Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Status
Not open for further replies.
Ahaaa,kwa hiyo nani aliwaumba wanadamu?????.
Mkuu tukianza argument ya nani kaumba nani hatutafika mwisho maana maswali mengine kwa sasa hatuwezi yajibu, nikisema hakuumbwa na kiumbe chochote ukagoma ukasema ni mungu nikiuliza mungu kaumbwa na nani utanijibu?
Ukijibu hakuumbwa then kwa nini isiwe same thing kwa binadamu?
 
Wewe umefunga.... Mwenzio anakula inakuuma nini...?? Hivi hawa ndugu zetu kama wana wakristo wanaishi nao watawaruhusu kula kweli? Au ndio ukiajiliwa au kuishi na muislam lazima ufate matakwa yake ya kidini...



Ukila unawatamanisha na wao wanaweza kuvunja ramadhan.,, Unaijua njaa au unaiskia??

Njaa mbaya inaweza kukufanya ukaiba., ama ukafanya chochote cha ajabu., Ndo wanachokwepa nahic.,, KUTAMANISHWA.
 
mimi niulize tu.. tena kwa nia nzuri kabisa
hivi huyu Mungu wawaislam nilazma atetewe kwa kila jambo yani, hata hili la hiari (kufunga) pasipo hata hiyana mnalazimishana na kuekeana sharia, kufunga naamini ni jambo la kiroho na ktk roho hamna shurti na kama ipo ni sawa na kumlazimu mtu kunafki na kufanya uongo... imani iliyo kamili haina kusukumana hii ya kusukumana ni utumwa tu au nyie ni wa tumwa wa dini maana hata sisi ni watumwa wa Yesu aliye hai ndio maana tu watii na weledi kwake hasa kwa hiari na kuvunjika moyo. Nyie embu badilikeni majini yenu, magaidi yenu na hata wabakaji wa mtoto wa miaka 6 wenu na wanawake wenye mimba hata majambazi yakikamatwa kama lile la juzi utasikia alakibaru..!! afu badae mnamfata shetwani maka kumpiga mawe mbona hafagi mkaacha mazambi yenu , ajabu sanaaa.
 
Hii haikubaliki! Kama Zanzibar imekuwa nchi ya KIISLAM itangazwe wazi tufaham
 
Unachokisemea Mkuu ni kitu kilishazoeleka miaka nenda miaka rudi,na hata wakristu wa Zanzibar wanakiona ni sehemu ya sheria,msiingize mambo ambayo hayapo jamani kama hujui ni bora kuuliza wanaojua zaidi utapewa sababu
Nini nachotakiwa kujua hapa? Nimuulize nani anayejua? Kwani msingi wa hoja ni nini? Sheria inasemaje hapa? Wewe unayejua niambie ni sheria ipi inayosema kuwa ukila hadharani mwezi wa Ramadhani ushitakiwe? Si suala la mazowea bali sheria, lazima ujue kuna minority ambao lazima sheria iwalinde pia.
 
Duniani hakuna haki na usawa haki na usawa vipo mbinguni. hizb wamekatwazwa kufanya kongamano lao la wazi la kidini la kuukaribisha mwezi kwa kigezo kuwa ni kikao cha siri, zanzibar wamekataza kula mchana kwa kigezo kuwa ni utaratibu wa nchi hiyo toka enzi na enzi za mababu. Tunachojifunza matakwa ya wengi huwa yanafwatwa zaidi ukichunguza kwa undani kuliko matakwa ya wachache katika eneo husika.
 
Labda mimi ndio sijui hv zanzibar ina endeshwa na sheria za dini ya kiislaam???
 
Tangu lini kula limekuwa kosa LA jinai? Kwani kufuata IMANI ya dini Fulani ni lazima? Kifungu kipi cha sheria atakachoshitakiwa mtu kula hadharani!
Nini maana ya kula hadharani? Je hotelini ni sehemu inahesabika kuwa ni hadharani?
Je kufungua hoteli ili kuhudumia wasio waislam au waislam walioamua kutokufunga ni kosa?
Kwani mtu mzima kumwona mtu anakula kuna tatizo gani?
 
Yaani nimebanwa kiu ya maji nisinywe hadharani! Basi MAJI na juice zisiuzwe hadharani!
 
basi Zanzibar iitwe Islamic State Of Zanzibar, imani sio kupelekeshana.... so hao wasiokuwa waislam waishi katika hali gani angali mfungo hauwahusu?
 
Ukiona mambo ya Mungu yanalazimishwa kwa mtutu wa bunduki jua hapo kuna unafiki mkubwa. Kuna watu wengi sana watashinda njaa wala si kufunga.
Mambo ya imani yanatakiwa yawe ya hiari na ndio Mungu anakubali hilo jambo. Wao wakazane kuelimisha jamii yao umuhimu wa kufunga Ramadhani na thawabu zake, halafu wawa ache wale watu wafanye uamuzi, maana ukiweka sheria ya kudhibiti atakayeonekana hajafunga, bado hujamsaidia mtu yule ambaye alitaka kula lakini ukamtisha au ukafunga hoteli. Hiyo ni logic amabayo wala haitaji ubishi.
Hajazuiwa mtu kula na serikali hata akiwa muislam na ale lakini asile hadharani hukumu ya kutokufunga ni kati yake na mungu wake kwani wangapi hawafungi lakini wanakula ndani huku nje wanaonyesha kama wamefunga na hakuna mtu anayejua isipokuwa mungu anajua yote
 
