Yaya aliyemtesa mtoto Uganda aomba msamaha

Yaya aliyemtesa mtoto Uganda aomba msamaha

We yule mtt ni mdogo sana, hajui hata kuongea at least angekua anaweza kuwaambia wazazi wake nini anafanyiwa.

Mie sitaki hata kuikumbuka Ile video, iliniumiza roho sana. Afungwe tu, kama hana akili atapata akili akiingia huko jela

Hivi unajua ukiwa abused,kisaikolojia inakuathiri huwezi kusema?.....watu wanabakwa hawasemi......watoto wenu wanakuwa abused na walimu kwa mboko na hawasemi.....ni watoto wachache sana wenye courage ya kusema wamepigwa/wameonewa na walimu.....na wazazi wachache sana wanaconfront walimu kwa hizi issues......mara nyingi zinakuwa ignored wakidhani watoto wao 'wanadeserve'punishments wanazopata........

Ningekubali huyu dada aende kny jela kama jela zetu zingekuwa zina
Pima watu akili na kuwapa matibabu sahihi....manake huyo dada sio mzima.....angefanyiwa counseling na kupewa follow up plan ya ugonjwa wake,waone atasaidiwa vipi kny community ili awe better individual,na kisha kuachiwa huru aishi maisha yake ila awe BANED kufanya kazi zinazohusisha watoto....na records zake zote za ugonjwa pamoja na hii event ya kupiga mtoto ziwe kny system.............ila ooh my kwa nilivyosikia issues za kuliwa kiboga huko jela lol plus matatizo ya akili,nina wasiwasi wasije wakamuabuse akatoka na roho mbaya kushinda sasa......akatoka chinja chinja looking for revenge........hii ni hatari kwa watu wa kawaida............

Hata ingekuwa mwanangu ingeniuma,ila tunajifunza kusamehe...kwa mfano hapa kuna majambazi,wachawi,wafiraji etc wote tuna madhambi yetu au kwa vile hamna cctv zinazotuona kama huyo dada??......ukiona unataka KUMKOMESHA huyo dada kwa kitendo alichofanya basi jua una roho ya kinyama ndani yako....hauna tofauti na wale wanaochoma vibaka........
 
Hivi sheria za uganda zinaelekeza nini mtu akiomba msamaha?

Mi najua ni kwenye Biblia ndio kuna haya mambo ya msamaha.

yeah! ya Mungu mpe Mungu na ya kaisari mpe kaisari, la sivyo hakuna haja ya kuwepo mahakama na mahakimu kama tayari kuna sheria.
 
Nakubaliana na wewe kabisa. Kwanza tayari keshasamehewa, kwani kitendo cha kufunguliwa mashtaka ya kutesa mtoto badala ya jaribio la kuua, tayari huo ni msamaha. Vinginevyo alikuwa anataka kuua yule, na alistahiki mashatak ya kujaribu kuua. Hivyo, angalau apigwe hata hiyo miaka 15 tu itakuwa keshasamehewa


sheria lazima ichukue mkondo wake otherwise kusingekuwa na ulazima wa kuwepo kwa sheria, au laa sheria zote zingekuwa mtu akivunja sheria na akaomba msamaha basi anasamehewa na kesi inaisha, so na ahukumiwe kulingana na kosa alilofanya, kifungo ni msamaha tosha kwake
 
Back
Top Bottom