Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

Niliwahi kushauri kitu hiki katika moja wapo ya mitandao ya kijamii na leo narudia. Ningetamani kuona ibara hii katika katiba "IWAPO MBUNGE ATAJIUZURU KWA HIARI YAKE BASI CHAMA KILICHOMDHAMINI KICHANGIE ASILIMIA 50 YA BAJETI YA UCHAGUZI MDOGO NA GHARAMA ZOTE ZITAKAZOONGEZEKA NA IWAPO CHAMA KIKIMFUKUZA UANACHAMA MBUNGE WAKE BASI KICHANGIE 100% YA GHARAMA ZA UCHAGUZI MDOGO.

NA MCHANGO HUU WA UCHAGUZI UTAPUNGUZWA KATIKA RUZUKU YA CHAMA NDANI YA KIPINDI MAALUM"
Tungekuwa na hii kitu ktk katiba yetu ya Kafulila na gamba la Igunga tusingeyasikia na tungeokoa kiasi kikubwa cha fedha za walipa kodi wenye njaa,hawana mikopo ya elimu,hawana barabara,walimu wanaoidai serikali na mengine kibaooo, nawasilisha

wazo lako zuri sana, lakini nani wa kulitekeleza katika nchi hii ambapo watoa maoni hawaheshimiki? ukitoa maoni yako utaitwa mchochezi
 
Namuunga mkono Zitto kumkaribisha Kafulila nyumbani, ila angalizo Kafulila aache ambition zake
 
Sasa Kafulila atajua ubaya wa kubebewa akili.
 
Sina hakika alichosema mh Zitto kuwa ni msimamo wa CDM..Nadhani ni mawazo binafsi na kilam mtu ana haki kikatiba kutoa mchango wake ki mtazamo...Ila nashauri msemaji mkuu wa CDM atoe tamko rasmi na kama wako tayari kumrejesha kundini kama Kafulila ataridhia..Mtu hujifunza kutokana na makosa!! Kama kuna makosa alifanya akiwa CDM nadhani kuna somo amejifunza..Tumpe tena nafasi na hii uwe mkakati madhubuti ya kuchukua majimbo yote ya KG!!! Pipoooz....
 
Vyama vina katiba zao na hizo katiba zimeweka utaratibu wa kufikisha malalamiko kunakohusika. Nccr ilivurugika wakati ule waMrema kwa kuwa Nidhamu ilitoweka kila mtu anasema lake

Busara zaidi inatakiwa itumike kukiko kujali mistari ya katiba, ambazo zimejaa kasoro nyingi za kiufundi, ni vema kujali na masahi ya wananchi, kumbuka wananchi hawakumchagua kwa sababu ni mwakilishi wa NCCR, bali walimchagua kwa sababu wanaamini atakuwa mwakilishi wao mzuri, na wapigakura wenye vyama na wasio na vyama walimpa kura, sasa katka kesi kama hiyo wanashirikishwa vipi? au wananchi ni kupelekewa mtu wa kumpigia kura tu? baada ya hapo hawana nguvu yoyote bali ni viongozi wachahche wa chama? ndyo maana voter turnout inazidi kushuka kila mwaka, ni kwa sababu wapiga kura wanaona kuwa nguvu kubwa ya mchakato wa kuwapata wawakilishi wao bado ipo mikononi mwa chama na si wananchi hivyo hata kujitokeza kupiga kura wanaona hakuna sababu, unaweza mchagua mbunge leo, baada ya wiki mbili akafukuzwa uanachama, jimbo linakosa mbunge bila ridhaa ya waliomchagua ni kama vile mbunge amefariki dunia.
 
Mbowe mbona unakuwa mnafiki, kwani Chadema walivyowafukuza madiwani Arusha hawakutumia busara!

Au Arusha gharama sio kubwa!
Siasa sio magazijuto kuwa lazima uanze kufungua mabano maamuzi ya kisiasa yanategemea hali na mazingira yaliyopo, incident ya Kafulila ni tofauti na ya madiwani.
 
MHESHIMIWA ZITO ATOA KAULI KWENYE UKURASA WAKE WA FB Zitto Z Kabwe Leo kwa masikitiko makubwa sana nimesoma kwenye vyombo vya habari kwamba ndugu David Kafulila kavuliwa uanachama wa chama chake. Kwa hatua hii David anakuwa amepoteza Ubunge wa jimbo la Kigoma Kusini licha ya kwamba alichaguliwa na wananchi bila kujali vyama (NCCR-M wanachama wake huko Kigoma Kusini hawafiki hata asilimia 10 ya wapiga kura wote). Haya ndio madhara ya Katiba ya sasa. Katakana na historia ya kisiasa baadhi ya watu wanajaribu kunihusisha na matatizo ya chama cha NCCR-M. Napenda kuweka wazi kwamba sihusiki kwa namna yeyote ile na migogoro ya chama kile. Ninaomba nisihusishwe na mambo yasiyonihusu. Ni dhahiri kwamba kuvuliwa uanachama kwa David ni jaribio kubwa kwa mfumo wetu wa demokrasia kama ilivyokuwa huko nyuma wakati kina Erasto Tumbo walipovuliwa uanachama wa chama chao cha UDP. Ninaamini NCCR-M watamaliza matatizo yao kwa mujibu wa katiba ya chama chao na ndugu David Kafulila atazikabili changamoto hizi kama kiongozi kijana wa kisiasa na kuona hii kama fursa badala ya kukata tamaa. Ifahamike wazi kabisa kwamba David ni mtu huru mwenye mawazo yake na maamuzi yake. Kwamba sisi ni marafiki wa karibu na kwamba tunatoka mkoa mmoja haina maana kwamba lolote afanyalo ama nimemtuma au ninahusika. Ninaheshimu misimamo yake na siku zote huwa nipo upande wa anayeonewa, kudhulumiwa na mnyonge. Msimamo huu wa msingi usiwape watu nafasi ya kunihusisha na mambo ya chama dhaifu kisicho na dira kama NCCR-M. Kafulila akumbuke kwamba hakufukuzwa CHADEMA, alijiondoa mwenyewe. Milango yetu ipo wazi kwa mujibu wa Katiba, Kanuni na taratibu za chama chetu. Ndg. Kabwe Zuberi Zitto, Mb
 
Kafulila karibu sana CDM bila shaka sasa umekomaa.
 
Kafulila karibu sana CDM bila shaka sasa umekomaa.
Nafikiri amemtambua mchawi wake ni nani. I've always said that in politics, your enemies can't hurt you, but your friends will kill you.
 
Habari zilizonifikia kutoka source ya kuaminika ni kuwa Kafulia amefanya kikao na Chadema leo kwa madhumuni ya kurudi kwenye chama hicho. Nimedikezwa kwamba ameona kwenda mahakamani ni ngumu na pia kukata rufaa ndani ya chama ni ngumu pia maana uwezekano wa kumsamehe ni mdogo maana anahitalafiana na mbatia kuhusu jinsi ya kuongoza chama. Mbatia yeye anataka chama kiwe ccm B wakati kafulila anataka chama kiwe cha upinzani
 
Aache kuzurura huyu,,na zitto si kamkaribisha?sioni kama ni uamuzi sahihi wa chadema kumeza matapishi.
 
Peoooooooooooooooooples poooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooweeeeeeeeeeeeeeeeer!
 
Nyumbani kwako ni nyumbani hata kama ni kubaya. Kwa Baba yako ni kwako. Karibu nyumbani kijana mpotevu.
 
Back
Top Bottom