Yaliyonikuta leo stanbic bank kariakoo sokoni

Yaliyonikuta leo stanbic bank kariakoo sokoni

magilapeak

Senior Member
Joined
Aug 6, 2013
Posts
132
Reaction score
27
Wakuu leo majira ya saa sita na nusu mchana nilienda kulipa school fees ya kijana wangu benki ya stanbic tawi la kariakoo sokoni, nikampa cashier bundle la pesa akazitia kwenye mashine, moja ya noti za shs 10000 ikakwama, basi cashier akatabasamu, akaniambia ile noti ni fake,nikaichukua nikaiangalia,water marks zote zipo vizuri,na sio fake, nikamuomba staff mwenzake pale receiption aiangalie maana mteja ndani mle nilikuwa mimi tu, akaangalia akasema iko sawa, niliporudi kwa cashier nikakuta ndani ya teller counter vijana wawili wako nae ndani, nikamrudishia cashier aendelee, yeye akang'ang'ania kuwa ni feki na wale vijana nao wakaangalia wakawa wanam-support yule cashier lakini nikaona kabisa ni mchezo wa kuigiza, nikamwambia anirudishe ili nimpe noti nyingine. hapo ndipo shughuli ilipoanza,mmoja wa wale vijana kule ndani mweupe hivi akasema haiwezekani, lazima tuitoboe akimaanisha mi niondoke au anikabidhi kwa askari, akiwa kama anaenitisha, sasa mle ndani niko peke yangu, ikabidi nimpigie jamaa yangu alie jirani na eneo ili anisaidie, akasema anakuja, nilipokata simu tu, yule kijana mweupe akaniambia chukua hela yako zoezi la kunikabidhi kwa askari likaishia hapo, tafsiri yake walikuwa wanataka kunidhulumu elf kumi yangu.sasa nimebaki na swali benki sio sehemu salama tena?
 
safi sana kama umekomaa wakakurudishi...ndio mtindo wao huo na ule wa kudondosha noti chini ya miguu yake kabla ya kuweka kwenye mashine ya kuhesabia.. nikiendaga benki huwa natoa macho kila step coz walishaniliza.....
 
Wakuu leo majira ya saa sita na nusu mchana nilienda kulipa school fees ya kijana wangu benki ya stanbic tawi la kariakoo sokoni, nikampa cashier bundle la pesa akazitia kwenye mashine, moja ya noti za shs 10000 ikakwama, basi cashier akatabasamu, akaniambia ile noti ni fake,nikaichukua nikaiangalia,water marks zote zipo vizuri,na sio fake, nikamuomba staff mwenzake pale receiption aiangalie maana mteja ndani mle nilikuwa mimi tu, akaangalia akasema iko sawa, niliporudi kwa cashier nikakuta ndani ya teller counter vijana wawili wako nae ndani, nikamrudishia cashier aendelee, yeye akang'ang'ania kuwa ni feki na wale vijana nao wakaangalia wakawa wanam-support yule cashier lakini nikaona kabisa ni mchezo wa kuigiza, nikamwambia anirudishe ili nimpe noti nyingine. hapo ndipo shughuli ilipoanza,mmoja wa wale vijana kule ndani mweupe hivi akasema haiwezekani, lazima tuitoboe akimaanisha mi niondoke au anikabidhi kwa askari, akiwa kama anaenitisha, sasa mle ndani niko peke yangu, ikabidi nimpigie jamaa yangu alie jirani na eneo ili anisaidie, akasema anakuja, nilipokata simu tu, yule kijana mweupe akaniambia chukua hela yako zoezi la kunikabidhi kwa askari likaishia hapo, tafsiri yake walikuwa wanataka kunidhulumu elf kumi yangu.sasa nimebaki na swali benki sio sehemu salama tena?

Kama walitaka kuitoboa wangefaidika vipi?

Hizi mashine za kuhakiki noti zina precision gani?

Je, haiwezekani kwamba mashine imekosea na hivyo wewe huna makosa na wao hawana makosa kwa kutaka kutoboa/ kuhusisha polisi kwa walichofikiri ni noti isiyo halali?

Hivi noti isiyo halali iliyochapwa kwa ufundi kabisa, hawa watu wa benki wanaweza kuigundua kwa macho? Naangalia uwezekano wa kwamba nioti ni halali na mashine imekosea, na hawa watu wanaamini mashine haikosei kwa hiyo wanafikiri tu noti si halali.

Pia, una hakika noti yako ni halali?

