Katavi: Wanawake 15 wamekamatwa Mpanda kwa kufanya biashara ya ngono

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Baraza la Madiwani Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imeibuliwa hoja ya baadhi ya wamiliki wa nyumba ambao wamekuwa wakipangisha mabinti na Wanawake wanaofanyabiashara haramu ya ngono ambapo imekuwa kero na kinyume cha uvunjifu wa Sheria na Maadili ya jamii.

Hamis Misigalo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mpanda Hoteli na William Mbogo Diwani wa Kata ya Majengo wamesema Wanawake hao wamekuwa kero na kikwazo katika maadili ya Mtanzania ambapo kila wanapokamatwa na kuchukuliwa Sheria kali lakini bado wamekua wakirudi katika nyumba hizo ambapo wameomba Sheria kali itungwe ya kuthibiti tabia hiyo ya Wanawake kuishi katika madangulo.

Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda Deudatus Kangu amesema jumla ya makahaba 15 wamekamatwa katika Kata ya Shanwe ambapo amesema sheria kali zitachukuliwa dhidi yao ikiwemo faini.

Biashara haramu ya ngono inayofanywa na baadhi ya mabinti na wanawake katika baadhi ya mitaa ya manispaa imekithiri wamekuwa wanafukuzwa na kukamatwa lakini bado ongezeko linakua kubwa kila kukicha.
 
Wateja wapo ndio maana wanafanya hiyo biashara. Naam ni biashara kongwe hakuna wa kuidhibiti ipo na itazidi kuwepo kwa kuwa suala la ndoa limekuwa kizingimkuti. Hayo makahaba utakuta wengine waliwahi kuolewa wakaachika na wengine ni mabinti ambao hawaoni umuhimu wa kuolewa wakiangalia zaidi hali ya uchumi wa familia itakuaje wakiingia kwenye ndoa, na wengine ni wake za watu waliobobea kwenye biashara ya ngono.
 
Wateja wapo ndio maana wanafanya hiyo biashara. Naam ni biashara kongwe hakuna wa kuidhibiti ipo na itazidi kuwepo kwa kuwa suala la ndoa limekuwa kizingimkuti. Hayo makahaba utakuta wengine waliwahi kuolewa wakaachika na wengine ni mabinti ambao hawaoni umuhimu wa kuolewa wakiangalia zaidi hali ya uchumi wa familia itakuaje wakiingia kwenye ndoa, na wengine ni wake za watu waliobobea kwenye biashara ya ngono.
Hao machangu nao wabadilike, wenzao wanatumia simu kufikia watrja wao
 
Wakikamatwa wanapewa adhabu gani? Kuna ambao wamewahi kuhukumiwa kifungo?
 
Umeme, afya, maji, Barbara za mtaani, sungu sungu, usafi wa mazingira, vikundi vya ujasiriamali, mikopo ya kina mama na vijana, shule za primary na secondary halmashaur ya mpanda, vituo vya polisi etc
 
Wanafanya biashara kishamba wanashindwa nini kufungua account insta yenye jina Malaya mnato Mpanda.Wafanye delivery kimya kimya
 
Wanafanya biashara kizamani
Mimi huwa kuona watoto wa kike wakiwa nusu uchi barabarani ukipita wanakufuata
 
Kama sio sumu wanajisumbua

Ushamiri popote wa biashara hutegemea mlaji ,hao madiwani kazi hizo wawachie wateuliwa ukiwa mchaguliwa kama diwani hao WALAJI wanaweza kujibadili kuwa vichinjio
 
Baraza la Madiwani Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi imeibuliwa hoja ya baadhi ya wamiliki wa nyumba ambao wamekuwa wakipangisha mabinti na Wanawake wanaofanyabiashara haramu ya ngono ambapo imekuwa kero na kinyume cha uvunjifu wa Sheria na Maadili ya jamii.

Hamis Misigalo ambaye ni Diwani wa Kata ya Mpanda Hoteli na William Mbogo Diwani wa Kata ya Majengo wamesema Wanawake hao wamekuwa kero na kikwazo katika maadili ya Mtanzania ambapo kila wanapokamatwa na kuchukuliwa Sheria kali lakini bado wamekua wakirudi katika nyumba hizo ambapo wameomba Sheria kali itungwe ya kuthibiti tabia hiyo ya Wanawake kuishi katika madangulo.

Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Mpanda Deudatus Kangu amesema jumla ya makahaba 15 wamekamatwa katika Kata ya Shanwe ambapo amesema sheria kali zitachukuliwa dhidi yao ikiwemo faini.

Biashara haramu ya ngono inayofanywa na baadhi ya mabinti na wanawake katika baadhi ya mitaa ya manispaa imekithiri wamekuwa wanafukuzwa na kukamatwa lakini bado ongezeko linakua kubwa kila kukicha.
Aisee loh
 
Back
Top Bottom