Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa

Yah: Kuunga mkono CHADEMA kwa sasa

Kuna watu wanatisha humu duh ushauri wao ni kama sumu.
Watu wanaandika tu ila wahajuhi what is like to be in the battle field has kwenye inch yenye demokrasia changa kama bongo.
Watu hawa hatuna uhakika kama hata wata piga kura wakiwa ughaibuni....watu hawa ni hatari
 
Mlalahoi,

Ukiwa na bondia wako na unajua ni dhaifu, utaendelea kumpeleka kwenye ulingo bila kumuandaa ipaswavyo kisa ni lazima apigane tuu? Je akipigwa mpaka kuzimia na akizinduka kisaikolojia akawa amedhoofika utaendeleza mbinu na mazoezi yale yale ambayo yalimfanya ashindwe pambano la kwanza hata la saba?

Nimekosoa ile soft approach ya kutotaka kutoana ngeu na CCM, ile soft approach ya kuogopa kunyimwa Ruzuku au mgao wa fedha. Nimewasihi Chadema watunishe msuli kwa kila jambo kila mwaka wa bajeti na kila kisichoeleweka na wasiridhike na kauli nyepesi nyepesi au ahadi mbofumbofu.

Lakini bado wameendelea kuburuzwa na barudhuli CCM, ndio maana nauliza na nakubaliana wakishinda then what ikiwa wao wako defensive na hata wakishinda ushindi wao hautakuwa na nguvu za kutosha kuwaweka kando CCM wasiharibiwe fursa yao ya kutawala?

Sisi kama Taifa, matokeo ya kupata Uhuru tukiwa wachanag tumeyaona, leo hii mkoloni karudi kiulaini kwa mikopo, misaada na uwekezaji. Leo uwezo wa kujitawala hatuna tunamtegemea Mwekezaji na tunaogopa mkorofisha kwa kuwa hatuna nguvu za kusimama wenyewe wima na kujilinda.

This is the fate of opposition ambao bado wanaonyesha woga na udhaifu. Hata huko kujitolea mhanga si kule kwa kusema "kudadeki mpaka tone la mwisho" bali ni kule kwa kuogopa kuiudhi CCM na Serikali yake na kuhofia ubabe wa CCM kama vile walivyofanyiwa Mtikila na Lamwai.

Then you have a serious problem ya watu wasio na uwezo wa kujiamini bila kutegemea. Sasa kama kwa CCM wanahofia, kwa hao wengine Mafisadi, Wawekezaji na mawakala wa Mkoloni watafanyaje , huku CCM naye anawasumbua?

HIvyo tutafakari hayo yote sasa hivi si kwa nia ya kusema tusiendelee mbele na kuing'oa CCM, lakini tujue wazi huko tunakokwenda na tujiandai kikamilifu na si kubahatisha kwa kusema ngoja tufanikiwe kwanza.

Tena kama kauli za uhakika (self assured) zingetoka mapema na hata leo hii kujiuza kwa Upinzani kumpasha Mtanzania kuwa si suala la nia na sababu tu kuwa zipo, bali hata uwezo upo, umati mkubwa wa Watanzania usingeingia mashaka.

Tuna miezi mitatu ya kuuza ujumbe wa tumaini, utakaoonyesha kuwa hili si jaribio tena bali ni kujiamini na tuko tayari kwa lolote na hata kutoa kafara kuing'oa CCM.

Je Upinzani uko tayari kutumia turufu hiyo kwa Mtanzania atakayepiga kura?

Mkuu,another side of the story ni HUJUMA ZINAZOFANYWA NA CCM.Hivi kama Rostam,Lowassa na mafisadi wengine wanaweza kumwaga pesa dhidi ya wana-CCM wenzao (ambao hawana madhara makubwa kwao zaidi ya kukemea au pengine kupongeza ref kujiuzulu kwa Lowassa)kwa vile tu wanawaona kuwa kikwazo katika ufisadi wao,wanawekeza kiasi gani kuhakikisha type za watu kama Dkt Slaa ambaye hachelei to call a spade a spade (ref List of shame) hawaingii madarakani.

Natambua kuwa kuna mapungufu ndani ya vyama vyote vya siasa.Natambua pia kuwa miongoni mwa vyama vya upinzani kuwa "waharibifu" na wasindikizaji kama akina Mrema.Lakini naamini kabisa kwa namna Chadema ilivyoshikilia bango suala la ufisadi angalau wametuonyesha wanatambua kikwazo kikuu cha maendeleo yetu ni nini.Naamini pia kuwa kwa uelewa huo itakuwa rahisi kwao kuu-employ kukomesha ufisadi pindi wakiingia madarakani.

Hizo chaguzi ulizotolea mfano tatizo kubwa na mazingira yaliyopo ambapo CCM "inakaba hadi kona".Mkuu wa Mkoa ana waraka wa kuwabana wapinzani,DC na waraka kama huo...RSO,DSO,RPC,OCD...the list goes on...na hapo hatujajumuisha "wasimamizi wa uchaguzi",viumbe ambao ajira yao inategemea "baraka za CCM".

Natambua mkuu,hata kama tunatofautiana kimtizamo,una uchungu wa hali ya juu kuhusu hali ya mambo huko nyumbani.Binafsi naendelea kuamini kuwa pasipo kuondoa kansa hii inayotishia kuharibu mwili mzima,sio tu kuwa safari yetu itachukua muda mrefu bali pia kuna hatari ya kutumbukia kwenye korongo refu along the way.

I just hope Dkt Slaa atapitishwa na Chadema kisha Watanzania wote (wenye uchungu wa kweli kwa nchi yetu) watampa sapoti ya nguvu ili tuwape red card mafisadi.Penye nia pana njia.
 
Kuna watu wanatisha humu duh ushauri wao ni kama sumu.
Watu wanaandika tu ila wahajuhi what is like to be in the battle field has kwenye inch yenye demokrasia changa kama bongo.
Watu hawa hatuna uhakika kama hata wata piga kura wakiwa ughaibuni....watu hawa ni hatari
Ni sumu tena kali Mutu lakini kwa JF haimwagiki kirahisi wataimba hadi wachoke wenyewe. Wanatuambia eti tusubiri kwanza tujifunze kutawala ndipo tuing'oe CCM, kwani CCM walijifunza kutawala wapi ndipo wakaingia.

Hawajui machungu waliyonayo watanzania, wao wako ughaibuni watoto wao wanasoma kwa benefits hawajui hata kuwa watoto wetu ni jana tu walifukuzwa shule kwa kukosa mchango wa tuisheni wa shilingi mia tano, wao wakikosa kazi wanalipwa Jobseekers allowance.

Ndio hao hao wanatuambia tusubiri hadi machungu yawe makali ndipo tumtafute mganga, je kama ni ugonjwa wa kansa si utakuwa sugu hautibiki tena, uzuri tumewajua na lengo lao tumelijua hawatupi tabu.
 
Sasa ukitafakari kwa makini, hili la wapinzani na Chadema na mtazamo wa Watanzania wengi kuwa kwanza tuing'oe CCM, lakini inaelekea bado hatujajiandaa vya kutosha kuweza kuongoza tukishaiondoa CCM.
Si kwamba nadai CCM ibakie madarakani au isiondolewe, lakini kama Bibi Ntilie alivyobainisha kwenye barua ya Mnyika, yaelekea Chadema bado hawajajiandaa na hawajiamini kuwa wana uwezo wa kuongoza Taifa. Dua lao ni CCM ianguke, ndipo wao waanze kujifunza na kujipanga ni vipi waongoze Tanzania.
Ndiyo maana Mwanakijiji anauliza, then what?


Ikiwa mfupa wa TAMISEMI ambapo huko ndipo safu ya kwanza ya kuongoza nchi, Chadema walikukwepa wala hawakujituma kupata viti angalao nusu ya mkoa kama Dar, iweje leo tudhanie kuwa wataweza kuwa makini na uwezo wa kuongoza nchi kwenye Serikali Kuu na Bunge?


Makovu haya hayaweza kusawazishwa pamoja na hili la sasa la kuvizia mabaki ya CCM yaanguke ndipo yaingie Chadema na kuhakikisha walau Chadema wanaweza pata viti 70 vya ubunge.

Ni kutokana na hayo, ndio maana nakubaliana na Mwanakijiji kuhoji je tukishaing'oa CCM, then what? Maana inaelekea kama vile tulivyopata Uhuru au vile Kikwete alipata Urais, bado hatujajiandaa kuongoza na hatujiamini kuwa tuna uwezo wa kutawala.

Kila udhaifu wa CCM umetolewa majukwaani, lakini hapajawahi tolewa alternative solution ambayo ikakubalika hata ndani ya Chadema yenyewe, kila mara tunaambiwa "Subirini tuingie Ikulu". Je ina maana Chadema na Upinzani hauwezi kuanza kuleta maendeleo Tanzania mpaka viingie Ikulu?

Miaka mitano, bajeti ya nchi imekuwa ikiongezeka na matumizi ya hali ya juu. Ripoti ya mkaguzi mkuu CAG kwa miaka mitatu inaonyesha udhaifu wa Serikali kuu ambao umeimarisha ubadhirifu na rushwa. Lakini sijasikia hata siku moja hoja ya kutungwa Sheria au kusitisha Bajeti kutoka kwa Upinzani ili Serikali ijirudi na kurekebisha mfumo wake wa matumizi na hata kubana matumizi. Je wajibu huu ambao kawaida hufanywa na Chama cha Upinzani kama haukufanywa na Chadema na wenzao, bado mtasema tusubiri wakiingia madarakani?

Labda nihitimishe kwa kutoa mtazamo mwingine. TUfanye kwamba Upinzani umeshinda Uchaguzi Mkuu kwa asilimia 51% hiyo 49% ni ya CCM, pale Bungeni na hata Urais ni wa Upinzani. Inapokuja kwenya ufanyako kazi na utekelezaji hasa kwenye ngazi za Tawala za Mikoa (TAMISEMI), watendaji wengi wa kisiasa takriban asilimia 95% ni CCM ambao walishinda Udiwani na uchaguzi wa TAMISEMI 2009. Je Upinzani utawezaje kufanya kazi yake kwa ukamilifu bila mvurugano na hawa watu wa CCM ambao watakuwa wakisikiliza sauti za wale 49% walioko Bungeni?

Kila mtu anataka CCM iondoke, lakini hatuko tayari kukipa chama nafasi eti kikajifunze kazi kama Kikwete alivyofanya au kuwa ni Chama kisicho na wenye uwezo wa kutosha kuongoza na kufanya kazi kitendaji kama zile Tanzania ilivyopata Uhuru wake.

Baya zaidi, bado mpaka leo Chadema na Upinzani havieleweki Ki-Sera kwa Watanzania na hatujui watakuja na mipango gani ya Kisiasa na kimaendeleo kwa kueleweka kuliongoza Taifa la Tanzania.

Hivyo basi, inabidi tujiulize, je tuko tayari kuendelea kubahatisha kama Kikwete kwa miaka miwili ili kuelewa nini wajibu wa kuongoza nchi na kuwa na sera zinazoeleweka au ni lazima tujiamini na kuingia tukiwa tayari na Sera zetu zikieleweka kwa Wananchi ambao hawatahitaji miaka miwili kuzielewa na kuanza kuzifanyia kazi?

Uchambuzi mzuri Rev, mapambano yana stages, huwezi kutarajia kumng'oa adui bila kuwa na mipango na hatua madhubuti. Mwenye kusikia atasikia. Kama hili la Dr Slaa kugombea uraisi litawagharimu Chadema na Wtz kwa ujumla
 
Ni sumu tena kali Mutu lakini kwa JF haimwagiki kirahisi wataimba hadi wachoke wenyewe. Wanatuambia eti tusubiri kwanza tujifunze kutawala ndipo tuing'oe CCM, kwani CCM walijifunza kutawala wapi ndipo wakaingia.

Hawajui machungu waliyonayo watanzania, wao wako ughaibuni watoto wao wanasoma kwa benefits hawajui hata kuwa watoto wetu ni jana tu walifukuzwa shule kwa kukosa mchango wa tuisheni wa shilingi mia tano, wao wakikosa kazi wanalipwa Jobseekers allowance.
Ndio hao hao wanatuambia tusubiri hadi machungu yawe makali ndipo tumtafute mganga, je kama ni ugonjwa wa kansa si utakuwa sugu hautibiki tena, uzuri tumewajua na lengo lao tumelijua hawatupi tabu.

Sasa hii imekaa kama kuna uchu na chuki za madaraka.....duh siasa za TZ at it's best, sio kwa faida ya wananchi
 
Kama haya maswali waneulizwa kina Nyerere wakati wakipigania kumwondoa mkoloni ingekuwa kazi mubwa..
Hivi kweli wewe Mwanakijiji unafikiria watu wanataka kuiondoa CCM ili iwe nini?...mkuu wangu pengine sikusomi vizuri lakini mtu atataka kuondoa CCM madarakani asijue kwa nini ama kitafuata nini..sasa kwa nini wanagombea madaraka!..Bila shaka Chadema watachukua madaraka na kuhakikisha sera walizouza kwa wananchi na kukubaliwa zinafanya kazi..

Samahani lakini hivi unachotaka wewe ni madaraka yatagawanywa vipi au? maanake hata Ufisadi ni sehemu tu ya sababu za kuing'oa CCM madarakani ndani ya swala kubwa la Katiba yetu..miiko na maadili yapo ktk katiba na haya yote ni maswala yatakayopewa nafasi ktk bunge la kwanza hivyo kama wewe unalo tofali lako beba jiunge na kesho utaingia nalo bungeni kwa sababu tusifikirie kabisa kwamba Chadema wakichukua nchi basi nao watuburuze na sera ambazo wewe Mwanakijiji unazikubali..

Siku zote mhitaji ndiye husema anachokitaka na mbunge ni mwakilishi wa mawazo hayo,hivyo hata ngazi ya Kitaifa Chadema watafanya tu kile kinachohitajika na wananchi wakizingatia titikadi yao itawezesha vipi kupatikana kwake. Kila itikadi mkuu wangu ina mbinu ya kuleta kitu kile kile kinachohitajiwa Kitaifa..

LENGO ni moja isipokuwa kuna njia tofauti za kufikia lengo hilo.. Hata JK na CCM wanafikiria wanakwenda sawa kufikia maisha bora kwa kila mwananchi..Sii Chadema, CCM, NCCR TLP na wengine woote wanaamini adui yetu mkubwa ni Ujinga, Umaskini na maradhi isipokuwa tofauti zao zinakuja ktk mbinu na vipaumbele vya kutokomeza vitu hivi..

Kifupi CCM wanaamini kuvua wao kisha wape samaki maskini wasiojiweza na Chadema wanasema mfundishe maskini kuvua, kesho atakwenda mwenyewe kuvua samaki! Bado una shaka gani? mbona mimi niliwasoma mapema!
Mkuu nimekusoma ndani ya mistari yako.
Na jana wametupa chaguo sahihi la mgombea na siye kuwa na chembe ya uoga hasa linapokuja swala la kitaifa.Siyo huyu Dr.wa kikwere kila siku nina list ya wezi,walafi,wauza bwimbwi halafua anashindwa kuyataja majina.

mbele tunasonga na kura tutampigia na ninaimani hata mkuu MMKJJ atampigia pia DR.Slaa.

Ee Mungu tuongoze watz tupate mwanga bora wa kuyaona maisha katika mwanga bora zaidi,, Amen.
 
Kuna watu wanatisha humu duh ushauri wao ni kama sumu.
Watu wanaandika tu ila wahajuhi what is like to be in the battle field has kwenye inch yenye demokrasia changa kama bongo.
Watu hawa hatuna uhakika kama hata wata piga kura wakiwa ughaibuni....watu hawa ni hatari
Kama wanaandika na wewe umepata kuyasoma waliyoandika,basi yatafakari kwa kina na chukua hatua sahii kutoka kwa kichwa yako.
Maana kuandika kwao ndiyo faida kwako kuyaona,soma na kufanya tafakuri sahihi ili kujua nni kifanyike inchi isonge mbele!
 
Nilifahamu juu ya mazungumzo ya baadhi ya uongozi wa juu wa CCJ na Chadema kwa muda kidogo; Yalitokana vile vile na ushauri wa watu mbalimbali kuwa CCJ iunganishe nguvu na Chadema. Hata hivyo hadi hivi sasa kilichofanyika ni baadhi tu yaviongozi wake kujiunga na Chadema na siyo CCJ nzima. Kuna sababu.

Wapo wanaosema kwa vile hawa ndugu zetu wameingia Chadema basi CCJ na wazo la CCJ nalo limekufa kwa hiyo sote tuliounga mkono CCJ tuinamishe vichwa vyetu kwa kushindwa na kujiunga na Chadema. Hizi ni fikra potofu. Ni potofu kwa sababu zinafikiria Chama kikifa au kikishindwa ina maana mawazo yake nayo yameshindwa. Yanafikiria kuwa kama watu wakitoka kujiunga na chama kingine au kutoka katika siasa maana yake siasa za chama hicho nazo zimeshindwa.

Ukweli unabakia kuwa ukweli kwamba siasa za kutaka ushirikiano wenye lengo la kuitoa tu CCM madarakani halafu ndiyo tujue tunataka kufanya nini ni siasa ambazo katika dhamira yangu siwezi kuziunga mkono. Siasa za kutosema nini unataka kufanya, kwa vipi na kwa muda gani ukionesha ukali kuhusu ufisadi miye siziwezi kwa sababu niaamini tatizo la Tanzania ni ufisadi kuliko kitu kingine chochote kile.

Kutuambia kuwa "panya hawakamatani" lakini hutuambii wewe utawakamata vipi na kwa namna gani, haitoshi vile vile.

Chadema ni tumaini kubwa sana kwa wengi wetu na kwa muda mrefu limekuwa kwangu ni tumaini vile vile. Lakini bado haijataka kuvuta mstari ule wa kiungozi kwa miaka kadhaa sasa. Siamini kama ndani ya siku chache zilizobakia wataweza kuvuka mstari huo. Na watakapogundua kuwa walipaswa kuuvuka watajikuta wanagalagazwa kwenye uchaguzi mkuu huku wakilalamika "CCM", "Tume ya uchaguzi", "Wizi wa kura", "Vyombo vya dola".

Ninawatakia kila la kheri wale wanaojiunga na Chadema wakiamini kitabeba matarajio yao. Hiyo ni demokrasia na kwa hakika kabisa nawatakia mafanikio.

Kwangu mimini bora nirudi na kutokuwa na chama nikiendelea kusimamia fikra na itikadi na mambo ninayoyaamini kuliko kupanda treni ambalo siju linakwenda wapi na kwa nini ati kwa sababu wengine wamepanda na wanashangilia!

Kundi zima la wabunge wa CCM wanaweza kutoka baada ya bunge kuvunjwa na kujiunga na Chadema na kutoka hao akapatikana mgombea wa Urais wa Chadema kama inavyotarajiwa. Hii inaweza kuwa habari kubwa sana na mtikisiko kwa jukwaa la siasa. Kwa wengine hilo laweza kutosha kabisa kufanya waamini kuwa saa ya mabadiliko imefika. Kwangu mimi bado nitaangalia kwa macho ya shuku hadi nijue wanataka kufanya nini. Wakisema wanataka tu KUINDOA CCM MADARAKANI au KUONGEZA IDADI WA WABUNGE, nitawaangalia halafu nitacheeeeeeeka!

