Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa

Here is the problem that I see with Mwanakijiji. First, I've got to give it up to him...the phrase 'giving up' does not exist in his book. Secondly, and this is what I see is his main problem (not necessarily a bad problem). He has a propensity for ballyhooing things. I often say it to myself that this guy would've made a good salesman (if he's not one already). He has a way with words that he can persuade just about anyone into believing in something he believes in. I remember when he launched his KLHNews...man...you should've heard how he was hyping it up...but where is it now? It's defunct. And the same thing goes for this CCJ thing. He almost got me sold into believing they were for real.

KUla dala NN.Nimekugongea lisenki likubwa kwa kuwa siruhusiwi kugonga mara mbili,ningefanya hivyo.
 
Wanajamvi,
Wakati tunasoma shule ya upili hapo kitambo ilitokea tukataka kugoma kuingia darasani. Kuna mwanafunzi mmoja alikuwa mstari wa mbele sana kuhamasisha huo mgomo kwa kutoa hoja mbalimbali za ushawishi ili watu washiriki mgomo.Kwa vile alivyokuwa anajua kupanga hoja watu wote tukawa tunamsikiliza yeye kwa kial hatua anayopanga. Lakini ajabu sana baadaye sasa tulipotaka kuanza kugoma aka backslide na kuanza kutoa hoja za kutoamini kuwa katika mgomo huo kutapatikana tija yoyote. Basi nakwambia akaanza kujenga hoja kuwa yeye anaona ni vyema tumuite mkuu wa shule tuongee naye tu kuliko kugoma, na akasema yeye anaweza kumuita mkuu wa shule hata saa sita usiku akaja kuongea nasi. Kutokana na jinsi tulivyokuwa tunamuamini basi kwa shingo upande tukakubaliana na mawazo yake, tukaacha mgomo, akamuita mkuu wa shule akazungumza na sisi na akatimiza kiduchu madai yetu kwa muda fulani baadaye kidogo hali yetu ikawa vile vile.

Baadaye tulikuja kugundua kuwa yule mwanafunzi alikuwa anatumiwa na uongozi wa shule na alikuwa na ni mtu wa usalama wa taifa hadi leo.

Wakati wa mgogoro wa NCCR Mageuzi na Mrema niliwahi kumuuliza Marando kuwa Je Mrema anatumiwa na CCM kuimaliza NCCR. Marando alijibu kuwa hafikiri hvyo ila alisema kuna watu wanaweza kutumika bila kujijua kuwa wanatumika. Kwa maana nyingine alimaanisha kuwa matendo ya Mrema yanabomoa upinzani kwa faida ya CCM bila yeye kujijua kuwa anatumika kuisaidia CCM (labda alijua toka wakati huo ukizingatia kauli zake za sasa)

KAZI YA KWANZA YA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA NI KUSHIKA DOLA ILI CHAMA HICHO KIWEZE KUTEKELEZA MIKAKATI AU SERA ZAKE KUWALETEA WANANCHI MAENDELEO. MAMBO YA SERA AU ITIKADI HAYO WANANCHI HAWAJUI. HATA LEO UKIMUULIZA MAKAMBA ITIKADI YA CCM NI IPI? HATAKUWA NA JIBU LA MOJA MOJA, UMEWAHI KUSIKIA HATA CCM WAKISEMA ITIKADI YAO NI IPI? .CCM HAWANA SHIDA NA MAMBO YA ITIKADI KAZI YAO WANALETA MAENDELEO TU SASA NYIYI NDO MUFANYE ANALYSIS KAMA WANAFUATA ITIKADI IPI.

Mimi ni mwanacham hai wa CCM kitendo cha hawa defectors kutoka CCJ kimenishtua sana, sijui kitu gani kitafuata. Kwa hiyo kama mwana ccm nawashangaa ''wapinzani'' au wataka mabadiliko wanaobeza hatua hiyo. Hao ndo ambao wanatutumikia CCM bila wao kujijua.
 
Inabidi turudi nyuma kidogo ili tumwelewe Mwanakijiji anasukumwa na nini zaidi katika huu mjadala. Wakati umaarufu wa Chadema unavuma na Operation Sangara imekuwa tishio, Mwanakijiji alizua maswali haya;

