Ya Polisi na vyama vya siasa Tanzania

Nonda

JF-Expert Member
Nov 30, 2010
13,358
4,304
WanaJF,

Jeshi la polisi hapa Tanzania linaongozwa na nani ?

Wakuu wa mikoa ? wakuu wa wilaya ? au wakuu na maofisa wa jeshi hili ?

Wamepata mafunzo wapi? Kivukoni? Au vyuo vya Polisi?

Kazi ya jeshi la polisi ni nini ? Kubambikia raia kesi ? Kulinda usalama wao na mali zao?

Je chombo hichi ni cha umma au ni miliki ya chama fulani cha siasa ?

Mimi sijawahi kusikia hata siku moja kuwa imetokea mkutano wa Chama Cha Mapinduzi kimezuiliwa kufanya mkutano, au « hakikupewa kibali ».

Je wewe msomaji unakumbukumbu ya CCM kuzuiliwa wasifanye mkutano ? Au kutokupewa kibali cha mkutano ?

Hili la kibali ,ni dhana potofu, any way, Chama cha siasa hakiombi kibali cha kufanya mkutano, bali wanatakiwa kutoa taarifa in advance, ili polisi iweze kujiandaa kulinda usalama katika mkutano.

Sasa nikuulize wewe msomaji. Mara ngapi umeshasikia kuwa mkutano wa CHADEMA, NCCR, CUF umezuiliwa au haujapewa kibali ?

Hutokea vyama ambavyo vilikwishatoa taarifa ya kufanya mkutano na kuambiwa kuwa polisi haina askari wa kutosha kulinda tukio siku hiyo. Lakini inapotokea Chama hicho kikisema « sisi tutafanya mkutano wetu hivyo hivyo »

Utashangaa ! Polisi hii iliyosema haina askari wa kutosha kulinda mkutando, huanza mapema kufunga barabara zinazoelekea sehemu ya tukio. Polisi hii hii inaazima askari kutoka sehemu za jirani kuhakikisha wana askari wa kutosha kuzuia mkutano usifanyike lakini hawana askari wachache wa kulinda mkutano.

Je Polisi wana maelezo ya kutosheleza kueleza ni kwa nini ni mikutano ya vyama vya upinzani tu ndio wao huwa hawana askari wa kulinda tukio ?

Ni kwa nini mara nyingi « hawatoi kibali » cha mkutano kwa vyama vya upinzani ?

Je Polisi yetu inafanya kazi kwa msukumo wa kisiasa ?

Kama ni hivyo, Tendwa ana nafasi ipi katika kuuondoa uoza huu ?
 
tatizo tulilonalo ni ccm kuwa chama dola. bila dola hamna ccm, na kwa kujua hivyo vyombo vya dola ikiwemo polisi wanajiona kuwa wanawajibika kuilinda CCM kwa kila hali wakati wahanga wakubwa wa sera za ccm ni hao hao polisi, angalia maisha yao yalivyo ya taabu, nyumba zao, mishahara yao n.k, halafu wanajidai wao ni ccm sana. wakati mwingine mtu unajiuliza hawa watu wanakili sawasawa? au ndio yale ya Plato wa zama za kale kuwa maaskari kwa wale wasiofikiri sawasawa.
 
Sote ni mashahidi wakati wa uchaguzi mkuu jeshi la polisi lilijitahidi kufanya kazi zake kwa mujibu wa sheria. Inaelekea jambo hilo liliwahudhi wakubwa, na kuna tetesi baadhi ya ma RPC walionywa, matokeo yake mambo yamekuwa tofauti katika ucha guzi wa madiwani. haina budi kadri ccm inavyozidi kupoteza mvuto ndivyo tutakapozidi kushuhudia matumizi mabaya ya jeshi hilo.
 
Aisee nimesikia bbc network Africa ya saa tatu usiku kuwa watu zaidi ya 10 wameuawa kwa risasi za moto.

Mwenye habari zaidi atupe wana JF
 
Mbona kwenye taarifa ya habari ya kwetu hawajatangaza? Kama ni kweli hao polisi wachukuliwe hatua haraka iwezekana hivyo
 
Mbona kwenye taarifa ya habari ya kwetu hawajatangaza? Kama ni kweli hao polisi wachukuliwe hatua haraka iwezekana hivyo

Polisi wanatimiza wajibu kutokana na order za wakubwa wao.Hawa wakiadhibiwa tunawaonea. Kama sheria itachukua mkondo wake iwe ni kwa mabosi wao wanaotoa hizo order.
Aibu!!!
 
kumradhi ni bbc network africa ya saa nne,Mwakilishi wa BBC aliyeko Dar es salam amesema wamejaribu kuwasiliana na kamanda wa polisi wa Arusha,simu imefungwa na sasa hivi vurugu zinaendelea hivyo kuna uwezekano wa watu zaidi ya hao kufa,walioko Arusha tupeni habari kutoka huko
 
Haya ndo yale niliyoyasema! This is a new chapter which i'l change the history of TZ na kuwa NCHI YA VURUGU!
 
....Ngoja tuwapigie CNN wamwage mtama kwenye kuku wengi ili huyu **** akitembeza bakuli tena wamtimulie mbali. Pia tuta m twitter Gibbs ili amtonye Jaluo kuwa yule msanii safari hii amtoe benzi, maana ni kama kenya vile....
 
10 wauwawa kwenye ghasia mjini Arusha


100721174848_wilbroad_slaa_226x170_nocredit.jpg

Dr Wilbroad Slaa naye pia amekamatwa


Watu wasiopungua kumi wameripotiwa kuuwawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mji wa Arusha Tanzania, kwenye makabiliano baina ya Polisi na wafuasi wa chama cha upinzani cha CHADEMA.

Ghasia zilianza baada ya Polisi kumkamata mwenyekiti wa kitaifa wa chama hicho Freeman Mbowe na mbunge wa Arusha mjini Godbless Jonathan Lema, wakiwa wanaelekea kuhutubia mkutano wa kisiasa.

Baadaye polisi pia walimkamata aliyekuwa mgombea wa chama hicho cha CHADEMA kwenye uchaguzi wa Urais uliofanyika mwezi Oktoba Dr Wilbroad Slaa.

Taarifa zinasema biashara kadhaa zilichomwa moto kwenye vurugu hizo.

Kwa mujibu wa waandishi wa habari mjini Arusha, Polisi walikuwa wamewakataza viongozi wa CHADEMA na wafuasi wao kufanya maandamanao kabla ya mkutano wa kisiasa wa Jumatano, lakini mamia ya wafuasi wa chama hicho wakawafuata viongozi hao walipokuwa wanaelekea eneo la mkutano.

Bwana Slaa amenukuliwa akisema maandamano hayo yalikuwa ya kupinga ufisadi katika serikali mpya ya Rais Jakaya Kikwete.

Polisi walifyatua risasi hewani mara kadhaa kutoa tahadhari kwa maelfu ya wafuasi waliokwenda kutaka viongozi wao waachiwe huru, na baadaye wakafyatua gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya.

Walioshuhudia wanasema Polisi waliendelea kufyatua risasi mchana kutwa, huku wafuasi wa CHADEMA wakiendelea kukabiliana na askari Polisi katika maeneo mbali mbali ya mji wa Arusha.

Kwenye mkutano huo wa kisiasa, Dr Slaa aliwataka Polisi kumwachilia huru Bwana Mbowe na wengine, na pia akamtaka Rais Kikwete kujiuzulu.

Hadi kufikia Jumatano jioni hakuna taarifa iliyokuwa imetolewa na serikali kuhusu mzozo huo.

Kumekuwa na mvutano wa kisiasa nchini Tanzania tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa Urais ambao vyama vya upinzani vinadai ulikuwa na udanganyifu.

Kufuatia uchaguzi huo shinikizo zinaendelea za kutaka Tanzania iwe na katiba mpya tofauti na iliyopo sasa, ambayo hairuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais kupingwa mahakamani yanapotangazwa na tume ya uchaguzi

Source: BBC swahili
 
Hii inabadilisha historia ya Tanzania sasa! Na hali itaendelea kuwa mbaya zaidi inapaswa kesho Watanzania wote waandamane kwa kulaani mauaji ya Watanzania wasiokuwa na hatia yaliyotokea leo.
 
At least 10 people!!!!!!!! meaning idadi yaweza kuwa zaidi.

Maandamano ni haki ya raia lakini Tanzania inabidi uruhusiwe na polisi.
Sijui polisi wataendelea kuua watanzania wenzao mpaka lini.

Yet CCM tends to preach peace and tranquillity
 
Our blood shall irrigate our victory, rest in peace sons and daughters of the land
 
Mlale salama watu wa arusha, tutakesha pamoja hadi kieleweke!
 
mkuu,

hii ripoti umeisikia peke yako?

siku hizi JF ina junior members wengi lakini wanazungumza kama seniors!!

wewe umeiskiliza saa ngapi? umeisikia mwenyewe? jee lugha inapanda? Unaelewa ung'enge?



Nonda JF ni forum ya watu wenye source na sio wapayukaji......msome ANFAAL amekupa na source usiwe hayo mambo ya lugha inapanda manake nini......kaka kuna mitandao unatakiwa ucheki unapopata news......
 
Back
Top Bottom