Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,150
- 137,132
Kama anajutia asamehewe tu. Adhabu ya kushambuliwa na jamii ya kimataifa inamtosha sana.
Hapana aisee. Ni muhimu apewe adhabu ya kifungo.
Kama anajutia asamehewe tu. Adhabu ya kushambuliwa na jamii ya kimataifa inamtosha sana.
Mimi ningekuwa ndio mzazi wa yule mtoto nadhani ni mimi ambae ningekuwa kizimbani leo kwa kesi tofauti kabisa...Anayeweza kusema anamsamehe ni yule mtoto aliyeteswa.
Afunge huyo dada roho mbaya al shabab wana afadhari sababu wanaua watu wazima. Video hile inatisha.mie wanangu walishindwa kuiona bali waliishia kulia tu. Pamoja na kifungo anatakiwa kuombea atokwe pepo chafu
Mimi ningekuwa ndio mzazi wa yule mtoto nadhani ni mimi ambae ningekuwa kizimbani leo kwa kesi tofauti kabisa...
Lakini ms chaga tukija kwenye vitabu vya dini anayeomba msamaha anapaswa kusamehewa embu tujiulize ni mangapi sisi tuliomkosea muumba na je kama yeye angekuwa na moyo mgumu wa kutosamehe unafikiri kuna mtu angebaki leo hii?
Sijui amefikiria iwapo mtoto angepoteza maisha ingekuaje au yule mtoto akionyeshwa ile video kweli atamsamehe. Nafiri angepimwa kwanza kama yuko vizuri kichwani nina mashaka nae huenda anatatizo la akili.
![]()
Jolly Tumuhirwe
Mfanyakazi wa nyumbani aliyenaswa kwenye kanda ya video akimchapa na kumkanyaga mtoto nchini Uganda, amefikishwa mahakamani leo.
Mfanyakazi huyo Jolly Tumuhirwe aliambia mahakama kuwa anajulia kile alichokifanya na hata kuomba msamaha. Ameshitakiwa kwa kosa la kumtesa mtoto Arnella.
Licha ya taarifa ya polisi kusema Jolly atashitakiwa kwa kosa la jaribio la ,mauaji, kiogozi wa mashitaka alimshitaki Jolly kwa kosa la kumtesa mtoto mdogo.
Jolly Tumuhirwe ameomba mahakama kumsamehe kwa kumtesa mtoto
Bi Tumuhirwe alikiri makosa yake na kuomba msamaha. Hakuna wakili yeyote aliyemwakilisha Jolly mahakamani licha ya mmoja wa mawakili mashuhuri kusema angemwakilisha Jolly bila malipo.
Kesi hio imeakhirishwa hadi Jumatano, wakati ambapo hakimu anatarajiwa kutoa hukumu yake dhidi ya Jolly.
Huenda akafungwa jela miaka 15 au kutozwa faini ya dola mianne au adhabu zote mbili.
CHANZO: BBC
Wazazi wamsamehe,ila waiache dola ifanye kazi yao!Miss u sana!msamaha utakaomfaa ni kifungo tu ili iwe fundisho kwake na kwa wengine wenye tabia kama hiyo, ule sio ubinadamu hata kidogo kumtesa mtoto mdogo vile hata kama sio wako.