Zamani ilikuwa raha

Zamani ilikuwa raha

Hapa naahidi mbele ya chama-
cha mapinduzi nitakulinda mpaka kufa,
tumeachiwa jukumu la kukulea wewe.

Kumbuka mapinduzi bado mdogo,
wazazi wako wamefariki toka zamani......
............................................

Dah! unaimba kwa hisia zote za uzalendo. tehe tehe.....hakukuwa na tofauti kati ya chama na serikali
 
Four years!! Mkuu watu wame-date toka shule ya msingi hadi chuo kikuu na hawaoni ndani. Mchezo wanakuja kupewa siku ya ndoa (of coz hizi ni zile extreme cases lakini zilikuwepo za kutosha tu)

umenifurahisha
w
 
acha kudanganya wasiokuwepo wewe...uliona raha kula unga wa njano kisa tunakwenda kumpiga Iddi Amini!?
Watoto wa siku hizi ndio wanafaidi siku hizi picha uweki kwenye Albamu ni mwendo wa Selfie na kutupia Instagram kwa kuwa salamu ni WhatsApp hatutumiagi tena kalamu yale mambo ya kutuma barua leo inafika baada ya mwezi ww unadhani watu walikuwa wanafurahi kusubiri kutafutia mke wa kuoa na baba yako nani alikuwa anapenda eti ugongi mpama uoe kudadeki siku hizi ukipewa namba ya simu tu ushakubaliwa

#Zitto

lakini hapo kwenye ndoa ilikuwa poa ndio maana baba na mama zetu mpaka leo wako pamoja
 
Kwenda sekondari ilikuwa ni heshima kwa jamii inayokuzunguka. Wakati wa kwenda shule husindikizwa na kundi la watu huku umesaidiwa sanduku. Tulipanda treni.

Tiketi tulitunza kwani nauli tulirejeshewa baada ya safari. Makonda wa treni (tt) walikuwa ni wahindi.

Mwl.alipohamishwa shule ilipikwa pilau, pia mashairi yaliimbwa.

Picha tulipiga studio tena baada ya kusevu kwa muda mrefu.... Tofauti na siku hizi ''selfie''.

Tulisikiliza RTD, kwa miziki idhaa ya biashara.

Range rover haikuruhusiwa ku paki benki. Peugeot 504 iliaminika ni gari ya wahuni/majambazi.
Namba za serikali ilikuwa stb, stc, std, stg. Za wahisani ilikuwa tx - plate number nyekundu.

Sikukuu ya saba saba ilifana sana kitaifa ilifanyika. Na mikoa mingine ilishiriki pia.

Vitabu madaftari shule za msingi ilikuwa bure. Daftari likijaa unapeleka kwa mwl.wa darasa anakupa jipya
ole wako karatasi zikutwe pungufu, viboko vilitawala mashuleni na nidhamu ilikuwepo pia.

Wanafunzi shule ya msingi baadhi walikuwa wananyoa ndevu.

Itaendelea.

Mkuu hapa tunakelewa wachache, wengi ni St Emmy wanaona mauzauza tu, Asante kwa kutukumbusha.
 
Enzi hizo mipira ya Shule (za msingi) ilikuwa ikihifadhiwa kwa Mwalimu Mkuu. Watoto wake weekend wanajichukulia mpira nakucheza. Watoto wa wakulima wanawaogopa watoto wa walimu hata kugusa vitu vyao ilikuwa ni vigumu.
 
  • Thanks
Reactions: awp
Imani ya TANU binadamu sawa, kila mtu aheshimiwe, ashiriki sawa katika taifa, Tanganyika ni nchi yetu. Siasa ya TANU hujenga Ujamaaa, nakusitiwisha raia, Usipojiunga na siasa hiyo wewe hujengi Tanganyika
 
tuliapishwa bila kujua ule wimbo wa-naapa naahidi mbele ya chama;pinduzi nitakulinda mpaka kufa najuta sana leo
mapinduzi nitakulinda ungali mdogooo
na wazazi wakoo wotee wamekuzaa wewee
 
Kumbukumbu zangu:

1. Disco Twiga, ghorofa ya tano, mtaa wa Samora.

2. DJ Kalikali (RIP) na nyimbo za breakdancing Rungwe Beach.

3. Kuogelea wakati wa sikukuu Afrikana. Tunawahonga Askari wa geti na kuingia na sufuria za pilau na chupa za mirinda moto. Nani anunue chakula bei za wazungu! Nakumbuka maandazi katika menu yao waliita " African cake".