mimi niulize tu.. tena kwa nia nzuri kabisa
hivi huyu Mungu wawaislam nilazma atetewe kwa kila jambo yani, hata hili la hiari (kufunga) pasipo hata hiyana mnalazimishana na kuekeana sharia, kufunga naamini ni jambo la kiroho na ktk roho hamna shurti na kama ipo ni sawa na kumlazimu mtu kunafki na kufanya uongo... imani iliyo kamili haina kusukumana hii ya kusukumana ni utumwa tu au nyie ni wa tumwa wa dini maana hata sisi ni watumwa wa Yesu aliye hai ndio maana tu watii na weledi kwake hasa kwa hiari na kuvunjika moyo. Nyie embu badilikeni majini yenu, magaidi yenu na hata wabakaji wa mtoto wa miaka 6 wenu na wanawake wenye mimba hata majambazi yakikamatwa kama lile la juzi utasikia alakibaru..!! afu badae mnamfata shetwani maka kumpiga mawe mbona hafagi mkaacha mazambi yenu , ajabu sanaaa.
Yote uliyosema ni chuki zimekujaa ila kuna moja umelisahau la kuhalalisha kuoana wanaume kwa wanaume hivi Yesu ndio aliwafundisha hivyo?Tena na vyeti munapeana hivyo mutajazaje ulimwengu
 
Wangeamua kwamba kila mhitimu was shahada ya uhandisi,abuni,au atengeneze kitu,au mfumo utakaosaidia jamii,wangefika mbari,
Haya mambo ya dini,ndio yanayoturudisha nyuma watu weusi
 
Mkuu tukianza argument ya nani kaumba nani hatutafika mwisho maana maswali mengine kwa sasa hatuwezi yajibu, nikisema hakuumbwa na kiumbe chochote ukagoma ukasema ni mungu nikiuliza mungu kaumbwa na nani utanijibu?
Ukijibu hakuumbwa then kwa nini isiwe same thing kwa binadamu?[/QUOMbona unababaisha sasa,inaonesha unaishi bila kujifahamu,na wala hufai kuitwa binaadamu,Kwa sababu unaukataa ubinaadamu,ina maana wewe Ni kiumbe tu,au sio.mbona sasa unajiita binaadamu,na asili ya neno hili haikuja kibahati mbaya,Kama zinavyoamini dini tatu kubwa za Jews,Christianity na Islam kutoka katika vitabu vyao Adam ni kiumbe wa kwanza kuumbwa,aliyepelekea kuwepo kwa wanaadamu hivi sasa,sasa falsafa yako wewe ipi,katika ufahamu wako wa hawa viumbe wanaoitwa binaadamu.wewe unasema usiniletea hayo,kwanza tusimuuingize Mwenyenzi Mungu,ambaye hatumuuoni ,tuanzie kwa binaadamu anayefanana na wewe ,Kwa mimi ninavyoamini,sio wewe unavyoamini,kwamba ametokana na Adam.ideology/falsafa yako wewe ni nani???,na unaweza kubahatisha umetokana na nini??.
 
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) imetoa onyo kwa wananchi watakaokula hadharani katika kipindi cha mchana wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma, Khamis Juma Maalim wakati akijibu swali la mwakilishi wa jimbo la Paje, Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua serikali inatoa tahadhari gani kwa watu watakaobainika kula mchana wakati wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Alisema utamaduni wa wananchi wa Zanzibar ni kuheshimu kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa makundi yote ikiwemo wa dini tofauti. Alifahamisha kwamba utamaduni huo upo hata kabla ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964 wa dini tofauti kuheshimu dini za watu wengine.

Alisema kazi ya kutoa elimu kuhusu ujio wa mwezi mtukufu wa Ramadhani imeanza kutolewa na Ofisi ya mufti ambayo ndiyo yenye jukumu la kushughulikia masuala ya mambo ya dini ya Kiislamu.

Alisema kazi kama hiyo imeanza kutolewa na maimamu wakuu wa misikiti mbalimbali Unguja na Pemba ikiwemo katika sala za Ijumaa ambazo hukusanya idadi kubwa ya Waislamu kwa wakati mmoja.

Alikiri kuwepo vijana wengi wanaoacha kufunga katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na kula hovyo pamoja na kuvuta sigara. Maalim alisema zipo taarifa kwamba hoteli nyingi hufanya kazi wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo wateja wake wakubwa ni vijana wa Kiislamu. Waislamu nchini wanatazamiwa kuanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wiki ijayo ambapo ibada ya funga ni moja ya nguzo tano za dini ya Kiislamu


Chanzo: Habari Leo
=====================================
Nataka kujua kipindi kwa kwaresma mbona hawakutoa tamko hili.

Kwaio wakristo wawe wanajificha wakati wa chakula cha mchana.

Hapana naona kuna harufu ya udini kuanza Zanzibar.
Uislaamu unaishi kwa nguvu za vitisho.

Vijana wa kisasa hawana mpango ila wanalazimishwa tu.
 
Wangeamua kwamba kila mhitimu was shahada ya uhandisi,abuni,au atengeneze kitu,au mfumo utakaosaidia jamii,wangefika mbari,
Haya mambo ya dini,ndio yanayoturudisha nyuma watu weusi
Kwa nini wewe umebeba bendera ya uyahudi??na wewe ni mtu mweusi,una mapenzi gani bendera hiyo???au na wewe una mambo ya dini.
 
Hawawezi kufunga ndio maana serikali inaamua kuwasaidia kwa kufunga mpaka mikahawa yote, kama sio hivyo wote wangekula.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom