Mwana
JF-Expert Member
- Aug 6, 2010
- 5,435
- 1,967
Brother nina mama yangu,ambaye hata nisipomuita mpendwa haibadilishi dhana kwamba nampenda sana, nina dada yangu Lightness ambaye nilimuahidi kusimama naye bega kwa bega na kwamba ningekuwa mtu wa mwisho kumchoka baada ya ulimwengu mzima kumkataa...
Namfahamu Mwenyezi Mungu,ambaye alitumia muda wake adhimu kunipa pumzi hii ya uzima,nina wadogo zangu mtaani ambao kwa namna moja ama ningingine nimekuwa roll model wao kwenye aspects tofauti tofauti, nina Rose wangu huyu ambaye pamoja na uamuzi aliouchukua nadhani ataumia sana akijua nimejidhuru kwa sababu yake,na kwa kuwa nilimwahidi kwamba nisingependa kushududia akidondosha chozi kwa sababu yangu...,
Sasa basi najaribu kureview nakala ya sababu zinazonifanya nifikirie kujiua,ili nijikatie rufaa mwenyewe kwenye mahakama ya rufani ya mapenzi kisha nafsi ikishinda moyo nisitishe uamuzi wa kujiua na kama itaonekana niliviolet vifungu vya sheria wakati wa uamuzi wa kuijiua basi Rose anihukumu kwa kunirudisha kwenye kifungo cha kumpenda maisha!
Mwhisho wa yote mfikirie mama yako mazazi ambaye naamini ndio anayekupenda kwa dhati na kutoka moyoni kuliko mtu yoyote hapa ulimwenguni. Hebu ahirisha basi kwa ajili yake na dada yako, wadogo zakona ndugu zako wengine. Kuna siku nakwambia utakuja hapa JF nakutuambia jinsi ulivyompata huyo umpendae kuliko hata huyo Rose amini nakuambia. Na ulivyotaja umri wako bado una muda wa kutosha kumpata umpendae na atakae kupenda.