Kumbuka kuna miungu zaidi ya 3000. Unataka story ya mungu yupi nikwambie kaanzia wapi?
Ni kama siku hizi tu story zinaanza polepole za mtu zinaanza kukuzwa, chukulia mfano Elon Musk, na mambo yake ya kutaka kupeleka watu Mars, kuweka renewable energy sources kwenye kila nyumba, its science leo tunaelewa hivyo, ila kuna kikundi cha watu wachache wanamuona jamaa kama mwokozi vile, story zinasambaa polepole, zinakuzwa, inafika muda watu wanaanza kuzikisia zimekuzwa kweli utadhani jamaa kageuka mungu anataka kukomboa wanadamu, sasa kwa leo unaweza ona upuuzi maana tumeendelea, ila miaka elfu kadhaa nyuma, hata kipaji cha kawaida tu mtu unaonekana very extraordinary, people were ignorant ukilinganisha na leo. Soma biblia na quran uone vifungu vinavyopingana mule, anayesema vinaongelea amani namshangaa sana, maana vimejaa utumwa, ukandamizaji wa wanawake, mauaji, tena in plain direct text.
Ungezaliwa alafu usijazwe dini kichwani ukaachwa hadi ufike umri wa mtu mzima tuseme miaka 20, alafu ukaanza kuambiwa kuna mungu, mtu aliyetenganisha bahari kwa fimbo, ungeamini kweli? hehehe