Ziara ya Samia Mkoani mwanza kugawa zana za uvuvi: Serikali iongeze maeneo ya hifadhi ya mazalia ya samaki na kutenga visiwa vya uwekezaji wa kitalii

chiembe

JF-Expert Member
May 16, 2015
12,003
20,665
Rais Samia atakuwa na ziara mkoani mwanza mwishoni mwa mwezi January 2024.

Namshauri atoe maelekezo kwamba yaongezwe maeneo ya hifadhi ya mazalia ya samaki ambayo yatakuwa na kinga ya kisheria kwa watu kutofanya uvuvi. Kila mkoa ambao ziwa lipo, kuwe na eneo tengefu la mazalia ya samaki, wavuvi wasiguse huko.

Kwa sasa kisiwa cha Rubondo ndicho kinafanya uhifadhi huo, na mahala hapo, samaki huwa wanalindwa dhidi ya uvuvi. Kwa maneno ya waliofika huko, unaweza kukuta samaki wakubwa sana.

Nashauri ziwa liwekewe maeneo zaidi ya uhifadhi ili kufanya hata vifaa anavyogawa viwe na tija ya muda mrefu.

La pili ni kutenga visiwa kwa ajili ya uwekezaji wa kitalii ndani ya ziwa victoria, kama alivyofanya Rais Mwinyi Zanzibar. Hili lifanyike mapema kabla visiwa havijavamiwq na makazi holela. Baada ya hapo itangazwe tenda kwa wawekezaji ambao watajenga mahoteli ya kisasa na kufanya utalii wa ziwa uongeze pato la taifa.

Mwisho, ni ufugaji wa samaki kwa vizimba, walau yatafutwe maeneo maalum, kwa vibali maalum, ufanyike ufugaji wa vizimba ndani ya ziwa chini ya uangalizi wa Wizara ya Uvuvi.

Ifike muda sasa tuache kufukuzana na samaki ziwani, tuwafuge kwa vizimba na mabwawa.
 
Bilashaka kupitia waziri mwenye dhamana ambae kama skosei nae yumo humu ndrani jukwaani , ameskia na amesoma vizur sana ushauri wako mujarabu kabisa kwa mustakabali wa sekta ya uvuvi, samaki na wavuvi wenyewe.

Mama anawapenda sana wavuvi Tanzania, na kwakweli waTanzania wanampenda mno Rais Dr Samia Suluhu Hassan
 
Pia kwenye hotuba ya bajeti ya mwaka huu wizara ya mifugo na uvuvi Waziri Ulega aliongelea kuanzisha mamlaka ya uvuvi itakayosimamia shughuli za uvuvi sijui amefikia wapi au zilikuwa ni siasa tu
 
Bilashaka kupitia waziri mwenye dhamana ambae kama skosei nae yumo humu ndrani jukwaani , ameskia na amesoma vizur sana ushauri wako mujarabu kabisa kwa mustakabali wa sekta ya uvuvi, samaki na wavuvi wenyewe....

Mama anawapenda sana wavuvi Tanzania, na kwakweli waTanzania wanampenda mno Rais Dr Samia Suluhu Hassan
Naam
 
Pia kwenye hotuba ya bajeti ya mwaka huu wizara ya mifugo na uvuvi Waziri Ulega aliongelea kuanzisha mamlaka ya uvuvi itakayosimamia shughuli za uvuvi sijui amefikia wapi au zilikuwa ni siasa tu
Ulega atupatie mrejesho, maana wizara yake ndiyo inasimamia mboga
 
Kuwaweka sawa Wasukuma na balaa la kumnanga mpendwa wao pale alipofariki.

Hatusahau kauli ya Wema hawafi mapema... kauli hii ilitolewa chini ya uratibu wa mgawa nyavu za uvuvi.
 
Rais Samia atakuwa na ziara mkoani mwanza mwishoni mwa mwezi January 2024.

