Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

Zitto amkaribisha Kafulila CHADEMA

Habari zilizonifikia kutoka source ya kuaminika ni kuwa Kafulia amefanya kikao na Chadema leo kwa madhumuni ya kurudi kwenye chama hicho. Nimedikezwa kwamba ameona kwenda mahakamani ni ngumu na pia kukata rufaa ndani ya chama ni ngumu pia maana uwezekano wa kumsamehe ni mdogo maana anahitalafiana na mbatia kuhusu jinsi ya kuongoza chama. Mbatia yeye anataka chama kiwe ccm B wakati kafulila anataka chama kiwe cha upinzani

CHADEMA ni chama makini kama vpi mrudisheni kambini huyu kijana,. NI BORA mara mia kuliko chibuda!
 
Kafulila amefukuzwa akitetea maslahi ya upinzani na amefanya kazi kubwa sana ya kuteketeza Nccr na CCM .NCCR imedhirika kuwa CCM B na hakuna mtu anayeweza kugombea Kupitia Nccr akashinda hapa kuna mtihani kwa Mkosamali!
Umesahau alivyoungana na Hamad Rashid kwenye ishu ya kambi rasmi ya upinzani? au na wewe ulikuwa unawaunga mkono.
 
Mbona vyama ni vingi tu, anaweza hata kwenda UMD au aende CCK. Tatizo wala si kutumikia wananchi kama alivyodai Kafulila (sababu ya kulia na kupiga magoti), jamaa anawaza mkwanja aliokuwa akilamba kila mwezi as Mbunge. Kazi kweli, naamini akirudi CDM atakuwa na fundisho tayari.
Suala ni Kafulila kurudi CDM harafu ukitaka kagombee naye kupitia CDM ukishinda watakusimamisha wewe! usipinge Kafulila kurudi CDM una agenda gani?Kama CDM imewapokea Akina Marando na Josephu Selasin hata ,Chacha Wangwe,kutoka NCcr kwa nini sio Kafulila?Acha wivu wa Mbatia!
 
Mimi ni mwanajeshi kifani. Jeshini tuna kanuni za mapambano. Kanuni muhimu ni kuwatambua askari mamluki. Utawatambuaje? Askari mamluki huwa wanapigana kwa juhudi sana mwanzo wa vita. Lakini wanapoona mmekaribia kupata ushindi wao huanza kuzembea, kurudi nyuma, kuokoa nafsi zao na kuwashambulia askari wenzao. Kwa mfano huu, mtawajua mamluki ndani ya chadema. Zitto kamkaribisha kafulila chadema. Lakini ni zitto huyo huyo hakumshauri kafulila asiondoke chadema. Alimwacha akaondoka na kumsaidia kwa fedha na kampeni hadi akashnda. ????
 
Mimi napendeza hata Hamad Rashid akifukuzwa Cuf akaribishwe CDM kama walivyopokelewa Prof Safari na Lwakatare.Kuendelea kuwakataa watu kutajenga sura Mbaya ya ukanda !
 
Eti hii nayo ni thread. Acha nicheke miee kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwa kwa
 
Mimi napendeza hata Hamad Rashid akifukuzwa Cuf akaribishwe CDM kama walivyopokelewa Prof Safari na Lwakatare.Kuendelea kuwakataa watu kutajenga sura Mbaya ya ukanda !
Kuhusu Hamad Rashid nakubaliana na wewe lakini sio kafulila maana kafulila kuna mchezo amekuwa akicheza na ZZK kwahiyo hao ni watu tofauti.
 
Hii inaweza kuwa thread fupi kuzidi zote zilizoandikwa humu JF...
 
jamani wana CDM,Kafulila hatufai kabisa atatumiwa na CCM kukivuruga chama,hao watu mm nawajua huwa wanlewa sana misifa ni kama ZITTO tu ngugu yake.Ni kupiga chini huyo dogo labda achukuliwe na CUF.
 
