Zanzibar Nchi au?

Zanzibar Nchi au?

thepresidar

Member
Joined
May 6, 2011
Posts
34
Reaction score
6
Jamani mi mwananchi wa kawaida nisaidieni,Hivi napo toka visiwa vya Unguja kuja tanganyika Napofika pale Bandari salama nikalipishwa ushuru wa kifa au bidhaa nlonunua huko visiwani Hii ina maana gani ukizingatia nchi hii ni moja,kwa mana nyingine kule ni mkoani zanzibar.ka sipo sahihi basi tuweke na wachukua mapato mikoa mingine yani ukinunua TV Dar ukifika Songea unatozwa ushuru,umenda bagamoyo umeleta samaki ukifika mwenge pale watu wachue kodi....What a joke of a country
 
Zanzibar sio nchi,Nchi ni TANZANIA TU BISHA HADI KESHO UKWELI NDO HUU, tatizo liko kwenye sheria zinazokufanya ulipie kodi.
 
Ni mkoa tu wa Tanzania ila upo kwenye karantiki sababu ya ujeuri wa wakazi wake. Mkuu wa mkoa wa huko ana makamu wawili na baraza kubwa la madiwani linaloitwa baraza wa walalamishi
 
Katiba inasema Zanzibar siyo nchi ila ni sehemu ya Tanzania.
 
kwa kifupi.....tuuu

zanzibar.....ni nchii tokea kipindi cha mkoloni.......ila ilipofika mwaka 1964.....nchii itwayoo tanganyika raisi wake
alimuomba raisi wa zanzibar waungane....ili wawe na taifa moja.....lililoitwa tanzania.......

ila tokea taifa liiitwe tanzania.....nchi ya tanganyika jina lake lilikufa....mpaka leo halisikiki....ila zanzibar jina lake bado lipo....
 
Zanzibar sio nchi,Nchi ni TANZANIA TU BISHA HADI KESHO UKWELI NDO HUU, tatizo liko kwenye sheria zinazokufanya ulipie kodi.[/QUOTE
MKUU TANZANIA NI JAMHURI YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR BILA YA ZANZIBAR HAKUNA TANZANIA....1963 KULIKUWA HAKUNA NCHI DUNIANI INAYOJULIKANA KWA JINA LA TANZANIA

MIMI NI MTANGANYIKA NA SITOJARIBU KATIKA MAISHA YANGU KUWASALITI MABIBI NA MABABU ZANGU NITA PROUD NA UTANGANYIKA WANGU KAMA WAZANZIBARI WANAVYO JI PROUD NA UZANZIBARI WAO

CECAFA-2012-Group-Stage.jpg
HUU NI USANII TOKEA LINI NCHI YETU YA TANGANYIKA ILIBADILISHWA JINA BILA YA SISI WATANGANYIKA KUJULISHWA?

HAKUNA NCHI ILIYOPEWA UHURU KWA JINA LA TANZANIA NCHI YETU TULIPEWA UHURU 1961 KAMA WATANGANYIKA
nyerere_speaking.jpg

SIKU HII NDIO SIKU TULIYOPEWA UHURU WETU WA TANGANYIKA
uhuru-wa-tanganyika-09-12-1961-mwalimu-julius-kambarage-nyerere.jpg

1961 UHURU WA TANGANYIKA 1963 KULIKUWA STILL BADO HAKUNA NCHI INAYOITWA TANZANIA
1961-Uhuru-Day-in-Karimjee-Hall.jpg
SHEREHE ZA MWANZO ZA UHURU WA TANGANYIKA 1961 AT KARIMJEE HALL

SASA IMEBAKI TUNAFANYWA KAMA MAPIMBI TUNADHARAULISHWA KATIKA DUNIA HII KWA VILE GENARATION HII KILA MTU ANAJUWA HISTORIA YA DUNIA:sleepy:
 
Jamani mi mwananchi wa kawaida nisaidieni,Hivi napo toka visiwa vya Unguja kuja tanganyika Napofika pale Bandari salama nikalipishwa ushuru wa kifa au bidhaa nlonunua huko visiwani Hii ina maana gani ukizingatia nchi hii ni moja,kwa mana nyingine kule ni mkoani zanzibar.ka sipo sahihi basi tuweke na wachukua mapato mikoa mingine yani ukinunua TV Dar ukifika Songea unatozwa ushuru,umenda bagamoyo umeleta samaki ukifika mwenge pale watu wachue kodi....What a joke of a country

Hadithi njoo ....paukwa..pakawa...watoto wanaitikia....hapo kale kulikua na nchi 2 jamhuri ya watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika ambazo zilikua zikiongozwa na serikali 2 ya Mapinduzi Zanzibar na ya Jamhuri ya Tanganyika....
mwaka 1964 serikali hizo zikaamua kuungana....yaani serikali mbili...(2) ..ile ya Tanganyika na ya Mapinduzi...ikaungana na kuamua kufanya serikali mbili(2) ....zijulikanazo kama serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
serikali ya Tanganyika ikawekwa ndani ya hiyo ya Tanzania na ile ya Mapinduzi ikaendeleo kuwepo...hivyo kilichobadilika kwa Tanganyika ni jina .....ila serikali iliyopo ina fanya kazi kwa niaba ya Tanganyika...
sasa jee nchi zenyewe ilikuaje?.....baada serikali kuungana Zanzibar wakabaki mpaka leo kama nchi ya Zanzibar.....nchi ipo...lakini tanganyika wao wameamua jina lao liwe Tanzania.....ila sasa hawa Zanzibar wamewapa Tanganyika kazi za kuwalinda, kuwapa kiti chao UN...na kwengine...
kwa hio utaona tumeungana nchi mbili tukabaki na nchi mbili..na pia tumeungana serikali mbili na kubaki na serikali mbili.....hichi ni kizungu mkuti cha 1+1=3
 
HIVI NDIO WENZETU WANAVYOJIVUNIA NA PROUD NA UZANZIBARI WAO

Khamis-Mcha-wa-Zanzibar-akishangilia-goli.jpg
KenyaZanzibar-300x208.jpg
images

DSC+0078.jpg

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Uchumi na Mipango ya Maendeleo,katika utekelezaji wa kazi za Wizara hiyo katika Ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Zanzibar ( kulia) Makamo wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharif Hamad,na Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi,pia Katibu Mkuu Kiongozi Dk.Abduhamid Yahya Mzee,(kushoto).[Picha na RamadhanOthman,Ikulu.

IMG_0292.jpg

Rais Wa Zanzibar Dk Ali Shein Ashiriki Mahafali Ya Saba Ya Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA)Nakumtunuku Shahada ya Uzamivu ya Heshima ya Chuo Kikuu Cha Taifa SUZA Rais Mstaafu wa Zanzibar Dk Amani Abeid Karume,wakati wa sherehe za mahafali ya 7 ya chuo hicho.
IMG+++0103.jpg


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akiwa na ujumbe wake wakiongozwa kwa gwaride maalum wakati alipowasili katika kumbusho wa Baba wa Taifa la Vietnam, Ho Chi Minh Mousoleum,kuweka shada la mauwa,akiwa katika ziara rasmi ya Kiserikali,ya wikimoja.[Picha na Ramadhan Othman,Vietnam.]
 
zanzibar ni nchi ambayo haina uhalisia kwasababu bado wapo chini ya Tanzania kimataifa. ni nchi jina tu, lakini katika utendaji haijakamilika asilimia mia moja kuwa na utendaji wa nchi. mfano; uwakilishi wa UN, mabalozi nchi za nje n.k, ni muhimu tukaulinda muungano na kutatua utata huu wakati huu wa katiba mpya, na tuamue kunyoa au kusuka kama last resort.
 
Back
Top Bottom