Ze Utamu Blog: Ni aibu kubwa mno kwa taifa!

Status
Not open for further replies.
jaamani never trust anyone to take your photo when you are naked, not even your husband trust me. Akikupiga hata picha moja tafuta hiyo simu pasua chini kabisa, yani haribu. Tene maboifrendi ndo usijaribu kabisa
 
Wazee hii ni noma sana watu wazima na kuweka picha za uchi kwenye mtandao ambao hauko protected I SAY NO THEY HAVE TO BE BURNED FOR THIS HATUWEZI KUWAACHIA KIRAHISIRAHISI JAMANI TUSHIKAMANE KATIKA HILI HII NI BALAA KWA WATOTO WETU WANAOTEMELEA MITANDAO HII
 
Wazee hii ni noma sana watu wazima na kuweka picha za uchi kwenye mtandao ambao hauko protected I SAY NO THEY HAVE TO BE BURNED FOR THIS HATUWEZI KUWAACHIA KIRAHISIRAHISI JAMANI TUSHIKAMANE KATIKA HILI HII NI BALAA KWA WATOTO WETU WANAOTEMELEA MITANDAO HII
 
Naomba namba ya clouds, kupiga simu/msg au email kipindi cha leo tena niwaambie wawaonye.
 
Naomba namba ya clouds, kupiga simu/msg au email kipindi cha leo tena niwaambie wawaonye.

Tena fanya kuwakumbushia kwa sababu bafikiri ugomvi kati ya huyo TK na Mange uliandikwa na gazeti moja la udaku last week kama sikosei.. yaani ni uchafu tu. Sikumbuki ni gazeti gani but niliona picha zao kwa mbali wakiwa wamepigwa na wazungu wao... kichwa cha habari sikumbuki kilikuwa ni nini.

Halafu tunalalamika Tanzania masikini!! utajiri tutautoa wapi wakati muda mwingi tunatumia kufanya maroroso badala ya kuzichanga?
 
Nimesoma all the posts, nakudodosa kiduchu kwenye hizo blogu jamani, hizi laana tunazipeleka wapi kama nchi...?? maendeleo tutapata wapi wakati watu wako busy kuchafuana?
 
kweli CottonEyeJoe, ni risk, kupublisize zaidi. Sijui tufanyeje, natamani ifutike leo sasa hivi!!
 
Last edited by a moderator:
kweli cottoneyejoe, ni risk, kupublisize zaidi. Sijui tufanyeje, natamani ifutike leo sasa hivi!!

...Kama unaweza una i hack blog, au unapeleka mashambulizi ya Virusi tu, 'aliyekuwemo na asiyekuwemo', atayefungua hizo blog naye analizwa
 
Jamani ongeeni taratibu wasisikie wakahamia huku.

Binafsi napata kichefuchefu kusikia habari hizo.

Any way kila kitu kina wafuasi maana hata siku ya kiama kuna watakaofuata makao ya shetani.\

AIBU AIBU AIBU
 
Katika mambo ambayo sikuweza fikiria hata wanajamii ya kwetu kuanza haya mambo hata sijui kulikoni,matumizi mabaya ya vyombo na hawa watu wanao fanya haya mambo sio mabumbuwazi lazima wawe wenye akili ila tu ustaarabu,heshima,utu na hekima hakuna kabisa,mbona wao kama wenye blog hawajiweki katita mauchafu hayo!!!
 
Dada/Mama WomanOfSubstance afadhali umeiweka habari hii kwa mtindo huu, Kuna mwanachama mmoja (mwanamama) aliiweka hapa wiki iliyopita, Lakini ilikaa kwa mtindo ambao haukuwa mzuri kuichangia, nami ndio nilipata muda wa kupita huko kuangalia kilichoandikwa/bandikwa. Kwa ukweli niliogopa na kushindwa kuamini kwanini tumefika hapo. Nimeona baadhi ya picha/ majina ya watu ninaowafahamu na ambao najua wazi kuwa hawana tabia hizo za ujinga.

