Yanga yasimamisha maandamano msikiti wa Makonde kupisha Adhana

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,921
30,265
DAR-ES-SALAAM YANGA AFRICANS YASIMAMISHA MAANDAMANO MSIKITI WA MAKONDE ILIPOTOKA ADHANA

Waandamanaji wa Yanga waliokuwa katika maandamano makubwa wakiwa wamebeba kikombe chao cha ubingwa wa Ligi ya Tanzania walichokabidhiwa Mkwakwani Stadium Tanga wakitokea Uwanja wa Julius Nyerere wakielekea klabuni kwao walisimama kwa muda wakiwa kimya na kusimamisha ngoma zao na shamrashamra zote mara tu waliposikia adhana kutoka Msikiti wa Makonde.

Msikiti wa Makonde uko kwenye kona ya Mtaa wa Msimbazi na Swahili sehemu yenye shughuli nyingi sana nyakati za mchana.

Hapa si mbali na Mtaa wa Twiga yalipo Makao Makuu ya Yanga.

Mara waandamanaji waliposikia, "Allahu Akbar, Allah Akbar," breki za pikipiki zilizokuwa zikiongoza maandamano na magari yaliyokuwa nyuma zilipigwa.

Umma ukasimama ukiwa kimya hadi adhana ilipokamilika kuadhiniwa.

Msikiti wa Makonde ni msikiti ambao ulichelewa sana kukarabatiwa kugeuzwa kuwa msikiti wa kisasa pale misikiti ya Dar es Salaam ilipoanza kujengwa upya miaka ya 1970.

Sheikh Ali Abbas aliyekuwa mshabiki mkubwa ya Yanga ambae sasa ni marehemu alipata kuniambia kuwa ikiwa nataka kuona misikiti ya zamani ya Dar es Salaam ya 1940 niende nikasali Msikiti wa Makonde.

1687012149388.png

1687012235979.png

1687012274450.png

 
DAR-ES-SALAAM YANGA AFRICANS YASIMAMISHA MAANDAMANO MSIKITI WA MAKONDE ILIPOTOKA ADHANA

Waandamanaji wa Yanga waliokuwa katika maandamano makubwa wakiwa wamebeba kikombe chao cha ubingwa wa Ligi ya Tanzania walichokabidhiwa Mkwakwani Stadium Tanga wakitokea Uwanja wa Julius Nyerere wakielekea klabuni kwao walisimama kwa muda wakiwa kimya na kusimamisha ngoma zao na shamrashamra zote mara tu waliposikia adhana kutoka Msikiti wa Makonde.

Msikiti wa Makonde uko kwenye kona ya Mtaa wa Msimbazi na Swahili sehemu yenye shughuli nyingi sana nyakati za mchana.

Hapa si mbali na Mtaa wa Twiga yalipo Makao Makuu ya Yanga.

Mara waandamanaji waliposikia, "Allahu Akbar, Allah Akbar," breki za pikipiki zilizokuwa zikiongoza maandamano na magari yaliyokuwa nyuma zilipigwa.

Umma ukasimama ukiwa kimya hadi adhana ilipokamilika kuadhiniwa.

Msikiti wa Makonde ni msikiti ambao ulichelewa sana kukarabatiwa kugeuzwa kuwa msikiti wa kisasa pale misikiti ya Dar es Salaam ilipoanza kujengwa upya miaka ya 1970.

Sheikh Ali Abbas aliyekuwa mshabiki mkubwa ya Yanga ambae sasa ni marehemu alipata kuniambia kuwa ikiwa nataka kuona misikiti ya zamani ya Dar es Salaam ya 1940 niende nikasali Msikiti wa Makonde.

MashaaAllah
Lilikuwa ni jambo jema na bora kabisa ❤️
 
DAR-ES-SALAAM YANGA AFRICANS YASIMAMISHA MAANDAMANO MSIKITI WA MAKONDE ILIPOTOKA ADHANA

Waandamanaji wa Yanga waliokuwa katika maandamano makubwa wakiwa wamebeba kikombe chao cha ubingwa wa Ligi ya Tanzania walichokabidhiwa Mkwakwani Stadium Tanga wakitokea Uwanja wa Julius Nyerere wakielekea klabuni kwao walisimama kwa muda wakiwa kimya na kusimamisha ngoma zao na shamrashamra zote mara tu waliposikia adhana kutoka Msikiti wa Makonde.

Msikiti wa Makonde uko kwenye kona ya Mtaa wa Msimbazi na Swahili sehemu yenye shughuli nyingi sana nyakati za mchana.

Hapa si mbali na Mtaa wa Twiga yalipo Makao Makuu ya Yanga.

Mara waandamanaji waliposikia, "Allahu Akbar, Allah Akbar," breki za pikipiki zilizokuwa zikiongoza maandamano na magari yaliyokuwa nyuma zilipigwa.