  • Je, yawezekana watu wanaokimbilia CHADEMA sasa hivi au wanaoiamini CHADEMA wanafanya hivyo si kwa sababu ya mapenzi yao kwa CHADEMA ilivyo bali kutokana na chuki yao kwa CCM na utawala wake wa mfumo wa kifisadi kwa miaka 45 iliyopita?
  • Je, yawezekana katika kutoridhika huku watu wamefumbia mapungufu makubwa ya kimuundo, kiitikadi, kichama na kimwelekeo ya CHADEMA ambayo yanaweza kujitokeza kwa nguvu kubwa endapo chama hicho kitashika madaraka ya nchi na hivyo kuturudisha kwenye "madudu" yale yale ya CCM?
  • Je, yawezekana kwa kuweka imani pofu (blind faith) kwa kundi la watu ambao wamejithibitisha mara kadhaa kuwa hawajamudu fani na sanaa ya siasa (sic !) na kuwa ni jopo la watu wenye mtazamo wa kisomi zaidi (elitist) kuliko wa kimwamko wa mabadiliko wanajiandaa kwa kukatishwa tamaa?
Bila kusuburi majibu ya mtu yeyote, Mwanakijiji alijijibu kwa kuuliza tena swali hili ambalo nafikiri linatupa mwanga kuhusu msimamo wake.
Katika kutafuta majawabu ya maswali haya siyo vyema kwa kweli kuendelea kuikumbatia CCM na madudu yake na kujaribu kuiokoa kwani ndio njia ya haraka ya kuleta mabadiliko ya haraka kuliko kukumbatia upinzani ulivyo sasa?
Kwa kuwa chati ya Chadema kwa wakati huo ilikuwa inapanda kwa kasi na ilianza kuwa tishio hivyo ilibidi zitafutwe mbinu za kuipunguzia makali yake. Enter CCJ, ilizaliwa kwa mtindo ambao haujawahi kutokea nchini na wengi tulivutiwa na staili na gia waliyoingia nayo. Wakati huo chama cha CUF kiliishashughulikiwa kwa kuning'iniziwa karoti na wao wakaingia kama vipofu vile (au lao moja ?) Kuna wengi tu wameshughulikiwa kimya kimya hadi humu JF na mtabaki tu mkijiuliza fulani na fulani wako wapi siku hizi ?

Mwanakijiji naomba majibu. Je, yawezekana hata Mpendazoe ameishtukia CCJ ?
 
Nadhani itabidi niende ndani zaidi kuelezea kile ninachokiita "Tatizo la Chadema". Natumaini nitaeleweka, na siyotkuwa nimechelewa. Niwatoe hofu kabisa kwangu mimi hata CCM ikiondolewa kesho madarakani sitolia!! Lakini sitorukaruka kwa furaha! Nitauliza swali hili hili ninaloliuliza sasa.. "then what"? Nakataa kabisa kuwa hatuwezi kuwa na ajenda ya uchaguzi inayosema "tuiondoe CCM kwanza"! Hii ni ajenda ya kuondoa chama kimoja na kukiweka kingine. Yatakuwa yale yale ya KANU na RAINBOW coalition! Well RAINBOW walifanikiwa kabisa kuiondoa KANU, lakini is Kenya better today than during KANU's rule? Tutapata majibu tofauti sana kwenye hilo. Je Zambia chini ya Chiluba baada ya kuiangusha ZANU je walikuwa bora zaidi kwa sababu kina Chiluba walitimiza ndoto yao ya kumuangusha Kaunda?


Hili swali hata kama mtalikwepa, mtalibeza au mtajaribu kuonesha kuwa hamlielewi mtalazimika kulijibu tu one of these days. I know you will.

Kwa vile linaonekana ni gumu mno/halielewi au halijaulizwa sawasawa itabidi nilivunje vunje katika vipande vyake vidogovidogo. CHADEMA WAKILIELEWA NA KULIJIBU KABLA YA UCHAGUZI WATASHINDA KWA KISHINDO!

Mkuu,pamoja na heshima kubwa niliyonayoa kwako lakini naomba kutamka kuwa mawazo yako katika suala hili yanafaa zaidi katika nchi ya KUFIKIRIKA.Hivi kwa busara zako unadhani hata tukikubali kwamba solution kwa sasa sio kuiondoa CCM,then tufanye hicho usichotaka kutuambia bayana,CCM itakuwa imelala tu pasipo kuhujumu huo mkakati unaopendekeza pasipo kuubainisha?Kwanini hujiuliza BAWATA ilihujumiwa,kwanini hujiulizi kwanini mashushushu wanapenyezwa kwenye NGOs na civil society kwa ujumla?

Inanilazimu ku-guess kuwa mkakati unaodhani utakuwa mafanikio as opposed to ajenda ya kuiondoa CCM ni kutengeneza mazingira yatakayowezesha kuwapo serikali ya watu kwa ajili ya watu.Wazo zuri lakini kufanikiwa kwake ni sawa na jithada ya kutengenisha chumvi ndani ya bahari wakati ukiwa baharini tena kwa kutumia chandarua.It simply wont work.Nilipata F ya fizikia ndio maana nikaamua kuwa "ngwini" lakini nakumbuka kwenye masuala ya velocity kuna ishu ya kuneglect pressure (kama nimepatia,remember I got an F).Lakini kwenye siasa ya uhalisia huwezi ku-neglect pressure kutoka kwa ruling party kuhakikisha inaendelea kuwa madarakani,huku ikitumia vyombo vya dola kuhujumu kila jitihada za kuleta mabadiliko ya kweli katika jamii.

