Zamani ilikuwa raha

Zamani ilikuwa raha

hizi hadithi zilikuwa zina mafunzo makubwa

nimewakumbuka Mr & Mrs Daudi, Baraka na Neema na Neema atakuwa ameolewa sasa
Musa ameshakuwa babu, Neema yupo zake kijijini ni mwalimu mkuu shule ya msingi, anakaribia kustaafu sasa, Baraka ndo anasoma masters yake UK, akirudi tu atapewa unaibu waziri kama JK bado atakuwa madarakani.
 
Wakuu mie nimelimiss jarida la Bongo lilikuwa linatoka mara 1 kwa mwezi!
 
Ivi humu watu kila mtu was zamani?.... Kuna mwingine zamani yake Jana..you are so funny guys
 
mchakamchaka mnakimbizwa na mgambo huku mnaimba:

Jua lilee literemke mama; aiyaiya iya iya mama ...

Na ule wimbo mwingine wa kambona ameolewa na mwingereza mnaukumbuka?
Those days bwana, ilikuwa safi sana.
na jkt
tuliimba....
Bibi mweupe si mali
kiitikio:mama jenga
amefanyiwa mkeka
kiitikio:mama jenga
wa kuchezea kamari
kiitikio:mama jenga
mwenye kupata apate
kiitikio:mama jenga
mwenye kukosa akose
kiitikio:mama jenga

na wimbo mwingine ulikuwa
..... Frelimo eeeh
frelimo eee
.............
 
Nondo mla watu, kibanga ampiga mkoloni, brown ashika tama

vitabu vya someni kwa furaha,
bulicheka na mkewe lizabeti, Nunda mla watu, Uza ghali usiuze rahisi, vitabu vya alfu lela ulela, adili na nduguze, vingine kama paul ana mikono michafu, mandawa na manenge, tola usile gizani,
 
kokolikoo, maxi priest, athumani digadiga, (na huyu wa juzi super faby na queen vero)
bila kumsahau..............
Dj kali kali
kali kitii
nikicheza mwafurahi sana
basi mtambo zima taa
yoo baadae!
 
Watu wa zamani mlipata shida sana. Sijui hata mlikuwa mnatongozaje wakati kulikuwa hakuna simu... Inawezekana pia mlikuwa mnachapiana sana.. Na ndio pengine mkafikia hatua ya kutunga ule msemo kuwa "kuchapiwa ni siri ya ndani"
hivyo ni vijisemo vyenu tu watoto wa siku hizi,
Enzi hizo hakuna wivu wa kijinga, kwa sisi machalii wa Enzi hizo ukimtongoza demu akikukubalia ukienda kusarandia unamuunganisha na best yako wa karibu nae aonje utamu,
unakuta mdingi kaoa kamuacha mke kijijini labda kaenda Nairobi, Mombasa, Tanga, Arusha au Dar anakaa huko miaka miwili akirudi anakuta mkewe ana mtoto wa miezi 4 wala haulizi anamlea tu kama wa kwake, na kawaida wazee wa Enzi hizo akirudi kabla hajafika nyumbani anatuma mtu apelike mizigo kama ishara kuwa mwenye mali amekuja wale wakudandia wasifike tena,
 
hivyo ni vijisemo vyenu tu watoto wa siku hizi,
Enzi hizo hakuna wivu wa kijinga, kwa sisi machalii wa Enzi hizo ukimtongoza demu akikukubalia ukienda kusarandia unamuunganisha na best yako wa karibu nae aonje utamu,
unakuta mdingi kaoa kamuacha mke kijijini labda kaenda Nairobi, Mombasa, Tanga, Arusha au Dar anakaa huko miaka miwili akirudi anakuta mkewe ana mtoto wa miezi 4 wala haulizi anamlea tu kama wa kwake, na kawaida wazee wa Enzi hizo akirudi kabla hajafika nyumbani anatuma mtu apelike mizigo kama ishara kuwa mwenye mali amekuja wale wakudandia wasifike tena,

Haya bwana mkuu... Kweli zamani raha
 
yote tisa umesahau kuoa ilikuwa ni kuchagua bega yaani unamvizia binti ukimbeba tu kwako akilala kesho yake wazazi wa mvulana wanakwenda kujitambulisha ndoa tayari.
- ukilala na mvulana tayari ameshakua mmeo hata kama humtaki

-siku za gulio ndo siku za kutoka yaani ukienda gulioni wewe ni mkali ile mbaya
-zawadi kubwa mama akitoka sokoni ni mandazi
-baba alimiliki uchumi wote wa familia hata kama mama ndo kalima
-jamani kufagia samadi kila sbh kbla ya shule, na kulima bustani za mboga ni kawaida sanaaa
-siku mwl anakuja kutembelea mkoa wamnafunzi mnajipanga barabarani na kuimba nyimbo za kumpongeza
-mwenge wa uhuru ukija wilayani ni balaa mtaimba mashairi na kwaya ile mbaya
-shulen kulikuwa na siku ya mashundano ya kuimba kwaya katika wilaya na mshindi huenda mkoa hadi taifa
-umishumta ilikuwa balaa skati fupiii za netball lol!
ngoja nipike narudi..................[/QUOTE

Turudie kwenye RED
 
Naikumbuka sana drive in cinema!

Nakumbuka Elite na Metropole cinema arusha.

Matangazo ya kumbi za cinema yalikua yanaandikwa kwenye magazeti ya uhuru na mzalendo huku yakinakshiwa na picha za akina Rambo, Chuck Noris na Bruce Lee.
 
  • Thanks
Reactions: ram
Du umenikumbusha mbali sana!!!!!!

Zamani hakuna kunawa nyumbani! ni umande au mtoni au kama kuna mnaopitia mwendapo shleni.

Nakumbuka sanduku langu la mbao......MAHOGANY. Unapokelewa na wenzake kwa sauti ya nyuki..... mweee

Nakumbuka tuliitwa MUGIA.

Lakini kila kitu kilikuepo kuanzia malazi, daftari, msosi mboga ilopikwa na mafuta ya mawese, walimu wa kila soma.

Umalizapo form 4, kazi bwerere, ukifaulu kwenda form V sawa.!!!!
 
Mabasi binafsi hayakuwepo, yalikuwepo mabasi ya KAMATA aina ya FIAT na malori ya BEDFORD ya KAJIMA.

Kamata walikuwa na mabasi aina Leyland na Mercedes Benz, Kajima hii ni kampuni ya kijapani na walikuwa wanatumia malori aina ya Isuzu.
Nasahihisha tuu Mkuu
 
Ninazo kumbukumbu nying tu kama kula ugali wa yanga, kupeleka kijitabu kwa balozi kusainiwa kwa ajili ya mgao wa mafuta, sukari sabuni n.k kwenye duka la kata na ukifika foleni ni kuanzia asubuhi hadi jioni, muda wa kuziandika hapa ni mfinyu sana

Hahaa..kwan We ndugu ni enzi gan utoe na wew kumbukumbu zako za maisha?
 
Back
Top Bottom