Tokyo40
JF-Expert Member
- Jun 16, 2013
- 2,065
- 1,926
Shoga maarufu hapa mjini akiitwa Farouk.Ukimwita mtu Farouk enzi zile huo ugomvi wake ni wa kufa mtu. Siku hizi ushoga ni fasheni.Unazungumzia enzi za Maggot mkuu!
HIZO ZOTE NI HEKIMA NA BUSARA ZA BABA WA TAIFA,ati leo tuna madini,gesi na utalii..tunalipia Matibabu na elimu na maisha yamekua Kero kama sio nyoka mwenye makengeza basi utaomba ardhi ipasuke uingie!ndio maana nikasema tunatakiwa kama nchi si kusherehekea bali KUSIKITIKIA MIAKA 50 YA UHURU,tumuenzi Baba Nyerere!!
Kwenye atlas umenikumbusha kitambo kweli kuna mchezo wa kutafuta miji tulikuwa tunacheza 'mtu anataja mji/sehemu wengine mnatafuta.'
waliofeli ndio walienda private schools, ilikuwa aibu mtu kusoma pte school. leo ni sifa kusoma au kusomesha pte schools.
siku za sikukuu kulikuwa na tamaduni za kupeana chakula hasa pilau, kama mimi ni mkristo na ni krismass lazima pilau ipikwe na niwagawie jirani zangu hasa ambao sio wakristo, na wao vileviile ikifika sikukuu yao wanafanya hivyo hivyo....
Siku hizi ndo hamna raha wakati huo kila kitu kilikuwa kinasisimua kwani havikuwa vinapatikana kila mahali kama leo. Wali wa maharage ulikuwa mtamu kuliko chipis mayai/kuku leo, hata uji usio na chochote ulikuwa mtamu kuliko uji wa asali leo
Yaani miaka hiyo kwa kweli ulikuwa raha! Walimu walikuwa na mbinu za ufundishaji na sisi wanafunzi nao tulikuwa na mbinu zetu za kuelewa mambo! Darasa la sita unakuwa unajua nchi nyingi na miji mikuu kwa kila nchi! Pia unakuwa inawafahamu marais wote Wa Africa! Hiyo ya kutafuta miji ilikuwa kiboko, naona enzi hizo tuliifanya Tanzania nzima!
Yaani unawajua marais wa nchi Zote, miji mikuu ya nchi zote, na kila nchi inalima zao gani la biashara
Umeona eeh....
siku hizi sijui watu wanafuturia wapi, nakumbuka tulikuwa tumepanga nyumba ya waislam, tulikuwa tunafuturu mwanzo mwisho utadhani na sisi tumefunga, siku za sikukuu iddi au christmas ilikuwa hakuna ubaguzi mnashirikiana kupika na kula pamoja kama ndugu jamani, haya mamba hayapo tena nowdays, kweli zamani ilikuwa raha
Yaani miaka hiyo kwa kweli ulikuwa raha! Walimu walikuwa na mbinu za ufundishaji na sisi wanafunzi nao tulikuwa na mbinu zetu za kuelewa mambo! Darasa la sita unakuwa unajua nchi nyingi na miji mikuu kwa kila nchi! Pia unakuwa inawafahamu marais wote Wa Africa! Hiyo ya kutafuta miji ilikuwa kiboko, naona enzi hizo tuliifanya Tanzania nzima!
Thats true !! nilikuwa nimedunduliza na kuchanga pesa mwaka mzima zikafika $ 57 !! duuh wakati wa Opereshen hujumu uchumi eti wanyumbani wakanilazimisha nizichome moto !!iliniuma sana !! maana nilijinyima mda mrefu hatimae nikageuza pesa masizi na majivu !!
SwadaktaaaNitafutieee....... Unamwambia kamji kadogo kabisa kako pembeni mwa ramani, atasota huyo.....was very wonderful days
Kabisa mkuu.. Yaani leo form iv hata nchi za Africa hajui walau mini mikuu na viongozi kumi hawezi kitaja kabisa....
Mkuu Tokyo ahsante nimemuona kijana wangu Billy Whizz the fastest man on earth!