Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa

Kwa hiyo, Chadema wanatakiwa kuja na SABABU ambayo itajenga NIA ya wananchi kuungana nao kuiondoa CCM madarakani na sii swala la what next..Na hakika sababu yenyewe hakuna zaidi isipokuwa UFISADI.

duh!!! imenichukua karibu kurasa sabini kusema ulichosema wewe kwa mistari miwili. Kumbe uzee kweli hekima.
 
Mkuu Nguruvi,

Naona wewe ndiyo hujamwelewa Mwanakijiji. Tatizo kubwa la kwanza la Mwanakijiji ni kwamba amesema hana imani na siasa ya ushirikiano wa wapinzani. Hoja yake ninaiunga mkono ukizingatia historia za ushirikiano wa wapinzani hapa kwetu. Mara nyingi umekuwa ni ushirikiano wa kisanii. Tatizo ni kwamba ikifika wakati wa uchaguzi ndio utasikia hoja za kushirikiana, na kila chama kinataka kusimamisha mgombea wake kila jimbo hata kama hakubaliki/hauziki kwa wapiga kura.

Wangekuwa na nia ya kweli ya kushirikiana wangekuwa wanaanza mjadala wa kushirikiana miaka 2 au 3 kabla ya uchaguzi ili kuepusha migogoro ya kusimamisha wagombea. Lazima kuwe na makubaliano ya namna ya kumpata mgombea strong wa kuwakilisha wapinzani wote walioamua kushirikiana. Hii ni pamoja na kuandaa sera ambazo zitatumiwa na muungano wa wapinzani kwenye kampeni. Ushirikiano wa kukurupuka pindi uchaguzi unapokaribia, sioni kama unaweza kuleta ushindi kwa wapinzani..

Kaka, sio kila suala linaloendelea katika siasa ni lazima liwepo katika magazeti. Hawa jamaa wamekuwa katika mazungumzo na hata makubaliano ya kushirikiana katika muda wote na sio wakati wa uchaguzi tu. Kinachofanya lionekane zaidi wakati huu ni hali halisi ya uhutaji wa muungano ama ushirikiano huo na sio kuwa miaka ya nyuma hakukuwa na jitihada hizo.

omarilyas
 
Kaka, sio kila suala linaloendelea katika siasa ni lazima liwepo katika magazeti. Hawa jamaa wamekuwa katika mazungumzo na hata makubaliano ya kushirikiana katika muda wote na sio wakati wa uchaguzi tu. Kinachofanya lionekane zaidi wakati huu ni hali halisi ya uhutaji wa muungano ama ushirikiano huo na sio kuwa miaka ya nyuma hakukuwa na jitihada hizo.

omarilyas

Mkuu kwa kujua yanayoendelea ambayo wananchi hatuyajui inabidi tukupe cheo cha "coordinator of the opposition"... Hawa jamaa unaowazungumzia kama kweli wangelikuwa kwenye mazungumzo na makubaliano ya maana kwa nini wayafanye siri wananchi ambao ndio wadau wakuu tusiyajue? Kuweka bayana mazungumzo yao ingetupa sisi wananchi moyo zaidi badala ya kuyafanya ni 'yao' wao wazungumzaji kwa kipindi chote hadi mpaka uchaguzi umekaribia.
 
Mzee Mwanakijiji,
Mkuu nimekusoma sana kule kwenye - Chadema 2010: Kutoka HAPA kwenda KULE

Na sikupenda kwenda kule kuharibu Uhondo wa mada ile kwa kuanzisha hoja pinzani ndani ya elimu kubwa uloitoa. Nimeona bora kuleta hapa hoja zangu tuzijadili kwa mapana.