Umma ukasimama ukiwa kimya hadi adhana ilipokamilika kuadhiniwa.

Msikiti wa Makonde ni msikiti ambao ulichelewa sana kukarabatiwa kugeuzwa kuwa msikiti wa kisasa pale misikiti ya Dar es Salaam ilipoanza kujengwa upya miaka ya 1970.

Sheikh Ali Abbas aliyekuwa mshabiki mkubwa ya Yanga ambae sasa ni marehemu alipata kuniambia kuwa ikiwa nataka kuona misikiti ya zamani ya Dar es Salaam ya 1940 niende nikasali Msikiti wa Makonde.

Hii nayo Habari ya kuleta hapa. Mi nilifikiri wameandama kisa Bandari imeuzwa kumbe upuuzi wa mpira
 
Mida wa Adhana na kushusha Bendera haipishani Sana, hao waandamanaji walikuwa Wazalendo kiasi gani, au ni wadini tu kama mtoa mada?!
 
Hii nayo Habari ya kuleta hapa. Mi nilifikiri wameandama kisa Bandari imeuzwa kumbe upuuzi wa mpira
The....
Huu ni ukumbi huru mtu anaweza kuweka chochote anachopenda.

Hapakuwa na haja ya kutoa maneno yasiyopendeza.

Soma habari ya bandari hapo chini:
(Hii makala nilimwandikia mtu wa mfano wako nahali fulani).

CHUKI DHIDI YA WAZANZIBARI

Nasikitika sana kila ninaposoma hapa maneno yaliyojaa chuki, dharau na kejli dhidi ya Wazanzibari.

Picha niipatayo ni kuwa wengi wanaoonyesha chuki hizi sababu kubwa ni kuwa hawajui historia iliyopelekea mapinduzi ya Zanzibar mwaka wa 1964.

Historia ya kupigania uhuru wa Zanzibar ina mengi na Rais wa TANU Mwalimu Nyerere alihusika sana kwanza katika kusaidia kuundwa kwa ASP na kisha katika kusaidia kufanya mapinduzi kuangusha serikali ya ZPPP na ZNP.

Baada ya mapinduzi ndiyo nchi hizi mbili zikaungana kufanya Tanzania hii tunayoiona hivi sasa.

Kabla ya mapinduzi Zanzibar ilikuwa nchi huru kama ilivyokuwa Tanganyika.

Kwa nini Mwalimu alisaidia kuangusha serikali iliyokuwapo madarakani?

Wakati wa kupigania uhuru wa Zanzibar kulikuwa na propaganda kubwa kuhusu historia ya utumwa ikisemwa Waafrika waliteswa na Waarabu na ni lazima Waafrika walioko Zanzibar wasaidiwe kujikomboa.

Propaganda hizi zikawa sababu kubwa ya chaguzi za Zanzibar zikawa zenye vurugu na damu kumwagika.

Lakini katika propaganda hizi suala la Uislam Zanzibar halikujitokeza na sababu kubwa halikujitokeza ni kuwa Wazanzibari wote ni Waislam.

Ilipokuwa ASP imeshindwa uchaguzi na serikali ikawa ni ya ZPPP/ ZNP uamuzi wa ASP ukawa lazima yafanyike mapinduzi na Tanganyika ikasaidia sana kuhakikisha kuwa serikali ya Zanzibar inapinduliwa.

Serikali ikaanguka na baada ya kuanguka serikali Zanzibar na Tanganyika zikaungana.

Hapakuwa na hofu yeyote hata kwa mbali kuwa Tanganyika inaungana na Zanzibar nchi ya Waislam watupu.

Wala Zanzibar haikuwa na hofu kuwa Tanganyika ina Wakristo na hawa wanaweza wakawa tatizo kwao hapo baadae.

Kwa kipindi kirefu hapakuwa na chokochoko zozote kuhusu Zanzibar na Uislam wao ndani ya muungano.

Matatizo yalitokea kwa mara ya kwanza Zanzibar ilipojiunga na OIC mwaka wa 1993.

Hiki ni kisa kirefu lakini muhimu kilichojitokeza ni kuwa Zanzibar ilitambua kuwa itastahamiliwa katika muungano pale pindi itakapojiweka mbali na Uislam na Waislam.

Hapa ndipo linapokuja tatizo la "Waarabu" na Bandari ya Dar es Salaam.

Lakini hizi ni nchi mbili zilizokuwa huru na Zanzibar haikuwa na shida ya kuungana na Tanganyika.

Leo tunasoma hapa watu wanaandika maneno makali ya kutisha kuwa Wazanzibari wafukuzwe Tanganyika.

Maneno haya hayapendezi.
 