Chadema kinaweza kabisa kuwa chama ambacho kitachukua uongozi wa nchi mwaka huu, endapo tu KITATAKA.

MM
Mkuu kusema ukweli katika hili sinabudi kuunga nawe kwamba kuitoa CCM tu halafu mengine mbele kwa mbele haina tija kwa taifa na si Chadema tu na hivyo vingine pia kwa kukaa na fikra mgando kuwa mipango ya uongozi na maendeleo havifanyiki mpaka wameingia jumba jeupe.Hiyo ni dhana ya kuikimbia kabisa.
Utawala siyo jumba jeupe tu,mambo iko huku chini(TANISEMI)ambako ndo kila kitu.
Mfano mmoja na wa kweli kabisa pasipokwenda hata huko kunakoitwa vijijini.Uchaguzi ulofanyika 2009 wa hapa DAR jimbo la KAwe kata ya Mbweni viongozi wa CCM walirudi madarakani pasipo uchaguzi kufanyika kwani hakuna mgombea hata mmoja wa upinzani alikuwepo.
Sasa kwa mtindo huu ukiing'oa CCM unatwala vipi hapo???
Ifike mahali vyama vya upinzani vilitazame hili kwanza,na nina imani kwamba ndiyo chanzo cha kukosa madiwani na wabunge wengi ambao wangeweza kuvisaidia katika suala zima wa uongozi mzima.
 
Luteni

Nyerere alipouliza Watu wanakimbilia Ikulu kuna nini? Tulifurahia kauli hiyo kuwa lenga kina Kikwete, Lowassa na hata Malecela, Warioba na Msuya.

Sasa leo hii tukiuliza Lipumba n Chadema wanakimbilia nini Ikulu, tunaambiwa aah nyie roho korosho, mko majuu hamjui hali halisi!

Najua hali halisi zaidi yako, usifikiri kukaa nje basi ndio kuwa disconnected, kama niko disconnected as you think, nisingeling'amua la Richmond au Meremeta kuwa ni Uhujumu uchumi na kulipshikia bango!
 
Luteni

Nyerere alipouliza Watu wanakimbilia Ikulu kuna nini? Tulifurahia kauli hiyo kuwa lenga kina Kikwete, Lowassa na hata Malecela, Warioba na Msuya.

Sasa leo hii tukiuliza Lipumba n Chadema wanakimbilia nini Ikulu, tunaambiwa aah nyie roho korosho, mko majuu hamjui hali halisi!

Najua hali halisi zaidi yako, usifikiri kukaa nje basi ndio kuwa disconnected, kama niko disconnected as you think, nisingeling'amua la Richmond au Meremeta kuwa ni Uhujumu uchumi na kulipshikia bango!
Inavyoonekana hukumwelewa Nyerere au ulimwelewa ila unataka kupindisha kwa makusudi.
 
mimi mwenyewe kwa ukweli kutoka moyoni nahitaji mbadiliko haswa.lakini je?CHADEMA ndio chama mbadala kweli??!mpaka sasa sioni kitu kwenye upinzani zaidi ya blaah blaaah tu,usishangae hata huyo slaa katumwa kutulaghai tu kisha ccm inapiga mwendo kwa ushindi bwerere.sijui mi naona wapinzani watasindikiza tu na kuambulia ruzuku.
 
Nafikiri umefika wakati ambapo viongozi wa vyama vya upinzani wakaangalia alama za nyakati. Huu ni muda muafaka kwa vyama hivi kutoa ushirikiano wa pekee ili viweze kumuondoa SISIEMU na mafisadi wake kwenye UTAMU. Kwa mtazamo wangu, wakati huu unaruhusu kabisa chama cha upinzani kukamata madaraka Tanzania. Ingekuwa BUSARA kwa CUF na vyama vingine kuunga harakati za CHADEMA kuingia madarakani (MUUNGANO) kwa niaba ya wapenda maendeleo ya nchi yetu na vilevile vyama vingine pamoja na CHADEMA kui-support CUF upande wa Zanzibar. Sasa tuone SISIEMU watafanya nini kuwahadaa wananchi kuiba kura kurudi madarakani.
HUU NI MUDA MUAFAKA, TUACHE UBINAFSI...........Rangi za Mrema tulishaziona muda mrefu sana.
 
Je, Mwalimu aliposema upinzani wa kweli utapatikana tu mpasuko ndani ya CCM utakapotokea ina maana tuwe kama mafisi yanayokaa yakitokwa na mate yakisubiri siku mkono wa binadamu utakapodondoka. Shuhudia watu fulani fulani walivyoichangamkia CCJ eti tu kwa vile makapi yalikuwa yanasubiriwa yatoke CCM na kujiunga nayo na hapo CCJ ingekuwa imetakasika kiasi cha kuachiwa nchi. Sidhani kama tunataka kuiondoa CCM madarakani kwa sababu ya sera zake kwani nijuavyo CCM haina sera ya rushwa, CCM haina sera ya wizi, CCM haina sera ya ufisadi - la hasha. Tunataka kuiondoa CCM madarakani kwa vitendo vyake na viongozi wake ambao wameamua kutotenda yale wanayoyahubiri, kutotimiza yale wanayotuahidi na kutapanya rasilimali za taifa letu kama vile hazina mwenyewe.

Tunaelewa kabisa kuwa kuna msurururu mrefu wa wanaofaidika kutokana na kukaa kwao madarakani na watatumia kila mbinu kulinda hiyo hali hata ikibidi kudai kuwa hakuna mwananchi nje ya CCM anayeweza kuliongoza taifa. Mojawapo ya hizo mbinu ni kuanza kutukejeli kwa maswali kama tunataka kuiondoa CCM ili iweje huku wakijua fika kuwa bila CCM kuketishwa benchi hakuna mabadiliko yoyote yatakayowezekana kirahisi. Namshukuru Mwanamapinduzi Dr. Slaa ambaye pamoja na vizingiti vyote vinavyowekwa na vitakavyowekwa mbele yake na hawa chui waliovaa nguo za kondoo, ameamuru kuongoza haya mapambano ya kulinusuru taifa. Mrema wa JF wako wengi.
 
Luteni

Nyerere alipouliza Watu wanakimbilia Ikulu kuna nini? Tulifurahia kauli hiyo kuwa lenga kina Kikwete, Lowassa na hata Malecela, Warioba na Msuya.

Sasa leo hii tukiuliza Lipumba n Chadema wanakimbilia nini Ikulu, tunaambiwa aah nyie roho korosho, mko majuu hamjui hali halisi!

Najua hali halisi zaidi yako, usifikiri kukaa nje basi ndio kuwa disconnected, kama niko disconnected as you think, nisingeling'amua la Richmond au Meremeta kuwa ni Uhujumu uchumi na kulipshikia bango!



Nyerere alisema watu wasiende ikuli tusiwe na viongozi? usipindishe maneno either kwa makusudi au kwa uelewa wako mdogo.I'm afraid makusudi maana post zako zinyi nasoma anakuchukulia kuwa ni mwelewa vya kutosha.
 
Leo nina furaha kubwa sana na siwezi kuchangia kitu ktk mada hii. Na hakika hata Nyerere mwenyewe alipokuwa akiitangaza TANU walikutana na watu wenye kubeza chama kuwa hakikuwa tayari kuchukua uongozi kwa sababu hawakuona what next baada ya kumuondoa mkoloni.
Nachoweza kusema tu hapa ni kwamba Chadema hawawezi kuongoza kwa katiba yao isipokuwa kwa katiba ya nchi ambayo ndiyo mwongozo na dira ya Utawala. Kama dira hii ilipotoshwa kimazingara inarudishwa..

Ukifunga ndoa kuoa au kuolewa ni wazimu mtu akikuuliza what next kwani yeye alitaka iwe vipi?..
 
Leo nina furaha kubwa sana na siwezi kuchangia kitu ktk mada hii. Na hakika hata Nyerere mwenyewe alipokuwa akiitangaza TANU walikutana na watu wenye kubeza chama kuwa hakikuwa tayari kuchukua uongozi kwa sababu hawakuona what next baada ya kumuondoa mkoloni.
Nachoweza kusema tu hapa ni kwamba Chadema hawawezi kuongoza kwa katiba yao isipokuwa kwa katiba ya nchi ambayo ndiyo mwongozo na dira ya Utawala. Kama dira hii ilipotoshwa kimazingara inarudishwa..

Ukifunga ndoa kuoa au kuolewa ni wazimu mtu akikuuliza what next kwani yeye alitaka iwe vipi?..

Yup ,thats whatsup brother.
 
Nadhani itabidi niende ndani zaidi kuelezea kile ninachokiita "Tatizo la Chadema". Natumaini nitaeleweka, na siyotkuwa nimechelewa. Niwatoe hofu kabisa kwangu mimi hata CCM ikiondolewa kesho madarakani sitolia!! Lakini sitorukaruka kwa furaha! Nitauliza swali hili hili ninaloliuliza sasa.. "then what"? Nakataa kabisa kuwa hatuwezi kuwa na ajenda ya uchaguzi inayosema "tuiondoe CCM kwanza"! Hii ni ajenda ya kuondoa chama kimoja na kukiweka kingine. Yatakuwa yale yale ya KANU na RAINBOW coalition! Well RAINBOW walifanikiwa kabisa kuiondoa KANU, lakini is Kenya better today than during KANU's rule? Tutapata majibu tofauti sana kwenye hilo. Je Zambia chini ya Chiluba baada ya kuiangusha ZANU je walikuwa bora zaidi kwa sababu kina Chiluba walitimiza ndoto yao ya kumuangusha Kaunda?


Hili swali hata kama mtalikwepa, mtalibeza au mtajaribu kuonesha kuwa hamlielewi mtalazimika kulijibu tu one of these days. I know you will.

