Yericko Nyerere: Tofauti ya Usalama wa Taifa, CID na Military Intelligence

DaveSave

JF-Expert Member
Nov 20, 2010
440
634
Kumekuwa na mkanganyiko kidogo juu ya tofauti ya Jasusi, Shushushu, Kachero, Mpelelezi nk. Kwenye kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi nimeeleza kwa kirefu zaidi juu ya utofauti wa mambo haya muhimu matatu kwa Tanzania ambayo ni lazima kila mtu ayajue na kuyatofautisha kufuatia mageuzi ya dunia yanayokwenda kwa kasi sasa.

Nasi kama sehemu ya dunia hatutakiwi kuwa nyuma, kwanza tuanze na Usalama wa Taifa (TISS). Pili tuangalie idara ya Upelelezi (CID) na Tatu ni idara ya Intelijensia- Polisi "IO" (Intelligence Officer), naam leo naomba niwape dondoo tu kidogo, mengi yapo kitabuni....

1). Intelligence Officer (Afisa Usalama mfano kwa Tanzania tungesema usalama wa taifa (TISS) chombo hiki hakina mipaka ya utendaji kazi, yaani kazi yake ni ya jumla, inaweza kumulika popote iwe katika Jeshi la Nchi, Polisi na ama katika majeshi yote, iko kwenye kila eneo katika starehe burudani na katika huzuni yenyewe ipo. Haichunguzi mabaya tu bali mabaya na mazuri. Msingi mkubwa utendaji kazi wake ni wakificho unaolindwa kwa sheria kali na ya hatari.

2). Police Intelligence Officer (Afisa Usalama wa polisi, wao wanaita Intelijensia ya Polisi, Hawa ni tofa na idara ya upelelezi makosa ya Jinai. Hii idara iko chini ya Jeshi la Polisi, inafanya kazi sawa na Usalama wa Taifa na inashahabiana kwa kila kitu tofauti ni baadhi ya mafunzo kidogo tu, hii ndio inayohusika zaidi na masuala ya siasa na utawala, Ulinzi wa viongozi, Ujasusi wa kimtandao kwa maana ya kuingilia mawasiliano ya mtu yoyote nchini kwa maslahi ya Taifa, hawa ndio wanaokabiliana zaidi na vyama vya siasa)

3). Kuna idara ya Upelelezi wa makosa ya jinai au kwa lugha ya kitumwa ni Criminal investigation Department (CID) ipo chini ya Polisi nayo. Hii ingekuwa Marekani tungesema ni FBI.

Tofauti ya Usalama wa taifa (TISS) na Intelijensia ya Police (Police Intelligence Officer) ni kuwa Police intelligence officer wanajihusisha na ushushushu na ukachero wenye Ku-establish Element Of Crime.

Wakati TISS wanajishughulisha na kila kitu (personality za watu, tajiri, maskini, uchumi na kuhakikisha ustawi wa nchi kiujumla ikiwa na maana chochote which is likely to happen wawe wanakijua kiwe na madhara au laa). Izingatiwe hawa hufanya kazi zao kwa siri kubwa

Tofauti ya pili kati ya Usalama wa taifa na Intelligence Unity ya polisi ni "WHERE DO YOU REPORT", Police Intelligence Officer huripoti kwa wakuu mbali mbali wa polisi (IGP, CP, RPC,OCDs, OC-CIDs, OCS n.k)

Wakati Intelligence Officer wa TISS kwamjibu wa sheria Tanzania idara iliyoko chini ya ofisi ya Rais na wanawajibika kwa Rais moja kwa moja...ama atakaekasimishwa kupokea ripoti hiyo.

Lakin kimsingi kazi zao na muonekano wao are almost the same, same tactics, etc.

Thereafter kuna CID (Criminal investigation department) idara nyingine ndani ya polisi- hawa siku zote wanashughulika na matukio yakishatokea, kupeleleza kesi na kukusanya ushahidi, husonga mstari wa mbele hasa kwenye matukio ya ujambazi au uhalifu wa kutumia silaha, pia huonekana kwenye kutuliza ghasia wakiwa kiraia lakini wakivalia vest za kuzuia risasi, hao wanajihusisha na ujasusi wa ndani zaidi pia. Hapa sijagusia idara ya Usalama ya Jeshi (MI).

