SHULE YA KULIPIA ulikuwa msamiati husika
Aaaaah! Yaani 90s ndo zamani yako hiyo Mkuu?
yote tisa umesahau kuoa ilikuwa ni kuchagua bega yaani unamvizia binti ukimbeba tu kwako akilala kesho yake wazazi wa mvulana wanakwenda kujitambulisha ndoa tayari.-Matibabu ilikuwa bure. Hospitali za binafsi hazikuwepo labda za misheni.
-Ukivaa chupi ilikuwa ni dili kubwa!
-Hakukuwa na skini taiti
-Viatu ilikuwa tunanunua Bora
-Nyumba 10 alikuwa anaheshimika kama hakimu. Ukigombana na mkeo anakwenda kushitaki na kulala kwa mjumbe
-Ukimwi ulikuwa hakuna zaidi ya kisonono na kaswende
-Wasichana wa kazi walikuwa bwerere siku hizi ni shida!
-Hakukuwa na magril kwenye milango na madirisha
-Nyerere alikuwa kama Mungu
-Kawawa alikuwa alionekana kama kichekesho kwa stori za "Kawawa funika kikombe"
-Tulifanywe tuamini kuwa Kambona ni adui wa nchi yetu na nyimbo tuliimba
-Wakati ule wanafunzi kwenda kufanya kazi za mwalimu nyumbani kwake ilikuwa ni heshima kubwa, sasa hivi ni kesi
-Mashairi ya "Karudi baba mmoja" na "Sizitaki mbichi hizi" yalikuwa kichwani kwa kila mwanafunzi
-Jioni zilikuwa ni nyakati za kupiga hadithi na vitendawili au michezo ya kujificha. Siku hizi ni kuangalia TV
Nitaendelea......
Shairi la "SIZITAKI MBICHI HIZI" lilikuwa hivi Mkuu!Mkuu shairi la karudi baba mmoja nililiimba nikiwa darasa la 4 mwaka 2000 ila shairi la sizitaki hizi mbichi sikubahatika emu weka mistari yake!
Wanaposema raha yaani level of happyness among the people ilikuwa juu yaani pamoja na yote hayo watu walikuwa na furaha na wanaheshimiana na wanaishi kama ndugu
yote tisa umesahau kuoa ilikuwa ni kuchagua bega yaani unamvizia binti ukimbeba tu kwako akilala kesho yake wazazi wa mvulana wanakwenda kujitambulisha ndoa tayari.
- ukilala na mvulana tayari ameshakua mmeo hata kama humtaki
-siku za gulio ndo siku za kutoka yaani ukienda gulioni wewe ni mkali ile mbaya
-zawadi kubwa mama akitoka sokoni ni mandazi
-baba alimiliki uchumi wote wa familia hata kama mama ndo kalima
-jamani kufagia samadi kila sbh kbla ya shule, na kulima bustani za mboga ni kawaida sanaaa
-siku mwl anakuja kutembelea mkoa wamnafunzi mnajipanga barabarani na kuimba nyimbo za kumpongeza
-mwenge wa uhuru ukija wilayani ni balaa mtaimba mashairi na kwaya ile mbaya
-shulen kulikuwa na siku ya mashundano ya kuimba kwaya katika wilaya na mshindi huenda mkoa hadi taifa
-umishumta ilikuwa balaa skati fupiii za netball lol!
ngoja nipike narudi..................
chakachaka alipokuja dar mwaka 90 kiingilio laki moja pale makondeko nje ya jiji siku hizi diamond akiweka kiingilio elfu 50 mlimani city inakuwa matangazo kila kona
Mkuu unataka zaman yangu iwe miaka gan?labda we ni wa 60 lakn kwa wale waliozaliwa miaka ya 75 adi 80s wengi wao wana miaka 30 adi 45 na wengi wao ukiwauliza kipndi gan kilikuwa kizuri atakwambia 90s,kipindi cha salamander na magoti,ukitaka bolingo unaenda Tazara
Nimekuelewa Mkuu! Ni kweli eti hata katoto ka mwaka 2000 ukikauliza zamani ya kenyewe katasema mwaka 2000 ha ha ha ha haaaa!! Frank bwana eti zamani yake 90s! Ila tuwe waungwana tukisema zamani mtuachie Wa 70s angalau tuongee, nyie Wa 90s msubiri ikifika 2030 ndo mtaulizana zamani yenu!!
dada gfsonwin habari za masiku umehadimika?