Unakumbuka uliipata wapi? Ilikuwa mpya au chakavu? Ilikuwa katika serial numbers za kufuatana na hizo zilizokubaliwa? Maana kama kuna muendelezo wa serial numbers (kama umetoka kuzitoa kwenye ATM na ni mpya) halafu tisa zinakubaliwa, moja inakataliwa na mashine, hapo unaweza kusema mashine imechemsha.
 
Wakuu leo majira ya saa sita na nusu mchana nilienda kulipa school fees ya kijana wangu benki ya stanbic tawi la kariakoo sokoni, nikampa cashier bundle la pesa akazitia kwenye mashine, moja ya noti za shs 10000 ikakwama, basi cashier akatabasamu, akaniambia ile noti ni fake,nikaichukua nikaiangalia,water marks zote zipo vizuri,na sio fake, nikamuomba staff mwenzake pale receiption aiangalie maana mteja ndani mle nilikuwa mimi tu, akaangalia akasema iko sawa, niliporudi kwa cashier nikakuta ndani ya teller counter vijana wawili wako nae ndani, nikamrudishia cashier aendelee, yeye akang'ang'ania kuwa ni feki na wale vijana nao wakaangalia wakawa wanam-support yule cashier lakini nikaona kabisa ni mchezo wa kuigiza, nikamwambia anirudishe ili nimpe noti nyingine. hapo ndipo shughuli ilipoanza,mmoja wa wale vijana kule ndani mweupe hivi akasema haiwezekani, lazima tuitoboe akimaanisha mi niondoke au anikabidhi kwa askari, akiwa kama anaenitisha, sasa mle ndani niko peke yangu, ikabidi nimpigie jamaa yangu alie jirani na eneo ili anisaidie, akasema anakuja, nilipokata simu tu, yule kijana mweupe akaniambia chukua hela yako zoezi la kunikabidhi kwa askari likaishia hapo, tafsiri yake walikuwa wanataka kunidhulumu elf kumi yangu.sasa nimebaki na swali benki sio sehemu salama tena?

Hakuna bank wababaishaji kama Stanbic..walitakaga kumfanyia mchezo bi mkubwa kwenye account yake akiwahoji wanajibu dharau alichofanya alirusha makonde kisha akaenda kwa operation manager..mimi ndio nilikua mratibu wa ndundi hizo mbaka walirudisha pesa kwenye account..chezea mwanamke wa kingoni...Bank nyingine kwa UTAPELI NI TWIGA BANCORP
 
Kudadadeki!
Mkuu bora ulivyokomaa, mwizi mwizi tu hata akipewa uraisi ataendelea kuiba!
 
Mchezo huo upo sana na Bandarini pale long room...kuna siku nilikua nalipia ushuru wa gari jamaa akaniliza 30,000 akasingizia zimepungua wakati pesa nilikuwa nimetoka kuzitoa bank muda huo huo na sijatoa hata sent. Nilikasirika na nilizua timbwili kubwa sana pale...yaani wezi sana bank tellers...kuna haja ya kutoa mimacho uangalie kila anachofanya hasa unapoweka pesa nyingi....
 
Hakuna bank wababaishaji kama Stanbic..walitakaga kumfanyia mchezo bi mkubwa kwenye account yake akiwahoji wanajibu dharau alichofanya alirusha makonde kisha akaenda kwa operation manager..mimi ndio nilikua mratibu wa ndundi hizo mbaka walirudisha pesa kwenye account..chezea mwanamke wa kingoni...Bank nyingine kwa UTAPELI NI TWIGA BANCORP

Fafanua kidogo, alikuta hela pungufu?
 
Na hivyo vituo vya fedha za simu za viganjani ni kuwa makini sana navyo
 
Wanataka maisha mazuri wa-drive infinity wajenge mbezi beach kwa fedha za wizi umewakomesha kweli.
 
Fafanua kidogo, alikuta hela pungufu?

wanatabia ya kudokoa ndio maana wale tellers vijana anaanza kazi leo kesho ana altezza..mi nina washakaj zng wajk\\ko kwenye mabenki na wananithibitishia nhilo tena they're very proud of it!
 
Hawa watumishi wa benk waboreshewe maslahi yao waache tamaa,sisi wateja pia tuna shida zetu.
 
wanatabia ya kudokoa ndio maana wale tellers vijana anaanza kazi leo kesho ana altezza..mi nina washakaj zng wajk\\ko kwenye mabenki na wananithibitishia nhilo tena they're very proud of it!

Ok thanks
 
Hizi bank haziwawekei camera hao tellers? Mbona teknolojia hii ipo bwerere siku hizi?
 
Back
Top Bottom