pia kulikuwa na biashara ya yomboohapo kwenye red panahitaji ufafanuzi ile wanetu waelewe vyema by the way nitaongeza hapa;
- kuhamishiwa mtwara au sumbawanga kwa mfanyakzi ilikua laana tosha
- tulitishwa kupelekwa mafya (kisiwani)
- ukivaa chumpi mpya hasa za zabron au 007 lazima kale ka chuma kaonekane ili washikaji wajue umenunuliwa mpya
- matozi waliitwa magwangwe na maranyingi walikua hawatawazi
- wakuu wa wilaya waliweza kukutandika bakora mbele ya mkeo
- ubakaji ilikua tendo la kawaida tuuu lilitwa mande au mtungo
- tulisafiri kwa juma kwenda mtwara
- wakazi wa kigoma walijivunia biasha ya homela homela wenyewe wakiita pia bize
- form 4 alikua msomi na angeweza oa mtoto wa mwenyekiti wa kijiji
- ma bwana mifugo walitutibu gono pia kwa sindano za ng'ombe na tulipoa
- tulipanda foleni ili tupate kipande cha sabuni ya ilula
- chai walikunywa waungwana wa town sis zetu uji kwa asali
Watu wa zamani mlipata shida sana. Sijui hata mlikuwa mnatongozaje wakati kulikuwa hakuna simu... Inawezekana pia mlikuwa mnachapiana sana.. Na ndio pengine mkafikia hatua ya kutunga ule msemo kuwa "kuchapiwa ni siri ya ndani"
Thats true !! nilikuwa nimedunduliza na kuchanga pesa mwaka mzima zikafika $ 57 !! duuh wakati wa Opereshen hujumu uchumi eti wanyumbani wakanilazimisha nizichome moto !!iliniuma sana !! maana nilijinyima mda mrefu hatimae nikageuza pesa masizi na majivu !!Kipindi Edward Moringe(R I P amen) akiwa Waziri mkuu alipofanya opereshen kwa wahujumu uchumi watu walitupa pesa zao sio leo EPA mnawabembeleza warudishe na Escrow kubeba kwa sandarusi!Waliohujumu kwa kufungia sukari stoo ili wapandishe bei waliimwaga sukari mtoni.
Suruali za jeans hazikuwepo kulikuwa na suruali za codrai na surual za mabuga luuu, ndo zilikuwa fashion.
Ishi!......................................................
pia kulikuwa na biashara ya yomboo
siku za sikukuu kulikuwa na tamaduni za kupeana chakula hasa pilau, kama mimi ni mkristo na ni krismass lazima pilau ipikwe na niwagawie jirani zangu hasa ambao sio wakristo, na wao vileviile ikifika sikukuu yao wanafanya hivyo hivyo....
Weee Mtoto utakuwa umesoma kitabu cha maktaba! Maana hilo shairi tumeliimba miaka ya 80s! Kwa vitabu vyenu vya Ben & Co Ltd hamwezi kuyakuta hayo mashairi!!
Karudi baba mmoja, toka safari ya mbali
kavimba yote mapaja na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja, ili kumtaka hali
wakataka na kauli, iwafae maishani
Shairi la "SIZITAKI MBICHI HIZI" lilikuwa hivi Mkuu!
Hadithi inayokuja, ni ya sungura sikia,
Hadithi uliyongoja, leo ninakuletea,
Alitoka siku moja, njaa aliposikia,
Njaa aliposikia, Sungura nakuambia
Siku ile akaenda, Porini kutembelea,
Akayaona matunda, mtini yameenea,
Sungura akayapenda, mtini akasogea,
Mtini akasogea, Sungura nakuambia.
Sungura karukaruka, lakini hakufikia,
Matunda hakuyashika, mikononi hakutia,
Hakika alisumbuka, nguvuze zikapungua,
Nguvuze zikapungua, Sungura nakuambia.
Mtazame hapo juu, Sungura amelegea,
Mtazame na miguu, matunda anarukia,
Atafanya sikukuu, matunda akifikia,
Matunda akifikia, Sungura nakuambia.
Karuka tena karuka, matunda akarukia,
Mwisho Wake akachoka, kachoka hata mkia,
Penye mti akatoka, pembeni akasogea,
Pembeni akasogea, Sungura nakuambia.
Sizitaki mbichi hizi, Sungura akagumia,
Naona nafanya kazi, bila faida kujua,
Yakamtoka machozi, matunda akalilia,
Matunda akalilia, Sungura nakuambia.
Sio kama hakutaka, sasa nakupasulia,
Matunda aliyataka, ndiyo kisa akalia,
Tunajua hakufika, alichoka kurukia,
Alichoka kurukia, Sungura nakuambia.
Hadithi nimemaliza, nimekwisha simulia,
Jambo moja sikiliza, rafiki yangu sikia,
Usikose kujikaza, mazuri kukazania,
Utamshinda Sungura, utapata mbivu hizi.
Tulikua tunaudhulia mashindano ya disco lan'gata social hall na harbour's club walikuepo mabingwa wa kucheza style mbalimbali. Mabingwa wetu kama akina savy pops akiwa kijana mdogo kabisa kuchukua ubingwa akitokea mitaa ya keko. Akina Black Moses kinondo, Ngedere Morogoro. Du!! Ilikua hatari natamani siku zingerudi nyuma.
ametukumbusha enzi hizoAsante sana mkuu nimeipenda kwelikwel!
Shairi la "SIZITAKI MBICHI HIZI" lilikuwa hivi Mkuu!
Hadithi inayokuja, ni ya sungura sikia,
Hadithi uliyongoja, leo ninakuletea,
Alitoka siku moja, njaa aliposikia,
Njaa aliposikia, Sungura nakuambia
Siku ile akaenda, Porini kutembelea,
Akayaona matunda, mtini yameenea,
Sungura akayapenda, mtini akasogea,
Mtini akasogea, Sungura nakuambia.
Sungura karukaruka, lakini hakufikia,
Matunda hakuyashika, mikononi hakutia,
Hakika alisumbuka, nguvuze zikapungua,
Nguvuze zikapungua, Sungura nakuambia.
Mtazame hapo juu, Sungura amelegea,
Mtazame na miguu, matunda anarukia,
Atafanya sikukuu, matunda akifikia,
Matunda akifikia, Sungura nakuambia.
Karuka tena karuka, matunda akarukia,
Mwisho Wake akachoka, kachoka hata mkia,
Penye mti akatoka, pembeni akasogea,
Pembeni akasogea, Sungura nakuambia.
Sizitaki mbichi hizi, Sungura akagumia,
Naona nafanya kazi, bila faida kujua,
Yakamtoka machozi, matunda akalilia,
Matunda akalilia, Sungura nakuambia.
Sio kama hakutaka, sasa nakupasulia,
Matunda aliyataka, ndiyo kisa akalia,
Tunajua hakufika, alichoka kurukia,
Alichoka kurukia, Sungura nakuambia.
Hadithi nimemaliza, nimekwisha simulia,
Jambo moja sikiliza, rafiki yangu sikia,
Usikose kujikaza, mazuri kukazania,
Utamshinda Sungura, utapata mbivu hizi.
Zamani kweli raha,
Kipindi ikifika Ramadhani watu wanafutari nje na kila mpita njia anaweza kukaa na akala na majirani wote munakua pamoja