Zamani ilikuwa raha

Zamani ilikuwa raha

Yap kumbukumbu kama hz ndo tunazozitaka, thumbs up mkuu. Lete nyingine.

ImageUploadedByJamiiForums1426609336.880591.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1426609372.212601.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1426609388.280212.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1426609403.513490.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1426609422.081648.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1426609525.015561.jpg
 
HIZO ZOTE NI HEKIMA NA BUSARA ZA BABA WA TAIFA,ati leo tuna madini,gesi na utalii..tunalipia Matibabu na elimu na maisha yamekua Kero kama sio nyoka mwenye makengeza basi utaomba ardhi ipasuke uingie!ndio maana nikasema tunatakiwa kama nchi si kusherehekea bali KUSIKITIKIA MIAKA 50 YA UHURU,tumuenzi Baba Nyerere!!

Mkuu umenitia simanzi sana, juzi kati nimempeleka mtoto hospitali ana UTI nikapewa paracetamol 5..dah hali tete sana mungu atusaidie.
 
Kwenye atlas umenikumbusha kitambo kweli kuna mchezo wa kutafuta miji tulikuwa tunacheza 'mtu anataja mji/sehemu wengine mnatafuta.'

Nitafutieee....... Unamwambia kamji kadogo kabisa kako pembeni mwa ramani, atasota huyo.....was very wonderful days
 
waliofeli ndio walienda private schools, ilikuwa aibu mtu kusoma pte school. leo ni sifa kusoma au kusomesha pte schools.

au wana-repeat. na ndo maana "Wanafunzi shule ya msingi baadhi walikuwa wananyoa ndevu."

 
siku za sikukuu kulikuwa na tamaduni za kupeana chakula hasa pilau, kama mimi ni mkristo na ni krismass lazima pilau ipikwe na niwagawie jirani zangu hasa ambao sio wakristo, na wao vileviile ikifika sikukuu yao wanafanya hivyo hivyo....

jirani yetu mama Abdallah siku za eid sinia la mahamri lilikuwa linaletwa tena kwa upendo mwe!
 
Hahahahahaha lol! Siku kuna wali na maharage hata hutaki kucheza mbali na nyumbani 🙂🙂

Siku hizi ndo hamna raha wakati huo kila kitu kilikuwa kinasisimua kwani havikuwa vinapatikana kila mahali kama leo. Wali wa maharage ulikuwa mtamu kuliko chipis mayai/kuku leo, hata uji usio na chochote ulikuwa mtamu kuliko uji wa asali leo
 
Yaani miaka hiyo kwa kweli ulikuwa raha! Walimu walikuwa na mbinu za ufundishaji na sisi wanafunzi nao tulikuwa na mbinu zetu za kuelewa mambo! Darasa la sita unakuwa unajua nchi nyingi na miji mikuu kwa kila nchi! Pia unakuwa inawafahamu marais wote Wa Africa! Hiyo ya kutafuta miji ilikuwa kiboko, naona enzi hizo tuliifanya Tanzania nzima!

Yaani unawajua marais wa nchi Zote, miji mikuu ya nchi zote, na kila nchi inalima zao gani la biashara
 
Walimu walikuwa wanathaminiwa na Serikali haya mambo ya kusikia walimu hawajalipwa mabilioni ya pesa zao halali hayakuwepo kabisa, siku hizi unasikia wanaidai Serikali bilioni 16 halafu Serikali inataka kuwadhulumu mchana kweupe kwa kudai haidaiwi na walimu!!! Ngoja waje mafisadi wa Richmond waseme wanaidai Serikali $110 million, serikali hii dhalimu itaunga mkono kwamba ni kweli inadaiwa. Ngoja waje wakwapuzi wakwapue bilionu 200 za walipa kodi pale BoT Serikali hii dhalimu itakuwa mstari wa mbele kudai zile si pesa za umma.

Yaani unawajua marais wa nchi Zote, miji mikuu ya nchi zote, na kila nchi inalima zao gani la biashara
 
Umeona eeh....

siku hizi sijui watu wanafuturia wapi, nakumbuka tulikuwa tumepanga nyumba ya waislam, tulikuwa tunafuturu mwanzo mwisho utadhani na sisi tumefunga, siku za sikukuu iddi au christmas ilikuwa hakuna ubaguzi mnashirikiana kupika na kula pamoja kama ndugu jamani, haya mamba hayapo tena nowdays, kweli zamani ilikuwa raha

siku hizi watu wanafuturia Hyatt, dining kwao, na hii ya kufuturisha zamani siikumbuki
 
gazeti la Sani lilikuwa likitoka anakuwa nalo mtu mmoja tu shule nzima, but mtapokezana by the time linakufikia kuna pages zishaota ukungu, zingine zomelowa maembe, mate, kamasi etc
 
Yaani miaka hiyo kwa kweli ulikuwa raha! Walimu walikuwa na mbinu za ufundishaji na sisi wanafunzi nao tulikuwa na mbinu zetu za kuelewa mambo! Darasa la sita unakuwa unajua nchi nyingi na miji mikuu kwa kila nchi! Pia unakuwa inawafahamu marais wote Wa Africa! Hiyo ya kutafuta miji ilikuwa kiboko, naona enzi hizo tuliifanya Tanzania nzima!

Kabisa mkuu.. Yaani leo form iv hata nchi za Africa hajui walau mini mikuu na viongozi kumi hawezi kitaja kabisa....
 
Dah! Chezeya Moringe Sokoine weye!!!! Niliwahi kuambiwa miaka hiyo pamoja na nchi yetu kuwa maskini dhahabu ilikuwa haijaanza kuvunwa, gesi haijagunduliwa lakini shilingi yetu ilikuwa na nguvu sana duniani $1 ilikuwa sawa na shilingi 5 na pound moja ya kwa mama (UK) ilikuwa sawa na shilingi 20 yetu sasa hivi ni midabwada mitupu shilingi yetu imeshuka utadhani ni dollar ya Zimbabwe.

Thats true !! nilikuwa nimedunduliza na kuchanga pesa mwaka mzima zikafika $ 57 !! duuh wakati wa Opereshen hujumu uchumi eti wanyumbani wakanilazimisha nizichome moto !!iliniuma sana !! maana nilijinyima mda mrefu hatimae nikageuza pesa masizi na majivu !!
 
kutoka dodoma kwenda mwanza usafiri ulikuwa ni wa train tu, na inabidi u-book ticket mwaka mzima
 
Duuh nimecheka sana na pia nimekumbuka mambo mengi sana
 
Kabisa mkuu.. Yaani leo form iv hata nchi za Africa hajui walau mini mikuu na viongozi kumi hawezi kitaja kabisa....

Siyo form IV tu, Mkuu hebu mkamate yeyote aliyeko chuo kikuu mweke kati akutajie nchi 20 na marais wake kama ataweza!! Hii ni aibu kwa nchi yetu!!
 
Back
Top Bottom