Kwa vile linaonekana ni gumu mno/halielewi au halijaulizwa sawasawa itabidi nilivunje vunje katika vipande vyake vidogovidogo. CHADEMA WAKILIELEWA NA KULIJIBU KABLA YA UCHAGUZI WATASHINDA KWA KISHINDO!

Mkuu, naomba nikutaarifu tu kuwa, Kenya ni bora zaidi sasa kuliko wakati wa uongozi wa KANU. Hasa kipindi ambacho KANU iliondolewa madarakani. Hiyo ni kweli na dhahiri. Nimeishuhudia.

Zambia pia ni bora zaidi kuliko kipindi chochote cha ZANU. Na hasa kipindi ambacho ZANU iliondolewa madarakani. Hii pia ni kweli na nimeishuhudia.

Mkuu, ukweli unabaki kuwa, mabadiliko ndio njia pekee ya kupata nafuu yoyote. Tumeshaona nini CCM inachoweza kukifanya kwa kukijaribu kwa miaka 18 tangu kuanzishwa kwa chama hicho na miaka mingine 15 tangu kuanzishwa kwa mfumo wa siasa za vyama vingi. Ninaimani kabisa kuwa, kwa mtiririko wa siasa za TZ kama hakuna disciplinary actions zitakazochukuliwa kwa mfumo huu wa utawala wa chama kimoja pamoja na umasikini unaotumaliza, kuna jambo baya zaidi litakaloikumba nchi yetu kuliko kama tutabadili kwa sababu zozote ziwazo.

Tusiogope mabadiliko. Tuogope kutobadilika. Kwani hata mgonjwa mahututi hutamani aachiwe apumzike badala ya kupelekwa hospitali kama chaguo lake la kwanza. Wakati mwingine, ukikaa sana juani, unaweza kudhani kuwa hapo ndipo mahali pazuri zaidi kuliko kama ukiwa kivulini. Hakuna faida ya uoga wa mabadiliko.

Ni jambo jema kuwa sasa tumesikia kuwa Dr. Wilbroad Slaa ameteuliwa/amechaguliwa/amejitolea kugombea u-Rais kwa kupitia chama cha upinzani (CHADEMA). Hakuna kitu ambacho nimekuwa nikiombea kuwa busara, hekima, mapenzi na moyo wa ujasiri umjae Mheshimiwa huu ili aweze kuchukua hatua kama hiyo. Sasa kwa mara ya kwanza kabisa najua kuwa kura yangu ya uRais inakwenda wapi na niko tayari kushawishi na kuomba kila mpenda mema, mjali hali za watu wote kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa Rais wa Tz kuanzia muda Rais mpya anaotakiwa kutangazwa atakuwa Dr. W. Slaa.

Naamini kuwa Dr. Slaa hatakuwa na roho ya kutojali kama Rais wa CCM alieshika madaraka kwa miaka mitani akifanya mzaha na kutojali umasikini wa Taifa lake, heshima ya nchi na malengo ya wananchi wake ambao walimuamini na kumkabidhi madaraka makubwa kabisa ya uongozi wa nchi. Naamini pia kuwa endapo Dr. Slaa atashinda na kuwa Rais, ataheshimu na kuthamini madaraka ya cheo hicho kuliko Rais aliepo na anaetaka kugombea tena. Naamini kwa busara, hekima na uthabiti wa Dr. Slaa, nchi hii itakuwa bora zaidi kuliko inavyoenda sasa. Itaheshimika zaidi na itafikia malengo ya kweli kwa kasi zaidi kuliko sasa ama wakati mwingine wowote.

Sabau za imani yangu kwa Dr. Slaa ni nyingi. Ila baadhi tu, ni kama ifuatavyo:

1. Kwa kuwa ametoka chama cha upinzani atakuwa na changamoto nyingi zaidi kuweza kushawishi wananchi kuwa kuchagua upinzani ni jambo jema na linaloweza kuleta tija, maendeleo na ufanisi mkubwa kuliko kung'ang'ania CCM

2. Usomi, hekima, busara na heshima aliyonayo vinamuwezesha kutathmini na kutekeleza kwa imani na uaminifu ahadi zake nyingi kwa ufanisi zaidi

3. Uzoefu wake katika siasa za nchi na ufahamu wa siasa zisizofaa unamfanya afae zaidi kuongoza Taifa kwa ufanisi mkubwa. Nadhani Dr. SLaa ndie kiongozi/mwanachama wa upinzania aliekaa Bungeni kwa muda wote na kwa muda mrefu zaidi kuliko viongozi wengine na sia jabau kuliko viongozi wengi sana ndani ya CCM

4. Chama chake kikiweza kujipanga na kuamua kutekeleza matakwa ya wananchi kwa uwezo wao wote, kina nafasi kubwa ya kufanikiwa sana. Kwani ni chama ambacho kina wasomi wengi, vijana na wenye ari na nia ya kuona mabadiliko chanya.

Sababu ni nyingi, lakini niahisi hizi zinatosha kwa manufaa ya mjadala huu.
 
Recta,
Nimemsoma Mwanakijiji kule ktk mada yake mpya kuhusiana na hili, kazungumzia (CHUKI) na nimegundua kwamba Mwanakijiji anazungumzia what next ktk hatua ya kwanza ambayo inakitaka chama Chadema kuweka SABABU, NIA na hatimaye kupata UWEZO wa kukiondoa chama CCM. Na huo uwezo ndio tunauomba hapa pasipo sababu. nadhani sasa hivi nimempata vizuri sana.

Pasipo SABABU watu hawawezi kuunda UMOJA ili kumwondoa CCM, na ni kutokana na sababu hiyo ndipo NIA ya kumwondoa mtu au chama madarakani hutokea hivyo nadhani kosa dogo alilofanya hapa ni kuweka hili neno what next badala ya kuuliza SABABU ambayo itajenga NIA, kwani ikumbukwe tu kwamba hata Marekani walipoweka NIA ya kumwondoa Saadam Hussein walikuja na SABABU pamoja na kwamba ilikuwa ya uongo na uzushi, sababu ambayo iliwajaza watu (HOFU -Fear) kubwa inayoweza kuzaa CHUKI (Weapon of Mass Destruction). Ingawa hawakufanikiwa sana kupata UMOJA wa nchi za kimataifa, lakini ilikuwa na nguvu kubwa ya mvuto wakawapata wachache waliohofia na wakaweka NIA.

Na hata kabla ya kuvamia Afghanstan, Marekani tena walizua tena SABABU nyingine 9/11 (Hofu) ili kuivamia nchi hiyo, hivyo waliweza kujenga NIA ya kuwasaka Al Qaeda popote walipo duniani..Sasa tofauti na Marekani au hata mageuzi ya kisiasa, Chadema imeonyesha kukerwa na Ufisadi kama walivyochukia watanzania wengine, lakini chuki hii haikuzaa NIA isipokuwa walikaa pembeni na kukubali matokeo. Leo imefika wakati wa uchaguzi mkuu, Chadema wanaonyesha NIA ya kumwondoa CCM kwa kero zake na sii chuki inayolingana na sababu kubwa wananchi wanataka kuona CCM ikitokomezwa.

Sasa ndani ya mioyo ya watu wengi wanashindwa kuunganisha picha hizi mbili..Kwa nini Chadema inataka kumwondoa CCM madarakani? ni zipi haswa sababu au ndio kutokana na mfumo uliopo kwamba imefikia wakati wa Uchaguzi, basi chama hiki kama vyama vinginevyo hawana budi wala hila isipokuwa kugombea kwa sababu ni swala la demokrasia!.

Ikiwa ndivyo basi Chadema wanaiondoa CHUKI ya wananchi, wanaaondoa pia NIA ya wananchi kujiunga ktk mapambano haya kwani pasipo sababu ya dhati ni sawa na mtumwa kubebeshwa mzigo usijue alichobeba... Waswahili wanasema wanauziwa mbuzi ndani ya gunia. Hii ndio hofu ya wengi na pengine Mwanakijiji mwenyewe anasita kuchukua silaha na kusimama msitari wa mbele kwani pasipo sababu au sababu za kizushi siku zote haziwezi kushinda vita.

Ni kweli maneno yake Mwanakijiji kwamba Marekani wameshindwa vita ya Iraq kwa sababu ile sababu ya awali ilikuwa uongo na Uzushi hivyo umoja wa Mataifa walishindwa kuungana na uongo ule usokuwa na ushahidi wakutosha, na mimi katika imani yangu naamini kabisa ukimzushia mtu jambo ambalo sii la kweli, basi hata mafanikio yake hayawezi kudumu..Na ndio maana Marekani wamejikuta wakipigana vita visivyokwisha na hatimaye nina hakika Marekani watachoka na kushindwa..Iraq itabakia Somalia nyingine, nchi iliyoharibiwa kwa matakwa ya binadamu.

Kwa hiyo, Chadema wanatakiwa kuja na SABABU ambayo itajenga NIA ya wananchi kuungana nao kuiondoa CCM madarakani na sii swala la what next..Na hakika sababu yenyewe hakuna zaidi isipokuwa UFISADI.
 
KUDOS to CHADEMA.......................kwa kumchagua Dr Slaa kuwa mgombea wa Urais wa Tanzania..........ninasema.....hii ni BIG PLUS si kwa CHADEMA TU bali hata kwa vyama vingine vya upinzani.................once again hongereni sana Watanzania................sasa ni Watanzania na goli......tushindwe wenyewe.............
 
Kwa upande mwingine chadema nao wawe makini wasije wakawa kama NCCR mageuzi ya wakati ule ambapo ilisambaratika baada ya uchaguzi. all in all tunawatakia kila lakheri katika michakato yao angalau wapunguze vijembe na majivuno ya CCM ambayo yanatulaza njaa kila siku.
Na wewe tuwe pamoja, usiwatakie kila la kheri tafadhali unga mkono juhudi hizi, tulete mabadiliko.
 
Back
Top Bottom