Hivi unafahamu kuwa miongoni mwa sababu zinazopelekea waheshimiwa kutojihangaisha sana na kuondoa umasikini ni kwa vile umasikini huo unawasaidia wao kuendelea kuwapo madarakani?Unadhani Watanzania watapopiga hatua na kumudu maisha yao pasipo kusubiri pishi za mchele (in form of takrima) watakubali kuuza uhuru na kura zao kwa doti za kanga,kilo za sukari au hizo pishi za mchele?Katika mantiki hiyohiyo ya namna umasiki wa Watanzania wengi unavyotumika kama mtaji wa CCM,jithada zozote za kumkwamua Mtanzania asitegemee ridhaa ya CCM zitakumbana na nguvu kubwa za vyombo vya dola ambavyo kwa kiasi kikubwa zina symbiotic relationship na CCM.JK anapoteau washkaji zake kuongoza vyombo vya dola anafahamu vema kuwa atawalinda nao watamlinda.

Unaweza kutushwishi hapa kuwa kuiondoa CCM sio ufumbuzi wa matatizo ya Tanzania lakini unachoshindwa kusema hadharani ni ukweli kwamba CCM kwa sasa ni zaidi ya chama cha siasa.Ni mfumo onevu wa kifisadi unao-survive kwa kulinda hata majambazi as long as wanausaidia mfumo huo kudumu.Utamwambia nini afisa usalama anayeamini kuwa laiti Chadema au CUF ikiingia madarakani atakosa ajira kwa vile aliingizwa kwenye taasisi hiyo kutokana na ushkaji wa mzazi au nduguye na kigogo flani?

Tumeshuhudia Obama na Democrats walivyofanya kila liwezekanalo kuwaondoa Republicans.Hizo changes alizoahidi Obama (hata kama hazijaonekana) zitawezekana tu kwa vile Democrats wako madarakani.Wamarekani walikuwa wamechoshwa na Bush na neo-cons wenzie na njia pekee ilikuwa kuwaondoa madarakani japo kwa muda.Licha ya ukweli kwamba sera za Democrats zilichangia kuwaondoa wapinzani wao (kwa maana ya kuwavutia wapiga kura),ukweli unabaki kuwa dhamira ya kuwaondoa Republicans (iliyokuwa shared na Democrats na Wamarekani wengi) ndiyo hatimaye ilisababisha Obama kuingia Ikulu.

Hizi habari za sera,mikakati na alinacha kama hizo tumekuwa tukizisikia tangu tunapata uhuru.Kwani kuna chama chenye sera za kupendeza na kutoa matumaini kama CCM.Hebu rejea manifesto ya Kikwete 2005.Laiti angeweza kutimiza japo 10% tu ya mazuri aliyoahidi basi sasa hivi tungekuwa sio tu tuko mbali kiimaendeleo bali pengine tungetamani urais wake usiwe na kikomo.Kwa vile wewe ni Mwafrika mwenzangu,naamini unafahamu fika kuwa kikwazo cha maendeleo ya bara letu hakijawahi kuwa kokusekana sera tamu zenye kuleta matumaini.Tatizo ni utekelezaji wa sera hizo.Sasa unapoletea habari za sera,itikadi na ngonjera kama hizo nashindwa kanisa kukuelewa.Kinachotufanya baadhi yetu tuiamini Chadema ni kwamba angalau wamesimamia yale yanayotarajiwa na Watanzania walalahoi.Yani pamoja na hekima zako zote huamini kuwa Chadema imechangia kwa kiasi kikubwa kufunua ishu kama za ufisadi kama wa EPA ,Meremeta,Tangold,List of Shame,nk?Hivi hudhani kuwa mtu kama Dkt Slaa amekuwa na manufaa sana kwa Watanzania zaidi ya Kamati Kuu nzima ya CCM au hata kabineti nzima kuuuubwa ya JK?Wafanye kipi kukuridhisha kuwa angalau wao wameonyesha njia kwa namna flani licha ya vitisho na manyanyaso ya kusimamishwa ubunge (refer ishu ya Zitto)?

Kwa kumalizia,tafsiri ya haraka ya mkakati wako ni doing nothing is better than doing something.Nasema hivyo kwa vile umeshabainisha kuwa ni bora kubaki na CCM kuliko kuwa na chama mbadala unachodhani kitarudia madudu yaleyale ya CCM.Kwahiyo mwenzetu ukipatwa na malaria kisha ukatumia dawa lakini baada ya muda malaria ikarejea tena basi unaamua kuacha kuitibu kwa vile unahofia kuwa itarejea tena?Unahofia kuwa kuiondoa CCM madarakani kunaweza kusiwe ufumbuzi wa matatizo yetu hivyo ni bora kubaki na CCM?

Binafsi naamini kabisa kuwa unatuelewa sana tuotaka kuiona CCM iking'oka madarakani ila kwa vile ulishaamua tangu awali kusimama upande wa pili unaona kujumuika nasi ni kama kubadili dini.Ni vizuri kuwa na msimamo na pia ni sehemu ya matumizi mema ya jhaki yako ya kikatiba kuamini kile unachodhani ni sahihi hata kama wengi hawakiamini.However,japo imani ni imani,kuna tofauti kati ya kumwamini Mungu na kumwamini shetani.Na hapa sizungumzii idadi ya wanaomwamini Mungu dhidi ya wanaomwamini shetani bali naangalia itikadi za Mungu dhidi ya za shetani.Katika namna hiyo hiyo,kuamini kuwa ufumbuzi sio kuing'oa CCM madarakani sio kosa la jinai au dhambi,lakini katika uhalisia,hiyo ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
 
sawa.. tufanye hivi.. tuunge mkono Chadema iingie madarakani halafu tujue mbele ya safari watafanya nini na madaraka hayo kuhusiana na matatizo ya wananchi wetu. Tumeendeshwa kwa muda mrefu bila ya kuwabana CCM na kuwaacha waongoze wapendavyo. Sasa chama kingine kinataka kushika madaraka tunaambiwa tuamini tu kuwa wanataka madaraka vizuri na tusiwabane kujua wanataka kuyatumia madaraka hayo vipi. Kwamba, kwa kadiri ya kwamba wanataka kuingia madarkani na kuwanyang'anya CCM madarakani basi hilo latosha.

Madaraka yana tabia moja mbaya sana; tabia ambayo yakiachwa bila kuhojiwa na kusimamiwa huharabu wenye madaraka hayo. Lakini naambiwa tusijiulize hili kuhusu Chadema kwa sababu lengo lao ni "noble" ambalo ni kuindoa CCM madarakani. How sad!..

Nilitarajia wanaotaka Chadema iingie madarakani wangetaka kujua madaraka hayo yatatumikaje kushughulikia mafisadi Tanzania, mfumo wa utawala wa kifisadi, kwa vipi na kwa gharama gani na kwa kasi gani. Lakini hili si muhimu kwao. Hilo treni la imani linaloenda msikotaka kukujua nyinyi pandeni, shangilieni na imbeni nyimbo za shangwe. Labda na mimi nitalipanda siku moja. Lakini nitalipanda pale tu nitakapokuwa na uhakika treni letu linataka kutupeleka wapi na wa kwa vipi. Mambo ya kwenda kuteremshwa njiani.... ndiyo haya haya ya CCM.
 
Wewe Mwanakijiji vyama vyote vilivyoleta mabadiliko ya kijamii (social transformation) vina vinara wao wa kuvionesha nini cha kufanya. Kuna walioandaa Marshal Plan. Pia waliosadifu Freedom Charter. Sasa kwa nini usiwape CHADEMA hayo unayotaka watekeleze? Au ulikuwa unawafanyia 'charm offensive' hao CCJ tu?
 
Halafu Mkuu,japo ni kweli kuwa kuondoka kwa KANU hakujawa ufumbuzi kwa matatizo ya Wakenya,ni vema pia kungalia mifano mingine ya kuleta matumaini.Hivi kwa mfano wakati wa uchaguzi huru wa kwanza nchini Afrika Kusini,ungewashauri Weusi wa Sauzi wasikiondoe chama cha kikaburu madarakni kwa vile ANC ingeweza kuendeleza yaleyale ya chama cha makaburu?Au kwanini hatuendi mbali kidogo japo hapohapo barani Afrika na kuiangalia Ghana?Naamini hujasahau namna prophets of doom walivyokuwa wakijaribu kuwatisha Waghana na kuwaaminisha kuwa nchi hito bila Jerry Rawlings haiwezekani?Leo hii Ghana ni moja ya mataifa ya Afrika ya kupigiwa mstari (at least kwa standards za Kiafrika).

Kwa hapa Uingereza,majuzi tu wapiga kura wa hapa walijikuta na uchaguzi mgumu wa aidha kuendelea kuiweka Labour madarakani lisha ya chama hicho kushindwa ku-meet matarajio yao au kuwarejesha tena Wahafidhina (Conservatives) ambao pamoja na kumbukumbu mbaya walizonazo Waingereza kuhusu chama hicho safari hii kilionekana kina majibu ya matatizo yanayoikabili nchi hii.As a result,Labour ikatoswa.Japo ni mapema kuhukumu kama uamuzi huo ulikuwa wa busara au la,doing nothing was not an option.

Na hata huko Marekani mlipo,si kweli kwamba Wamarekani walikuwa na uhakika wa asilimia 100 kuwa Democrats watakuwa bora zaidi ya Republicans.Lakini kwa vile watu walishachoshwa na Bush na Republicans wenzake,wakaonelea ni bora kuwatosa.Na kwa upande mwingine,kutoswa kwa Republicans kunatoa somo zuri kwa Democrats kuwa wakirejea madudu ya watangulizi wao,nao watatoswa.