Namshauri atoe maelekezo kwamba yaongezwe maeneo ya hifadhi ya mazalia ya samaki ambayo yatakuwa na kinga ya kisheria kwa watu kutofanya uvuvi. Kila mkoa ambao ziwa lipo, kuwe na eneo tengefu la mazalia ya samaki, wavuvi wasiguse huko.

Kwa sasa kisiwa cha Rubondo ndicho kinafanya uhifadhi huo, na mahala hapo, samaki huwa wanalindwa dhidi ya uvuvi. Kwa maneno ya waliofika huko, unaweza kukuta samaki wakubwa sana.

Nashauri ziwa liwekewe maeneo zaidi ya uhifadhi ili kufanya hata vifaa anavyogawa viwe na tija ya muda mrefu.

La pili ni kutenga visiwa kwa ajili ya uwekezaji wa kitalii ndani ya ziwa victoria, kama alivyofanya Rais Mwinyi Zanzibar. Hili lifanyike mapema kabla visiwa havijavamiwq na makazi holela. Baada ya hapo itangazwe tenda kwa wawekezaji ambao watajenga mahoteli ya kisasa na kufanya utalii wa ziwa uongeze pato la taifa.

Mwisho, ni ufugaji wa samaki kwa vizimba, walau yatafutwe maeneo maalum, kwa vibali maalum, ufanyike ufugaji wa vizimba ndani ya ziwa chini ya uangalizi wa Wizara ya Uvuvi.

Ifike muda sasa tuache kufukuzana na samaki ziwani, tuwafuge kwa vizimba na mabwawa.
Atajisomba mwanza Sana na wala si katavi ,Rukwa,kigoma au njombe. Kanda ya ziwa mnajua kuwashika
 
Rais Samia atakuwa na ziara mkoani mwanza mwishoni mwa mwezi January 2024.

Namshauri atoe maelekezo kwamba yaongezwe maeneo ya hifadhi ya mazalia ya samaki ambayo yatakuwa na kinga ya kisheria kwa watu kutofanya uvuvi. Kila mkoa ambao ziwa lipo, kuwe na eneo tengefu la mazalia ya samaki, wavuvi wasiguse huko.

Kwa sasa kisiwa cha Rubondo ndicho kinafanya uhifadhi huo, na mahala hapo, samaki huwa wanalindwa dhidi ya uvuvi. Kwa maneno ya waliofika huko, unaweza kukuta samaki wakubwa sana.

Nashauri ziwa liwekewe maeneo zaidi ya uhifadhi ili kufanya hata vifaa anavyogawa viwe na tija ya muda mrefu.

La pili ni kutenga visiwa kwa ajili ya uwekezaji wa kitalii ndani ya ziwa victoria, kama alivyofanya Rais Mwinyi Zanzibar. Hili lifanyike mapema kabla visiwa havijavamiwq na makazi holela. Baada ya hapo itangazwe tenda kwa wawekezaji ambao watajenga mahoteli ya kisasa na kufanya utalii wa ziwa uongeze pato la taifa.

Mwisho, ni ufugaji wa samaki kwa vizimba, walau yatafutwe maeneo maalum, kwa vibali maalum, ufanyike ufugaji wa vizimba ndani ya ziwa chini ya uangalizi wa Wizara ya Uvuvi.

Ifike muda sasa tuache kufukuzana na samaki ziwani, tuwafuge kwa vizimba na mabwawa.
Mnagawa baada ya kuwachomea nyavu na mitumbwi yao?
 
Kuwaweka sawa Wasukuma na balaa la kumnanga mpendwa wao pale alipofariki.

Hatusahau kauli ya Wema hawafi mapema... kauli hii ilitolewa chini ya uratibu wa mgawa nyavu za uvuvi.
Wasukuma hawanaga hizo, na JPM hakuwa msukuma
 
Wasukuma hawanaga hizo, na JPM hakuwa msukuma
Wasukuma labda hawajielewi, Jiwe alitaka kujifanya Mhaya ila wakamkataa mepema maana wahaya wanajielewa, ila wasukuma wakaamini kuwa ni mwenzao

 
Back
Top Bottom