Sasa ukitafakari kwa makini, hili la wapinzani na Chadema na mtazamo wa Watanzania wengi kuwa kwanza tuing'oe CCM, lakini inaelekea bado hatujajiandaa vya kutosha kuweza kuongoza tukishaiondoa CCM.
Si kwamba nadai CCM ibakie madarakani au isiondolewe, lakini kama Bibi Ntilie alivyobainisha kwenye barua ya Mnyika, yaelekea Chadema bado hawajajiandaa na hawajiamini kuwa wana uwezo wa kuongoza Taifa. Dua lao ni CCM ianguke, ndipo wao waanze kujifunza na kujipanga ni vipi waongoze Tanzania.
Ndiyo maana Mwanakijiji anauliza, then what?
Ikiwa mfupa wa TAMISEMI ambapo huko ndipo safu ya kwanza ya kuongoza nchi, Chadema walikukwepa wala hawakujituma kupata viti angalao nusu ya mkoa kama Dar, iweje leo tudhanie kuwa wataweza kuwa makini na uwezo wa kuongoza nchi kwenye Serikali Kuu na Bunge?
Makovu haya hayaweza kusawazishwa pamoja na hili la sasa la kuvizia mabaki ya CCM yaanguke ndipo yaingie Chadema na kuhakikisha walau Chadema wanaweza pata viti 70 vya ubunge.
Ni kutokana na hayo, ndio maana nakubaliana na Mwanakijiji kuhoji je tukishaing'oa CCM, then what? Maana inaelekea kama vile tulivyopata Uhuru au vile Kikwete alipata Urais, bado hatujajiandaa kuongoza na hatujiamini kuwa tuna uwezo wa kutawala.
Kila udhaifu wa CCM umetolewa majukwaani, lakini hapajawahi tolewa alternative solution ambayo ikakubalika hata ndani ya Chadema yenyewe, kila mara tunaambiwa "Subirini tuingie Ikulu". Je ina maana Chadema na Upinzani hauwezi kuanza kuleta maendeleo Tanzania mpaka viingie Ikulu?
Miaka mitano, bajeti ya nchi imekuwa ikiongezeka na matumizi ya hali ya juu. Ripoti ya mkaguzi mkuu CAG kwa miaka mitatu inaonyesha udhaifu wa Serikali kuu ambao umeimarisha ubadhirifu na rushwa. Lakini sijasikia hata siku moja hoja ya kutungwa Sheria au kusitisha Bajeti kutoka kwa Upinzani ili Serikali ijirudi na kurekebisha mfumo wake wa matumizi na hata kubana matumizi. Je wajibu huu ambao kawaida hufanywa na Chama cha Upinzani kama haukufanywa na Chadema na wenzao, bado mtasema tusubiri wakiingia madarakani?
Labda nihitimishe kwa kutoa mtazamo mwingine. TUfanye kwamba Upinzani umeshinda Uchaguzi Mkuu kwa asilimia 51% hiyo 49% ni ya CCM, pale Bungeni na hata Urais ni wa Upinzani. Inapokuja kwenya ufanyako kazi na utekelezaji hasa kwenye ngazi za Tawala za Mikoa (TAMISEMI), watendaji wengi wa kisiasa takriban asilimia 95% ni CCM ambao walishinda Udiwani na uchaguzi wa TAMISEMI 2009. Je Upinzani utawezaje kufanya kazi yake kwa ukamilifu bila mvurugano na hawa watu wa CCM ambao watakuwa wakisikiliza sauti za wale 49% walioko Bungeni?
Kila mtu anataka CCM iondoke, lakini hatuko tayari kukipa chama nafasi eti kikajifunze kazi kama Kikwete alivyofanya au kuwa ni Chama kisicho na wenye uwezo wa kutosha kuongoza na kufanya kazi kitendaji kama zile Tanzania ilivyopata Uhuru wake.
Baya zaidi, bado mpaka leo Chadema na Upinzani havieleweki Ki-Sera kwa Watanzania na hatujui watakuja na mipango gani ya Kisiasa na kimaendeleo kwa kueleweka kuliongoza Taifa la Tanzania.
Hivyo basi, inabidi tujiulize, je tuko tayari kuendelea kubahatisha kama Kikwete kwa miaka miwili ili kuelewa nini wajibu wa kuongoza nchi na kuwa na sera zinazoeleweka au ni lazima tujiamini na kuingia tukiwa tayari na Sera zetu zikieleweka kwa Wananchi ambao hawatahitaji miaka miwili kuzielewa na kuanza kuzifanyia kazi?