Zitto amrushia 'kijembe' Prof. Muhongo

Zitto amrushia 'kijembe' Prof. Muhongo

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo,Zitto Z. Kabwe amempiga kijembe mtangazania wa CCM,Prof. Sospeter Muhongo.

Kijembe hicho kilibandikwa kwenye ukurasa wa twitter wa Zitto kinahusu gesi asilia.

Zitto amedai kuwa hapo nyuma kidogo,watanzania waliaminishwa kuwa mkombozi wao ni dhahabu.

Sasa wanaaminishwa kuwa mkombozi wao ni gesi,aliongeza Zitto.

Ni Prof. Muhongo tu ndiye aliyeelezea utegemezi wa gesi katika kukuza uchumi.

Ilikuwa wakati akitangaza nia ya kuwania Urais kwa tiketi ya CCM.

Bifu la Escrow linaendelea?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Tabora)
 
ZZITO umejuaje kuwamhaiwezekani? yeye kama mtalamu anaaminimhivyo subili ashidwe hacha majungu.
 
Km kweli basi nina hakika zitto alikuwa anauza sura tu.....ALIISHA SEMA AMECHOKA SASA SIJUI ANATAKA NINI TENA. Natamani bora nimsikilize TUMBILI atakuwa na kitu kipya. zitto is just an opportunist
 
Muhongo katumia falsafa ya kusadikika. Kila nyumba kuunganishwa na bomba la gesi?????!!!! Labda tusemee tu kwa pamoja NDIYO MZEE!!!!

Jamaa anawadharau sana watz eti kwa vile muda mwingi ameishi na kusoma ujerumani. Alifikia hata kuongea kijerumani cha kuokoteza, tunaokijua tulikuwa tunamsikiliza tu kwani hakukuwa na nafasi ya kuuliza maswali
 
Kwa reserve ya gesi tuliyonayo na kwa uzoefu wake Prof. Muhongo anajua fika kuwa hawa wawekezaji wakilipa share kisawasawa tunatajirika kikwelikweli. Dhahabu ni udhaifu wa viongozi wamehongwa wakaiachia kwa wezi wa kizungu. Namuunga mkono Muhongo.
 
Hivi kwanza yuko wapi huyu mdogo wetu,mana hapa Kigoma simuoni.Au yupo kwake Dar alafu aje awadanganye ile misukule yake hapa eti nimwenzao wakati haishinao wakati wa shida?
 
Jamaa anawadharau sana watz eti kwa vile muda mwingi ameishi na kusoma ujerumani. Alifikia hata kuongea kijerumani cha kuokoteza, tunaokijua tulikuwa tunamsikiliza tu kwani hakukuwa na nafasi ya kuuliza maswali

Atumie mavuno ya escrow account kuwapelekea maji ya bomba wanakijiji anakotoka itatosha maana ndio watakao palilia hata kaburi lake baada ya kufa
 
Muhongo siyo kiongozi hawezi uongozi sense akufundishe. Sisi with wa Mtwara hatumpendi hata kidogo. Hivi mnajua kuwa gesi yote anyotambia huyo prof ipo Mtwara na Lindi sisi tunasema hafai. Iketokea akawa raisi lazima umwagaji wa damu utatokea
 
Atumie mavuno ya escrow account kuwapelekea maji ya bomba wanakijiji anakotoka itatosha maana ndio watakao palilia hata kaburi lake baada ya kufa

N alengo lake kutoka moyoni mwake haikuwa kuwania urais bali alikuwa anajitangaza na eti kujaribu kujisafisha ili wampe ubunge.....Kwa watz walivyo wajinga wanawweza kumpa ubunge
 
Jamaa anawadharau sana watz eti kwa vile muda mwingi ameishi na kusoma ujerumani. Alifikia hata kuongea kijerumani cha kuokoteza, tunaokijua tulikuwa tunamsikiliza tu kwani hakukuwa na nafasi ya kuuliza maswali

Mtu akiongea ukweli mnasema anadharau
 
Kwa reserve ya gesi tuliyonayo na kwa uzoefu wake Prof. Muhongo anajua fika kuwa hawa wawekezaji wakilipa share kisawasawa tunatajirika kikwelikweli. Dhahabu ni udhaifu wa viongozi wamehongwa wakaiachia kwa wezi wa kizungu. Namuunga mkono Muhongo.

Mali ya mjinga/mpumbavu huliwa na wajanja! Reserve ipo kubwa, lakini viongozi akiwemo Muhongo wanaaminishwa kuwa hakuna mtaji na wataalam, nao wanaimba wimbo huo huo huku wakubaliana na mikataba ambayo hata mababu zetu ambao hawakwenda shule wasingekubaliana nayo!
Ukoloni wa siku hizi ni wa kutawala akili za viongozi na wasomi wa makoloni!
 
Mtu akiongea ukweli mnasema anadharau

Neno ukweli is very judgemental.............Sawasawa na kusema kasema ukweli kwa sababu amesema jina lake halikutajwa kwenye mgawo pale mkombozi bank wkt hatujui nani waligawiwa pale stanbic....
HII CCM NA HII NCHI NI ZAIDI UIJUAVYO
 
Back
Top Bottom