Zitto amrushia 'kijembe' Prof. Muhongo

Zitto amrushia 'kijembe' Prof. Muhongo

Kama CCM watakuwa wa kuendelea kuongoza nchi, basi na waache porojo nyingi na wamsimamishe Prof. Muhongo. Huyu muhemishimiwa yuko makini (smart) sana katika utendaji na katika kupangilia mikakati.

Kama ulisikiliza hotuba yake ya kutangaza nia, tukio ambalo halikuwa na makuu, kwa watu makini watakubaliana na yeye kuwa nchi yoyote duniani haiwezi endelea bila tafiti. Hili ni suala ambalo viongozi ama wanasiasa wengi wamekuwa wakilipa uzito mdogo sana na kujikita zaidi kwenye mambo ambayo ni ya kufunika kombe (cosmetic), ambayo mara nyingi yanakuwa sio endelevu

Muhongo awe Rais ha ha ha vijana acheni matani.
 
Muhongo siyo kiongozi hawezi uongozi sense akufundishe. Sisi with wa Mtwara hatumpendi hata kidogo. Hivi mnajua kuwa gesi yote anyotambia huyo prof ipo Mtwara na Lindi sisi tunasema hafai. Iketokea akawa raisi lazima umwagaji wa damu utatokea

Unajua kuna Gesi nyingi Bagamoyo , Tanga ziwa Rukwa na ziwa Tanganyika usjidanganye kwa hila Tanzania kila sehemu ni neema subiri utasikia maeneo mengi huko Mtwara ndio mwanzo tu usijivunie kwa hicho kidogo. Na rasilimali isitugawe watanzania .
 
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Tabora)
hamjamaliza tu shughuli ya kutanganza nia huko?? naona nyie mmeamua kuja kimila zaidi!! haya bana!! Mgetembelea pia IKULU ya Chief Lungusha pale Sikonge kupata baraka zaidi.
 
Nampa muhongo kura amesema ataniletea bomba la gas na maji ya bomba hadi huku ukerewa nansio

KABLA YA GESI YA MTWARA KULIKUWA NA BADO TUNAYO DHAHABU JE ILIKUFIKIA MPAKA KWAKOOO??:confused2:
 
Muhongo katumia falsafa ya kusadikika. Kila nyumba kuunganishwa na bomba la gesi?????!!!! Labda tusemee tu kwa pamoja NDIYO MZEE!!!!
Napiga picha za maboma na tembe kufungwa mabomba ya gesi wakati maji yamekuwepo tangu kuumbwa kwa dunia lakini serikali imeshindwa kupeleka mabomba ya maji kwenye kila nyumba! Siasa ni balaa maana prof. haoni aibu kusema uongo hadharani kisa madaraka.
 
Baadhi ya wanasiasa wanawaaminisha wananchi kuwa gesi asilia itatatua matatizo yote ya wananchi na nchi kwa jumla, na wengine wanaamini kwamba gesi ndo itaweza kulipa deni la taifa,ila gesi ni kama madini itawanufaisha wateule wachache sana................waacheni wananchi waendelee kujitafutia mikate yao na familia zao,msiwajaze maneno wakawaamini,wakiandamana mtawalipua kwa risasi na mabomu.Ukiacha gesi kuna rasilimali ngapi nchi hii jamani?Juzi Prof Muhongo ameitaja nchi kama India ambayo leo hii anaitolea mfano,ila India na baadhi ya nchi za South East Asia hazikuendelea kwa sababu ya rasilimali za asili,ziliendelea kwa kuwekeza kwenye RASILIMALI WATU.
Kuna sera 2 ambazo India iliwekeza
1.Sera ya Elimu
2.Sera ya Viwanda
3.Sera ya ushindani (Haikuwa rasmi)India alikuwa akishindana na China kwa kusomesha vijana na kuwapeleka nje wakasome.
China aliwekeza katika sera 3-4
1.Sera ya elimu
2.Sera ya Kilimo
3.Sera ya Viwanda
4.Sera ya Teknolojia (ambapo yeye na India walikuwa wakinunua teknolojia nje na kuleta nyumbani,huku wakiwatumia vijana wao waliowasomesha ndani na nje kuziendeleza).
Akitokea Kiongozi akatuambia kuwa tutaendelea kwa gesi au rasilimali yoyote ya asili ni Muongo.Nchi huendelea kwa kuwekeza kwenye rasilimali watu "HUMAN CAPITAL DEVELOPMENT"Ndio maana sisi na Malaysia,India,China,South Korea,Hong Kong even Japan we were almost similar by 1970s,leo wametuacha mbaaaaali,naamini miaka mitatu ijayo twaweza anza kuomba misaada MALAYSIA.
Mkoroshokigoli
 
Jamaa anawadharau sana watz eti kwa vile muda mwingi ameishi na kusoma ujerumani. Alifikia hata kuongea kijerumani cha kuokoteza, tunaokijua tulikuwa tunamsikiliza tu kwani hakukuwa na nafasi ya kuuliza maswali

Nasikia ni mmanyema wa kariakoo, je, kimanyema anakijua? Kizaramo anakijua? Kiingereza anakijua? Au anadhani akijua Kijerumani hadhi inapanda? HKuna watu tumezaliwa huko na bado hatuzungumzi lugha hiyo! Yeye ni ulimbukeni tu, ambayo ni mbaya ktk umri wake.

Huyu ni mtu ambaye binafsi sijawahi kumuona kuwa ana matumizi ya maana. Zipo kazi ambazo naweza nikampa lakini siyo siasa aliyoingia. Sitegemei apange la maana kwa mwananchi. Sijui mwaka huu atakuwa na dili gani maana posho ya kuachia majimbo hataipata.
 
ZZITO umejuaje kuwamhaiwezekani? yeye kama mtalamu anaaminimhivyo subili ashidwe hacha majungu.
Subili ashidwe hacha majungu = Subiri ashindwe acha majungu (Siamini kama ni typing error kwa maneno yote hayo utakuwa unatatizo kubwa mzee,ndio mana ni rahisi kwako kukubali ya Muhongo kwamba atasambaza bomba la gesi na maji kila nyumba ya Mtanzania)
 
ZZK ashakuwa mufilisi, nampa kama mwaka mmoja atakuwa amechoka kama mrema na cheyo.
 
Nasikia ni mmanyema wa kariakoo, je, kimanyema anakijua? Kizaramo anakijua? Kiingereza anakijua? Au anadhani akijua Kijerumani hadhi inapanda? HKuna watu tumezaliwa huko na bado hatuzungumzi lugha hiyo! Yeye ni ulimbukeni tu, ambayo ni mbaya ktk umri wake.

Huyu ni mtu ambaye binafsi sijawahi kumuona kuwa ana matumizi ya maana. Zipo kazi ambazo naweza nikampa lakini siyo siasa aliyoingia. Sitegemei apange la maana kwa mwananchi. Sijui mwaka huu atakuwa na dili gani maana posho ya kuachia majimbo hataipata.

Pale alikwua anaosha tu nyota yake kwa ajili ya ubunge sio urais.....NA WATZ WALIVYO WAVIVU WA KUFIKIRI (kwa mujibu wa mkapa) UTAKUTA WANAMPA UBUNGE.....
 
Back
Top Bottom