Kunguru HAFUGIKI..........NI vyema akagombee cheo cha Kikwete CCM
 
Umesahau pia kuwa aliungana na CUF kuipiga vita chadema kuhusu kambi rasmi ya upinzani? Umesahau yeye na hamad walivyochukua fasta siti pale bungeni kuchukua nafasi baada ya chadema kutoka nje? Labda kama na nyie mko nyuma ya mpango wa Zitto kabwe.
Nakumbuka sana nilikuwa Bongo siku hiyo na sikuamini niloyasikia... Haya ndio matatizo ya Kafulila hupandwa jazba akashindwa kuelewa kwamba Upinzani hata siku moja huwezi kwenda na chama tawala kumwangusha chama kingine kwa sababu zako binafsi..
Lakini naona kajirudi toka katiba mpya yeye na Rashid wamegundua kwamba walikuwa wakitumiwa tu bungeni na kujenga uadui na vyama vingine wakati vyeo wamepeana wao wenyewe..Kafulila na Rashid sidhani kama wako ktk kamati ya bunge hata moja ingawa wao ndio walikuwa wasemaji wakubwa.
 
Chadema kimemkaribisha mbunge huyo kujiunga na chama hicho baada ya kufukuzwa NCCR-Mageuzi. Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe kupitia ukurasa wake wa Facebook alisema: “Kafulila akumbuke kwamba hakufukuzwa Chadema ila alijiondoa mwenyewe”.

"Milango yetu ipo wazi kwa mujibu wa Katiba, Kanuni na taratibu za chama chetu,"alisema Zitto. Hata hivyo, Zitto ameeleza kuwa anaamini NCCR Mageuzi watamaliza matatizo yao kwa mujibu wa katiba ya chama chao na Kafulila atazikabili changamoto hizo kama kiongozi kijana wa kisiasa badala ya kukata tamaa.
"Ifahamike wazi kabisa kwamba David ni mtu huru mwenye mawazo yake na maamuzi yake. Kwamba sisi ni marafiki wa karibu na kwamba tunatoka mkoa mmoja,"alisema na kukanusha taarifa zinazomuhusisha yeye na Kafulila kuhusu mgogoro ndani ya NCCR Mageuzi.

"Napenda kuweka wazi kwamba sihusiki kwa namna yeyote ile na migogoro ya chama kile. Ninaomba nisihusishwe na mambo yasiyonihusu. Ni dhahiri kwamba kuvuliwa uanachama kwa David ni jaribio kubwa kwa mfumo wetu wa demokrasia kama ilivyokuwa huko nyuma wakati kina Erasto Tumbo walipovuliwa uanachama wa chama chao cha UDP."

Zitto alisema haina maana kwamba lolote afanyalo ama Kafulila amemtuma yeye au anahusika na kuongeza kwamba, anaheshimu msimamo wake siku zote na huwa yupo upande wa anayeonewa, kudhulumiwa na mnyonge. "Msimamo huu wa msingi usiwape watu nafasi ya kunihusisha na mambo ya chama dhaifu kisicho na dira kama NCCR-Mageuzi,"alisema.
SOURCE: MWANANCHI YA 20-12-2011
 
jamani wana CDM,Kafulila hatufai kabisa atatumiwa na CCM kukivuruga chama,hao watu mm nawajua huwa wanlewa sana misifa ni kama ZITTO tu ngugu yake.Ni kupiga chini huyo dogo labda achukuliwe na CUF.
Hapana hapa unakosea kwa sababu Kafulila ni mbunge na anahitajika na wananchi wa Kigoma hivyo sio swala la kukifaa chama bali wananchi. Ni wananchi wanaomtaka Kafulila na sii kwamba tunamtaka Kafulila ktk uongozi wa chama.
 
mara karibu milango wazi, mara wamalize migogoro huko NCCR lipi ni lipi hapo!!!!
 
Back
Top Bottom