Kwa vyovyote itakavyokuwa,hata kama mtu anafanya umalaya na ujinga, lakini si ustaarabu kumbandika kwenye blog bila idhini yake,kwa mtazamo wangu,nafikiri hatufundishani kwa Mtindo huu, Jamii ya wastaarabu ina namna ya kutatua matatizo yake kwa njia za ustaarabu zaidi kuliko hizi tunazoziona sasa.

****Kumbukeni hawa tunaowaumbua humu ni ndugu na Dada zetu.... Kwa taarifa tu wanaoendesha blog hizi wanatafutwa na mwenye blog mojawapo amekwishafahamika,na wanaohusika wanafanya naye mawasiliano,ni wazi kuwa baada ya muda mfupi Blog hizo hazitokuwa hewani.

Lakini kwa namna yoyote itakavyokuwa Watanzania wenzangu tujaribu kujenga Jamii yenye Heshima na Ustaarabu...Hata kama una matatizo na mtu tafuta njia muafaka ya kutatua matatizo yenu bila kuyaweka wazi kwa watu yasiyowahusu..Naamini wengine waliotukanwa kule ni wanachama hapa....Jaribuni kuangalia upya mienendo yenu,kwa sababu maneno yaliyosemwa huko si mazuri,na kwa mtazamo wangu hamuwezi kuyakanusha yote.

Tujirekebishe na tujaribu kuheshimiana na kuheshimu privacy za watu.Hakuna mtu aliye mkamilifu,kila mtu ana mapungufu yake. Tukubali ushauri na kuomba misamaha pale tunapowakwaza wenzetu.Hiyo tu ndiyo itakayotufanya tuishi kwa amani na furaha. Nimesikitishwa mno na Blogs hizo, nami pia kama mwana-adam inabidi nijifunze kumjua bin-adam yupi ni ni rafiki wa kweli na yupi ni hasidi....

Hapa Forum kama Familia moja, Tujiunge kwa pamoja kukemea Tabia hizi mbovu...Naomba kutoa hoja.
 
Last edited by a moderator:
Watanzania bwana hatueleweki.....hivi tatizo ni nini kwenye blogs zile? ni mwenye blog au aliepiga picha za utupu....twende mbeel turudi nyuma yanayosemwa mule kuna ukweli ndani yake...

na wanajuana vizuri watoa maoni mule.....sasa nyie mnataka nini? ni bora waanikwe ili wajirekebishe au waachwe waendeleze libeneke na kusambaza virusi?
 
Watanzania bwana hatueleweki.....hivi tatizo ni nini kwenye blogs zile? ni mwenye blog au aliepiga picha za utupu....twende mbeel turudi nyuma yanayosemwa mule kuna ukweli ndani yake...

na wanajuana vizuri watoa maoni mule.....sasa nyie mnataka nini? ni bora waanikwe ili wajirekebishe au waachwe waendeleze libeneke na kusambaza virusi?

View point yako itabadilika haraka sana siku ukifungua hiyo blog ukakuta picha ya mwenza au dada iko hapo.
 
View point yako itabadilika haraka sana siku ukifungua hiyo blog ukakuta picha ya mwenza au dada iko hapo.
Tena ntafurahi sana maana itakuwa imenirahishia matatizo.....
lol kumbe tatizo ni kuwaona ndugu zenu?...... tusiwe wanafiki
 
...haya sasa, mnaona vijembe vya 'utamulicious' wa kujing'ata ulimi vilivyo infectious!? ...Mwezi Mtukufu huo upo kona jamani, wengine tushaanza swaumu ya mfungo wa Shaaban, Calm down buddies.
 
Tatizo Kubwa Nililoliona Mimi Katika Wavuti Hizo Ni Mabadiliko Ya Mtindo Wa Maisha Yanayotokana Na Umri Yaani Kukua Na Mabadiliko Ya Mazingira.

