DOKEZO Zahanati ya Mashati (Rombo) kuwa hatarini kutokana na nyufa ni dalili za kukosekana uwajibikaji Serikalini

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Papasa

JF-Expert Member
Nov 2, 2018
1,947
4,131
Snapinsta.app_424921327_748998040158856_2907431944532205095_n_1080.jpg

Snapinsta.app_424480685_2394751827369583_6659830516952618122_n_1080.jpg

Zahanati .png

Nimeona hili habari, isome kisha nami nitatoa maoni yangu...

Zahanati ya Mashati, Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro, iliyotajwa kujengwa zaidi ya miaka tisini iliyopita ipo hatarini kuanguka baada ya zahanati hiyo kuwa na nyufa hali ambayo inatishia usalama wa wagonjwa pamoja na watoa huduma katika zahanati hiyo.

Akizungumzia namna zahanati hiyo inavyotishia usalama wa wakazi wa maeneo hayo Diwani wa Kata ya Katangara Mrere, Venance Malle, amesema zahanati hiyo inahudumia wakazi wa Katangara Mrere na Kisare, hivyo ameiomba Serikali kufanya ukarabati wa zahanati hiyo.

Maoni yangu:
Serikali ilipaswa kumalizana na mambo ya Zahanati miaka 20 nyuma huko lakini bado ni tatizo hata sasa lakini cha ajabu wanajifia kujenga Zahanati katika Karne hii tena kwa hela mikopo hii ni aibu na umaskini wa akili, ukila na kipofu usimshike mkono.

Hizi ni dalili za uzembe na kukosekana kwa uwajibikaji kwa baadhi ya mamlaka ndani ya Serikali.
 
Panya wapo na harakati za kutafuna na kuzamisha boti zinazotusafirisha baharini 🤣
 
Back
Top Bottom