Wee mzee punguza udini, sasa yanga kusimama kupisha adhana nayo habarii??
Coca...
"Wee mzee," kunita hivi si adabu.
Unaweza ukasema, "Mzee Mohamed."

Hii ghadhabu yako ni kwa mimi kutaja adhana?
Hili ndilo limekuudhi?

Unaijua historia ya mji huu wa Dar-es-Salaam watu wa dini tofauti walivyokuwa wanastahiana?
Hujaona picha za Mwalimu Nyerere yuko peke yake katikati ya Waislam?

Hii chuki wewe kakufunza nani?
 
Ndio ni habari, na Allah amzidishie kheri huyu ndugu yetu Mohamed Said

So, Kuwa na heshima kwa huyu mzee, na kwa wote bila kujali umri, aleyommba gekke, kuwa na heshima, na uache mara moja kumuita "wee mzee" mzee said ni sawa na baba au babu yako.
Sol...
Hiyo picha ya kwanza ni ya Shariff Abdallah Attas.

Shariff Attas alikuwa mkusanyaji ushuru Kariakoo Market.
Market Master Abdul Sykes.

Mwalimu Nyerere alipoacha kazi ya ualimu 1955 akaenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes.
Hapa ndipo Nyerere alipojuana na Shariff Attas kwa karibu sana.

Asubuhi Mwalimu akawa anakwenda ofisini kwa Abdul Sykes kusoma magazeti na kuonana na watu mashuhuru wa Dar es Salaam na pale atakaa hadi mchana wakati wa chakula.

Ikifika muda huo Shariff Attas atamchukua Mwalimu watakwenda pamoja nyumbani kwa Abdul Sykes kwa ajili ya chakula cha mchana.

Abdul anabakia ofisini kwake kuendelea na kazi.

Picha ya pili wa kwanza kulia ni Bi. Chiku bint Said Kisusa mke wa Shariff Attas akimsindikiza Mwalimu Nyerere Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam safari ya kwanza UNO 1955.

Yuko Bi, Tatu bint Mzee na Bi. Titi Mohamed na Mwalimu huyo hapo katikati.

Picha ya tatu ni Abdul Sykes Ukumbi wa Arnautoglo katika dhifa ya kumuaga Nyerere safari ya pili UNO 1956.

Safari ya kwanza UNO Mwalimu aliagwa ndani ya jengo la Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Hii ndiyo historia ya nchi yetu.

Hii ndiyo misingi ya umoja iliyowekwa na wazee wetu.

1687200114859.jpeg

Shariff Abdallah Omar Attas
View attachment 2662586
1687200911571.jpeg


 
DAR-ES-SALAAM YANGA AFRICANS YASIMAMISHA MAANDAMANO MSIKITI WA MAKONDE ILIPOTOKA ADHANA

Waandamanaji wa Yanga waliokuwa katika maandamano makubwa wakiwa wamebeba kikombe chao cha ubingwa wa Ligi ya Tanzania walichokabidhiwa Mkwakwani Stadium Tanga wakitokea Uwanja wa Julius Nyerere wakielekea klabuni kwao walisimama kwa muda wakiwa kimya na kusimamisha ngoma zao na shamrashamra zote mara tu waliposikia adhana kutoka Msikiti wa Makonde.

Msikiti wa Makonde uko kwenye kona ya Mtaa wa Msimbazi na Swahili sehemu yenye shughuli nyingi sana nyakati za mchana.

Hapa si mbali na Mtaa wa Twiga yalipo Makao Makuu ya Yanga.

Mara waandamanaji waliposikia, "Allahu Akbar, Allah Akbar," breki za pikipiki zilizokuwa zikiongoza maandamano na magari yaliyokuwa nyuma zilipigwa.

Umma ukasimama ukiwa kimya hadi adhana ilipokamilika kuadhiniwa.

Msikiti wa Makonde ni msikiti ambao ulichelewa sana kukarabatiwa kugeuzwa kuwa msikiti wa kisasa pale misikiti ya Dar es Salaam ilipoanza kujengwa upya miaka ya 1970.

Sheikh Ali Abbas aliyekuwa mshabiki mkubwa ya Yanga ambae sasa ni marehemu alipata kuniambia kuwa ikiwa nataka kuona misikiti ya zamani ya Dar es Salaam ya 1940 niende nikasali Msikiti wa Makonde.

Unafiki tu huo wanaheshi adhana lakini walio wengi hata hawaswali
 
Mzee mdini sanaa wee, basi hapo roho yakoo kwatuu. Lol
kazi ipo.
Dhana ya kuheshimu uhuru wa wengine ni ngumu sana kwetu wanadamu.

Kuna siku nasikiliza CNN, wanacover namna LGBT wananyanyasika kwenye blacks community Marekani, sikutegemea kwa namna wao wanavyopigania BLM wawe wanalalamikiwa kunyanyasa wengine.
 
Back
Top Bottom