Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

KUFUKUZWA KWA KOSA LA KI-FIKRA NCCR-MAGEUZI NA KUBAKISHWA KAMA SHUJAA KWA KOSA LA UFISADI DHIDI YA TAIFA KULE CCM IPI NI HATARI ZAIDI?

CHADEMA tuendelee kutumia vema kanuni hii ya
"Working with a LESSER DEVIL" si tu kwa huyu Kafulila bali hata kwa makundi mengine hasimu kule CCM ili kukiimaarisha chama zaidi kabla ya kushika dola mapema Novemba 2015.

Ingawaje binafsi bado sijamuondolea kibendera chekundu huyu kijana Kafulila na Zitto mwenyewe kwa mienendo yao yenye maswali mengi sana huko nyuma, lakini kwa kuzingatia hiyo kanuni yetu mpya hapo juu basi sina budi kukubliana na uongozi wangu utkavyoona inafaa.

Lakini hata akiruhusiwa kujiunga tena ni sharti aturidhishe kwamba anajutia makosa yake, atakua mpambanaji wa kweli chamani kuliko rafiki yangu Zitto ambaye siku hizi 'kaishiwa na risasi' kwenye bunduki yake ya kisiasa na kwamba atakua team-player mwenye nidhamu ili kuharakisha azma ya umma kuking'olea mbali Magamba 2015.
 
Habari zilizonifikia kutoka source ya kuaminika ni kuwa Kafulia amefanya kikao na Chadema leo kwa madhumuni ya kurudi kwenye chama hicho. Nimedikezwa kwamba ameona kwenda mahakamani ni ngumu na pia kukata rufaa ndani ya chama ni ngumu pia maana uwezekano wa kumsamehe ni mdogo maana anahitalafiana na mbatia kuhusu jinsi ya kuongoza chama. Mbatia yeye anataka chama kiwe ccm B wakati kafulila anataka chama kiwe cha upinzani

Nilikuwa najifunza Formula za Ms Excel leo mwalimu wangu akanifundisha formula hii hapa:

=ibange-i=bange
 
Aache kuzurura huyu,,na zitto si kamkaribisha?sioni kama ni uamuzi sahihi wa chadema kumeza matapishi.

CDM haikumfuza. Alijiondoa mwenyewe baada ya kuvuliwa uofisa habari wa chama. Akiamua kurudi yeye ndiye atakuwa amekula matapishi yake.
 
Its too early for him to come out with a reasonable decision ... should take time, be patient and sort out everything in a cool, calm mind ... I guess he is still in deep shock ...!
 
CHADEMA haijawahi kumfukuza Kafulila, ila alivuliwa wadhifa wake kama msemaji , yeye mwenyewe ndio alijiondoa. . . .
Akija hakuna kuramba Matapishi. . ! Kwakua hatuwahi kutapika.
He is like concubine. Ukivuliwa madaraka kwa maslahi ya wengi ndo unajiondoa miongoni mwao? Kafulila hafai kwenda CHADEMA, yeye na Mwenyekiti HENCHE ni samaki na ndoana majini. Ni mgogoro mtupu mnaoutafuta. Ni bora akaenda CCM kuliko kupokelewa na upande wowote wa upinzani. Kilichomuondoa CDM ni tamaa ya kuutaka uenyekiti wa BAVICHA ili wapange mikakati(na wenzake anawajua) ya kuutwaa uenyekiti wa CDM. sio siri. ninanukuu" David ni rafiki yangu hata akihamia wapi lazima nimpigie kampeni ya ubunge
 
Lakini WanaCDM kabla hatujamkaribisha Kafulila lazima tujiulize ni nini kilimfanya uvuliwe title ya Uafsa habari na muhimu pia tujiulize ni nini kilimuondoa CDM. Na swali jingine la kujiuliza ni kwamba je ni nini kilimfukuzisha NCCR. CDM lisiwe kimbilio la wakosefu. Nadhani mnakumbuka wakati Kafulila alipokuwa CDM alivyoyumbisha chama kwa msaada wa rafiki yake wa karibu aliyehakikisha CDM haishindi katika Jimbo hilo. Tusiwe wepesi wa kusahau naomba tutafakari kwa kina.
CDM haikumfuza. Alijiondoa mwenyewe baada ya kuvuliwa uofisa habari wa chama. Akiamua kurudi yeye ndiye atakuwa amekula matapishi yake.
 
KUFUKUZWA KWA KOSA LA KI-FIKRA NCCR-MAGEUZI NA KUBAKISHWA KAMA SHUJAA KWA KOSA LA UFISADI DHIDI YA TAIFA KULE CCM IPI NI HATARI ZAIDI?

CHADEMA tuendelee kutumia vema kanuni hii ya
"Working with a LESSER DEVIL" si tu kwa huyu Kafulila bali hata kwa makundi mengine hasimu kule CCM ili kukiimaarisha chama zaidi kabla ya kushika dola mapema Novemba 2015.

Ingawaje binafsi bado sijamuondolea kibendera chekundu huyu kijana Kafulila na Zitto mwenyewe kwa mienendo yao yenye maswali mengi sana huko nyuma, lakini kwa kuzingatia hiyo kanuni yetu mpya hapo juu basi sina budi kukubliana na uongozi wangu utkavyoona inafaa.

Lakini hata akiruhusiwa kujiunga tena ni sharti aturidhishe kwamba anajutia makosa yake, atakua mpambanaji wa kweli chamani kuliko rafiki yangu Zitto ambaye siku hizi 'kaishiwa na risasi' kwenye bunduki yake ya kisiasa na kwamba atakua team-player mwenye nidhamu ili kuharakisha azma ya umma kuking'olea mbali Magamba 2015.
Ni hoja nzuri. Ndio maana hata mimi naona mtu kama Shibuda hakuna sababu ya kuhangaika nae ni afadhali kumnyamazia tu maana ni tabia yake, he is a lesser evil!
 
Naunga mkono Kafulila kurudi CHADEMA, kwa kuwa daima alisimama kama mpinzani, na aliungana na chadema kule bungeni kupinga sera za kifisadi na kidikteta za CCM. Hata katika sakata la katiba ni kafulila na mkosamali waliokuwa bega kwa bega na wabunge wa CHADEMA katika kuukataa uozo wa CCM. For sure kafulila ni mpinzani wa kweli. Apewe nafasi nyingine CHADEMA.
 
Raia yeyote wa Tanzania, mwenye umri zaidi ya miaka 18 akikubali misimamo ya CHADEMA na katiba ya chama akaribishwe kuwa mwanachama. Hata kama hapo awali alitofautiana na uongozi katika matamshi na mienendo yake, akiomba radhi, anaweza kurudi chamani.

CHADEMA hakitakuwa chama cha kitaifa kama kitabagua Watanzania. Suala la kuongoza au kushika wadhifa ktk chama ni tofauti. Hilo litategemea uwezo wa mwanachama, haiba yake na jinsi wanachama wenzake wanavyomkadiria.

Kwa hiyo nashauri CHADEMA wamkaribishe David Kafulila kuwa mwanachama tena. Hata wale wanaCCM waliokuwa wanatushambulia na kututukana hadharani, wakitambua umahiri, umakini na uzalendo wetu; na kwamba hiki ndicho chama kinachoweza kutatua matatizo yetu, wakaribishwe. Karibu hata Wassira, Kikwete na mlolongo wote wa wahasimu wetu.
 
Chadema itafanya jambo la busara na la kuheshimika sana endapo hawatomruhusu huyu Kafulila arudi chadema.
 
Back
Top Bottom