Meja Jenerali Isamuhyo
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 3,103
- 9,585
Wakuu kwema…
Tuwape elimu ndogo vijana wa sasa kuhusu namna baadhi ya huduma zamani ilibidi upange foleni kwa kufika ofisi husika ili uhudumiwe.
1. Luku
Ili upate huduma ya kununua umeme (luku) ilikuwa lazma ufike kwenye ofisi za Tanesco. Baadae wakaongeza huduma kwenye baadhi ya vituo vya kuuzia mafuta (sheli).
Yaani unaenda kununua umeme jioni, unakuta foleni ndefu na hapo ombea network isisumbue mtalala giza kwenu.
2. Malipo ya DStv lazma uende ofisini kwao.
Miaka hiyo nakumbuka mzee akienda kulipa DStv kule Kinondoni Makaburini zilipokuwa ofisi pekee za Dstv kwa Tanzania nzima. Ikishalipiwa kule anapiga simu kuuliza vipi chaneli zimefunguka, kabla hajatoka ofisi zao.
3. Simu za TTCL za mezani
Malipo lazma uende ofisini kwao.
Nilichokuwa napenda kuhusu TTCL ni kuwa walikuwa wanatoa vitabu vyenye namba za simu zote nchi nzima. Ulikuwa ukiwa na shida na mtu unatafuta jina lake kwenye kitabu cha TTCL unakuta namba zake unampigia.
4. Malipo ya Maji NUA baadae
Ukiletewa ankara ya maji basi utalazimika kufunga safari kwenda ofisi zao zilipo ili uweze kufanya malipo.
Huduma gani imesahaulika? Ongeza
Tuwape elimu ndogo vijana wa sasa kuhusu namna baadhi ya huduma zamani ilibidi upange foleni kwa kufika ofisi husika ili uhudumiwe.
1. Luku
Ili upate huduma ya kununua umeme (luku) ilikuwa lazma ufike kwenye ofisi za Tanesco. Baadae wakaongeza huduma kwenye baadhi ya vituo vya kuuzia mafuta (sheli).
Yaani unaenda kununua umeme jioni, unakuta foleni ndefu na hapo ombea network isisumbue mtalala giza kwenu.
2. Malipo ya DStv lazma uende ofisini kwao.
Miaka hiyo nakumbuka mzee akienda kulipa DStv kule Kinondoni Makaburini zilipokuwa ofisi pekee za Dstv kwa Tanzania nzima. Ikishalipiwa kule anapiga simu kuuliza vipi chaneli zimefunguka, kabla hajatoka ofisi zao.
3. Simu za TTCL za mezani
Malipo lazma uende ofisini kwao.
Nilichokuwa napenda kuhusu TTCL ni kuwa walikuwa wanatoa vitabu vyenye namba za simu zote nchi nzima. Ulikuwa ukiwa na shida na mtu unatafuta jina lake kwenye kitabu cha TTCL unakuta namba zake unampigia.
4. Malipo ya Maji NUA baadae
Ukiletewa ankara ya maji basi utalazimika kufunga safari kwenda ofisi zao zilipo ili uweze kufanya malipo.
Huduma gani imesahaulika? Ongeza