Hayawi hayawi sasa yamekuwa. Hatimaye mbunge machachari wa kutoka Kigoma, muheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe ameamua kubadilisha dini yake kutoka kwenye uislamu kuelekea kwenye ukatoliki. Vyanzo vya karibu na muheshimiwa Zitto vimeeleza kwamba, sababu ya bwana Zitto kubadilisha dini ni sababu binafsi na wala siyo za kichama kama inavyodhaniwa na wengi. Inasemekana ndugu Zitto ana uhusiano wa kimapenzi na msichana wa kikatoliki ambaye ndiyo chanzo kikubwa cha muheshimiwa huyo kuachana na uislamu na kuwa miongoni mwa kondoo watakaookolewa na bwana yesu. Kama ambavyo bwana yesu alisema kwamba "mimi ndiyo njia ya kuelekea kwa baba", inasemekana kwamba muheshimiwa Zitto amekubaliana na mpenzi wake wamwabudu Mungu kwa kupitia njia hiyo. Ingawa kuna miongoni mwa wakereketwa wa chadema wamesikika wakinung'unika kwamba hii ni janja tuu ya bwana Zitto ili aweze kukwapua madaraka ya juu kabisa ya chamahicho. Chama hicho ambacho kina wafuasi lukuki katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha kimekataa kukanusha au kuthibitisha habari hizi.