Majok majok
JF-Expert Member
- Aug 3, 2023
- 609
- 1,563
CAF wanathibitisha ubora wa Yanga kivitendo ndio maana wameiteua kuingia kwenye tuzo zao za kuchagua Timu Bora barani Africa kwa mwaka 2023.
Yanga ni timu pekee kwa Ukanda wa Africa Mashariki iliyoingia kugombania tuzo hizo!
Yanga hawakuingia kwa bahati mbaya bali wamebebwa kwa mafanikio yao na usajili bora wa kikosi husika walichonacho, ndio maana pia wametoa Kipa Djigui Diara kugombania tuzo ya kipa Bora barani Afrika!
Unaposema timu yako ni Bora basi CAF wenyewe ndio wenye vigezo halisi vya kujua timu gani ni Bora na sio propaganda za kwenye mitandao na vijiwe vya kahawa!
Timu nyingine ambazo kutwa nzima zinashinda kwenye media na kujiita Bora sijaziona na wala sijaona hata mchezaji wao mmoja ameingia kwenye tuzo hizo za Afrika, kupiga domo na porojo bila uhalisia ni sawa na kumnyemelea kiziwi ukidhani anakusikia!
Kitendo cha CAF kuichagua Yanga kuingia kwenye tuzo hizo ni ishara tosha ya kwamba yanga iko vizuri na itaendelea kuwa vizuri siku hadi siku!
Kongole Eng. Hersi Said na Menejiment nzima kwa kazi kubwa mnayoendelea kuifanya na Mungu awabariki.👏👏👏👏
Yanga ni timu pekee kwa Ukanda wa Africa Mashariki iliyoingia kugombania tuzo hizo!
Yanga hawakuingia kwa bahati mbaya bali wamebebwa kwa mafanikio yao na usajili bora wa kikosi husika walichonacho, ndio maana pia wametoa Kipa Djigui Diara kugombania tuzo ya kipa Bora barani Afrika!
Unaposema timu yako ni Bora basi CAF wenyewe ndio wenye vigezo halisi vya kujua timu gani ni Bora na sio propaganda za kwenye mitandao na vijiwe vya kahawa!
Timu nyingine ambazo kutwa nzima zinashinda kwenye media na kujiita Bora sijaziona na wala sijaona hata mchezaji wao mmoja ameingia kwenye tuzo hizo za Afrika, kupiga domo na porojo bila uhalisia ni sawa na kumnyemelea kiziwi ukidhani anakusikia!
Kitendo cha CAF kuichagua Yanga kuingia kwenye tuzo hizo ni ishara tosha ya kwamba yanga iko vizuri na itaendelea kuwa vizuri siku hadi siku!
Kongole Eng. Hersi Said na Menejiment nzima kwa kazi kubwa mnayoendelea kuifanya na Mungu awabariki.👏👏👏👏