Military intelligence ambayo kwa Tanzania inaitwa Idara ya Utambuzi na Usalama Jeshini (MI) kazi yake kuu ni kukusanya taarifa za kijeshi ndani na nje ya nchi, inafanya utafiti kwa kukukusanya taarifa, kuzichakata, na kuzidurufu zote, Lakini pia inafanya shughuli za kiraia pia ambazo maranyingi huwa zinafanywa na TISS. Hii nayo imewekwa kila maeneo ya nchi kwamaslahi ya nchi in a militias zaidi.

UJASUSI ni baba wa yote hayo hapo juu. Hawa wote kwapamoja wanaitwa MAJASUSI na wanafanya kazi ya UJASUSI chini ya Idara/Taasisi za UJASUSI. Lakini katika fasili stahiki ya kiswahili, Jasusi ni yule afisa usalama anayefanya kazi baina ya nchi na nchi au nje ya nchi yake na hata ndani ya nchi yake lakini kwa maslahi ya nchi nyingine.

Kwaundani zaidi, Soma Kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi.

Pata kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi popote ulipo kwa gharama ndogo kabisa ya 80,000 tu.

Nunua sasa kwa
0715865544
0755865544
(Yericko Nyerere).

Dar ni Free delivery.
Nje ya Dar nauli ni 8,000

FB_IMG_1685032320015.jpg
 
Basi TISS na MI zimeshindwa kazi yake.

Kama Mr Kuku, JATU walipita na pesa za watu na TISS hawakutoa alert kwa watu wanaohusika hadi mabilioni yakaliwa TISS hawana kazi vinginevyo hizo pesa zilimnufaisha Sponsor
Una uhakika hao uliowataja hawakipata mgao wao. Maana hapa bongo inshu ya TEGETA ESCROW majaji maaskofu mapadre mawaziri wabunge walipata migao yao.
 
Elimu uliyotoa hapa,ni very shallow,Haina Cha upekee,labda kwa vijana wenye elimu ya kidato Cha nne kushuka chini.
Mambo ya ujasusi,usalama wa taifa,elimu IPO nyingi mtandaoni.
Ukitaka kujua operations,na jinsi hizi taasisi za national intelligence,military intelligence,police intelligence,ni kusoma vitabu vya historia ya mossad,CIA,kgb,vilivyoandikwa na majasusi wastaafu,au waandishi wa habari wenye upeo mkubwa kuhusu haya mambo,
KGB,tafuta vitabu vya general oreg kalugin,kuhusu FBI,CIA,soma watu kama Edgar Hoover,Au wakurugenzi wastaafu wa CIA,NSA nk.
Miaka ya 90,Elvis Musiba kwenye novel zake za legendary Willy Gamba,alielezea vzr sana operations za kijasusi kuliko unachokieleza hapa!!
Haupo deep bro!!!!
 
Ni 20% tu ya ulichoandika ndiyo kina ukweli.

Huoni aibu kuweka mambo yasiyo sahihi mbele ya wanayoyajua? Tena kupitia maandishi ya kitabu?
Kufahamu haya mambo lazima ujue majukumu ya taasisi wanazotumikia kwanza kabla ya kuchanganya majukumu ya intelijensia za JWTZ, PT na TISS.
Acha janja janja kaka!
 
Elimu uliyotoa hapa,ni very shallow,Haina Cha upekee,labda kwa vijana wenye elimu ya kidato Cha nne kushuka chini.
Mambo ya ujasusi,usalama wa taifa,elimu IPO nyingi mtandaoni.
Ukitaka kujua operations,na jinsi hizi taasisi za national intelligence,military intelligence,police intelligence,ni kusoma vitabu vya historia ya mossad,CIA,kgb,vilivyoandikwa na majasusi wastaafu,au waandishi wa habari wenye upeo mkubwa kuhusu haya mambo,
KGB,tafuta vitabu vya general oreg kalugin,kuhusu FBI,CIA,soma watu kama Edgar Hoover,Au wakurugenzi wastaafu wa CIA,NSA nk.
Miaka ya 90,Elvis Musiba kwenye novel zake za legendary Willy Gamba,alielezea vzr sana operations za kijasusi kuliko unachokieleza hapa!!
Haupo deep bro!!!!
Ahsante mkuu
Nalog off
 
Zamani walikuwa wajiandikia huu utumbo
Kinakuja kigrupu chake cha kupenea like na kulishana matango, na kumpamba sana
JF ya sasa unakula mikuki ya mbavu, ukileta vitu vya kujitungia na kuokotaokota.....
 
Back
Top Bottom