In same way,hata kama Chadema haijahitimu kwa asilimia 100,moto waliouanzisha dhidi ya ufisadi angalau umetuthibitishia kuwa sio watu wa maneno tu bali vitendo pia,hata kama vitendo hivyo vilimaanisha akina Zitto kusimamishwa ubunge na akina Slaa kutishiwa kupelekwa mahakamani.Unless unahofia kuwa wakiingia madarakani watabadili katiba na kuwawezesha kukaa madarakani milele,5 years later tutakuwa katika nafasi ya kuwa-reward kwa kuwachagua tena au kuwaadhibu kwa kuturejesha kwenye zama za CCM.

Binafsi ningetamani sana kuiona CCM ikiendelea kutawala minus mafisadi.Unfortunately,hiyo ni zaidi ya kutegemea damu kutoka kwenye jiwe.Uhai wa mbu ni damu wa mwanadamu,na uhai wa nzi ni takataka.Kadhalika uhai wa CCM ni katika ufisadi.Imwadhibu Manji au Rostam kisha zawadi za mahekalu na Vogue kwa nyumba ndogo zao watapata UNDP?Waimarishe utawala bora unaozingatia maadili na sheria ili waende jela?Wampe nguvu zaidi za kisheria Utouh ili teni pasenti ziishe na mishahara hew irejeshwe hazina?TAKUKURU iimiarishwe ili dili jingine kama la Richmond lisizae Dowans?Na polisi wasiipendelee CCM ili wapinzani wasikike?Na Usalama wa Taifa wakumbushwe wajibu wao wa usalama wa taifa ili usalama wa mafisadi ubaki mikononi mwa sungusungu au Group 4?

Ingependeza sana kuwa na chama chenye sera nzuri na itikadi inayoeleweka.Lakini nadhani sera ya haraka tunayohitaji sasa hivi ni kupambana na ufisadi.Na katika hilo angalau Chadema wametuonyesha wanaweza.By the way,kama JK anatuambia kuwa awamu yake ya kwanza ilikuwa ni kujifunza uongozi licha ya chama chake kuwa madarakani miaka nenda miaka rudi,kwanini basi Chadema nayo isipewe fursa ya kujifunza ikiwa kazini,lakini tofauti na CCM,chama hicho kinaweza kuendelea kilipo sasa katika vita yake dhidi ya mafisadi?
 
sawa.. tufanye hivi.. tuunge mkono Chadema iingie madarakani halafu tujue mbele ya safari watafanya nini na madaraka hayo kuhusiana na matatizo ya wananchi wetu. Tumeendeshwa kwa muda mrefu bila ya kuwabana CCM na kuwaacha waongoze wapendavyo. Sasa chama kingine kinataka kushika madaraka tunaambiwa tuamini tu kuwa wanataka madaraka vizuri na tusiwabane kujua wanataka kuyatumia madaraka hayo vipi. Kwamba, kwa kadiri ya kwamba wanataka kuingia madarkani na kuwanyang'anya CCM madarakani basi hilo latosha.

Madaraka yana tabia moja mbaya sana; tabia ambayo yakiachwa bila kuhojiwa na kusimamiwa huharabu wenye madaraka hayo. Lakini naambiwa tusijiulize hili kuhusu Chadema kwa sababu lengo lao ni "noble" ambalo ni kuindoa CCM madarakani. How sad!..

Nilitarajia wanaotaka Chadema iingie madarakani wangetaka kujua madaraka hayo yatatumikaje kushughulikia mafisadi Tanzania, mfumo wa utawala wa kifisadi, kwa vipi na kwa gharama gani na kwa kasi gani. Lakini hili si muhimu kwao. Hilo treni la imani linaloenda msikotaka kukujua nyinyi pandeni, shangilieni na imbeni nyimbo za shangwe. Labda na mimi nitalipanda siku moja. Lakini nitalipanda pale tu nitakapokuwa na uhakika treni letu linataka kutupeleka wapi na wa kwa vipi. Mambo ya kwenda kuteremshwa njiani.... ndiyo haya haya ya CCM.

Mkuu,hivi kweli kabisa unaona Chadema hawajafanya lolote dhidi ya ufisadi?Hata ku-risk maisha yao kwa kuweka hadharani list of shame si lolote si chochote?Hata kufukua uozo wa EPA bado haitoshi kutueleza angalau wao wanaweza kunyoosha kidole pale CCM inapoficha mkono mzima mfukoni?

Hivi Mkuu,kama akina Dkt Slaa wanaweza kuhatarisha maisha yao na ya watoa habari wao kuibua nyaraka mbalimbali zinazohusiana na ufisadi,watashindwaje wakiwa madarakani kwenda mbali zaidi na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria wahusika?

Mkuu,sidhani kama kuna haja kwa Chadema au chama kingine chochote kile kutueleza namna kitakavyoshughulikia ufisadi kwa sababu kila Mtanzania mwenye akili timamu anafahamu nini kinapaswa kufanywa kwa mafisadi.Je ungependelea Chadema warejee kauli kama ya JK kuwa "NAWAFAHAMU WALA RUSHWA KWA MAJINA ILA NAWAPA MUDA WA KUJIREKEBISHA"?

