Zito abadili dini

Zito abadili dini

Kama amechagua kumfuata Yesu iwe kwa sababu yoyote ile basi kachagua fungu lililo jema tena kwa wakati muafaka. Uliza kwa nini mto wa mbu wakristo wameumizwa na kuharibiwa mali zao. Sio mara chache ukisikia mwislam kakristika waislam wanakuja juu sana, lakini mkristo akisilimu wakristo kimya hawana kelele, maisha ni kama kawa.

Hakuna jipya kwa Kabwe kukristika. Tumwombee kwa Mungu amnyoshee mapito yake na kuwa kioo, afanikiwe katika mambo yake kama katika roho yake. Huyo aliyemfanya akatolike naye Mungu ambariki sana. Kama amefanya hivyo kwa kutumia njia mbaya pia Mungu amhurumie na kumsamehe ilimradi amemrudisha kondoo mmoja zizini.
 
Hii imekaa vibaya,naona watu wamekosa vitu vya msingi vya kujadiliwa hapa katiika jamvi la watu wenye akili zao. Kama ni kweli ama si kweli haina maslahi yeyote kwa jamii ya Watanzania.

Hivyo basi, naomba moderator uifute hii thread haraka iwezekanavyo.
 
Mnaposema chadema ni chama cha kikatoliki
halafu zitto kabadili dini ili apewe uongozi....
Halafu mnasema ni jambo labinafsi lisijadiliwe...

Are you people serious???????????????
 
Sasa atabadili na jinsia....na bado ikabaki kua sio sababu za kisiasa...
 
So What?!?inatusaidia nini kujua dini ya mtu?let us focus on issues na sio personalities!aaaah....acheni hizo
 
Hayawi hayawi sasa yamekuwa. Hatimaye mbunge machachari wa kutoka Kigoma, muheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe ameamua kubadilisha dini yake kutoka kwenye uislamu kuelekea kwenye ukatoliki. Vyanzo vya karibu na muheshimiwa Zitto vimeeleza kwamba, sababu ya bwana Zitto kubadilisha dini ni sababu binafsi na wala siyo za kichama kama inavyodhaniwa na wengi. Inasemekana ndugu Zitto ana uhusiano wa kimapenzi na msichana wa kikatoliki ambaye ndiyo chanzo kikubwa cha muheshimiwa huyo kuachana na uislamu na kuwa miongoni mwa kondoo watakaookolewa na bwana yesu. Kama ambavyo bwana yesu alisema kwamba "mimi ndiyo njia ya kuelekea kwa baba", inasemekana kwamba muheshimiwa Zitto amekubaliana na mpenzi wake wamwabudu Mungu kwa kupitia njia hiyo. Ingawa kuna miongoni mwa wakereketwa wa chadema wamesikika wakinung'unika kwamba hii ni janja tuu ya bwana Zitto ili aweze kukwapua madaraka ya juu kabisa ya chamahicho. Chama hicho ambacho kina wafuasi lukuki katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha kimekataa kukanusha au kuthibitisha habari hizi.
KWANI AKIBAKI KATIKA UISLAMU HAWEZI KUPATA MADARAKA HAYO? KUNA UHUSIANO GANI KATI YA CHEDEMA NA UKATOLIKI?
 
Habari hii ingewekwa kwa macelebrity hapa si mahali. ukitaka kuamini hilo angalia comments za watu uone kama wamecheka.
 
Back
Top Bottom