John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imekutana leo Mei 20, 2022 kusikiliza mashauri yaliyowasilishwa yakiwahusu Ofisa wa Yanga, Haji Manara na Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez.
Katika mashauri hayo Yanga iliwasilisha malalamiko yake kuhusu Barbara ikidai aliichafua Yanga alipokuwa akihojiwa na kituo cha redio Nchini Afrika Kusini hici karibuni.
Simba nayo iliwasilisha malalamiko kuhusu Manara kutoa shutuma zisizo na ukweli kuhusu Simba kupitia mitandao ya kijamii. Mashtaka yalianza kusikilizwa Mei 14, 2022 na yataendea kusikilizwa hadi Mei 21, 2022.