Sehemu kubwa ya mchakatuo wako nimeukubali isipokuwa sehemu moja tu ulipogusia Mahusiano ya Itikadi, sera na Ilani kwa kuitazama Chadema. Na nitakueleza kwa kirefu baadaye isipokuwa sasa hivi nitasema kwamba yale makosa unayoyaona kwa sera za Chadema ndizo zinazokufanya wewe usiwe muumini wa mrengo wa kati - (Reform Party). Sidhani kama sera zao hazikulingana na mrengo wa kati

Pili, mimi naamini kabisa kwamba Itikadi au elimu yoyote ya kiitikadi hutokana na mazingira yaliyopo. Vyama vyote vya Conservative, Progressive na hata Liberal, itikadi zao zimeibuka baada ya fikra chachu ku challenge malengo ya itikadi iliyotangulia hivyo kuweka ushindani wa kifikra mbele ya wananchi ambao ndio wenye kuguswa na uhuru nahaki ya sheria zitokanazo na mfumo huo. Kwa hiyo Hawa jamaa zetu wanapotaka ku challenge CCM ni lazima itokane na mazingira yaliyopo kutofungamana na itikadi iliyotawala pamoja na ile pinzani ktk kutekeleza ibada zake.

Na hakika Conservative wa Marekani hawako sawa kwa kila kitu na wale wa UK, Japan, Ufaransa au China wala hao Democratic wote hawafanani kwa kila kitu.
Mara zote fikra chachu za kuzaa hizi itikadi kiutawala zimetokana na KUPINGA sheria tangulizi iliyokataza au inayoruhusu wajibu fulani kutoka kwa wananchi. Na huwezi kupinga tu ili mradi unapinga pasipo reasoning, na ndipo unakuta wazo moja huzaa fikra ikaleta Falsafa ambayo kwa kukubalika ikawa Itikadi (imani) inayofuatwa na wafuasi wake kupinga sheria iliyotokana na sera au itikadi inayowaongoza watu hao.

Trust me mkuu wangu ktk hili hakuna mawazo mbadala wala itikadi inayoweza tungwa na kuwa UNIVERSAL isipokuwa wazo,fikra,falsafa na Itikadi zote zimetokana na WATU katika MAZINGIRA waliyokuwepo wao. Hata Mapinduzi ya China yamefanyika na Wajamaa kupinga Wajamaa wenzao ktk hatua za kiutawala ambazo hazikufungamana na itikadi yenyewe.

Kwa hiyo ndio maana unanikuta mimi Mkandara nasimama mrengo wa KULIA nikiwa Tanzania, lakini huku majuu nimekaa KUSHOTO na siasa za nyumbani kwangu zipo kati kushoto - LIBERAL kwa sababu ni mazingira uliyopo ndiyo hutengeneza maamuzi mengi ya kisheria. Kama vile leo siwezi kukubaliana na baadhi ya sheria za kiislaam kutumika ktk mazingira ya Tanzania. Na ndio maana ukifuata falsafa ya mrengo wa kulia (conservatism) ktk nchi zetu maskini, hakika mambo mengi yatapingana na itikadi hiyo ya nchi za magharibi (tajiri) pamoja na kwamba wao wanaona wanayo kila haki ya ku conserve asili na tamaduni zao lakini sio sisi.

Nitaendelea zaidi baadaye kuhusiana na Chadema. kama kuna hoja au swali tuanzie hapa.
 
Mengi yatazungumzwa kuhusu Dk Slaa, Chadema na hatua yao ya kugombea urais wa Tanzania. Ni jambo jema na lenye kuishibisha demokrasia, lakini kwa upande mwingine wanatoa changamoto kubwa kwa CCM kujipanga upya kwani tayari wameanza kushikwa na mchecheto. Kama mtakumbuka vyema walikuwa wamepanga kumpunguzia Kikwete kazi za kuzunguka nchi nzima. Sasa Slaa amewatisha na wamebadili mwelekeo. Idadi ya vikao vyao nayo imeongezeka sana kwa sasa kuhusu namna ya kupata ushindi wa kishindo zaidi ya mwaka 2005.
 
Back
Top Bottom