Zaidi ya heka 6 za Mahindi zimefyekwa Mjini Mpanda

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Wakati Serikali inahamasisha Wananchi kujishughulisha na shughuli za Kilimo ili kujikwamia kimaisha, baadhi ya Wakulima katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamefyekewa Mahindi ikidaiwa ni kosa kupanda mazao marefu mjini.

Lucia Balizio ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Msasani na Nestori Kameme mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hoteli wamekerwa kwa kufyekewa mahindi yao ambapo wamedai kila mwaka wanapanda Mahindi katika mashamba hayo ambayo ndio mkombozi wa maisha yao.

Jovinari Deus ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Msasani na Christina Mshani Mwenyekiti wa Mtaa wa Mpanda Hoteli wamesema baadhi ya Wananchi hawahudhurii katika mikutano ya hadhara ambapo ndipo maelekezo ya Serikali hutolewa huku wakisisitiza mazao marefu kutopandwa katika mitaa yao.

Nao baadhi ya Wananchi katika Manispaa ya Mpanda wametoa maoni yao kwa kutoridhishwa na tukio hilo la kufyeka mahindi yaliyopandwa ndani ya Manispaa ya Mpanda lakini wanadai ni bora busara zingetumika ili kuzinusuru familia hizo kuziingiza katika maisha ya kuomba omba hasa katika mwaka huu wa 2023/2024 kwani tegemeo lao limeondolewa.

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf amesema licha ya katazo la kupanda mazao marefu ndani ya viunga vya manispaa lakini amekerwa na kitendo hicho cha kufyeka mahindi ya wakulima hao.

Aidha, Jamila amesema viongozi wa Manispaa watakaa kikao ili kuona namna bora ya kuwalipa wakulima hao.
 
Kuna viongozi wanakaa ofisini wanataka kutatua matatizo makubwa kwa akili ndogo, wanasema msipande mahindi maeneo ya mjini kwa kuwa yanaleta wezi/vibaka pasipo kujua sababu za msingi za wezi/vibaka.
Je hao wezi/vibaka hawawezi jificha maeneo mengine licha ya kutokuwepo kwa mahindi?
Hao waliokata mahindi hawana busara, hata kama mtu kavunja sheria, ni vema wangeenda kwenye vyombo vya kisheria ili kupata tafsiri sahihi.
 
Walifanya wapi research na kujua kuwa mahindi yanaleta wezi? Huu utaratibu wa kufyeka chakula ni wa hovyo sana.
 
Wakati Serikali inahamasisha Wananchi kujishughulisha na shughuli za Kilimo ili kujikwamia kimaisha, baadhi ya Wakulima katika Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamefyekewa Mahindi ikidaiwa ni kosa kupanda mazao marefu mjini.
Inasikistisha na Inaudhi na inakera kwa pamoja kwakweli.
Lucia Balizio ambaye ni mkazi wa Mtaa wa Msasani na Nestori Kameme mkazi wa Mtaa wa Mpanda Hoteli wamekerwa kwa kufyekewa mahindi yao ambapo wamedai kila mwaka wanapanda Mahindi katika mashamba hayo ambayo ndio mkombozi wa maisha yao.
Nawashauri hawa wakina Balizio na Kameme wasiwaache hawa wapuuzi wa Manispaaa. Wawakalie makooni mpaka kieleweke
Jovinari Deus ambaye ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Msasani na Christina Mshani Mwenyekiti wa Mtaa wa Mpanda Hoteli wamesema baadhi ya Wananchi hawahudhurii katika mikutano ya hadhara ambapo ndipo maelekezo ya Serikali hutolewa huku wakisisitiza mazao marefu kutopandwa katika mitaa yao
Hoja mbofu kweli hii, Ati Wananchi hawahudhurii mikutano. Hivi kwanini hawa viongozi wasingefika huko mashambani na kuwashauri ipasavyo na hata kuwaonya wasipande mazao hayo "marefu"? Kabla ya kupanda na hawajaingia hasara? Sio hivyo tu unaweza kuta wanayo bajeti ya kichapisha vipeperushi ila hawakufanya hivyo ili wananchi hao wawe na taarifa.
.

Nao baadhi ya Wananchi katika Manispaa ya Mpanda wametoa maoni yao kwa kutoridhishwa na tukio hilo la kufyeka mahindi yaliyopandwa ndani ya Manispaa ya Mpanda lakini wanadai ni bora busara zingetumika ili kuzinusuru familia hizo kuziingiza katika maisha ya kuomba omba hasa katika mwaka huu wa 2023/2024 kwani tegemeo lao limeondolewa.

Waungane kwa kweli na kukemea tendo hili la kikatili
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuf amesema licha ya katazo la kupanda mazao marefu ndani ya viunga vya manispaa lakini amekerwa na kitendo hicho cha kufyeka mahindi ya wakulima hao.
Mkuu huyu awashugulikie wote waliohusika.
Aidha, Jamila amesema viongozi wa Manispaa watakaa kikao ili kuona namna bora ya kuwalipa wakulima hao

Wasiishie hapo tu, wamtafute mbunge wao aweze kulishughulikia swala hili kitaifa ili jambo hili lisitokee tena Nchini
Aisee.
 
Kuna viongozi wanakaa ofisini wanataka kutatua matatizo makubwa kwa akili ndogo, wanasema msipande mahindi maeneo ya mjini kwa kuwa yanaleta wezi/vibaka pasipo kujua sababu za msingi za wezi/vibaka.
Je hao wezi/vibaka hawawezi jificha maeneo mengine licha ya kutokuwepo kwa mahindi?
Hao waliokata mahindi hawana busara, hata kama mtu kavunja sheria, ni vema wangeenda kwenye vyombo vya kisheria ili kupata tafsiri sahihi.
Mungu - mzungu - Mchina -mwarabu -Mwafrika- Ibilisi
 
Back
Top Bottom