Nia Na Madhumuni Ya Mungu Kumuumba Binadamu Kabla Binadamu Hajamkosea Mungu Ni Kuwnadamu Aishi Kwa Raha Mstarehe Bila Msongo Wa Mawazo Yanayotokana Na Shida Za Kila Siku. Baada Ya Binadamu Kumuudhi Mungu Ndipo Tulipojikuta Tunataabika Kwa Shida Mbalimbali katika Jitihada Za Kujikwamua Kwa Shida Zinazotukabili Hasa Hili La Msongo Wa Mawazo Kujiburudisha Kwa Njia Mbali Mbali Ndio Kumekuwa Mkombozi Wetu. Kiuhalisi Amri Kumi Za Mungu Hatuwezi Kuzitimiza Tunazivunja Vunja Kila Siku Huku Mungu Akitusamehe Marasaba Sabini. Mkombozi Wetu Ni Amri Kuu Kuliko Zote Yaani Upendo.

Kutopendana Kwetu Ndio Zambi Yetu Kuu. TukifaniKiwa Kupendana Ndio Chanzo Cha Mafanikio Ya Maisha Yetu Hapa Duniani. Tukipendana Kwa Dhati Na Kweli Minyororo Yote Ya Chuki Na Hasira Itafunguka. Tukiwa Na UhaKika Na Usthibitisho Pasipo Shaka Kweli Hatupendani, Kila Mtu Anajijengea Himaya Yake Ya Kujipenda Mwenyewe.

Mungu Hadanganywi Anakuona Popotena Chochote Ufanyacho.ni HerI Umfiche Mungu Ubaya Wako/Mazowea Yako/tabiayako Kuliko Umfiche BINADAMU MWENZAKO. Kweli Kuna Wenzetu Wanampenda Mungu Mambo Yao Wanaweka Hadharani Hamfichi Mtu, Moyo Wake Safi Kwa Mungu Anasema Uzuri Wangu Ni Wakujivunia Uumbaji Wa Mungu.wengine Uzuri Wao Ni Wa Gizani Na Kujivunia Unafiki Wa Shetani, wengine Walifikiri Ukiwa Na Ukame Ukienda Pale Mteremko Wanakutana Na Mlima Basi Wanaporomosha Matusi Na Kashfa.Ishi Kwenye Mwanga Kama Uko Kweye Giza Na Ishi Kwenye Giza Kama Uko Kwenye MwanGa.

Kuwa Wewe Usiwe Na Wasifa Tofauti. Furahia Uhuru Wako Kikamilifu; kila Kitu Kiko Juu Yako Wewe Na Mungu Peke Yenu Wawili.
 
Baada ya kuchungulia kwenye mojawapo ya hizo blogs (I didn’t have enough guts to go to the second one) nimesikitishwa sana na niliyoyaona

Ndio inawezekana kuna wengine wanapenda picha zao ziwepo mle ndani kwa sababu wanazozijua wenyewe, lakini ni wazi kabisa kwamba wapo vilevile ambao ni victims tu….

Kwenye hizo picha wengine wanaonekana kabisa wamelewa…wachangiaji wengine hapo juu wamedodosa jinsi picha zinavyoweza kufanyiwa editing na watu wengine…

Vile vile sidhani kila mmoja aliyepigwa picha / aliyetoa picha kwa ridhaa yake anajua wazi kabisa kwamba itawekwa mtandaoni na picha mtandaoni maana yake ni picha hadharani yaani mtu yeyote mahala popote duniani anaweza akazitizama…,

Inaonekana mle picha zinabandikwa tu na story zinaandikwa tu, yaani kama nina chuki binafsi na mtu naweza kuiba picha yake.. hata kama ka pozi kawaida tu na amevaa nguo zake,.. nikatunga udaku wangu au nikaongeza chumvi na pilipili kwenye udaku niliosikia mtaani,.. nikabandika mle, kwisha habari!

Kumuua mtu sio tu kumtoa roho, kufanyiana hiyana kama hizo nako ni kuua jamani

Hivi kweli vyombo vya usalama havina habari na hii ishu au? Watu wa usalama wa taifa humu JF saidieni jamani!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom