Mzee Mwanakijiji;991260]Hii commitment ya dhati wewe unaijuaje?
Mkuu,list of shame,kufukua EPA na skandali nyingine bado haitoshi kuonyesha angalau Chadema wamekwenda mbali zaidi ya kutoa maneno pasipo vitendo?Na pengine,kama wasemavyo Waingereza,the answer is in the question.Kwani wewe commitment ya dhati ya CCJ wewe uliionaje?
Hiyo "dhamira ya dhati" kwa wanandoa unaiona vipi? Si inaanzia na kwenye "Ndiyo nataka".. baada ya kuulizwa "Je wewe x,y unakubali kumchukua".. au ndiyo mnasema tu tutajua mbele ya safari hiyo commitment?
Ofkoz,Chadema wameshatuonyesha wanataka kukomesha ufisadi kwa kuwatangaza mafisadi hadharani,kisha mafisadi wakatusaidia kuthibithisha tuhuma hizo kwa kutishia kwenda mahakamani lakini hakuna mmoja wao aliyefanya hivyo.Kwahiyo,kama ni "ndiyo nataka..." mifano ni lukuki katika namna chama hicho kilivyoweza kusimama kidete kwenye mapambano dhidi ya ufisadi na japo hawajaweza kumaliza kabisa tatizo hilo (kwa vile dola bado iko mikononi mwa CCM),yayumkinika kabisa kuamini kuwa hata swali "nakubali kumchukua" linajijibu hapohapo.
Hebu nipe msingi wa kuamini kuwa Chadema ilivyo sasa itatafsiri hizo ahadi kwa vitendo. Ni kitu gani kinakufanya uamini hivi? Usinielewe vibaya, sisemi kwamba hawawezi au hawatofanya, ninachosema msingi wa imani hiyo ni nini?
Nimeshakupa mifano ya namna walivyojitoa mhanga kuhamasisha mapambano dhidi ya ufisadi.Lakini hata tukiweka kando mifano hiyo HAI,naomba nikuulize nawe "HEBU TUPE MSINGI WA KUAMINI KUWA CCJ KAMA ILIVYO SASA ITATAFSIRI HIZO POROJO ZAKE KWA VITENDO".Na "KIPI KINAKUAMINISHA KUWA WATAFANYA WANACHOAHIDI KUFANYA?".Kadhalika,nami sisemi kuwa CCJ hawawezi au hawatofanya (kama watafanikiwa kujisajili na kuwa chama cha siasa badala ya "chama cha press conferences"),bali nami nahoji imani yako kubwa inatokana na nini maana angalau mie ninayeiamini Chadema nimeshawishiwa na harakati zao katika miaka mitano hii
Mifano yako ni mibaya kwa kweli japo inaweza kuvutia fikra nyepesi nyepesi.
Katika hilo sina la kusema kwa vile unachokiona wewe kuwa kibaya kinaweza kuwa kizuri kwangu na kwa wengine.Mara nyingi wanasosholojia wanaepepuka sana "kujipa madaraka ya kuhukumu" kwa vile kauli au matendo ya mwanajamii yanaweza kuwa na tafsiri au/na dhamira zaidi ya anayoiona mtoa hukumu.Japo unaona mifano yangu ni mibaya na inayoweza kuvutia hisia nyepesi,naomba kukupa mfano mwingine MREEEEFU kuhusu point of view
The optimist says the glass is half full.
The pessimist says the glass is half empty.
And the cynic... wonders who drank the other half.
The school teacher says it's not about whether the glass is half empty or half full, it's whether there is something in the glass at all.
Anyway... Attitude is not about whether the glass is half full or half empty, it's about who is paying for the next round.
The inquisitive troublemaker wants to know what's in the glass anyhow... and wants the rest of it.
The homebuilder sees the dirty glass, washes and dries it, then puts it away in a custom oak and etched glass cabinet that he built himself using only hand tools.
The worrier frets that the remaining half will evaporate by next morning.
The fanatic thinks the glass is completely full, even though it isn't.
The entrepreneur sees the glass as undervalued by half its potential
The logician says that where the glass is in process of being filled then it is half full; where it is in the process of being emptied then it is half empty; and where its status in terms of being filled or emptied is unknown then the glass is one in which a boundary between liquid and gas lies exactly midway between the inside bottom and the upper rim, assuming that the glass has parallel sides and rests on a level surface, and where it does not then the liquid/gas boundary lies exactly midway between the upper and lower equal halves of the available total volume of said glass.