Tunachohitaji sio kauli bali vitendo.Na kwa vile licha ya mazingira magumu na ya hatari yaliyokuwa yakiwakabili kama chama cha upinzani,Chadema walidiriki kuukomalia ufisadi,kwanini hicho kisiwe kigezo cha kuwaamini kuwa wanaweza kupambana na ufisadi KWA VITENDO as opposed na AHADI au MANENO matupu kama unavyotaka wewe (unaposema hawajatuambia watafanyaje.Mbona CCM wametuambia watafanyaje na hawajafanya?)

Kama umeweza kuiamini CCJ kwa MANENO yake matamu (kama yaliyomo kwenye manifesto za CCM) sijui kunakuwa na ugumu gani katika kuiamini Chadema kwa MATENDO yake machache lakini yenye impact kubwa kwa taifa!

Na kama kuifuata Chadema ni sawa na kudandia treni isiyojulikana inakwenda wapi,hivi kuifata CCJ sio sawa na kudandia hewa kwa kudhani ni treni?Angalau anayepanda treni isiyojulikana inakokwenda anaweza kubaini njiani kuwa amechukua usafiri usiomfaa,na hivyo kutafuta namna nyingine ya kwenda aendako.What about aliyedandia hewa? (Hewa here stands for a "non-existent party" like CCJ,chama cha mzaha ambacho viongozi wao wanamtaka msajili kuhakiki wanachama ilhali baadhi ya viongozi haohao hawana kadi za uanachama).
 
It's very simple... wakuu zangu tusipoteze nguvu zetu bure nimemgundua huyu Mwanakijiji kuwa hajiungi na Chadema kwa sababu yeye hakubaliani na mrengo wa kati. He is what he say a Conservative - far right yaani left iliyozidi hadi kuwa kulia!
Kuna mshikaji wangu mmoja alinambia Ukiwa Hanolulu huwezi kusema Amerika iko West ila iko East, China ndio iko West...Hivyo tujaribu kumwelewa lugha yakena tumsamehe.
Huyu huyu anatangaza sana umuhimu wa Itikadi, lakini ndiye huyu anatetea sana haki ya mgombea binafsi asiyekuwa na itikadi!
Kaazi kweli kweli....
 
Mwanakijiji,
Ungetarajia CHADEMA waseme yapi watafanya wakiingia madarakani ili uwaunge mkono? Wakati mwingine sio sahihi kusubiri CHADEMA waseme watafanya lipi wakiingia madarakani, tujiunge nao tuwaambie wanalotakiwa kulifanya kwa ajili ya TAIFA letu. Tusiwe kama waganga wa kienyeji ambao hawakwambii dawa wanazokutibia zinatokana na nini.
Wako watu mle ndani ya CHADEMA ni wasikivu sana tu.
 
Mwanakijiji,
Ungetarajia CHADEMA waseme yapi watafanya wakiingia madarakani ili uwaunge mkono? Wakati mwingine sio sahihi kusubiri CHADEMA waseme watafanya lipi wakiingia madarakani, tujiunge nao tuwaambie wanalotakiwa kulifanya kwa ajili ya TAIFA letu. Tusiwe kama waganga wa kienyeji ambao hawakwambii dawa wanazokutibia zinatokana na nini.
Wako watu mle ndani ya CHADEMA ni wasikivu sana tu.

oh yeah?
 
Nilipata kutahadharisha hapa kuwa hii option ya kuanzisha CCJ ilichelewa kidogo,na kutokana na mechanics za CCM watawakwamisha tu....lakini hili la Mpendazoe & Co nalikubali kabisa,pamoja na yote yanayoropokwa juu yao,sadly yule mwenzao nadhani ni katibu anatia binzari katika chai,kwamba ni wasaliti....kaka Lyatonga nae kaingia ngomani sasa anacheza sindimba na hii ni sangula....uhuru wa demokrasia ni lazima uheshimiwe wakina Wassira,Tambwe na Mtemvu wamehama vyama mara ngapi?mbona leo wamo CCM na nyadhifa pia?Sidhani kama Mpendazoe shida yake ni ubunge tu...angeendelea kuwa hivyo...kwa kuwaunga mkono mafisadi kama Serukamba...MMKJ big up
 
Nimefuatilia mjadala huu kwa umakini kabisa na nimebaini kuwa kuna waliomwelewa Mzee MKJJ na wengine aidha hawakumuelewa au wanapingana na hoja yake kwa kuwa tu imetolewa naye.

Kwa wanaopingana na hoja ya ''What then'' wamenikumbusha simulizi za kale ikiwemo ya Vita ya Majimaji. Katika simulizi hizo, kuna jamii ilipatwa na matatizo ambapo baada ya kwenda kwa mganga wakaambiwa watafute Ng,ombe Mweusi mwenye baka jekundu kichwani. Kwa kuona kuwa sharti hilo ni rahisi, hawakutaka kujua baada ya kupatikana ng'ombe huyo, what then. Hata hivyo, kutokana na aina hiyo ya ng,ombe kutokuwepo katika jamii yao, walihangaika sana kumtafuta mpaka walipokaribia kukata tamaa ndio akapatikana.

Kutokana na furaha ya kumpata yule ng'ombe, walifanya sherehe kubwa, ambapo walikunywa na kula hadi wakasahau shida zao. Walipokuja kukumbuka kuwa licha ya kupatikana kwa ng'ombe,wamfanye nini, wakaanza kuulizana ambapo kati yao wote hakuwepo mwenye jibu, ndipo walipokata shauri la kurudi kwa yule mganga kuulizia wamfanye nini yule ng'ombe. Kwa bahati mbaya wakakuta yule mganga amefariki siku walipomaliza sherehe za kusherekea kupatikana kwa ng'ombe.

Hata wakati wa harakati za vita ya Majimaji, baada ya wananchi kuambiwa kuwa kuna mganga ana uwezo wa kugeuza risasi kuwa maji, wengi wa waliokwenda kwake, hawakusubiri maelekezo ya what then baada ya kunywa dawa ile, na badala yake wakaenda kuanzisha vita.

Kutokifikiria ''what then'', ndiko kunakoigharimu hata CCM kwa sasa kwani baada ya kuingia kwa mfumo wa Vyama vingi, haikujua dhamana iliyoko mbele yao na kusahau kuwa wao ni Chama cha Mpito katika ujenzi wa nchi inayotumia Mfumo wa Vyama vingi.

Hawakujua kuwa wao sio chama tawala tena, bali ni Chama Jenzi cha kuweka misingi Imara ya utawala wa nchi.

Lakini kibaya zaidi wakadhani kuwa bado wako kwenye zama za mawazo sahihi ya viongozi na kudhani kuwa nchi haihitaji mjadala wa Kitaifa utakaoweka Mwelekeo Mpya wa Kitaifa ambamo vyama vyote vya siasa vinapaswa kutekeleza sera kwa kufuata mwelekeo huo.

Kung'ang'ania kuingia madarakani bila kujua what then, hakuna maana yoyote na sio ajabu wakajikuta wanafanya yaleyale ya CCM ambayo tunayapinga.

Vyama vya upinzani pengine ningevipa tano yangu, iwapo vingejenga hoja kuwa vinataka kuing'oa CCM ili vifanye kazi ya kuweka misingi ya Mwelekeo wa Taifa letu kitu ambacho nadhani siyo ajenda yao.

Kwa kutofanya hivyo, ni kuandaa mazingira ya kukurupuka na kuanzisha migogoro mingine isiyokwisha.
 
It's very simple... wakuu zangu tusipoteze nguvu zetu bure nimemgundua huyu Mwanakijiji kuwa hajiungi na Chadema kwa sababu yeye hakubaliani na mrengo wa kati. He is what he say a Conservative - far right yaani left iliyozidi hadi kuwa kulia!
Kuna mshikaji wangu mmoja alinambia Ukiwa Hanolulu huwezi kusema Amerika iko West ila iko East, China ndio iko West...Hivyo tujaribu kumwelewa lugha yakena tumsamehe.
Huyu huyu anatangaza sana umuhimu wa Itikadi, lakini ndiye huyu anatetea sana haki ya mgombea binafsi asiyekuwa na itikadi!
Kaazi kweli kweli....
Mkandala, hii " Kaazi kweli kweli..." pia inaweza kuwa ni sehemu ya kazi tuu!.
 
Chama Pekee ni CHADEMA hivyo kuna haja ya kuungana mkono mzee mwanakijiji

Josh, hili tunalijua. Tatizo ambalo naamini mimi na ninahisi kila mtu anashindwa kuelewa ni hivi huyu MKJJ, wakati anatuambia na kuimba ngonjera ya mabadiliko lazima uchaguzi huu alimamanisha nini? Maana, baada ya rai yake hiyo, muda muda tu, tukasikia CCJ- mara MKJJ mwanachama muanzilishi- mara wamenzisha on-line registration kuingia CCJ ili kuharakisha idadi ya wanachama!! Kufumba na kufumbua CCJ wana makabrasha lukuki ofisini kwa Tendwa kudai "permanent registration". Hapo tukasema sasa yaweza kuwa tofauti!!!

Yakazuka yaliyozuka, wote twayajua, mwishwe CCJ ziii... Tukapewa moyo, ooh Diplomatic Corps...bla bla bla... Matokeo ya hapo, wanachama wa CCJ wakaachwa solemba!! Hata Mkuu MKJJ akanyamaza, hakuna mbwembwe tena. Watu wakasema sana humu suala la kuunganisha nguvu na CHADEMA maana ndo chama kinachoweza kushabihiana na CCJ. MKJJ, anakuja na maswali yake "then what" Sisi tunasema si mukaongee huko na CHADEMA, maana si wana sera zao wamekiwshatoa.... mkuu anang'ang'ania tu "then what"

Mimi naanza kupata mashaka he must be on his mission. :pound:
 
Nimefuatilia mjadala huu kwa umakini kabisa na nimebaini kuwa kuna waliomwelewa Mzee MKJJ na wengine aidha hawakumuelewa au wanapingana na hoja yake kwa kuwa tu imetolewa naye.

Napenda watu wanaochukua muda kufikiria kwa undani kile kinachosemwa badala ya kurusha madongo kwa mtu binafsi - ad hominem. Kwa vile wengi wetu hatupendi kuiona CCM madarakani hata kwa siku moja zaidi basi tunatakiwa kushangilia kundi la wanaosema "tuiong'oe madarakani". Wengine wanasema "sera si muhimu" na wengine hata sera zenyewe hawazijui.

Hivi nikimuuliza mtu kuwa sera za Chadema kuhusu Usalama wa Taifa ni nini, mtaniambia nini? - haijalishi tuing'oe tu CCM madarakani tutajua mbele ya safari. Nikiuliza sera za Chadema kuhusu ulinzi ni nini? mtu atanionesha sijui mistari SITA TU ya sera ya Ulinzi lakini wanataka "tuing'oe CCM madarakani". Embu niulize ni mabadiliko gani wanayataka kwenye ofisi ya CAG na Mwanasheria Mkuu ili kuleta utawala bora? Wataniambia haijalishi, "Sisi tunataka CCM ing'olewe madarakani hayo mengine tutayajua baadaye!. Sijui ni maono gani ya kiuongozi ambayo yamefungamana na chuki isiyotaka kufumbua macho!




Kung'ang'ania kuingia madarakani bila kujua what then, hakuna maana yoyote na sio ajabu wakajikuta wanafanya yaleyale ya CCM ambayo tunayapinga.

Wao wanakwambia haijalishi!! Kwamba madarakani mikononi mwao yatakuwa salama zaidi kuliko mikononi mwa CCM au mtu mwingine! Tukiuliza kwanini? hawasemi wanataka tuamini tu kuwa CCM ikiondolewa basi itakuwa ni tiba ya matatizo yetu hata kama hatujui dawa tunayohitaji ni nini na kwa kiwango gani na kwa haraka gani! Tunaambiwa, tusiwe na wasiwasi kwani Chadema "imefanya mambo mengi kuhusu vita dhidi ya ufisadi". Really? Katika kesi zote zinazoendelea za ufisadi ni ipi ambayo Chadema imeomba hata iwe "rafiki wa mahakama"? HAKUNA. Hata kesi ya mgombea binafsi CHadema ilikuwa na uwezo wa kuomba kuwa rafiki wa mahakama lakini HAIKUFANYA HIVYO, lakini tunaambiwa twende tu tuamini!! Katiba inaruhusu mwananchi kufungua kesi ya mashtaka yeye mwenyewe (mtikila amefanya hivyo), Chadema haijafanya hivyo kwanini?

Wanasema "mwanakijiji unahoji maswali mengi bwana, sisi tuing'oe tu CCM halafu mengine tutayajua mbele ya safari".



Kwa kutofanya hivyo, ni kuandaa mazingira ya kukurupuka na kuanzisha migogoro mingine isiyokwisha.

Hii inaitwa hekima!

Labda wewe ni mtu wa pili au watatu ambaye ametumia muda kufikiria nini tunachouliza.

Kweli tunatakiwa kuiachilia nchi yetu kwa uongozi mwingine bila kuwa absolutely sure ya kile tunachokitaka kwao alimradi tu ati tuna common enemy. I say NOT ME SIRE AND NOT YET! Kila ndege huruka na mbawaze!
 
Wao wanakwambia haijalishi!! Kwamba madarakani mikononi mwao yatakuwa salama zaidi kuliko mikononi mwa CCM au mtu mwingine! Tukiuliza kwanini? hawasemi wanataka tuamini tu kuwa CCM ikiondolewa basi itakuwa ni tiba ya matatizo yetu hata kama hatujui dawa tunayohitaji ni nini na kwa kiwango gani na kwa haraka gani! Tunaambiwa, tusiwe na wasiwasi kwani Chadema "imefanya mambo mengi kuhusu vita dhidi ya ufisadi". Really? Katika kesi zote zinazoendelea za ufisadi ni ipi ambayo Chadema imeomba hata iwe "rafiki wa mahakama"? HAKUNA. Hata kesi ya mgombea binafsi CHadema ilikuwa na uwezo wa kuomba kuwa rafiki wa mahakama lakini HAIKUFANYA HIVYO, lakini tunaambiwa twende tu tuamini!! Katiba inaruhusu mwananchi kufungua kesi ya mashtaka yeye mwenyewe (mtikila amefanya hivyo), Chadema haijafanya hivyo kwanini?

Mkuu MKJJ, Asante sana. Umenena yaliyomo kichwani kwangu.

Mkuu hebu nisaidie, wakati CCJ wanfanya mazungumzo na vyama vingine (specifically CHADEMA); ulikuwa unapata updates?
 
Back
Top Bottom