendawil hiki.
 

Pamoja na kuiba kura bado mgombea wa chadema alikuwa na watu millioni 2 plus. Sasa kura za Zenji za maruhani mlikuwa wangapi. Chadema wakipanga mikakati yao vizuri kwa kutumia nguvu ya watu wanaweza kufanya maajabu ambayo ytakuwa ni ukombozi wa walalohoi wa TZ wala msiwakatishe tamaa wako katika right track.
 
Kitendo cha zto kutoingia kabisa bungeni amewasupport wenzie waliotoka. Vipi kama angeingia halafu akaganda kwenye kiti wakati wenzie wanatoka?
Watu wote hawawezi kuwa sawa kimtazamo.
 
Jamani unajua mtu akiishaanza kuitwa mheshimiwa anajisahau na kudhani yeye anakaa nje ya sayari hii.Bora ule wakati wa zamani enzi zile za Mwalimu-Kambarage,maana wakati huo viongozi walikuwa hawaitani waheshimiwa ,sijui hili neno lilianzia wapi,wakati ule viongozi walikuwakiitana NDUGU,kwamfano pale bungeni tungesikia NDUGU Zitto .........,sasa hii muheshimiwa naona inawalewesha.Huu ni utangulizi tu sasa hoja yangu ni kwamba,kama Zitto na wenzake walikubaliana kupiga kura ilikuamua nini chakufanya mbele ya wa tz na dunia kwa ujumla,na yeye zitto alishiriki kupiga kura akimaanisha kwamba anasubiri kura ziamue,na kura za wengi zikaamua kwamba waingie ten watoke, sasa ilikuwaje yeye afanye kinyume.Sasa kama alijua hataki kufuata msimamo wa chama, basi asinge piga kura na badala yake angekaa nje tu.sasa kapiga kura a wengi wakashinda alaf sasa anasema anangoja kuadhibiwa na chama,hii maana yake nini,Maana yake ni jeuri na kutaka kujionyesha kwamba anaweza kujitofautisha na wenzake iliaone kwamba nini kitafanyika kwani anahisi yeye ni bora sana.Mimi silazimishi kwamba zitto angeingia lah hasha,maana hii ni democracia anaweza kuamua anavyoamini,lakini anaweza kufanya hivo kwa kufuata taratibu za chama,mfano kupiga kura au kutokupiga kura ni hiari yake,maana ya kupiga kura nikusubiri maamuzi ya wengi ndi yawe last decision.Sasa zitto anataka kutuambia kwamba hata ambao walipiga kura za uraisi na hawakumchagua kikwete,maana yake kikwete sio raisi kwani kura hazikuamua kama wanavyotaka wao.au kule kigoma kaskazini ambao hawakumchagu yeye zitto,basi sio mbunge wao,sasa kama hawakumtaka zitto awe mbunge na hawakutaka kutumunjia ya kura ilikufanya uamuzi wa kumkataa,kwa nini walipiga kura,wangeacha iliwanaomtaka wamchague.zitto anataka kutumia umaarufu wake kutufanya sisi ni wajinga kwai hata hivivyo zitto alianza kuwa kigeugeu ndani ya chama muda mrefu na hakuanza jana wala juzi,sasa kama yeye anataka kwenda ccm aende tu,maana chadema haimtegemei yeye,yeye aliikuta na akiondoka ataiacha na hiyo ndio democracia.Mbona ccm wakikubaliana maswala yao hawatuambii kwamba waliongea nini na walifanyaje huko ndani,sasa kisa cha zitto kupeleka kwa wanahabari na kuropoka ''tulipiga kura walioshinda wakaamua kuingia na kutoka'' sasa walikuwa wanapiga kura iliiweje na kama alijua hataki kuingia kwanini alipiga kura na kusubiri uamuzi wa kura?
 
