The Sheriff
JF-Expert Member
- Oct 10, 2019
- 617
- 1,801
Habari Wakuu,
Leo 10/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Shahidi Tumaini Swila jana Februari 9, 2022 aliomba ahirisho kwakuwa alikuwa hajisikii vizuri.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani Muda huu
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa
Wakili wa Serikali, Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba tuhairishe Kesi Mpaka Jumatatu, Kama atakuwa bado hajapona tunaweza Kutafuta Shahidi Mwingine Pia Mheshimiwa Jaji Kwa kutii Agizo la Mahakama Shahidi ameweza Kumtumia Ndugu yake aweze Kuja na Cheti cha Hospitali, lakini Original yake anaweza Kuja nayo yeye Mwenyewe pale atakapo pona
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba kama Dakika Moja na sisi tuweze Kuangalia Cheti cha Hospitali.
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Ndugu yangu Nassoro Katuga Nikianza na Hoja yenyewe ya Nyaraka Kutoka Hospitali, Nakumbuka Wakati natoa Hoja Jana, Tuliomba Shahidi atuletee Karatasi Kutoka Hospitali ya Serikali ambapo pia nafahamu Kwamba Askari Polisi anapopatwa na Ugonjwa anatakiwa kwenda huko, Nyaraka Walio leta Wenzetu Inatoka TMJ Super Polyclinic hii siyo Hospitali Ya Serikali Nyaraka hii inazidi Kuweka Wasiwasi zaidi Kwa Nini Mtu aende Kwenye Hospitali ambayo Haifahamiki
Nafikiri Jana tulikubaliana kuwa aje na Uthibitisho kutoka Hospitali ya Serikali Naomba Mahakama Ione kuwa sababu haina Logic wala hazipo Kama Mahakama itaona tofauti Basi Wenzetu Wasisitizwe
Kwa Mujibu Sheria Kesi katika Mahakama hii inatakiwa iishe ndani ya Miezi 9 Tukienda Kwa Mwenendo huu tutalazimika Kuomba Muda wa Nyongeza Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
Jaji: Hoja ya Kuhusu airisho Sijaona kama Umezungumzia Kuhusu Muda wa airisho
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Jumatatu ni Mbali sana, Kwa Vyovyote itakayokuwa, Sasa ni saa Nne, Mpka Kesho Saa Nne ni Zaidi ya Masaa 24 Wana akiba ya Mashahidi 11 zaidi. Basi tutafute kati hao Mashahidi 11 angalau tuairishe Kwa Leo tuweze Kuja Kuendelea Kesho
Wakili wa Serikali Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Wenzetu Kutoka kwa Wakili Peter Kibatala Wenzetu Wanasema Kwamba Shaeria na Tangazo la Serikali namba 259 inataka Kumaliza shauri hili ndani ya Miezi 9 tunalifahamu na tumelichukua
Suala la tukishindwa Kuleta Shahidi huyu, tulete shahidi Mwingine nalo tumelichukua Suala la Shahidi Kuleta Cheti cha Hospitali ya Serikali, Shahidi Tulikuwa tunaona hapa tangu Mwanzo Kila Muda alikuwa anaomba Kwenda Msalani Huko Ndipo alipo kuwa anatibiwa kupitia Daktari Wake
Kupata tiba kutoka kwa Daktari Wake ni Nusu ya tiba, Kuhusu Wasiwasi Wa hapo anapotibiwa wanaweza Kwenda Kuuliza na Kuonana na Daktari Wake. Tunasisitiza Sisi Ka Maafisa wa Mahakama hatufurahishwi na airisho Lolote Pasipo Sababu.
Kuhusu Kuairisha Mpaka Kesho na Sitakukubali Kwamba tuje Kesho halafu tukaja na Hadithi ya Kukosa Shahidi. Ndiyo Maana tukaomba tuahirishe Mpaka Jumatatu ili kama Shahidi hata Kama anatakiwa Kusafiri atakuwa amefika
Sisi tunaona Kuwa ni Busara Kuairisha Mpaka Kesho halafu tukaja na story, Mahakama Yako itachoka Kutusikiliza. Sisi tunaomba tupewe airisho Mpaka Jumatatu. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.