The scientist says a guess based on a visual cue is inaccurate, so mark the glass at the bottom of the meniscus of the content, pour the content into a bigger glass; fill the empty glass with fresh content up to the mark; add the original content back in; if the combined content overflows the lip, the glass was more than half full; if it doesn't reach the top, the glass was more than half empty; if it neither overflows nor fails to reach the top then it was either half-full or half-empty. Now what was the question again?
The grammarian says that while the terms half-full and half-empty are colloquially acceptable the glass can technically be neither since both full and empty are absolute states and therefore are incapable of being halved or modified in any way.
The waiter will hurry to replace the glass with a full one. For him there are no doubts: the glass was empty when he took it away; it is full in the bill that he brings you.
The magician will show you the glass with the full half at the top.
The physician says that the glass is not empty at all - it is half-filled with water and half-filled with air - hence, fully filled on the whole!
The musician says he/she is unimpressed with the promoter of the concert for not providing more alcohol.
The ineffective organization would discuss the question during the board of directors meeting, convene a committee to research the problem, and assign tasks for a root cause analysis, usually without a complete explanation of the problem to those assigned the tasks. The directors would consider the problem to be above the pay grade of those assigned root cause analysis tasks.
And more strangely:
The dog just wonders: can he eat the glass or will you throw it so he can bring it back... The cat wonders why the glass is only half full (or empty)... is it a trick... poison perhaps...
The eternally optimistic eccentric would say, the glass is consistently overflowing (or is that the neurotic?...)
The person who is no longer trapped in The Matrix (whatever one might call him/her) says: "There is no glass..."
More generationally:
The adolescent student says the glass is just another dirty trick played by the teacher to prove that students are dumb.
More scientifically:
The research scientist says that following initial observation and testing a working hypothesis for further research is: "The glass is both half full and half empty," and that these findings warrant further investigation with a more representative sample of glasses and contents, which may or may not be liquid.
The algebraic simultaneous equation theorist says that if the glass is equally half full and half empty, then half full = half empty; therefore ½ x F = ½ x E; therefore (by multiplying both sides of the equation by 2) we show that F = E; i.e. Full equals Empty!
The efficiency analyst says the glass is operating substantially below optimization level, being consistently exactly 50% under-utilized during the period of assessment, corresponding to an over-resourcing in meeting demand equating to precisely 200% of requisite capacity in volume terms, not accounting for seasonal trends and shrinkage, and that if the situation continues there is in theory opportunity for savings or expansion.
Lengo la mfano huo mreeefu ni kujaribu kujibu mtizamo wako kuhusu mifano ninayotumia
Nimeandika nyingi sana na ninaamini CCM watafanyia kazi mapema zaidi kuliko ndugu zetu wa upinzani.
At least hapa unatusaidia kutuonyesha your true colours.Sasa kama unaamini kuwa CCM watafanyia kazi mapema zaidi kuliko ndugu zetu wapinzani,sasa CCJ ni tawi la CCM au?Maana kama CCJ unayoipigia debe ni sehemu ya upinzani,na unaamini CCM watafanyia kazi matatizo yetu mapema kuliko wapinzani (including CCJ),umuhimu wa wapinzani (including CCJ) unatoka wapi tena?
Unaweza ukafikiria tatizo ni utekelezaji, lakini kuna tatizo kubwa zaidi linalofanya utekelezaji uwe mgumu. Fikiria kwa sekunde chache tu unaweza kufahamu.
Well,kwa mujibu wa uelewa wangu MDOGO,utekelezaji ni tatizo la msingi.Na napenda kukuthibitishia kuwa huwa nafikiria kabla ya kuandika japo hiyo haimaanishi kuwa kila nachofikiria na kuandika kitakuwa sahihi.Lakini kwa vile naamini wote tuna lengo moja,yaani kuona Tanzania ikiwa kwenye mwelekeo stahili,hudhani ingekuwa vema zaidi kama ungebainisha bayana kuwa tatizo kubwa zaidi ya utekelezaji ni lipi badala ya kunitaka nifikiri zaidi (which implies kuwa sikufikiri vya kutosha)?Wenzetu wenye ufahamu mkubwa mnaweza kuwa raslima muhimu kwa maendeleo ya taifa letu kama mtachangia mitizamo yenu katika namna ya majadiliano na kuelimishana badala ya kutuonyooshea vidole sie "tusiofikiri vya kutosha".
Well, tatizo liko kwenye sera vile vile. CCM haina nzuri kama wengi wanavyoamini. Ni mojawapo ya sera mbaya kabisa hasa katika miaka hii 20 iliyopita. Wakati wengine wanaamini kuwa CCM ina sera nzuri "vitabuni" mimi siamini hivyo kwani nimezisoma na kwa kweli hazitofautini kabisa na za Chadema. Sijui kama umepata nafasi ya kumsikiliza Kikwete leo.