Hivi hapa pana siri gani?walipanga watoke nje na wametoka na wengine mkaanzisha chokochoko kwamba wale ambao hawakwenda bungeni na kutoka nje yaani hawakuingia kabisa bungeni ni wasaliti kwa bahati Zitto ni mmojawapo na ndiyo ameenda kujisafisha na kueleza kinagaubaga.mpaka mtakapoacha kila analolifanya Mh.Zitto kuwa ni issue nafikiri naye hataacha kuwashangaza kwani anaelewa gharama ya vijineno vyenu kwa wapiga kura wake.
 
Kufanywa au kutofanywa wajinga inategemea mtu amnaelewaje na anatafsiri viti taratibu na sheria zinazosimamia eneo husika. Naamini mdogo wangu Zitto ana akili timamu na anafanya jambo bila kukurupuka kama unavyodhani. Demokrasia ni pamoja na kujua jinsi ya kuwa mwana dipromasia pia. Kijana huyu anajua kusoma nyakati...... big up ZITTO!!
 
Mwekeni pembeni letu jicho na masikio..............................!
 
1. Kama ulikuwa unanisoma ungeweza kuona kwamba mgawanyiko huu ulikuwa wazi hata kabla ya Zitoo kuusema, Zitto kathibitisha.

2. Zitto talks too much, there is such a thing as "too much information". Anataka kujifanya "A Profile in Courage". Lakini kuna tofauti kati ya courage na narcisissm. Hivi kulikuwa na ulazima gani wa yeye kusema haya? Naona kwa nini Zitto hakupewa uongozi wa upinzani.

Moja ya upuuzi wa kujiunga na chams, na moja inayofanya independent thinkers kupata ugumu kujiunga na chama, ni ukweli kwamba chama kikishaamua, unatakiwa kukubali. Ndiyo maana ya "collective responsibility". Kama swala lina uzito na unatofautiana na chama unaweza hata kujitoa kwenye chama. Watu walijitoa TANU enzi ya kupiga kura iliyoruhusu wazungu na waasia kupiga kura Tanganyika.

Kwa hiyo Zitto naye ilimbidi kwenda na maamuzi ya chama, kama tofauti zitazidi anaweza kuachia ngazi kwenda kwenye chama anachokipenda au kuanzisha chake.
 
Umenena watu wanasahau kwamba CCM Imefika hapo ilipofika kwasababu ya ukandamizwaji wa hoja na mitazamo tofauti,Sasa hiki chama kinasema mbadala lakini watu wakileta fikra mbadala wanaitwa wasaliti..............!Tanzania yetu wengi ni walewale na hata Hawa Chadema wakipewa Dola nafikiri mwendo utakuwa mdundo kama kopi ya CCM.
 

Zitto is wrong, anapaswa apewe adhabu! Je, ambao hawakumpigia kura Kigoma, wanahaki ya kusema 'sisi hatukumpigia kura'? La, hasha. Ukishaamua demokrasia itegemee kura, HESHIMU KURA.

Ndiyo maana mzee mapesa wa UDP aliadhibiwa na Sitta kwa kosa la kutowaunga mkono wapinzanni wenzake. Je, Sitta alifanya kosa? NO! Red must be red, and bluee must be blue...Tanzania ya leo, HUWEZI KUABURUZA WATU, after all, kila mtu ni kama maua tu hapa duniani. Hakuna cha fisadi wala mzalendo, sharti tuonje kaburi.

Zitto kukaa nyumbani (if it is true) bila kuja bungeni, ni sawa. Lakini kutoa siri za vikao vyao ni kosa.

Jeshini huwa watu hawa wanaitwa VIHEREHERE. Nadhani hajapita JKT? Au ndo ile ya miezi 6?
 

Kusema kupo kwenye siasa lakini si kila kitu ni cha kusema hasa ukiwa kiongozi. Zito ni naibu katibu mkuu. Kama hajui wajibu wake kama kiongozi kwenye chama basi ni kibaraka.
Nasikia amekuwa tajiri kipindi cha miaka mitano tu ya ubunge wake. Yumkini ikawa kweli au si kweli kwamba kanunuliwa. Ninaamini uongozi wa chama utamshughulikia vilivo na kwa busara.

