Yafuatayo hunitokea mara baada ya kunywa pombe

Wakuu poleni na majukumu ya kulijenga taifa letu pendwa la Tanzania. Pia poleni sana na mfumko wa bei uliopo nchini na dunia ni kwa ujumla.

Ndugu zangu wana JF, mimi ni mtumiaji wa masanga(pombe) japo mara chache chache. Na siku ambayo hutumia kinywaji hiki huwa ni Jumamosi kwa maana ya kwamba ndiyo siku ambayo nakuwa mapumziko.

Na pombe nazokunywa ni hizi hizi bia za kawaida yaani za watu wenye uchumi wa kati (Kilimanjaro, Serengeti, Castle) na wakati mwingine napiga hizi ngumu nyeupe.

Baada ya kunywa balaa huwa ni kesho yake napatwa na:
1. Huzuni
2. Huruma
3. Wasiwasi
4. Kutojiamini
5. Majuto
6. Majonzi

Kwa wataalam naombeni mawazo yenu yote hayo husababishwa na nini?

Maana kwa kuhofia kupatwa na niliyoyaeleza hapo juu, najikuta naogopa kutumia pombe tena

Mpaka hapo umeshagundua negativity za pombe,sawa Ni kuacha tu you gona lose nothing,tulikua hivyo now tunaejoy life with out liquor stress,maana hivyo vyote vinavyokutokea wewe vilipaswa visikutokee baada ya kupata masanga! Maana Ni kawaida ya pombe kumpa mtu artificial intelligence baada ya kulewa, issues Kama ujasiri wa kijinga,huruma kwa walevi wenzako, etc
 
Wakuu poleni na majukumu ya kulijenga taifa letu pendwa la Tanzania. Pia poleni sana na mfumko wa bei uliopo nchini na dunia ni kwa ujumla.

Ndugu zangu wana JF, mimi ni mtumiaji wa masanga(pombe) japo mara chache chache. Na siku ambayo hutumia kinywaji hiki huwa ni Jumamosi kwa maana ya kwamba ndiyo siku ambayo nakuwa mapumziko.

Na pombe nazokunywa ni hizi hizi bia za kawaida yaani za watu wenye uchumi wa kati (Kilimanjaro, Serengeti, Castle) na wakati mwingine napiga hizi ngumu nyeupe.

Baada ya kunywa balaa huwa ni kesho yake napatwa na:
1. Huzuni
2. Simanzi
3. Wasiwasi
4. Kutojiamini
5. Majuto ( kujiona mkosefu)
6. Majonzi
7. Pia nakuwa mwingi wa huruma.
Kwa wataalam naombeni mawazo yenu yote hayo husababishwa na nini?

Maana kwa kuhofia kupatwa na niliyoyaeleza hapo juu, najikuta naogopa kutumia pombe tena

Mkuu hizi wataalamu wanaziita withdrawal symptoms humtokea mtu masaa kadhaa baada ya pombe aliyokunywa kuisha mwilini halafu hajaongeza nyingine, hata mimi zimenisumbua Sana mpaka nimeamua kuachana na kamnyweso,
Kwa mfano nimekunywa Jana afu Leo asubuhi nisinywe baada ya masaa kadhaa najisikia wasiwasi, uoga, moyo unaenda mbio, huzuni na ikitokea nisiguse mpaka usiku silali na nikilala ni manightmare tu nashtuka moyo unaruka kichurachura.
Mwanzo sikutambua hizi dalili hivyo ikawa dawa ya moto ni moto nikijisikia hivyo naagiza k_veve nashushushia ghafla bin vuu dalili zote zinapotea. Si dalili nzuri ni mwanzo wa addiction especially pale utapoamua kuzirelief kwa kuongea ingine, mi ilibaki kidogo tu niwe addicted kwa sababu hiyohiyo. Saivi na Pambana sigusi Tena.
 
Mkuu hizi wataalamu wanaziita withdrawal symptoms humtokea mtu masaa kadhaa baada ya pombe aliyokunywa kuisha mwilini halafu hajaongeza nyingine, hata mimi zimenisumbua Sana mpaka nimeamua kuachana na kamnyweso,
Kwa mfano nimekunywa Jana afu Leo asubuhi nisinywe baada ya masaa kadhaa najisikia wasiwasi, uoga, moyo unaenda mbio, huzuni na ikitokea nisiguse mpaka usiku silali na nikilala ni manightmare tu nashtuka moyo unaruka kichurachura.
Mwanzo sikutambua hizi dalili hivyo ikawa dawa ya moto ni moto nikijisikia hivyo naagiza k_veve nashushushia ghafla bin vuu dalili zote zinapotea. Si dalili nzuri ni mwanzo wa addiction especially pale utapoamua kuzirelief kwa kuongea ingine, mi ilibaki kidogo tu niwe addicted kwa sababu hiyohiyo. Saivi na Pambana sigusi Tena.
Umeongea mule mule mkuu,hata mimi inabidi nianze zoezi la kuacha
 
Mimi sinywi pombe nadhani ni kwasababu ya ubahili wangu tu,ila nikionja kidogo huwa nachangamka,najihisi amani sana na ujasiri unaongezeka. Mwaka mzima naweza kujikuta nimekunywa bia tano tu kwa interval fulani.
 
Mimi👇😁😁😁
WAAM1YhRjc.jpeg
 
Back
Top Bottom