4. Kuvaa Kaunda Suti na raizoni ya Bora ya ghorofa tatu.

5. Sinema za Bruce Lee pale Empire. Makarate yake yanakufanya usimame kitini na kushangilia.

6. Picha za kihindi Avalon. Picha refu sana lakini kuna intermission katikati. Tunatoka nje na kununua mishikaki na soda na kuendelea kuona katili amjad khan anavyopigwa na amita bachan.

7. Kutembea na gari jumapili kwa kubali. Barabara yote yetu!

8. Kuangalia picha nyumbani katika mkanda wa Betamax pamoja na majirani WOTE.

9. Kula chokleti ya "cadbury" kutoka Kenya na "Big G" na "orbit". Tunatafuna pole pole isiishe utamu.

10. Kuuza vyakula kwa "ration". Sabuni ya kuogea ni mbuni au ya misaada. Mafuta ni ya nazi. Peremende ni " pipi ya kifua ya bluu".

11. Kutumia simu ya Nokia ya "mkate".

12. Kujifunza kuendesha gari katika uwanja wa Lugalo, upanga.
 
yaani very interesting.......nakumbuka Chidya boys Masasi walikuwa wanaitwa mbwa mwitu coz shule yao ipo milimani
 
Duh asante sana mkuu umenifanya niione 1979 live nilipoenda kuandikishwa darasa la kwanza, wakati huo vita vya Kagera vinanguruma kuelekea mwisho. Yaani unapenda shule kwa moyo wote.
Wakati wa sikukuu za kitaifa chakula kinapikwa mnakula shuleni, duh those were the sweet days.
 
Tulicheza mpira wa makaratasi na shule nzima ilitushangilia kwa nguvu ikiwa pamoja na waalimu wetu.

Halafu asubuhi kabla ya masomo tulikimbia mchakamchaka huku tukiimba nyimbo nyingi kama vile:

Idd Amini akifa,
mimi siwezi kulia,
Nitamtupa Kagera,
awe chakula cha mamba.

Mchakamchaka mnakimbizwa na mgambo huku mnaimba:

Jua lilee literemke mama; aiyaiya iya iya mama ...

Na ule wimbo mwingine wa Kambona ameolewa na Mwingereza mnaukumbuka?
Those days bwana, ilikuwa safi sana.
 
HIZO ZOTE NI HEKIMA NA BUSARA ZA BABA WA TAIFA,ati leo tuna madini,gesi na utalii..tunalipia Matibabu na elimu na maisha yamekua Kero kama sio nyoka mwenye makengeza basi utaomba ardhi ipasuke uingie!ndio maana nikasema tunatakiwa kama nchi si kusherehekea bali KUSIKITIKIA MIAKA 50 YA UHURU,tumuenzi Baba Nyerere!!

Miaka 50 ya uhuru::
Tumethubutu, tumejaribu, tumeshindwa, tujipange upya.
 
Udini haukuwepo, Watanzania walipendana na kusaidiana kwa hali na mali bila kujali huyu muislam au mkristo. Hakukuwepo na mafisadi kama ilivyo sasa. Viongozi walikuwa wanaheshimika kwa sababu badala ya kukwapua kwa ajili ya matumbo yao wengi wao walikuwa wanawatumikia Watanzania kwa faida yao na Tanzania. Wauza unga walikuwa hawapo tulikuwa tunasikia tu kwenye taarifa ya habari kuhusu wauza unga wa nchi za nje ambazo zote zilikuwa ni nje ya Afrika. Ikulu iliheshimika na Watanzania sio kama ilivyo sasa imegeuzwa kuwa danguro la mafisadi wanagawana pesa za umma walizokwapua ndani ya Ikulu.

Carlos enzi zake na biashara ya unga. Nimesahau jina la kwanza.
 
Hii ya juzi hapo 90 huyu mleta mada kwa namna alivyoandika yeye ni miaka ya mwisho ya 80 kurudi nyuma kwa Mwl Nyerere. Kipindi hicho hata private schools sidhani kama zilikuwepo na mara nyingi ilikuwa ukifeli ndio basi tena labda ukarudie darasa sehemu nyingine.

Shule za Private zilikuwa za kanisa au jumuiya ya wazazi.
 
Back
Top Bottom