Ukiwa mwanamageuzi huna haja ya kukatishwa tamaa na vitendo vya wanasiasa kama hawa. Ni mambo ya kawaida kwenye demokrasia changa kama hizi ambazo watu bado njaa zimetukaba koo. Mfano ni Kenya ambako kibaraka kimoja kinaitwa Kalonzo Musyoka ambaye ndiye makamu wa Rais wa sasa alisaliti chama cha ODM wakati wa uchaguzi 2007 akaunda chama dhaifu kinaitwa ODM Kenya. Wapiganaji wa kweli kama Odinga na wenzake hawakujali bali waliendelea na uchaguzi ambako walishinda lakini matokeo yalibadilishwa kama alivyo chakachua mkwere lakini kwao ilikuwa balaa la vita kwasabu watu hawakuwa tayari tena kutawaliwa na vibaraka kama kina Kalonzo.
Utajiuliza alichokipata Kalonzi kwa kuungana na Rais Kibaki PNU kinazidi kitu gani zaidi ya kujivunjia heshima na kuonekana msaliti. Amejivunjia heshima kwa kiasi kikubwa na sasa amekuwa mtu wa kuzomewa na watu hadharani maeneo mengi nchini Kenya make wanamwona kama mtu aliyewasaliti kusivovumilika huku ni makamu wa Rais.
Bahati mbaya hapa kwetu imekuwa tu watu wananunuliwa na CCM na haya yalikuwepo enzi za KANU ya Kenya ambako wanasiasa walinunuliwa kuondoa upinzani. Muda ulipofika wanunuzi na wanunuliwa mpaka leo wamebaki kwenye madimbwi na kaburi la KANU linaendelea kuota nyasi.
 
Yeye alihujumu chama kigoma kivipi?Si aliwaeleza kitendo cha kumuita mtu sisimizi na ambaye angekuwa asset baadae si vyema mlisema aende tu,aliwasihi sana kutoa adhabu mbadala kama mnaona Kafulila amekosea mkaona mnayaweza.Sasa mnamlaumu Zitto kwa lipi?Uongozi umevuna walichopanda kigoma period!
 

Unapopiga kura unasubi uamuzi wa mwisho na ndio utakuwa mtazamo na msimamo wa chama,huu ndio ukweli hata ccm wanapoamua maswala yao huwa kuna msimamo wa chama,mfano wagombea wa ccm walikatazwa kushiriki midahalo na huo ndio ulikuwa msimamo wa chama mapaka kampeni zilipoisha,hili lilikuwa ni agizo la chama na ilikuwa hivyo na hakuna aliepinga,sasa unataka kuniambia hakuna wagombea wa ccm waliokuwa wanatamani kuingia kwenye midahalo ilikutumia nafasi hii kufanya kampeni? mbona unabisha tu, zitto mwenyewe anakubali na kusema hizo ndizo gharama za democracia sasa wewe na huyo mdogo wako anaye jua kusoma nyakati,kwanini alipiga kura na kusubiria final decision ya kura huku akijua kwamba yeye anajua kusoma nyakati,siangekaa pembeni sasa hapo kafanya nini (-1+1=0) au tuseme SITAKI NATAKA ? alaf anadai anasubiri adhabu,kuna wakati mtu mzima anafanya vitu vya kipumbavu sana,ccm wakiwa na misimamo yao ya chama ni sawa ,lakini wengine wakiwa na misimamo ya vyama vyao ,sio saw bali ni kusoma nyakati, hapa mdogo wako anapima umuhimu wake ktk chama na kuona kwamba chama kitafanya nini.
 
jamani kutofautiana kimtazamo na kimuono ndani ya chama kimoja ndio kukomaa kidemokrasia,mm sioni kosa la zitto nawenzake kutoona uhalali wa kutoka anapoanza kuzungumza amir jesh mkuu
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…