Again,hapa ni suala la mtizamo tu.Last time I read nini CCJ wanataka kufanya sikuona tofauti kati yao na kinachohubiriwa na CCM.Sijui,labda baada ya kupata usajili wa kudumu CCJ watakuja na sera nzuri na zinazoambatana na guarantee ya kudumu ya utekelezaji wa sera hizo.
Ujamaa haukushindwa, haukujaribiwa ipasavyo. Ndiyo maana leo nchi zenye kufuata ujamaa (hata kwa jina jingine) zinazidi kuongezeka!
Mkuu,hata Uholanzi wanaweza kutoa maelezo kama hayo kuhusu fainali ya kombe la dunia dhidi ya Spain kwamba hawakushindwa bali "hawakujiandaa vya kutosha,hawakufanya mazoezi ipasavyo,nk".Lakini suala ni matokeo,mwisho wa pambano score board ilisomeka Spain 1 Holland 0.Na katika mantiki hiyohiyo,kama tunauzungumzia Ujamaa katika misingi ya KUFANIKIWA na KUSHINDWA,suala la whether ulijaribiwa vizuri au vibaya linapoteza umuhimu wake.Tangu lini kujaribu kitu vibaya kukawa na maana ileile ya kufanikiwa?Hoja ya kujaribiwa vibaya ingekuwa na uzito kama swali lingekuwa "kwanini ujamaa ulishindwa",ambalo kwa mtizamo wangu jibu jepesi linarejea kwenye hoja ya sera nzuri,utekelezaji mbovu.
Je haikuwa itikadi nzuri?Je sera mbalimbali zilizoambatana na itikadi hiyo hazikuwa na malengo mazuri kwa Watanzania?
Kwa mtizamo wangu,ambao ni ruksa kutoafikiana nao,baadhi ya mahubiri kuhusu ujamaa yaliwalenga walalahoi pasipo kuangalia kundi la watu kama akina Kingunge na vigogo wengine waliotuaminisha kuwa "binadamu wote ni sawa ilhali wao wanawekeza fedha za kigeni kwenye akaunti zao nje ya nchi".Kulikuwa pia na mapungufu ya kuwa putting too much ambition infront of common sense.Unapomhamisha mtu kwenye eneo productive na ambalo ana local connection na kumpeleka sehemu inayopata mvua kwa kudra za Mwenyezi Mungu untarajia nini?Na kwa vile tangu tupate uhuru,uchumi wetu ulielemea kwenye utegemezi wa misaada,hatukuwa tumejenga msingi wa kukwamisha "kujitegemea" kwetu?Je si kweli kwamba miongoni mwa sababu zilizopelekea "kifo cha ujamaa" ni uchumi tegemezi ambapo "wafadhili" walishinikiza matakwa yao,nasi kulazimika kuyafuata kwa vile hatukuwa na alternative nyingine?
Ninachosikia ni kuwa "twende tu" hata kama hakuna sera, hakuna ahadi, hakuna kipiimo twende tu tufuate jina!.. really? I'm still sane, at least the last time I checked.
Na sie tunaoamini kuwa ni muhimu kuiondoa CCM sasa tunasukumwa na ukweli kwamba tumeshasikia sera lukuki,ahadi kibwena,na vipimo vilivyozidi hata uwezo wetu lakini bado tuna mark-time...actually,tunarudi nyuma zaidi ya alipotuacha mkoloni.Kuhusu hiyo sanity,I believe hata sie tunaotaka CCM iondoke SASA ni sane pia (aidha vipimo vya wataalamu au uwezo wetu binafsi).Kudai CCM iondoke sasa hakumfanyi mtu kuwa insane.Na ni katika namna hiyohiyo si haki wala sahihi kuhitimisha kuwa mtu anayamini chama cha kizushi kama CCJ is not sane.
well, hakuna sababu ya kusubiri kwa kweli, nimeandika toka mwanzo, mwaka huu huu Chadema ikitaka kushika madaraka ya nchi 'INAWEZA'. Lakini hadi hivi sasa imethibitisha kuwa haitaki. Inaombea.
Labda uko sahihi maana inaelekea tatizo la KUTOTAKA linazidi kusambaa kwa vyama vya siasa kwani hata CCJ wangetaka kupata usajili wa kudumu wangeweza kupata lakini wametuthibitishia kuwa sio tu kuwa hawakutaka bali pia walikuwa na ajenda ya kuwazuga watu.Na angalau Chadema inaombea kwa vitendo kuliko CCJ inayoombea kwa press conferences na huruma ya mabalozi wa kigeni.