Mahakama ipo kimya kusubiri uamuzi mdogo wa Mheshimiwa Jaji (10:15 AM)
Bado Mahakama ipo kimya (10:27 AM)
Jaji: nimesikia Hoja zilizotolewa na pande zote mbili Kama ambavyo Imetolewa na Upande Wa Mashtaka Mahakama hii imekuwa na Spirit ya Kutaka Shauri liishe kwa Haraka nimekuwa nikisisitiza Mawakili wa pande zote Mbili kuzingatia Spirit hii
Ila jana Wakati Shahidi anatoa Ushahidi wake, Shahidi Aliomba Kusitisha Kutoa Ushahidi Na Kwenda Kupata Matibabu Maombi hayo Kwa kuwa yalikuwa ya Msingi, Mahakama Ilielekeza Kuwa Shahidi atakapo rudi Mahakamani Hapa atalazimika kululetea Uthibitisho
Mahakama Haikusema Uthibitisho huo lazima utoke Hospitali ya Serikali, Kwa sababu suala la Matibabu ni la Mtu Binafsi Mahakama ilisita Kutoa Maelekezo hayo Ingekuwa inaingilia Mambo Mengine
Nyaraka iliyokuja hapa Shahidi amepata Uthibitisho Kuanzia Tarehe 9 Mpaka 11 February
Kwa Maana hiyo Shahidi Kwa Kesho Hawezi Kuwepo Upande wa Mashtaka Wanasema Kwamba hawawezi Kuomba airisho Mpaka Kesho Sababu wanaogopa Kuja Kesho bila Shahidi.
Kwa sababu hiyo ni Busara Ya Mahakama Inaona ni Vizuri Kuairisha Mpaka Siku ambayo Shahidi ataweza Kuja Mahakamani
Kwa sababu Hiyo naairisha Mpaka Jumatatu na Kuelekea Upande wa Mashtaka Kuhakikisha Kuwa Jumatatu wanakuja na Shahidi hata Kama yule atakuwa bado hajapona Waje na Mwingine
Kwa Maana hiyo na airisha Shauri Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi na Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Siku hiyo
Jaji anatoka
Leo 10/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3. Shahidi Tumaini Swila jana Februari 9, 2022 aliomba ahirisho kwakuwa alikuwa hajisikii vizuri.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Swila aomba ahirisho kuwa hajisikii vizuri; kuendelea na ushahidi 10/02/2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani Muda huu
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa na Mohamed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa
Wakili wa Serikali, Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
- Pius Hilla
- Esther Martin
- Jenitreza Kitali
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Kuwatambulisha Mawakili
- Jeremiah Mtobesya
- Fredrick Kihwelo
- Sisty Aloyce
- Iddi Msawanga
- Michael Mwangasa
- Edward Heche
- Gaston Garubindi
- Hadija Aron
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji naomba tuhairishe Kesi Mpaka Jumatatu, Kama atakuwa bado hajapona tunaweza Kutafuta Shahidi Mwingine Pia Mheshimiwa Jaji Kwa kutii Agizo la Mahakama Shahidi ameweza Kumtumia Ndugu yake aweze Kuja na Cheti cha Hospitali, lakini Original yake anaweza Kuja nayo yeye Mwenyewe pale atakapo pona
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Naomba kama Dakika Moja na sisi tuweze Kuangalia Cheti cha Hospitali.
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Ndugu yangu Nassoro Katuga Nikianza na Hoja yenyewe ya Nyaraka Kutoka Hospitali, Nakumbuka Wakati natoa Hoja Jana, Tuliomba Shahidi atuletee Karatasi Kutoka Hospitali ya Serikali ambapo pia nafahamu Kwamba Askari Polisi anapopatwa na Ugonjwa anatakiwa kwenda huko, Nyaraka Walio leta Wenzetu Inatoka TMJ Super Polyclinic hii siyo Hospitali Ya Serikali Nyaraka hii inazidi Kuweka Wasiwasi zaidi Kwa Nini Mtu aende Kwenye Hospitali ambayo Haifahamiki
Nafikiri Jana tulikubaliana kuwa aje na Uthibitisho kutoka Hospitali ya Serikali Naomba Mahakama Ione kuwa sababu haina Logic wala hazipo Kama Mahakama itaona tofauti Basi Wenzetu Wasisitizwe
Kwa Mujibu Sheria Kesi katika Mahakama hii inatakiwa iishe ndani ya Miezi 9 Tukienda Kwa Mwenendo huu tutalazimika Kuomba Muda wa Nyongeza Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
Jaji: Hoja ya Kuhusu airisho Sijaona kama Umezungumzia Kuhusu Muda wa airisho
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Jumatatu ni Mbali sana, Kwa Vyovyote itakayokuwa, Sasa ni saa Nne, Mpka Kesho Saa Nne ni Zaidi ya Masaa 24 Wana akiba ya Mashahidi 11 zaidi. Basi tutafute kati hao Mashahidi 11 angalau tuairishe Kwa Leo tuweze Kuja Kuendelea Kesho
Wakili wa Serikali Nasorro Katuga: Mheshimiwa Jaji Tumesikia Hoja ya Wenzetu Kutoka kwa Wakili Peter Kibatala Wenzetu Wanasema Kwamba Shaeria na Tangazo la Serikali namba 259 inataka Kumaliza shauri hili ndani ya Miezi 9 tunalifahamu na tumelichukua
Suala la tukishindwa Kuleta Shahidi huyu, tulete shahidi Mwingine nalo tumelichukua Suala la Shahidi Kuleta Cheti cha Hospitali ya Serikali, Shahidi Tulikuwa tunaona hapa tangu Mwanzo Kila Muda alikuwa anaomba Kwenda Msalani Huko Ndipo alipo kuwa anatibiwa kupitia Daktari Wake
Kupata tiba kutoka kwa Daktari Wake ni Nusu ya tiba, Kuhusu Wasiwasi Wa hapo anapotibiwa wanaweza Kwenda Kuuliza na Kuonana na Daktari Wake. Tunasisitiza Sisi Ka Maafisa wa Mahakama hatufurahishwi na airisho Lolote Pasipo Sababu.
Kuhusu Kuairisha Mpaka Kesho na Sitakukubali Kwamba tuje Kesho halafu tukaja na Hadithi ya Kukosa Shahidi. Ndiyo Maana tukaomba tuahirishe Mpaka Jumatatu ili kama Shahidi hata Kama anatakiwa Kusafiri atakuwa amefika
Sisi tunaona Kuwa ni Busara Kuairisha Mpaka Kesho halafu tukaja na story, Mahakama Yako itachoka Kutusikiliza. Sisi tunaomba tupewe airisho Mpaka Jumatatu. Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji.
Mahakama ipo kimya kusubiri uamuzi mdogo wa Mheshimiwa Jaji (10:15 AM)
Bado Mahakama ipo kimya (10:27 AM)
Jaji: nimesikia Hoja zilizotolewa na pande zote mbili Kama ambavyo Imetolewa na Upande Wa Mashtaka Mahakama hii imekuwa na Spirit ya Kutaka Shauri liishe kwa Haraka nimekuwa nikisisitiza Mawakili wa pande zote Mbili kuzingatia Spirit hii
Ila jana Wakati Shahidi anatoa Ushahidi wake, Shahidi Aliomba Kusitisha Kutoa Ushahidi Na Kwenda Kupata Matibabu Maombi hayo Kwa kuwa yalikuwa ya Msingi, Mahakama Ilielekeza Kuwa Shahidi atakapo rudi Mahakamani Hapa atalazimika kululetea Uthibitisho
Mahakama Haikusema Uthibitisho huo lazima utoke Hospitali ya Serikali, Kwa sababu suala la Matibabu ni la Mtu Binafsi Mahakama ilisita Kutoa Maelekezo hayo Ingekuwa inaingilia Mambo Mengine
Nyaraka iliyokuja hapa Shahidi amepata Uthibitisho Kuanzia Tarehe 9 Mpaka 11 February
Kwa Maana hiyo Shahidi Kwa Kesho Hawezi Kuwepo Upande wa Mashtaka Wanasema Kwamba hawawezi Kuomba airisho Mpaka Kesho Sababu wanaogopa Kuja Kesho bila Shahidi.
Kwa sababu hiyo ni Busara Ya Mahakama Inaona ni Vizuri Kuairisha Mpaka Siku ambayo Shahidi ataweza Kuja Mahakamani
Kwa sababu Hiyo naairisha Mpaka Jumatatu na Kuelekea Upande wa Mashtaka Kuhakikisha Kuwa Jumatatu wanakuja na Shahidi hata Kama yule atakuwa bado hajapona Waje na Mwingine
Kwa Maana hiyo na airisha Shauri Mpaka Jumatatu Saa 3 Asubuhi na Washtakiwa Wataendelea Kuwa Rumande chini ya Magereza Mpaka Siku hiyo
Jaji anatoka