Matumizi ya pombe safarini ni hatari kwa uhai wako mwenyewe

Tlaatlaah

JF-Expert Member
May 18, 2023
8,184
11,607
Maisha ni zawadi kutoka kwa Mungu, lazima tutuinze na kuithamini zawadi hii muhimu kwetu sote. Tufurahie uhai na mema mengi ya Mungu alieyoyajaza katika ulimwengu huu.

Imeibuka kasumba kwa wanywaji pombe hasa vijana, mathalani, anasafiri kutoka mkoa moja kuelekea mkoa mwingine, kutumia vilevi hususani pombe.

Unakuta abiria huyo ama ana mzinga mkubwa wa Konyagi, K-vant au hivi vipombe flani vyenye flavor tofauti tofauti lakini kilevi ni kilekile, ambazo konyagi nao pia wameiga.

Baadhi yao wanakua wamejaza kwenye chupa za maji kukwepa kuonekana wanakunywa pombe, lakini wengine bila soni wanafakamia na michupa vilevile. Mnafika mwisho wa safari kijana kalewa chakari.

Sasa, shaka langu hapa ni kwamba ikitokea ajali, mtu huyu si, ni rahisi sana kupoteza maisha, kwasabb kupata ajali katika hali ya ulevi, hali ambayo inaweza kupelekea ashindwe kujiokoa mwenyewe panapostahili kujiokoa. Na mtu akishalewa akili yake inakua slow kumake decision, lakini pia anaweza akapitiwa usingizi fofofo ambao hata akiamshwa anaweza asiweze kuamka kabisa.

Lakini pia kwasababu pombe huchochea msukumo na mgandamizo wa damu kuwa wa kasi zaidi mwilini, mtumiaji pombe huyu akiumia anaweza kupoteza damu nyingi zaidi na hatimae akapoteza maisha pia.

Rai yangu kwa vijana na wanywa pombe safarini.

Kuweni wastahimilivu na wenye subra hadi mwisho wa safari ndipo kuzitafuta na kuzinywa vilivyo hizo pombe.

Pili, makondakta wa mabasi ambao pia miongoni mwa hutumia pombe wakiwa kazini, kuacha mara moja tabia hii isiyo yakiungwana, na kuwakemea abiria wanao tumia pombe ndani ya mabasi.

Mwisho ni kwa dereva bodaboda wote, ndugu zangu acheni izo mtaisha na kuwa walemavu wote. Kunywa pombe zako baada ya kazi, itakusaidia kuepuka ajali na ulemavu.

Ni kero na usumbufu kwa abiria wasiotumia aina hiyo ya kinywaji.

Asante.
 
Pombe inachokifanya ni kukondolea woga,kwahiyo unayoyafanya barabarani unayajua mwenyewe,Don't drink and drive
Screenshot 2023-11-14 165800.png
.....
 
Ila kaka kama kwako pombe haiswii kwanini usifokasi kwenye maji

Acha kupoteza muda wako kuanalaizi mareeeeeeeeefu kitu ambacho hauna mapenzi nacho. Hebu ashum ungeandika mareeeeefu hivyo kuhusu benefits of water
kama wewe usingesoma kabsaaaa na unavyopenda umbea
 
Jambo ambalo unatakiwa ulifahamu uyo dereva wa mkoa anayekuenda asilimia kubwa wengi wanatumia kilevi wakiwa safarini.
Safari ndefu zinachosha mno akili na mwili na zinakuletea hasira zisizo na maana,lakini ukipata valuer yako safari inakuwa fupi na yenye raha
 
Jambo ambalo unatakiwa ulifahamu uyo dereva wa mkoa anayekuenda asilimia kubwa wengi wanatumia kilevi wakiwa safarini.
Safari ndefu zinachosha mno akili na mwili na zinakuletea hasira zisizo na maana,lakini ukipata valuer yako safari inakuwa fupi na yenye raha
Mwisho wa mwaka huu ndrugu zangu tayari RIP zimeanza mapema sana kuliko mery Christmas in advance, Tujihadhari sana na uerevu wa kilevi usio na maana japo ni starehe. Tulianza na Mungu, Tumalize na salama na Mungu 2023...
 
Mwisho wa mwaka huu ndrugu zangu tayari RIP zimeanza mapema sana kuliko mery Christmas in advance, Tujihadhari sana na uerevu wa kilevi usio na maana japo ni starehe. Tulianza na Mungu, Tumalize na salama na Mungu 2023...
Hauwezi kuzuia kifo kila mtu lazima atakufa haijalishi unatumia kile au hautumii.
Maisha yafaa nini bila pombe?
 
27Pombe ni kama uhai kwa mtu ukinywa kwa kiasi.
Maisha yafaa nini bila pombe?
Imeumbwa iwafurahishe watu.

28Kunywa pombe wakati wake na kwa kiasi,
Kwaleta shangwe moyoni na furaha rohoni.
Usimkaripie jirani yako kwenye pombe,
Wala usimdharau anapofurahia karamu.
Usimwambie neno la kumwonya,
Wala usimsumbue kwa kumtaka alipe deni..


Kama wewe ni mkristo hiyo ni biblia inasema hivyo
 
Hauwezi kuzuia kifo kila mtu lazima atakufa haijalishi unatumia kile au hautumii.
Maisha yafaa nini bila pombe?
basi sawa kuna mwingine atasema maisha ya faa nini bila kunyanduana....

Rai yangu ni moja tu ndugu yangu, hakuna wa kukukataza kufakamia pombe zako, jihadhari na unywaji pombe ukiwa UNASAFIRI, singependa unikumbuke akati unakata roho kama ambavyo bodaboda hujutia kwa sauti "mamaaa nakufa kwasababu ya kiburi changu kukatiza mataa nikiwa nimelewa na bila tahadhari" huku utumbo wote nje na miguu haijulikani ilipo, semitrela la cement limefanya kazi yake...

hiyo singependa imtokee yeyote aliepitia bandiko hili, ni mbaya sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom